STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 22, 2015

Mwadui Fc ndiyo mabingwa wa FDL2014-2015

Kocha wa Mwadui, Jamhuri Kihwelu 'Julio
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/DSC_4165.jpg
Mabingwa wa FDL,. Mwadui Shinyanga walioizabua Wana Kimanumanu kwa bao 1-0
'KOCHA Jamhuri Kihwelu 'Julio'amedhihirisha kweli yeye ni bab'Kubwa baada ya kuiongoza timu yake ya Mwadui Shinyanga kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Africans Sports ya Tanga na kunyakua ubingwa wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL).
Mwadui imeibuka na ushindi huo katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi na kuzima ngebe za wapinzani wao waliotamba awali kushinda pambano hilo kudhihirisha kuwa Mwadui ni 'vibabu'.
Hata hivyo tambo hizo za Wana Kimanumanu zilizimwa kwa bao tamu la kichwa lililofungwa na Kelvin Sabato 'Kiduku' na kuwapa taji Mwadui ambao waliongoza katika kundi lao la ligi daraja la kwanza na kupanda Ligi Kuu msimu wa 2015-2016 mwaka mmoja baada ya kubaniwa na TFF msimu uliopita.
Mbali na Mwadui, nyingine zilizopanda ligi hiyo msimu ujao kuchukua nafasi ya timu nne zitgakazoshuka katika Ligi ya msimu huu inayozidi kushika kasi ni Africans Sports, Toto Africans na Majimaji-Songea.

No comments:

Post a Comment