STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 22, 2015

Bingwa wa FDL kujulikana leo Chamazi

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/DSC_4165.jpg
Mwadui Shinyanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhX4CPi_gLzDiNDFJxODqQK-bun_Lz_-fqogmOSBafonpNyQztxKsciMrA9kx7T2CAkfa14juJT5WVK1BxZPxkqTuD40uPWHMTtpatpKUHMvQpdWau2Aw3yYJfbYrgwYFAnwHWaIEFpT7c/s1600/sports.JPG
Africans Sports 'Wana Kimanumanu'
FAINALI za kusaka Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL), zinafanyika leo kwa pambano kati ya Mwadui Shinyanga dhidi ya Africans Sports mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi kuanzia majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
Awali mchezo huo wa fainali ulikuwa umepangwa kufanyika kwenye dimba la Uwanja wa Taifa, lakini kutokana na sababu zilizopo nje ya uwezo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF imepelekea mchezo huo kuhamishiwa Chamazi.
Mchezo huo wa fainali utaanza saa 10 kamili jioni, na utaonyeshwa moja kwa moja na kituo cha Azam TV ili kuwapa nafasi wapenzi na wadau wa soka waliopo mbali na hasa mikoani kuweza kushuhudia mchezo huo.
Bingwa wa Fainali ya Ligi Daraja la Kwanza atazawadiwa Kombe pamoja na medali, huku mshindi wa pili akipata kikombe na medali pia.
Viingilio vya mchezo huo ni tsh.5,000 kwa jukwaa kuu na tsh. 3,000 kwa majukwaa ya mzunguko.

No comments:

Post a Comment