STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 22, 2015

Liverpool yaua, Spurs, Everton zabanwa nyumbani

Hivi ndivyo vita vya Liverpool na wenyeji wao Soputhmapton ilivyokuwa Victor Wanyama akichuana na Jordan Hendeson

WAKATI klabu ya Tottenham Hotspur ikilamizika kupigana kiume kurejesha mabao mawili ili wasife nyumbani mbele ya West Ham Utd, Liverpool wameendelea kutoa dozi kwa kuicharaza Southampton kwa mabao 2-0 katika mfululzii wa Ligi Kuu ya England.
Spurs ikiwa nyumbani ilitanguliwa kufungwa mabao 2-0 kabla ya kuyarejesha baadaye na kuambulia sare ya mabao 2-2, shukrani za pekee zieende kwa Harry Kane aliyefunga bao la kusawazisha baada ya awali kukosa penati na mpira kumrudia na kuutumbukiza wavuni.
Katika mchezo mwingine timu ya mkiani ya Leicester City ilijitutumua na kulazimisha sare ya ugenini ya mabao 2-2 dhidi ya Everton kabla ya hivi punde Liverpool kuandikisha ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Southampton.
Mabao ya Phillipe Coutinho katika dakika ya tatu na jingine la kipindi cha pili lililofungwa na Raheem Sterling liliwapa vijogoo hao wa Anfield kupata ushindi huo uliowafanya wafikishe jumla ya pointi 45 na kulingana Spurs ingawa wameshindwa kuiengua Southampton katika nafasi ya tano wakati ligi ikiwa ipo raundi ya 26.
Katika pambano hilo wenyeji walilalamika kunyimwa penati mbili za wazi baada ya wachezaji wao kufanyiwa madhambi langoni mwa Liverpool.

Mwadui Fc ndiyo mabingwa wa FDL2014-2015

Kocha wa Mwadui, Jamhuri Kihwelu 'Julio
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/DSC_4165.jpg
Mabingwa wa FDL,. Mwadui Shinyanga walioizabua Wana Kimanumanu kwa bao 1-0
'KOCHA Jamhuri Kihwelu 'Julio'amedhihirisha kweli yeye ni bab'Kubwa baada ya kuiongoza timu yake ya Mwadui Shinyanga kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Africans Sports ya Tanga na kunyakua ubingwa wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL).
Mwadui imeibuka na ushindi huo katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi na kuzima ngebe za wapinzani wao waliotamba awali kushinda pambano hilo kudhihirisha kuwa Mwadui ni 'vibabu'.
Hata hivyo tambo hizo za Wana Kimanumanu zilizimwa kwa bao tamu la kichwa lililofungwa na Kelvin Sabato 'Kiduku' na kuwapa taji Mwadui ambao waliongoza katika kundi lao la ligi daraja la kwanza na kupanda Ligi Kuu msimu wa 2015-2016 mwaka mmoja baada ya kubaniwa na TFF msimu uliopita.
Mbali na Mwadui, nyingine zilizopanda ligi hiyo msimu ujao kuchukua nafasi ya timu nne zitgakazoshuka katika Ligi ya msimu huu inayozidi kushika kasi ni Africans Sports, Toto Africans na Majimaji-Songea.

Mnyama afa Shinyanga, Stand Utd yaifanyizia

Kikosi cha Simba
BAADA ya kufanikiwa kuondoa 'gundu' kwa Polisi Moro na kudai walikuwa wameianza rasmia Ligi Kuu, klabu ya Simba leo ametolewa nishai ugenini mjini Shinyanga kwa kukubali kipigo cha bao 1-0.
Kipigo hicho kimetolewa kwa Simba na timu ya Stand United katika pambano tamu lililochezwa kwenyue uwanja wa Kambarage na kuzima mbwembwe za vijana wa Msimbazi huku mashabiki wao wakiibua zogo.
Zogo hilo lililosababisha pambano hilo kusimama kwa muda ilitokana na imani kwamba lango la wapinzani wao lilikuwa limefukiwa 'vitu' ambavyo vilikuwa vikiwafanya vijana wao kushindwa kufunga mabao.
Bao pekee lililowaua Simba ya kocha Goran Kopunovic, liliwekwa kimiani na Mnigeria Absalim Chiibibele likiwa ni bao lake la tano msimu huu katika dakika ya 11 na kuwafanya Simba kuhaha kurirejesha bila mafanikio.
Kwa kipigo hicho Simba imesaliwa na pointi pointi 20 baada ya mechi 16 wakati Stand imefikisha pointi 18 baada ya mechi 16 pia na itavaana na Kagera Sugar katika mechi yao ijayo mjini Shinyanga.

