STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 22, 2015

Simba, Yanga Azam katika vita nyingine VPL

Kikosi cha Simba kitakachokuwa mjini Shinyanga,

Azam watakuwa uwanja wa nyumbani wa Chamazi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhErXyx1Zkj3OCoFFiXSN67k52f3gi-xri1jU6EVAQNSzUHaLOE-aGYio6UwnJav0_qsoTFjW-lII6MoCyTEDN6NO6aDEosezFiW3YLR8VtXdxto3puBagAfzT7oBKaY4iLz98CetK57ihU/s1600/IMG_0916.JPG
Kikosi cha Yanga kilichopo ugenini jijini Mbeya kuvaana na Mbeya City
VIGOGO vya Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba, Yanga na Azam zitakuwa kwenye viwanja tofauti kwa ajili ya kusaka pointi tatu muhimu katika mbio za kuwania ubingwa wa ligi hiyo.
Vinara Yanga wenyewe watakuwa kwenye uwanja wa Sokoine kwa mara nyingine tena kupepetana na wenyeji wao Mbeya City, ikiwa ni siku chache baada ya kugawa dozi ya mabao 3-0 dhidi ya Prisons.
Simba walioanza kushika kasi katika ligi hiyo baada ya kuchechemea kwa muda mrefu, pia ipo ugenini mkoani Shinyanga kwa ajili ya kupepetana na Stand United  kwenye uwanja wa Kambarage.
Mabingwa watetezi Azam watakuwa uwanja wa nyumbani wa Azam Complex, Chamazi kuikaribisha Prisons-Mbeya baada ya katikati ya wiki kubanwa mbavu na Ruvu Shooting na kutoka suluhu ya 0-0.
Yanga watakuwa na hamu ya kuendeleza rekodi yao ya kushinda mfululizo, ingawa Mbeya City ambayo imekuwa haina msimu mzuri safari hii ikiwa imeapa kumaliza uteja kwa wapinzani wao hao.
Mbeya City iliyopanda ligi kuu msimu uliopita, haijawahi kuifunga Yanga zaidi ya kulazimisha sare au kuambulia vipigo, kitu ambacho Kocha wake, Juma Mwambusi anaamini leo watavunja mwiko.
Hata hivyo Yanga imetamba kutaka kutoa dozi kwa lengo la kuongeza morali kabla ya kuondoka nchini kwenda Botswana kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya BDF XI.
Yanga inayoongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 28, mbili zaidi ya Azam yenye 26 itarudiana na BDF wiki ijayo mjini Gaborone baada ya wiki iliyopita kuwacharaza mabao 2-0.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro alisema hawaoni cha kuwazuia kuvuna pointi nyingine tatu jijini Mbeya wakati kikosi chao kimeandaliwa vema na kina morali mkubwa.
Muro alisema anafahamu Mbeya City ni timu ngumu na itataka kutumia vema uwanja wa nyumbani, lakini Yanga imejipanga kutoka na pointi zote ili kujikita zaidi kileleni kabla ya kwenda Botswana.
Wakati Yanga na Mbeya wakiwindana hivyo, Simba wenyewe wakiwa na furaha ya ushindi wa mabao 2-0 iliyopata ugenini mjini Morogoro dhidi ya Polisi wataivaa Stand United wakiwa na tahadhari kubwa.
Stand Utd imetoka kuwatoa nishai Mgambo JKT kwa kuicharaza mabao 4-1, kitu ambacho kinaonyesha namna gani wameanza kuizoea ligi hiyo wanayoicheza kwa msimu wao wa kwanza.
Katika pambano hilo kila timu itakuwa ikitegemea nyota wake, Simba ikitambia akina Emmanuel Okwi, Dan Sserunkuma, Eliasi Maguri na wengine huku Stand ikimtegemea Mnigeria Abasalim Chiibibele na Heri Mohammed wenye mabao manne kila mmoja katika ligi hiyo.
Katika mchezo wa kwanza uliochezwa Oktoba 4, mwaka jana timu hizo zilizoshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye uwanja wa Taifa.
Angalia msimamo wa Ligi Kuu ulivyo:

                                P   W    D    L    F    A   GD Pts
01. Yanga               14  08   04  02  18  07  11  28
02. Azam                14  07   05  02  22  12  10  26
03. Kagera Sugar    16  06   06  04  13  11  02  24
04. Simba               14  04   08  02  15  11  04  20
05. Ruvu Shooting  15  05   05  05  10  11  -1   20
06. Mtibwa Sugar    15  04   07  04  15  15  00  19
07. Coastal Union   16   04  07   05  11  11  00  19
08. Polisi Moro        16  04   07   05  12  14  -2  19
09. JKT Ruvu          15  05  04  06   14   15  -1  19
10. Ndanda Fc        16  05  04   07  14   18  -4  19
11. Mbeya City       14  04  05  05   09   11  -2   17
12. Mgambo JKT    14  05  02  07   08    15  -7  17
13.Stand Utd         15  03  06   06   13   18  -5  15
14. Prisons            14  01  08   05   10   15  -5   11
Wafungaji:
8-
Didier Kavumbagu(Azam)

7- Rashid Mandawa (Kagera Sugar)
6-
Samuel Kamuntu (JKT Ruvu), Ame Ali (Mtibwa), Simon Msuva (Yanga),
5-
Danny Mrwanda (Yanga), Kipre Tchetche (Azam)
4- Rama Salim (Coastal),  Emmanuel Okwi (Simba), Nassor Kapama, Jacob Massawe (Ndanda), Heri Mohammed, Abasalim Chiibibele (Stand Utd) , Malimi Busungu (Mgambo)
3- Ally Shomari (Mtibwa), Frank Domayo (Azam), Atupele Green (Kagera)
2-
Shaaban Kisiga, Dan Sserunkuma, Elias Maguli (Simba), Salum Kanoni, (Kagera Sugar) Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete, Mrisho Ngassa, Andrey Coutinho (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Mussa Said (Stand Utd), Ally Nassor (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi),Yahya Tumbo (Ruvu Shooting)

No comments:

Post a Comment