STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 23, 2014

Cargliari yamtimua kocha wake kisa...!

http://cdn.bleacherreport.net/images_root/slides/photos/002/654/635/hi-res-153607730_crop_650x440.jpg?1349634469BAADA ya timu ya Cargliari iliyopo Ligi Kuu ya Italia, Serie A kufanya vibaya mfululizo, uongozi wa klabu hiyo umemtupia virago kocha wake, Zdenek Zeman.
Kocha Zeman ametimuliwa baada ya Cargliari kupata ushindi katika mechi mbili msimu huu, kitu ambacho kimeufanya uamuzi kusitisha mkataba na kocha huyo kutoka Jamhuri ya Czech.
KOcha huyo wa zamani wa AS Roma ametimuliwa wakati timu hiyo ikiwa katika nafasi ya 18 katika msimamo wa Serie A. 
Kipigo cha mabao 3-1 walichopata ugenini dhidi ya vinara Juventus Alhamisi iliyopita ndio ulikuwa mchezo wa mwisho kwa kocha huyo mwenye umri wa miaka 67. 
Katika taarifa yake klabu hiyo ilimshukuru kocha huyo kwa kipindi chote ambacho wamekuwa naye kwa miezi kadhaa na kumtakia kila la heri popote atakapokwenda. 
Kocha wa zamani wa klabu ya Al Jazira, Walter Zenga ambaye kwa sasa hana kibarua anapewa nafasi kubwa ya kuchukua mikoba ya Zeman.

No comments:

Post a Comment