Yanga 'watamu' kama Mcharo! Yaifumua Mbeya City

Simon Msuva aliyeanza kufungua neema ya mabao Mbeya leo
Mrisho Ngassa  akadhihrisha amerejea upya Jangwani
Amissi Tambwe akamaliza udhia kwa kufunga bao la tatu
MABAO matatu kutoka kwa Simon Msuva, Mrisho Ngassa na Amissi Tambwe yameiwezesha Yanga kupata ushindi wa pili mfululizo jijini Mbeya baada ya kuicharaza Mbeya City kwa mabao 3-1.
Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ulichezwa kwenye uwanja wa Sokoine na kuiwezesha Yanga kuibuka na ushindi huo mnono ulioifanya izidi kujizatiti kileleni ikiwa na pointi 31 baada ya mechi 15.
Simon Msuva alianza kufunga katika kipindi kwanza kabla ya Ngassa 'kuzawadiwa' bao mara baada ya kipindi cha pili kutokana na mbwembwe za kipa David Burhan wa Mbeya City kumpoza.
Kipa huyo Bora wa msimu wa 2012-2013, alirudishiwa mpira na Steven Mazanda na badala ya kuupiga mbele alijaribu kumpiga chenga Ngassa aliyeunasa kilaini na kutumbukiza wavuni kaundika bao la pili la Yanga.
Amissi Tambwe aliunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Haruna Niyonzima na kuiandikia bao la tatu, wakati huo tayari wenyeji alishapata bao la kufutia machozi kupitia kwa Peter Mapunda.
Bao hilo la Mapunda limeitibua rekodi ya kipa Ally Mustafa 'Barthez'ambaye alikuwa amecheza muda wa dakika 704 bila kuruhusu wavu wake kutikiswa. Dakika hizo ni 630 za mechi sita na 74 za leo kabla ya Mapunda kumtungua kufuatia mabeki wake kushindwa kuokoa.
Kwa ushindi huo Yanga imejikita kileleni ikiwa na pointi 31 baada ya mechi 15 ikijiandaa kuondoka nchini kwenda Botswana kurudiana na BDF XI katika mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Simanzi! Christopher Alex hatunaye duniani!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgTo5gnxm0hxL2vl32ZTdKTWURp8bI9AhqxaS4u79wBsu7mcRP0Bn9ulEdWLFZaFH-QzfMXd4561SJIzpTRzFR-0cOFzLUd4bEqUojYVciaPBRvmiskU_my2Mc8MEQgDkCBkGg0-aT8C85u/s1600/426453_235934163168144_100002546855024_482737_173110702_n.jpg
Christopher Alex (wa tatu toka kulia) enzi za uhai wake akiwa na kikosi kilichoing'oa Zamalek mwaka 2003
KIUNGO nyota wa zamani wa klabu ya Simba na timu ya taifa, Taifa Stars, Christopher Alex Massawe amefariki dunia asubuhi ya leo.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo MICHARAZO imezipata mapema zinasema kuwa, kiungo huyo aliyekuwa akiugua kwa muda mrefu amefariki akiwa kalazwa katika Hospitali ya Milembe, iliyopo mkoani Morogoro.
Alex, anayekumbukwa kwa kupiga penati ya mwisho ya Simba iliyowavua ubingwa Zamalek ya Misri katika pambano la Ligi ya Mabingwa kati yao iliyochezwa mwaka 2013, alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kifua.
Mama mzazi wa Alex amethibitisha kutokea kwa kifo hicho ambaye alikuwa akiishi naye na kumuuguza kwa msaada wa wasamaria wema wakiwamo wadau wa soka.
Wakati klabu yake ya zamani ikiwa 'ímemsusa', mashabiki wa klabu hiyo na wengine wa soka walikuwa bega kwa bega na mama huyo kwa kuchangia fedha za matibabu, harambe kubwa ikiendeshwa na kituo cha Cloud's FM
Marehemu Christopher Alex, alizaliwa Septemba 12, 1975, na kupata elimu yake ya msingi katika shule ya msingi Uhuru na kumaliza katika shule ya Chamwino huko Dodoma mwaka 1993.
Alianza kucheza mpira kwenye timu ya daraja la nne ya Chamwino Utd na baadaye daraja la tatu akiwa na kikosi cha Aston Villa nayo ya Dodoma.

Mwaka 1999-2001, aliitumikia klabu ya CDA ya Dodoma, kabla ya kutimkia klabu ya Reli ya Morogoro mwaka 2002, na baadaye kujiunga na Wekundu wa Msimbazi Simba.
Marehemu ameacha mtoto mmoja aitwaye Alex.
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, jamaa na familia nzima ya marehemu Alex kwa msiba huo na kuwaombea Subira kwa Mungu kwa kukumbuka kuwa 'Kila Nafsi Itaonja Mauti'
Mungu aiweke roho ya marehemu Alex Mahali Pema Ameen!

