STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 28, 2011

Nyawela atuma salamu kwa wapinzani wa Extra



DANSA maarufu nchini ambaye kwa sasa ni kiongozi wa safau ya unenguaji wa bendi ya Extra Bongo, Hassan Mohammed 'Super Nyamwela', amewataka wapinzani wake kukaa chonjo na ujio wake mpya akiwa na bendi hiyo.
Nyamwela, aliyetokea African Stars 'Twanga Pepeta' amesema muda wa mwezi mmoja waliokuwa kambini amefanya mambo makubwa ambayo anaamini yatawasambaratisha wapinzani wao mara watakapotoka mafichoni.
Akizungumza mara baada ya bendi hiyo kutambulisha 'shoo' pamoja na moja ya vibao vyao vipya kwa waandishi wa habari jana, kwenye kambi yao iliyopo Mbezi-Louis jijini Dar es Salaam, Nyamwela alisema wapo kamili kwa vita.
Nyamwela alisema muda mmoja wa mwezi waliokaa kambini wameweza kuandaa shoo mpya ambazo hazijawahi kuonwa kokote.
"Kama ulivyoo, hiyo ni sehemu tu ya kazi ambazo tumekuwa tukizifanya tangu tuingie kambini na ambazo zitaanza kuonekana hadharani Ijumaa tutakapotoka mafichoni na kufanya shoo za mwishoni mwa wiki," alisema.
Alisema kikosi chao kinachoundwa na wanenguaji tisa akiwemo yeye Super Nyamwela, Super Danger, Master B na King Lion ambao ni wanaume, huku wa kike ni Angela Alloyce, Otilia Boniface, Husna Ramadhani, Lavia Edward na Jamila Nassor.
Naye rapa mpya wa bendi hiyo, Saulo John 'Ferguson' amewataka mashabiki wa muziki wa dansi kusubiri kupata vitu vipya toka kwake kuliko vile walivyokuwa wamezoea kuvipata alipokuwa Twanga Pepeta.
"Nina rapu kibao, lakini sitaki kumaliza uhondo, Ijumaa tunaanza kutoka kwa kufanya onyesho pale New Msasani Club, watu waje wamuone Ferguson mpya," alisema rapa huyo mmoja wa waimbaji wapya wa Extra Bongo.

Mwisho

EXTRA BONGO KUTOKA MAFICHONI




BENDI ya Extra Bongo iliyokuwa kambini kwa muda wa mwezi mmoja, inatarajiwa kutoka mafichoni Ijumaa wiki hii tayari kufanya maonyesho matatu ya kuzitambulisha nyimbo zao mpya pamoja na kuwaanika hadharani wanamuziki walya iliyowanyakua wakiingia kambini.
Hata hivyo kambi hiyo iliyokuwa eneo la Time Square Resort, Mbezi Louis, jijini Dar es Salaam, itavunjwa rasmi Jumatatu kabla ya kupata boti kwenda visiwani Zanzibar kutumbuiza.
Akizungumza kwenye utambulisho wa nyimbo na staili yao ya uchezaji kwa waandishi wa habari jana, Mkurugenzi wa bendi hiyo, Ally Choki 'Kamarade' aliiambia Micharazo kuwa, bendi yao iliyokuwa kambini kwa muda wa mwezi mmoja itatoka mafichoni Ijumaa kwa ajili ya kufanya maonyesho matatu mwishoni mwa wiki kabla ya kwenda Zanzibar Machi 12.
Choki, alisema siku watakayotoka mafichoni, Extra Bongo itafanya onyesho kwenye ukumbi wa New Msasani Club, na siku itakayofuata itakuwa TCC Changombe na kumalizia burudani zao za utambulisho wa nyimbo, wanamuziki na unenguaji wao mpya pale Mango Garden, Kinondoni.
"Tunatarajia kutoka hadharani Ijumaa, ambapo tutafanya maonyesho matatu siku ya Ijumaa, Jumamosi na Jumapili kwa kutambulisha nyimbo mpya na unenguaji tuliokuwa tunapika tukiwa kambini, ila kambi tutaivunja rasmi Jumatatu," alisema Choki.
Choki alisema baadhi ya nyimbo zilizokuwa zikipikwa wakiwa kambini ambazo zitatambulishwa rasmi kwa mashabiki ni Mtenda Akitendwa, Neema, Fisadi wa Mapenzi na nyinginezo.
"Hizo ni baadhi ya nyimbo tulizokuwa tukiziandaa, na tutazitoa sambamba na kuwatambulisha wanamuziki wetu wapya na aina ya uenguaji chini ya uongozi wa Super Nyamwela," alisema.
Choki alisema kuwepo kwao kambini kumeijenga vema bendi yao na watatoka hadharani kwa nia ya kuleta changamoto na mabadiliko katika muziki wa Tanzania.
"Tumekuja kuleta mabadiliko na wapenzi watarajie mambo makubwa toka kwetu kwani kikosi cha wanamuziki 23 tuliopo ni jeshi la maangamizi, kizuri ni kwamba tunatambulisha nyimbo mpya na video ya Mtenda Akitendwa,ambayo tumepiga tukiwa kambini," alisema Choki.
Naye mmoja wa marapa wa bendi hiyo, Ramadhani Mhoza 'Pentagone' alisema kambi imewaivisha na kwamba mashabiki wa muziki watarajie mambo makubwa toka kwao.
"Aisee asikuambie mtu tumeiva vya kutosha tukiwa tayari kwa kazi, ebu piga picha hapa Pentagon, kule Ferguson, Shikito, Bob Kissa, Hegga, Choki, Nyamwela na wengine unadhani atapona mtu kweli hapa?" alisema Pentagoni.
Kiongozi wa wanenguaji, Super Nyamwela, alisema kile walichokuwa wakikipika kimeshaiva na wapenzi wa muziki wajiandae kupata burudani kabambe toka kwao wakiwa ni tofauti na Super Nyamwela aliyekuwa Twanga Pepeta.
Kikosi kamili cha Extra Bongo kilichokuwa kambini na kinacghotarajiwa kuanza kuwasha moto jijini kabla ya kwenda Zenji, kisha wakati wa Pasaka kukimbiza Kanda ya Ziwa ni pamoja na Ally Choki 'Kamarade', Ramadhani Mhoza 'Pentagone', Saulo John 'Ferguson', Rogart Hegga 'Catapillar', Bob KIssa' na Athanas Montanabe 'Shikito' ambao ni waimbaji.
Wapiga gitaa ni Ephraem Joshua 'Kanyaga Twende' na Mfaume Zablon 'Baba Watoto' (solo), Sara Kindeki (Rhythms) na Hoseah Mgohachi (Bass), huku wapiga Kinanda wakiwa ni Pablo Mwendambali na Sebastian Lundandikija.
Anayekung'ita ngoma mbili maarufu kama Tumba au Conga ni Salum Issa 'Cha Kuku', wakati mkaanga chips (Drums) ni Victor Machine, wakati wanenguaji mbali na Super Nyamwela, pia kuna Danger Boy, Master B, King Lion, Otilia Boniface, Husna ramadhani, Angela Alloyce, Lavia Edward na Jamila Nassor 'Queen Jamila'.

