STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 22, 2015

Mo Farah aweka rekodi ya dunia

http://e0.365dm.com/15/02/660x350/mo-farah-birmingham-indoor-two-mile-record_3267495.jpg?20150221163812
Mwanariadha Mo Farah akimaliza mbio na kuweka rekodi mpya Birmingham
LONDON, England
MWANARIADHA Muingereza Mo Farah amevunja rekodi ya dunia ya mbio za ndani za Maili Mbili katika mbio za Birmingham Indoor Grand Prix.
Farah, 31, aliondoka uwanjani baada ya kumaliza mbio hizo kwa kutumia dakika 3.40 akiivunja rekodi iliyotanguliwa iliyowekwa na Muethiopia Kenenisa Bekele.
Hiyo ni rekodi ya kwanza kuwekwa na mwanariadha huyo bingwa mara mbili wa Olimpiki.
"Hii ina maana kubwa kwangu, " alisema Farah. "Napenda kuliwakilisha taifa langu, kutoa kitu fulani kwa watu wote. Siamini. "
Maandalizi ya kabla ya kuanza kwa mbio hizo za Jumamosi yalitawaliwa na malumbano dhidi ya mchezaji mwenzake Muingereza Andy Vernon.
Farah alidai kuwa Vernon alihoji uraia wake baada ya bingwa huyo mara mbili wa Olimpiki kushinda mbio za Ulaya za mita 10,000 mwaka 2014, huku Vernon akielezea kuwa huo ulikuwa ni upotoshaji mkubwa.
Pamoja na suala hilo lakini Farah hakutetereka kwani alitawala mbio hizo zilizofanyika jijini Birmingham, na kuwaacha Mkenya Paul Koech na Mmarekani Bernard Lagat na kushinda mbio hizo.
"Ni (malumbano na Vernon) ndio yaliyonihamasisha mimi, nilitaka kufanya hivyo, " alisema Farah.

No comments:

Post a Comment