Bingwa wa FDL kujulikana leo Chamazi

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/DSC_4165.jpg
Mwadui Shinyanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhX4CPi_gLzDiNDFJxODqQK-bun_Lz_-fqogmOSBafonpNyQztxKsciMrA9kx7T2CAkfa14juJT5WVK1BxZPxkqTuD40uPWHMTtpatpKUHMvQpdWau2Aw3yYJfbYrgwYFAnwHWaIEFpT7c/s1600/sports.JPG
Africans Sports 'Wana Kimanumanu'
FAINALI za kusaka Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL), zinafanyika leo kwa pambano kati ya Mwadui Shinyanga dhidi ya Africans Sports mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi kuanzia majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
Awali mchezo huo wa fainali ulikuwa umepangwa kufanyika kwenye dimba la Uwanja wa Taifa, lakini kutokana na sababu zilizopo nje ya uwezo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF imepelekea mchezo huo kuhamishiwa Chamazi.
Mchezo huo wa fainali utaanza saa 10 kamili jioni, na utaonyeshwa moja kwa moja na kituo cha Azam TV ili kuwapa nafasi wapenzi na wadau wa soka waliopo mbali na hasa mikoani kuweza kushuhudia mchezo huo.
Bingwa wa Fainali ya Ligi Daraja la Kwanza atazawadiwa Kombe pamoja na medali, huku mshindi wa pili akipata kikombe na medali pia.
Viingilio vya mchezo huo ni tsh.5,000 kwa jukwaa kuu na tsh. 3,000 kwa majukwaa ya mzunguko.

Mo Farah aweka rekodi ya dunia

http://e0.365dm.com/15/02/660x350/mo-farah-birmingham-indoor-two-mile-record_3267495.jpg?20150221163812
Mwanariadha Mo Farah akimaliza mbio na kuweka rekodi mpya Birmingham
LONDON, England
MWANARIADHA Muingereza Mo Farah amevunja rekodi ya dunia ya mbio za ndani za Maili Mbili katika mbio za Birmingham Indoor Grand Prix.
Farah, 31, aliondoka uwanjani baada ya kumaliza mbio hizo kwa kutumia dakika 3.40 akiivunja rekodi iliyotanguliwa iliyowekwa na Muethiopia Kenenisa Bekele.
Hiyo ni rekodi ya kwanza kuwekwa na mwanariadha huyo bingwa mara mbili wa Olimpiki.
"Hii ina maana kubwa kwangu, " alisema Farah. "Napenda kuliwakilisha taifa langu, kutoa kitu fulani kwa watu wote. Siamini. "
Maandalizi ya kabla ya kuanza kwa mbio hizo za Jumamosi yalitawaliwa na malumbano dhidi ya mchezaji mwenzake Muingereza Andy Vernon.
Farah alidai kuwa Vernon alihoji uraia wake baada ya bingwa huyo mara mbili wa Olimpiki kushinda mbio za Ulaya za mita 10,000 mwaka 2014, huku Vernon akielezea kuwa huo ulikuwa ni upotoshaji mkubwa.
Pamoja na suala hilo lakini Farah hakutetereka kwani alitawala mbio hizo zilizofanyika jijini Birmingham, na kuwaacha Mkenya Paul Koech na Mmarekani Bernard Lagat na kushinda mbio hizo.
"Ni (malumbano na Vernon) ndio yaliyonihamasisha mimi, nilitaka kufanya hivyo, " alisema Farah.