Saturday, February 26, 2011

MCHANGANYIKO WA HABARI

Kipigo chamchanganya kocha Toto


KIPIGO cha mabao 2-1 ilichopewa Toto Afrika na timu ya Mtibwa Sugar, kimemchanganya kocha wa timu hiyo ya Mwanza, Choke Abeid, aliyedai hakutegemea kama wangelala ila ameapa kupigana kufa na kupona kushinda mechi yao ijayo ya ugenini dhidi ya Kagera Sugar.
Toto ambayo kabla ya mechi hiyo iliidindia Simba na kisha kuilaza AFC Arusha, ilikumbana na kipigo hicho na kuiacha timu yao kwenye nafasi ya saba ikiwa na pointi 20, huku Choke akisema mipira ya faulo ya Mtibwa ndio iliyowamaliza.
Choke, mchezaji wa zamani wa Yanga, alisema Mtibwa walikuwa wazuri kwa mipira hiyo na kuwakwamisha kusogea nafasi waliopo, ingawa amesema wanajipanga vema kwa mechi ijayo ya Kagera itakayochezwa Machi 9.
"Kipigo kimetuchanganya, kwa vile tulijiamini tungeshinda, ila lazima nikiri mipira iliyokufa (faulo) ndio iliyotuumiza, ingawa tumekubali matokeo na kujipanga kwa mechi ijayo," alisema.
Choke, alisema licha ya mechi hiyo ijayo ni ngumu kutokana na Kagera kucheza nyumbani kwao, ila bado wanaamini wataenda kushinda ili kulipiza kisasi cha mabao 2-0 ilichopewa na wapinzani wao hao kwenye pambano lililochezwa jijini Mwanza, Oktoba 21, mwaka jana.
Kocha huyo alisema kuwepo kwa muda mrefu kabla ya pambano hilo, kutawapa fursa nzuri ya kurekebisha makosa yaliyowagharimu katika mchezo wao na Mtibwa Sugar ambao kwa ushindi huo imeweza kufikisha pointi 30 na kung'ang'ania nafasi yake ya nne waliopo.

***
Prisons yazifunda zilizopanda


TIMU ya Prisons ya Mbeya, imezitaka timu zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara kukomaa na kutokubali kushuka daraja kirahisi kwa sababu, huko chini ni kugumu mno.
Prisons imetahadharisha kuwa bora hata hiyo Ligi Kuu yenyewe kuliko ligi daraja la kwanza Tanzania Bara ambapo kila timu inakuwa inatafuta nafasi ya kupanda daraja.
Katibu wa timu hiyo Antony Hau amesema tangu timu yao ishuke daraja miaka miwili iliyopita imekuwa ikijitahidi kupanda bila mafanikio kutokana na ugumu uliokuwepo.
"Yaani naziambia timu zinazoshiriki Ligi Kuu zikomae zisishuke daraja huku ni hatari, kubaya, ni kugumu sana, huko juu unakutana na timu zilizogawanyika, zingine zinataka ubingwa, zingine kubaki daraja, huku kila mmoja anataka kupanda kwa hiyo ligi inakuwa ngumu sana, " alisema.
Pamoja na hayo, Hau amesema kuwa utaratibu wa kutafuta timu za kupanda Ligi Kuu wa kuweka kituo kimoja kama michuano fulani haufai.
"Maana ya ligi ni timu zizungukane, zicheze nyumbani na ugenini, sasa ligi ya kituo kimoja, si ligi kwa maana ya ligi ni michuano fulani tu au kombe," alisema.
Alishauri kuwa ligi daraja la kwanza iwe inachezwa nyumbani na ugenini kama Ligi Kuu ili timu ziwe na nafasi pana ya kucheza mechi nyingi na pia kuondoa uwezekano au hisia ya mwenyeji kubebwa na kupanda daraja.
Ligi daraja la kwanza Tanzania Bara imemalizika na tayari timu za Coastal Union, Villa Squad, JKT Oljoro, na Moro United zimefanikiwa kuingia Ligi Kuu.
***

