STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 20, 2015

Yamoto Band watua UK tayari kwa shoo wa kesho


Kikosi kizima cha Yamoto Band ndani ya jiji la London tayari kwa makamuzi ya jumamosi hii ndani ya ukumbi wa Royal Regency Monor Park London

Yamoto Band Touchdown London this morning., safe and sound.Now let's Get it...Let's Goooo. ..Made in East Africa 2015 ,Yamoto band Live in London Royal Regency Banquite .



Wakijiachia na mmoja wa mabosi wake







Enock Bella akiosha maji

Wacheza filamu nchini waonywa

Mlela akipeana mkono na Katibu Mtendani wa Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fisoo
Na Genofeva Matemu, Maelezo
WASANII wa filamu nchini wameshauriwa kutumia taaluma waliyonayo kupanua wigo wa filamu nchini na kuitangaza Tanzania duniani kote kwa kuzingatia matumizi mazuri ya lugha ya Kiswahili katika filamu wanazozitengeneza.
Rai hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu, Joyce Fisoo, juzi alipokutana na wasanii waliotarajia kuondoka jana kwenda Uingereza kurekodi filamu ya 'Sabasi' na Kampuni ya Didas Entertainment iliyopo nchini humo.
Fisoo alisema kuwa baadhi ya wasanii nchini wamekuwa makontena yanayopitisha biashara haramu kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine hivyo kuwaomba wasanii wanaokwenda Uingereza kuachana na tabia hiyo bali watumie fursa waliyoipata kuiwakilisha Tanzania vizuri na kutengeneza filamu bora itakayowawezesha kujulikana na kufungua fursa za kushirikishwa katika filamu na nchi nyingine duniani.
Aidha, Fisoo aliwataka wasanii hao kuheshimu sheria, kanuni na taratibu za Uingereza kwani kwa kufanya hivyo watakuwa mabalozi bora na kutoa nafasi kwa wasanii wengine kupata fursa hizo.
Naye Mama wa Didas Entertainment, Nuru Idrisa, aliwataka wasanii wa Bongo Movie waliopata nafasi ya kurekodi filamu na Didas Entertainment kujiheshimu na kuvaa mavazi ya staha yatakayostiri miili yao muda wote watakaokuwa nchini Uingereza kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wamelinda heshima ya nchi.
Akitoa neno la shukrani, msanii wa Bongo Movie, Yusuph Mlela, aliishukuru Bodi ya Filamu kwa kuwa bega kwa bega na wasanii na kuwaahidi wadau wa filamu nchini kazi bora na yenye tija katika jamii.
Filamu ya 'Sabasi' inatarajiwa kurekodiwa hivi karibuni nchini Uingereza na Kampuni ya Didas Entertainment na kuwashirikisha wasanii Mlela, Esha Buhet na Husna Athumani, na ni filamu ya pili kurekodiwa na kampuni hiyo na kuwashirikisha wasanii kutoka Tanzania. Filamu ya kwanza kurekodiwa na kampuni hiyo iliyowashirikisha wasanii kutoka Tanzania ni ile ijulikanayo kwa jina la 'Mateso Yangu Ughaibuni'.

Balotelli alianzisha tena Liverpool

3f
Muunganiko wa picha zilizochapishwa na Daily Mail zinazomuonyesha Balotelli na nahodha wake, Steven Gerrard
Balotelli akifunga penati yake
Balotelli took the ball off Liverpool captain Jordan Henderson and fellow striker Daniel Sturridge to take the penaltyMARIO Balotelli, aliifungia Liverpool mkwaju wa penati dakika tano kabla ya kumalizika kwa pambano lao dhidi ya Besiktas ya Uturuki, lakini ameibua mambo.
Kitendo chake cha kulazimisha kuipiga penati hiyo kimemtibua nahodha wa timu ya Liverpool Steven Gerrard anayemshutumu kwa utovu wa nidhamu.
Balotelli alifunga penalti hiyo na kuiwezesha Liverpool kuibuka washindi wa bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Ndogo ya Ulaya, katika uwanja wa Anfield.Hali hiyo ilijitokeza baada ya kushindwa kuelewana na nahodha wa mchezo huo Henderson na Daniel Sturridge juu ya nani abebe jukumu la kupiga penalti hiyo.
Gerrard amesema: "Henderson ni nahodha na Balotelli kwa kiasi fulani alionyesha kumkosea adabu katika hali hiyo."
Gerrard ambaye kwa sasa ni majeruhi, alikuwa mchambuzi katika matangazo ya mchezo huo kwenye televisheni ya ITV ya nchini Uingereza.
Katika mechi nyingine timu ya Tottenham Hotspur ililazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Fiorentina wakati Everton wakipata ushindi mnono wa mabao 4-1 ugenini dhidi ya Young Boys ya Uswisi.

NASAHA ZA IJUMAA-SIRI SIRINI