Simba, Yanga Azam katika vita nyingine VPL

Kikosi cha Simba kitakachokuwa mjini Shinyanga,

Azam watakuwa uwanja wa nyumbani wa Chamazi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhErXyx1Zkj3OCoFFiXSN67k52f3gi-xri1jU6EVAQNSzUHaLOE-aGYio6UwnJav0_qsoTFjW-lII6MoCyTEDN6NO6aDEosezFiW3YLR8VtXdxto3puBagAfzT7oBKaY4iLz98CetK57ihU/s1600/IMG_0916.JPG
Kikosi cha Yanga kilichopo ugenini jijini Mbeya kuvaana na Mbeya City
VIGOGO vya Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba, Yanga na Azam zitakuwa kwenye viwanja tofauti kwa ajili ya kusaka pointi tatu muhimu katika mbio za kuwania ubingwa wa ligi hiyo.
Vinara Yanga wenyewe watakuwa kwenye uwanja wa Sokoine kwa mara nyingine tena kupepetana na wenyeji wao Mbeya City, ikiwa ni siku chache baada ya kugawa dozi ya mabao 3-0 dhidi ya Prisons.
Simba walioanza kushika kasi katika ligi hiyo baada ya kuchechemea kwa muda mrefu, pia ipo ugenini mkoani Shinyanga kwa ajili ya kupepetana na Stand United  kwenye uwanja wa Kambarage.
Mabingwa watetezi Azam watakuwa uwanja wa nyumbani wa Azam Complex, Chamazi kuikaribisha Prisons-Mbeya baada ya katikati ya wiki kubanwa mbavu na Ruvu Shooting na kutoka suluhu ya 0-0.
Yanga watakuwa na hamu ya kuendeleza rekodi yao ya kushinda mfululizo, ingawa Mbeya City ambayo imekuwa haina msimu mzuri safari hii ikiwa imeapa kumaliza uteja kwa wapinzani wao hao.
Mbeya City iliyopanda ligi kuu msimu uliopita, haijawahi kuifunga Yanga zaidi ya kulazimisha sare au kuambulia vipigo, kitu ambacho Kocha wake, Juma Mwambusi anaamini leo watavunja mwiko.
Hata hivyo Yanga imetamba kutaka kutoa dozi kwa lengo la kuongeza morali kabla ya kuondoka nchini kwenda Botswana kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya BDF XI.
Yanga inayoongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 28, mbili zaidi ya Azam yenye 26 itarudiana na BDF wiki ijayo mjini Gaborone baada ya wiki iliyopita kuwacharaza mabao 2-0.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro alisema hawaoni cha kuwazuia kuvuna pointi nyingine tatu jijini Mbeya wakati kikosi chao kimeandaliwa vema na kina morali mkubwa.
Muro alisema anafahamu Mbeya City ni timu ngumu na itataka kutumia vema uwanja wa nyumbani, lakini Yanga imejipanga kutoka na pointi zote ili kujikita zaidi kileleni kabla ya kwenda Botswana.
Wakati Yanga na Mbeya wakiwindana hivyo, Simba wenyewe wakiwa na furaha ya ushindi wa mabao 2-0 iliyopata ugenini mjini Morogoro dhidi ya Polisi wataivaa Stand United wakiwa na tahadhari kubwa.
Stand Utd imetoka kuwatoa nishai Mgambo JKT kwa kuicharaza mabao 4-1, kitu ambacho kinaonyesha namna gani wameanza kuizoea ligi hiyo wanayoicheza kwa msimu wao wa kwanza.
Katika pambano hilo kila timu itakuwa ikitegemea nyota wake, Simba ikitambia akina Emmanuel Okwi, Dan Sserunkuma, Eliasi Maguri na wengine huku Stand ikimtegemea Mnigeria Abasalim Chiibibele na Heri Mohammed wenye mabao manne kila mmoja katika ligi hiyo.
Katika mchezo wa kwanza uliochezwa Oktoba 4, mwaka jana timu hizo zilizoshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye uwanja wa Taifa.
Angalia msimamo wa Ligi Kuu ulivyo:

                                P   W    D    L    F    A   GD Pts
01. Yanga               14  08   04  02  18  07  11  28
02. Azam                14  07   05  02  22  12  10  26
03. Kagera Sugar    16  06   06  04  13  11  02  24
04. Simba               14  04   08  02  15  11  04  20
05. Ruvu Shooting  15  05   05  05  10  11  -1   20
06. Mtibwa Sugar    15  04   07  04  15  15  00  19
07. Coastal Union   16   04  07   05  11  11  00  19
08. Polisi Moro        16  04   07   05  12  14  -2  19
09. JKT Ruvu          15  05  04  06   14   15  -1  19
10. Ndanda Fc        16  05  04   07  14   18  -4  19
11. Mbeya City       14  04  05  05   09   11  -2   17
12. Mgambo JKT    14  05  02  07   08    15  -7  17
13.Stand Utd         15  03  06   06   13   18  -5  15
14. Prisons            14  01  08   05   10   15  -5   11
Wafungaji:
8-
Didier Kavumbagu(Azam)

7- Rashid Mandawa (Kagera Sugar)
6-
Samuel Kamuntu (JKT Ruvu), Ame Ali (Mtibwa), Simon Msuva (Yanga),
5-
Danny Mrwanda (Yanga), Kipre Tchetche (Azam)
4- Rama Salim (Coastal),  Emmanuel Okwi (Simba), Nassor Kapama, Jacob Massawe (Ndanda), Heri Mohammed, Abasalim Chiibibele (Stand Utd) , Malimi Busungu (Mgambo)
3- Ally Shomari (Mtibwa), Frank Domayo (Azam), Atupele Green (Kagera)
2-
Shaaban Kisiga, Dan Sserunkuma, Elias Maguli (Simba), Salum Kanoni, (Kagera Sugar) Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete, Mrisho Ngassa, Andrey Coutinho (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Mussa Said (Stand Utd), Ally Nassor (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi),Yahya Tumbo (Ruvu Shooting)

Chungulia video mpya ya Vanessa Mdee ft Barnaba-SIRI