Pondamali:Haya yataibeba Villa Ligi Kuu


BAADA ya kuirejesha Villa Squad katika Ligi Kuu Tanzania Bara, kocha wa timu hiyo, Juma Pondamali 'Mensah' ameupa uongozi wa klabu hiyo mambo manne ya kuyatekeleza iwapo wanataka Villa isishuke tena daraja.
Villa ambayo ilishuka daraja msimu wa 2008-2009, ilirejea tena kwenye ligi hiyo baada ya kushika nafasi ya tatu katika Ligi Daraja la Kwanza ikiungana na timu za JKT Oljoro, Coastal Union na Moro United.
Kutokana na kutambua ugumu wa Ligi Kuu ulivyo kocha, Pondamali alisema ni vema uongozi wa klabu ya Villa ukajipanga mapema kuhakikisha timu yao hairejei ilikotoka kwa kufanya mambo manne muhimu ambayo anaamini yakaibeba klabu hiyo.
Pondamali, kipa wa zamani wa kimataifa aliyewahi kung'ara na klabu za Pan Afrika, Yanga na AFc Leopard, alisema jambo la kwanza ambalo uongozi wa Villa unapaswa kutekeleza ni kuongeza wachezaji wapya 12 katika kikosi chao ili kukiimarisha.
"Kikosi kinahitaji wachezaji wapta 12 kwa ajili ya kukiimarisha, hivyo ni vema uongozi ukalitekeleza hilo, Ligi Kuu Tanzania Bara ni ngumu na ina ushindani hivyo inahitaji wachezaji mahiri na wenye uwezo wa kuibeba timu," alisema.
Aliongeza kuwa jingine ni viongozi kuzungukia na kuhudhuria kwenye michuano yote ya ya mchangani kwa nia ya kusaka wachezaji wapya, akidai mbinu hizo ndizo zilizoisaidia na kuipa sifa Ashanti United iliwahi kutamba kwenye ligi kuu msimu kadhaa iliyopita.
"Mambo hayo yakifanywa naamini Villa tutadumu kwenye ligi, vinginevyo hata mie sintoweza kuendelee kukaa na klabu hiyo, hilo naliweka wazi," alisema Pondamali ambaye pia ni kocha wa makipa wa timu ya taifa, Taifa Stars akisaidiana na Mdemark Jan Poulsen.
Pondamali alitoa mapendekezo hayo katika mahojiano na kituo cha Radio One, akizungumzia mafanikio ya timu yake kurejea ligi kuu na mikakati ya kuzuia isishuke tena kama awali.
***

Mao, ahofia ratiba ya Ligi Kuu


KIUNGO mahiri wa timu ya soka ya Azam, Himid Mao, amedai ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara bado inaonyesha hali ya upendeleo kwa baadhi ya timu kitu ambacho amesema sio haki.
Mao, mtoto wa kwanza wa nyota za zamani wa kimataifa nchini, Mao Mkami aliyewahi kung'ara na timu za Pamba na Simba, alisema ni vema TFF ikaangalia upta ratiba ya ligi hiyo.
Kiungo huyo aliyeteuliwa katika kikosi cha timu ya taifa ya vijana U23 kinachojiandaa kwenye Cameroon, alisema kwa ratiba iliyopo ni wazi ni vigumu kwa timu yao ya Azam kuendelea kukaa kileleni na kutwaa ubingwa.
"Ratiba ya sasa haitendi haki kwa baadhi ya timu, angalia Simba na Yanga zimecheza mechi chache, lakini bado wanapewa mapumziko marefu, hali ambayo haifanyi ligi iwe tamu, leo Azam tupo kileleni, lakini nafasi yetu sio ya kudumu kwa kuwa wenzetu wana mechi chache," alisema.
Alisema ni kweli vigogo hivyo vilikuwa vikiiwakilisha nchi kimataifa, ila kwa vile zilisharejea zingepaswa kucheza viporo vyao ili uwiano wa mechi uwe sawa na kuifanya ligi ichangamke zaidi.
Mao, alisema sio kama ana hofu ya timu yao kutwaa ubingwa, ila anaona kuwepo kwa tofauti na mechi kunaweza kutumiwa vibaya na timu zingine kuwavurugia mipango yao.
"Unajua kila mchezaji Azam akili yake kwa sasa ni kuona tunakuwa mabingwa, hivyo tunataka tufukuzane na wenzetu kama inavyotakiwa na sio kuachana kwa mechi katika ratiba kwani ni mbaya kwa upangaji wa matokeo," alisema.
Mkali huyo anayechekelea kuifungia timu yake kwa mara ya kwanza kwenye mechi za Ligi Kuu walipocheza na African Lyon na kuwalaza mabao 3-0, alisema anaamini pamoja na dosari ya ratiba bao Azam wataweka rekodi Tanzania Bara msimu huu.
Azam ambayo iliyokuwa ikiongoza kwenye msimamo wa ligi hiyo kabla ya mechi ya jana kati ya Simba na Mtibwa Sugar, ndio inayoongoza kwa kufunga mabao mengi hadi sasa ikiwa na mabao 32, yenyewe ikiruhusu mabao 11 tu.
***

