STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 31, 2013

Liverpool yazinduka EPL, yaifumua Aston Villa kwao

http://cache.images.globalsportsmedia.com/news/soccer/2013/3/31/315082header.jpg
Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard akishangilia bao la jioni ya leo

MABINGWA wa zamani waUlaya, Liverpool jioni ya leo imezinduka tena kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kupata ushindi wa mabo 2-1 ugenini mbele ya wenyeji wao Aston Villa.
Mkwaju wa penati iliyopigwa na nahodha Steven Gerrard katika dakika ya 60 ndiyo iliyoihakikisha Liverpool ushindi wa pointi tatu muhimu baada ya kwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa bao 1-0 lililotupiwa kambani na Mbelgium mwenye asili ya DR Congo, Christian Benteke.
Benteke alifunga bao hilo katika dakika ya 31, akimaliza kazi nzuri ya Gabriel Agbonlahor.
Wageni waliingia kipindi cha pili kwa kasi na iliwachukua dakika mbili tu kusawazisha bao kupitia Jordan Henderson na dnipo kwenye dakika ya 60 Gerrard akatupia mpira wavuni kwa penati  baada ya Luis Suarez kuangushwa langoni mwa Aston Villa alipokuwa akienda kumsalia kipa wa Brad Guzan.
Hata hivyo ushindi huo wa leo umeiacha Liverpool katika nafasi ya saba, ikiwa imecheza mechi 31, ikiwa nyuma ya wapinzani wao, Everton walioishinda jana bao 1-0 dhidi ya  Stoke City.

Maiti sasa zafikia 29 ajali ya jengo lililoporomoka Dar

Zoezi la kusaka miili zaidi ya watu likiendelea kufanywa kwa umakini mkubwa
Mojawapo ya magari kibao yaliangukiwa pia na jengo hilo
Wengine walikuwa ndani ya magari yao wakati mjengo ukiporomoka na kuwafunika
Jengo pacha... ujenzi wa jengo hili lililopakana na jingine lililoanguka umesitishwa kwa muda na serikali ili kupisha uchunguzi kwani mwenye jengo hili ndiye mmiliki wa lile lililoanguka na pia kampuni ya ujenzi ni ileile, mkandarasi ni yuleyule na mahala penyewe ni hapa hapa, kwenye makutani ya barabara ya Morogoro na Indira Gandhi.   

Jengo pacha la ghorofa 16... ujenzi wa ghorofa hili umesimamishwa kupisha uchunguzi. Mmiliki wa jengo hili ndiye mmiliki wa lile lililoanguka, kampuni ya ujenzi ni ileile, mkandarasi ni yuleyule na mahala penyewe ni hapa hapa kwenye makutani ya barabara ya Morogoro na Indira Gandhi.  
Idadi ya miili ya watu walionasuliwa kutoka katika kifusi cha jengo la ghorofa 16 lililoporomoka juzi wakati likiendelea kujengwa kwenye makutano ya Morogoro Road na Indira Gandhi sasa imefikia 29, imefahamika.  

"Hadi sasa tumeshapata miili ya watu 29 kutoka kwenye kifusi cha mabaki ya jengo lililoanguka," Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick amesema leo Machi 31, 2013.

Ameongeza kuwa waokoaji sasa wanaendelea kusaka miili zaidi katika lililokuwa jengo la chini ambako kulikuwa na ghala la vifaa na inadhaniwa kuwa huko ndiko kulikokuwa na watu wengi zaidi; na kwamba zoezi la kusaka miili litaendelea mpaka wahanga wote wapatikane.

Rais Jakaya Kikwete, ambaye alitembelea eneo la tukio juzi katika siku ya Ijumaa Kuu, ameagiza kwamba wahusika wote waliosababisha maafa hayo wafikishwe mbele ya mkono wa sheria na hadi sasa, polisi wamesema kuwa tayari wameshawatia mbaroni watuhumiwa wanne.

GOLDEN BUSH VETERANI YAIZAMISHA WAHENGA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEigEXcYZjHBYFe7oOEgW5OFabOhx7fWDF32Rsh1DNIyJgIuc8Evl-_yJ_6-t3SWerT20D7radHa4TQSZKy32dCj_g7jev9QWI1KeveOocs9OaXA0c4U8BREl7bBYDCuQ4pz95KuTxPJFBI/s1600/Golden+Bush+Veterani.JPG
Kikosi cha Golden Bush Veterani
 
WAKALI wa soka la maveterani jijini Golden Bush Veterani jioni ya leo imeisherehekea vyema sikukuu ya Pasaka baada ya kuwafumua wapinzani wao wakuu, Wahenga Fc kwa kuwalaza mabao 2-1 katika pambano maalum lililochezwa kwenye uwanja wa Kinesi, Ubungo Dar es Salaam.
Mchezo huo uliochezwa huku mvua kubwa ikinyesha na kuhudhuriwa na Kamanda wa Polisi, Thobias Andengenye ulishuhudiwa Wahenga wakitangulia kupata baop la kuongoza lililotumbukizwa wavuni na Albert Shao.
Hata hivyo Golden Bush iliyokuwa ikiongozwa na nahodha wake, Onesmo Wazir 'Ticotico' ilisawazisha bao hilo kupitia kwa nyota wa pambano hilo, Sadick Muhimbo na kufanya hadi mapumziko timu hizo ziwe nguvu sawa.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko ya wachezaji ambapo iliongeza uhai wa pambano hilo ambalo pande zote zilionyesha kulikamia na kuhiotaji ushindi ili kulinda heshima mbele ya mwenzake, japo utelezi na maji yaliyosababishwa na mvua iliyokuwa ikinyesha ilipunguza utamu wa soka la timu hizo.
Golden Bush ilifanikiwa kuandika bao la pili la la ushindi kupitia kwa 'Super Sub' wao De Natale alifumua shuti kali baada ya mabeki wa Wahenga kuzembea kuokoa mpira langoni mwake.
Mpaka filimbi ya mwisho ya mwamuzi wa pambano hilo, Ally Mayay ilipolia kuashiria pambano hilo limemalizika Wahenga walijikuta hoi kwa wapinzani wao kwa kula kichapo cha mabao 2-1.