STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 23, 2014

Katibu Mkuu mpya wa Yanga aahidi makubwa Jangwani


TIBO
Katibu Mkuu wa Yanga, Dk Tiboroha akizungumza na waandishi wa habari, huku Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Jerry Muro akiwa makini.

SIKU chache baada ya kutangazwa kushika nafasi ya Ukatibu Mkuu ndani ya klabu ya Yanga, Dk Jonas Tibohora aahidi makubwa kwenye klabu hiyo.

Dk, Tobohora akizungumza leo jijini alisema kuwa, ndoto yake ni kuona Yanga ikijiendesha kiuchumi.
Katibu mkuu huyo amesema anataka kuiongoza Yanga kujiendesha kiuchumi, katika mpango wake huo anataka kuanza kutengeneza kikosi imara cha ushindani ikiwa ni pamoja na kutengeneza mifumo bora ya soka la vijana klabuni hapo
Lengo kubwa la kuwekeza kwenye timu za vijana ni kujalibu kupunguza ghalama za kununua wachezaji kutoka nje,pia amesema sasa ni muda wa klabu hiyo kunufaika na nembo ya klabu hiyo kibiashara.

Dk Tobohora amechukua nafasi ya Beno Njovu aliyemaliza mkataba na kutotaka kuendelea kwa madai ya kutingwa na majukumu mengi binafsi.

No comments:

Post a Comment