Bakule ajiuengua TOT-Plus

MWANAMUZIKI Badi Bakule 'Jogoo la Mjini', amejivua uongozi wa bendi ya TOT-Plus 'Achinengule' ili kutoa nafasi kwa wengine kuongoza jahazi hilo.
Bakule, alimeiongoza TOT tangu mwaka 2005 alipowapokea Mwinjuma Muumin na Ally Choki waliowahi kuiongoza bendi hiyo kwa nyakati tofauti.
Akizungumza na Micharazo, Bakule alisema amelazimika kuachia ngazi kwa sababu chini ya uongozi wake haoni maendeleo yanayopigwa na bendi.
"Kila mwaka tumekuwa na mipango ya maendeleo isiyotekelezeka, hivyo bora niachie ngazi ili nipishe wenzangu kuongoza bendi," alisema.
Alisema amemuandikia 'bosi' wake, Kapteni Mstaafu John Komba kumjulisha rasmi dhamira yake na kwamba hatarajii kiongozi huyo kupinga uamuzi wake.
Alisema katika kipindi chote cha miaka mitano aliyokuwa kiongozi, hakuwahi kuamini kwamba Muumin na Choki waliondoka kwa sababu uongozi hautekelezi ahadi zake kwa vitendo, sasa ameamini.
"Naomba nieleweke kuwa sijaondoka TOT, nilichofanya ni kuachia ngazi nafasi ya uongozi baada ya kuona kwa muda wote huo bendi haipigia hatua za maendeleo na badala yake inazidi kuanguka," alisema Badi.
Alipoulizwa kuwa hatua hiyo inawezekana ni moja kati ya kuondoka kundini, Badi alisema kila jambo linawezekana na kwamba wakati wa kuamua vinginevyo ukifika anaweka wazi.
Micharazo ilipowasiliana na Komba kwa simu haikupokelewa ingawa taarifa zilizotufikia wakati tunakwenda mitamboni zinasema baada ya barua hiyo kumfikia mkurugenzi, alilazimika kuitisha kikao cha dharura na wanamuziki makao makuu ya bendi.
***
Extra Bongo kutoka mafichoni

BENDI ya Extra Bongo, iliyokuwa kambini karibu wiki tatu sasa, inatarajia kuvunja kambi hiyo na kuanza maonyesho yake kama kawaida.
Extra ilijichimbia kambini eneo la Mbezi Louis, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya maandalizi ya albamu yao mpya ya pili siku moja baada ya kuibomoa Africana Stars 'Twanga Pepeta' kwa kuwanyakua wanamuziki wake sita.
Ikiwa kambini, bendi hiyo pia imefanikiwa kurekodi video mbili za nyimbo zao za Neema na Under 18.
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa bendi hiyo, Ally Choki Extra Bongo inatarajia kuingia mitaani kuanzia Ijumaa wiki hii itakapofanya onyesho maalum la kuwatambulisha wanamuziki wapya iliowachukua toka Twanga Pepeta.
Choki alisema onyesho hilo litafanyika katika ukumbi wa New Msasani Club na kufuatiwa na lingine la Jumamosi litakalofanyika katika ukumbi wa TCC-Chang'ombe.
"Jumapili tutarudi rasmi katika ukumbi wetu wa nyumbani wa Mango Garden ili kuendelea kutoa burudani sambamba na kuwatambulisha wanamuziki wapya," alisema.
Wanamuziki hao wapya ni Super Nyamwela, Super Danger, Otilia Boniface (wanenguaji) Hoseah Mgohachi (besi), Saulo John 'Ferguson' na Rogert Hegga (waimbaji).
Aliongeza kuwa kwa sasa bendi hiyo imekuwa ikifanyia mazoezi nyimbo nyingine mpya za 'Fisadi wa Mapenzi' na Chuki ambazo ni miongoni mwa zile zitakazokuwa kwenye albamu hiyo ya pili, huku wakiwa wanatambia mtindo na rapu mpya kutoka kwa wakali hao wapya.

