STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 20, 2015

Balotelli alianzisha tena Liverpool

3f
Muunganiko wa picha zilizochapishwa na Daily Mail zinazomuonyesha Balotelli na nahodha wake, Steven Gerrard
Balotelli akifunga penati yake
Balotelli took the ball off Liverpool captain Jordan Henderson and fellow striker Daniel Sturridge to take the penaltyMARIO Balotelli, aliifungia Liverpool mkwaju wa penati dakika tano kabla ya kumalizika kwa pambano lao dhidi ya Besiktas ya Uturuki, lakini ameibua mambo.
Kitendo chake cha kulazimisha kuipiga penati hiyo kimemtibua nahodha wa timu ya Liverpool Steven Gerrard anayemshutumu kwa utovu wa nidhamu.
Balotelli alifunga penalti hiyo na kuiwezesha Liverpool kuibuka washindi wa bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Ndogo ya Ulaya, katika uwanja wa Anfield.Hali hiyo ilijitokeza baada ya kushindwa kuelewana na nahodha wa mchezo huo Henderson na Daniel Sturridge juu ya nani abebe jukumu la kupiga penalti hiyo.
Gerrard amesema: "Henderson ni nahodha na Balotelli kwa kiasi fulani alionyesha kumkosea adabu katika hali hiyo."
Gerrard ambaye kwa sasa ni majeruhi, alikuwa mchambuzi katika matangazo ya mchezo huo kwenye televisheni ya ITV ya nchini Uingereza.
Katika mechi nyingine timu ya Tottenham Hotspur ililazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Fiorentina wakati Everton wakipata ushindi mnono wa mabao 4-1 ugenini dhidi ya Young Boys ya Uswisi.

No comments:

Post a Comment