STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 31, 2013

Liverpool yazinduka EPL, yaifumua Aston Villa kwao

http://cache.images.globalsportsmedia.com/news/soccer/2013/3/31/315082header.jpg
Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard akishangilia bao la jioni ya leo

MABINGWA wa zamani waUlaya, Liverpool jioni ya leo imezinduka tena kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kupata ushindi wa mabo 2-1 ugenini mbele ya wenyeji wao Aston Villa.
Mkwaju wa penati iliyopigwa na nahodha Steven Gerrard katika dakika ya 60 ndiyo iliyoihakikisha Liverpool ushindi wa pointi tatu muhimu baada ya kwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa bao 1-0 lililotupiwa kambani na Mbelgium mwenye asili ya DR Congo, Christian Benteke.
Benteke alifunga bao hilo katika dakika ya 31, akimaliza kazi nzuri ya Gabriel Agbonlahor.
Wageni waliingia kipindi cha pili kwa kasi na iliwachukua dakika mbili tu kusawazisha bao kupitia Jordan Henderson na dnipo kwenye dakika ya 60 Gerrard akatupia mpira wavuni kwa penati  baada ya Luis Suarez kuangushwa langoni mwa Aston Villa alipokuwa akienda kumsalia kipa wa Brad Guzan.
Hata hivyo ushindi huo wa leo umeiacha Liverpool katika nafasi ya saba, ikiwa imecheza mechi 31, ikiwa nyuma ya wapinzani wao, Everton walioishinda jana bao 1-0 dhidi ya  Stoke City.

No comments:

Post a Comment