Simba, Mtibwa ni kisasi kitupu kesho





SIMBA na Mtibwa Sugar kesho zinakutana katika mechi yenye sura na mvuto wa pekee kwa aina yake ligi kuu bara, huku wekundu hao wa Msimbazi wakipania kuiporomosha kileleni mwa msimamo Azam FC na wapinzani wao wakipania kulipa kisasi cha kupoteza mechi ya kwanza.
Hata hivyo ushindi kwa Simba utawapeleka kileleni kwa muda tu, kwani watani wao wa jadi--Yanga wanaoshika nafasi ya pili wanaweza kuwashusha juu iwapo wataifunga Ruvu Shooting keshokutwa uwanja wa Uhuru.
Azam ina pointi 35 sawa na Yanga, lakini vijana wa Jangwani wako nyuma kwa tofauti ya mabao ya kufungwa na kufunga, na Simba inaweza kufikisha pointi 37 kama itashinda mchezo wa kesho.
Kwa upande wao Mtibwa wenye kumbukumbu nzuri ya kuwalaza Yanga, wamepania kuwazima vigogo Simba, na iwapo hilo litatimia watakuwa wamekaza mwendo wa kuelekea kileleni kwa kufikisha pointi 33.
Mtibwa imetangaza vita kwa Simba kutokana na kipigo cha bao 1-0 kwenye mechi ya kwanza iliyoghubikwa na mazingira ya tuhuma za rushwa kabla ya mechi kuchezwa.
Mtibwa itamkosa mlinda mlango wake namba moja, Shaaban Kato ambaye anatumikia adhabu ya kutocheza mechi kufuatia kuonyeshwa kadi nyekundu kwenye mechi dhidi ya Toto Afrika ya Mwanza.
Kocha msaidizi wa Mtibwa, Mecky Mexime na bosi wake Tom Olaba, kila mmoja kwa nyakati tofauti wamesema wamejiandaa kushinda mechi hiyo.
"Nia yetu si kulipa kisasi tu, tumepania kushinda mechi zote zilizosalia na kutwaa ubingwa," alisema Maxime.
Olaba alilalamikia kadi nyekundu ya Kado, lakini hata hivyo alisema kukosekana kwa mlinda mlango huyo si tatizo la kuwanyima ushindi.
"Kwetu sisi hakuna mechi rahisi, hivyo maandalizi tunayofanya ni kwa ajili ya mechi ngumu," alisema Mexime, nahodha wa zamani wa Mtibwa na Taifa Stars.
Simba wenyewe waliokutana jana kujadili mambo mbalimbali, wamesema wamepania ushindi kabla ya kwenda Zanzibar kuiwekea kambi Simba.
Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema wamejiandaa vizuri kwa mechi hiyo.
"Tukimaliza mechi, Jumatatu asubuhi tunakwenda Zanzibar kwa ajili ya kuweka kambi kabla ya mechi inayofuata," alisema Mtawala.
Mtawala alisema Simba itaenda Zenji na kikosi chake chote isipokuwa Uhuru Seleman ambaye bado anauguza goti, huku Emmanuel Okwi, Joseph Owino na Hillary Echessa wakirejea toka kwenye majeruhi.
Simba na Yanga zinatarajiwa kukutana kwenye mechi ya marudiano itakayochezwa Machi 5 kwenye dimba la Taifa, Simba ikiwa na deni la kipigo cha bao 1-0 iliyopewa na Yanga kwenye mechi ya awali iliyochezwa jijini Mwanza kwa bao tamu la Jerry Tegete.
Mwisho

Simba wazidi kuikamia Mazembe

BAADHI ya nyota wa klabu ya Simba, wametamba kuwa hawana hofu yoyote juu ya pambano lao dhidi ya TP Mazembe ya DR Congo kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Wachezaji hao wa Simba wamesema licha ya kutambua ugumu watakaopata kwa wapinzani wao ambao ni mabingwa watetezi, bado wana imani ya kurejea rekodi ya mwaka 2003 walipoing'oa waliokuwa mabingwa watetezi wa michuano hiyo, Zamalek ya Misri.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili katikati ya wiki iliyopita, wachezaji wa Simba walisema kama wawakilishi wa Tanzania wataendelea kupigana kiume kuona wanasonga mbele hata kama TP Mazembe wanatisha kwa sasa katika soka la kimataifa.
Beki wa kushoto wa Simba, Juma Jabu, alisema kama mabingwa wa Tanzania wataenda Congo kupigana kiume kuipeperusha bendera ya nchi kwa kushinda, ingawa wapo watu wanaoikatia tamaa.
Jabu, alisema hata mwaka 2003 Simba ilipuuzwa ilipopangwa na Zamalek, lakini walipigana kiume na kuing'oa mabingwa hao watetezi jambo linalowezekana kutokea msimu huu.
"Hakuna ubishi Mazembe ni wazuri na wanatisha Afrika na Dunia kwa ujumla, lakini kama wawakilishi hatutishwi nao, tutapigana kiume ili kusonga mbele, muhimu Watanzania watupe sapoti badala ya kutukatisha tamaa," alisema Jabu maarufu kama JJ.
Mchezaji mwingine aliyejinadi kutokuwa na hofu na Mazembe ni Rashid Gumbo, aliyekiri ni kweli Mazembe wanatisha, lakini bado wanaweza kufungika kama timu zingine muhimu mipango mizuri na kujituma kwao uwanjani.
"Tukijipanga na kucheza jihad uwanjani tunaweza kuweka maajabu, TP Mazembe ni timu kama timu zingine licha ya kuwa tishio, tutapigana kuhakikisha tunashinda," alisema Gumbo.
Kauli ya wachezaji hao zimekuja wakati wadau wengi wa soka wakiwemo wanaojiita wachambuzi wakiikatisha tamaa Simba kwa madai haiwezi kutoka kwa mabingwa hao watetezi katika mechi zao za raundi ya kwanza .
Simba ilipata fursa hiyo kwa kuing'oa Elan de Mitsodje ya Comoro kwa jumla ya mabao 4-2, ambapo katika mechi ya awali ilitoka suluhu ugenini kabla ya kushinda mechi ya marudiano iliyochezwa uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.

Mwisho

Friday, February 25, 2011

NYota wa Simba waikamia Mtibwa Sugar J'pili

BAADHI ya nyota wa timu ya Simba, wametamba kuwa wataisambaratisha Mtibwa Sugar watakaoumana nao siku ya Jumapili.
Mabingwa hao watetezi wataikaribisha Mtibwa kwenye uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam katika pambano la mfululizo wa michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
Katika mechi yao ya awali iliyochezwa mjini Morogoro na kughubikwa na kashfa ya rushwa, Simba iliisambaratisha Mtibwa kwa bao 1-0.
Pamoja na kutambua ugumu wa pambano hilo, ambalo Mtibwa wameshanadi kutaka kulipiza kisasi na kujiweka kwenye nafasi nzuri katika msimamo wa ligi hiyo, wachezaji wa Simba wamedai hawatishiki kwa kuamini watashinda.
Juma Jabu 'JJ' beki wa kushoto wa mabingwa hao watetezi, alisema anaamini mechi ya kesho itakuwa na matokeo mazuri kwao kutokana na kiu yao ya kutaka kutetea tena taji lao.
"Hatuna shaka Mtibwa tutawasambatarisha, ili tuweze kutimiza lengo letu la kutetea taji, hivyo wanasimba wasiwe na hofu," alisema Jabu.
Jabu, alisema wanataka kushinda mechi hiyo ili kujiweka vizuri kabla ya kuvaana na watani zao, Yanga Machi 5 kisha kwenda kuvaana na TP Mazembe kwenye mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Naye kiungo mshambuliaji, Rashid Gumbo alijinasibu hana hofu na mechi hiyo ya kesho wala ile ya watani zao, Yanga.
Gumbo, alisema hawawezi kurudia makosa waliyofanya kwenye pambano lao na Toto Afrika ambapo walilazimishwa sare ya 2-2 na hivyo kuitahadharisha Mtibwa ikae chonjo kwa kipigo.
"Wasitarajie mteremko, hatufanyi makosa kama ya Mwanza, tulipolazimishwa sare na Toto," alisema Gumbo mmoja wa wafungaji vinara wa klabu hiyo.
Kama Simba itaifunga Mtibwa ni wazi itarejea kileleni tena ikiiengua Azam, lakini itaombea pia watani zao watakaoshuka dimbani Jumatatu wafanye vibaya ili wasiporomoshwe kwenye msimamo kabla ya kukutana Machi 5.

Mwisho

Mwaisabula aungana na OLaba kumsikitia Kado

KOCHA wa zamani wa klabu ya Yanga, Kennedy Mwaisabula, ameungana na kocha wa Mtibwa Sugar, Tom Olaba kuilalamikia kadi nyekundu aliyopewa kipa Shaaban Kado, siku chache kabla ya kuvaana na timu ya Simba.
Kado, anayeichezea pia timu ya taifa, Taifa Stars, alionyeshwa kadi hiyo katika mechi baina ya timu yake na Toto Afrika na kumfanya alikose pambano la kesho dhidi yao na Simba litakalochezwa kwenye uwanja wa Uhuru, jijini Dar.
Mwaisabula maarufu kama 'Mzazi' alisema kitendo cha Kado kulikosa pambano la kesho limepunguza ladha kutokana na ukweli kipa huyo ndiye mhimili wa Mtibwa Sugar na hivyo kuipungizia nguvu timu yake.
Kocha huyo aliyewahi kuzinoa timu kadhaa ikiwemo Bandari-Mtwara, Cargo, Twiga Sports, Villa Squad na TMK United, alisema kwa jinsi mazingira ya kadi hiyo ilivyotolewa huko Mwanza anahisi kama kuna 'mchezo mchafu'.
Alisema japo hana hakika, lakini huenda kadi hiyo imetolewa kwa nia ya kuidhofisha Mtibwa katika mechi yao ya kesho, kitu alichodai mambo kama hayo yanachangia kuporomosha kiwango cha soka la Tanzania.
"Nadhani ifikie wakati mambo kama haya ya ujanja ujanja kwa nia ya kuzibeba timu kubwa zikaachwa ili soka lisonge mbele, nimesikitishwa na kadi ya Kado kwa vile imepunguza msisimko kwa pambano lao na Simba," alisema.
Kauli ya Mwaisabula imekuja siku chache, tangu kocha wa Mtibwa, Mkenya Tom Olaba kulalamikia kadi hiyo iliyotolewa na mwamuzi Judith Gamba, akidai imeinyong'onyesha timu yake kwa ajili ya pambano hilo dhidi ya Simba.
Kado alipewa kadi na mwamuzi huyo baada ya kuilalamikia penati iliyopewa wenyeji wao, Toto Afrika ambapo pambano lilishia kwa Mtibwa kushinda 2-1.

Mabondia kuzipiga kuwachangia wahanga wa mabomu


MABONDIA mbalimbali kutoka mikoa tofauti wanatarajiwa kupigana katika michuano maalum kwa nia ya kusaka fedha za kuwasaidia wahanga wa milipuko ya mabomu ya Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaam.
Michuano hiyo itakayochezwa sehemu nne tofauti ndani ya mikoa ya Dar, Pwani na Morogoro, imeratibiwa na kampuni ya Funiko Inc, chini ya uratibu wa mkurugenzi wake, Rowland Raphael Chulu 'Chen Lee Master'.
Chulu alisema michezo ya kwanza itafanyika kwenye ukumbi wa Hugho Tower Pub, Kigogo-Mburahati Machi 6, ambapo yeye atapigana na K kutoka Tanga pamoja na kusindikizwa na mapambano mengine ya utangulizi.
Aliwataja mabondia wengine watakaopigana siku hiyo ni Deus Tengwa atakayepigana na Kitonge wa Arusha, Abbas dhidi ya Abuu, Rahim Cobra na Abdul, Masoud Fighter dhidi ya Mrisho Mwana, Husseni Magali na Idd Rashid na Said Omary atapigana na Jembe wa Majembe.
"Pambano la pili litafanyika Machi 13 eneo la Bunju kwenye ukumbi wa Proud Tanzania, ambapo nitarudiana na K, na wiki inayofuata tutakuwa Bagamoyo kwenye ukumbi wa Police Mass ambapo nitachapana na Juma wa huko huko," alisema.
Alisema onyesho la tatu litachezwa kwenye ukumbi wa Makuti-Pub, Ifakara mkoani Morogoro kwa kuumana na Charles wa huko wakisindikizwa na michezo mingine ya utangulizi.
Chulu, aliyewahi kung'ara kwenye Kick Boxing kabla ya kutumbukia kwenye utayarishaji wa filamu nchini, alisema fedha zote zitakazopatikana kwenye maonyesho ya michezo hiyo zitapelekwa kwa wahanga.
Tangu tukio la milipuko ya mabomu litokee wiki mbili zilizopita watu mbalimbali wamekuwa wakitolea kuwasaidia wahanga, ambapo kesho kwenye uwanja wa Uhuru wasanii wa Bongofleva na wale wa filamu wataumana kusaka fedha za kuwasaoidia wahanga hao wa Gongo la Mboto.

Mwisho

Thursday, February 24, 2011

20% kuzindua Malumbano J'pili





MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abbas Hamis Kinzasa '20 Percent' anatarajia kuzindua na kuitambulisha rasmi albamu yake mpya iitwayo 'Ya Nini Malumbano' siku ya Jumapili.
Uzinduzi huo utakaosindikizwa na wasanii kadhaa nyota nchini unatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Club Masai, Oysterbay jijini Dar es Salaam chini ya utaribu wa kampuni ya King Kif Entertainment.
Akizungumza na Micharazo leo asubuhi, mkurugenzi wa kampuni hiyo, Sigfred Kimasa 'King Kiff', alisema maandalizi ya onyesho hilo yamekamilika ikiwemo wasanii nyota kibao kukubali kumsinidikiza mkali huyo ambaye anasifika kwa nyimbo zenye mafunzo na ujumbe mwanana.
"Msanii 20 Percent atazindua albamu yake ya Ya Nini Malumbano, akisindikizwa na wasanii kadhaa nyota, katika onyesho litakalofanyika Jumapili kwenye ukumbi wa Club Maisha," alisema.
Aliwataja wasanii watakaomsindikiza mkali huyo ambaye pia ni mahiri katika uigizaji filamu ni pamoja na 'swahiba' wake, Seleman Msindi 'Afande Sele'. Man Wter ambaye pia ni mtayarishaji wa albamu hiyo, Ney wa Mitego, Sajna, Linex na Uncle G.
Mbali na kibao cha Ya Nini Malumbano, albamu hiyo ya 20 Percent ina nyimbo nyingine kama Tamaa Mbaya ambao umekuwa ukitamba kwenye vituo kadhaa vya redio nchini, Neno la Mwisho na Nimerudi Salama.
Nyimbo nyingine ni Nyerere, Nia Yao, Mwema, Naficha, Kubadili Mwendo na Ya Nini Malumbano.
Hiyo ni albamu ya tatu ya msanii huyo ambaye anatamba pia na nyimbo za Money Money, Bangi na nyingine, awali alitoa albamu za Money Money na Mama Neema ambazo zinadaiwa kufanya vema sokoni licha ya nyimbo zake kumpa tuzo kadhaa za muziki nchini.

.

Tuesday, February 22, 2011

Dokii ana scandal na JB



MSANII nyota wa muziki na filamu, Ummy Wenceslaus 'Dokii' amefyatua kazi yake mpya iitwayo 'Scandal' iliyowashirikisha wakali kadhaa wa fani hiyo nchini.
Filamu hiyo inayozungumzia masuala ya mapenzi na hila za baadhi ya watumishi wa Mungu, inatarajiwa kuachiwa mitaani kuanzia mwezi ujao ikiwa imetungwa na Dokii mwenyewe na kuongozwa na Adam Kuambiana.
Akizungumza na micharazo, Dokii, aliyeng'ara na michezo ya kuigiza kupitia kituo cha ITV akiwa na kundi la Mambo Hayo, alisema ndani ya filamu hiyo aliyoitunga mwenyewe, kuna wasanii mahiri kama Jacob Stephen 'JB'.
"Baada ya kimya tangu nilipoachia filamu ya Money Transfer, nimekamilisha kazi mpya iitwayo Scandal' ambayo nimeigiza na wasanii kadhaa nyota akiwemo mkali, JB, Colleta Raymond, Tini White na wengine," alisema Dokii.
Dokii aliwataja wasanii wengine waliopo ndani ya filamu hiyo ni pamoja na Jacqueline Pentezel 'Jack wa Chuz', Ramadhani Ally 'Taff', Tini White, Kishoka na wengine.
"Ni filamu ya kusisimua kwa jinsi ilivyoigizwa na ujumbe uliopo ndani ya kazi hiyo mpya," alisema Dokii.
Dokii, ambaye pia ni muimbaji wa muziki wa Injili amewahi kutamba na filamu kama Yoland, Hard Love Moro, Bad Friend, My Nephew, Lonely Heart na nyinginezo.
Kwa muda mrefu msanii huyo alikuwa wakiwachanganya mashabiki wake wakidhani ni Mkenya kutokana na kupenda kwake kuigiza lafudhi ya taifa hilo, ingawa ukweli yeye ni mwenyeji wa mkoa wa Morogoro.

Mwisho

Msalaba Wangu upo kwa Teddy

MTUNZI anayekuja juu katika fani ya utunzi wa riwaya, Teddy Chacha, amejitosa kwenye filamu na kuibuka na kazi mpya iitwayo 'Msalaba Wangu'.
Filamu hiyo inayozungumzia masuala ya kijamii na hasa kuwepo kwa imani potofu juu ya watu wenye ulemavu, imeshirikisha 'vichwa' kadhaa nyota vya fani ya uigizaji nchini akiwemo Pembe, 'Bi Hindu' na Charles Magali 'Mzee Magali'.
Akizungumza na Micharazo, Teddy alisema filamu hiyo ni zao la moja ya hadithi zake zinazochapishwa kwenye magazeti mbalimbali likiwemo NIPASHE, ambapo inazungumzia familia moja inayomkataa mtoto wao aliyezaliwa mlemavu wa akili.
Teddy, alisema filamu hiyo ni kama simulizi la kweli kutokana na kisa alichowahi kusimuliwa na kusema ni moja ya kazi yenye kuelimisha na kuiasa jamii juu ya kuepukana na mila na desturi potofu.
"Ni moja ya kazi yenye mafunzo na hasa kutokana na wahusika kubeba uhusika wao kwa kiwango cha hali juu," alisema Teddy.
Aliongeza kuwa filamu hiyo aliyotunga na kuiongoza mwenyewe, imerekodiwa na kampuni ya Magambo Entertainment na kwa sasa inamalizwa kuhaririwa kabla ya kutafutiwa soko tayati kuwapa wadau wa filamu burudani yenye mafunzo kwao.
Teddy, aliwataja washiriki wa filamu hiyo ni pamoja na Pembe, Bi Hindu, Mzee Magali, mtoto Yasin Kamba ambaye ndiye mhusika mkuu, Mohammed Hamis, Josephine Joseph na wengine.

Aisha Bui: Kisura anayetamba Bongo Movie




HANA muda mrefu tangu atumbukie kwenye faini ya uigizaji, lakini makali yake kupitia baadhi ya kazi alizoshiriki, zimemfanya Aisha Fat'hi maarufu kama Aisha Bui, kuwa tishio kwa waigizaji wakongwe wa kike.
Mwenyewe anakiri aliingia rasmi kwenye fani hiyo mwaka juzi kutokana na kuvutiwa na Wema Sepetu, licha ya kudai alipenda uigizaji licha ya kutowahi kujaribu tangu alipokuwa mdogo.
"Wema ndiye aliyechangia kujiingiiza kwangu kwenye filamu kutokana na kuvutiwa nae, ila tangu utotoni nilikuwa naipenda fani hiyo sambamba na ile ya uchoraji," alisema.
Alisema alipenda sana kuchora utotoni, kipaji ambacho anaamini kama angekiendeleza angefika mbali kwa vile alikuwa mahiri kuliko maelezo.
Filamu yake ya kwanza kumtangaza mwanadada huyo ni My Book, kisha kushiriki zingine kama Saturday Morning, Better Days, Not Without My Son, Continous Love na sasa ameibuka na Second Wife.
Aisha anayependa kuogelea, kufanya mazoezi na kupika, alisema kati ya kazi zote alizoshiriki ile ya Saturday Morning ndio filamu bomba kwake kwa jinsi alivyoigiza kwa umahiri.
"Saturday Morning, ndiyo picha kali kwangu wala sio siri," alisema kisura huyo.
Akiwa na ndoto za kuja kuwa muigizaji wa kimataifa, Aisha anasema hakuna anachochukia maishani mwake kama dharau ya uongo.
"Uongo na kufanyiana dharau ni vitu nisivyopenda maishani mwangu,"
Aisha Fat'hi aliyezaliwa mwaka 1983, alisema fani ya filamu nchini inazidi kupiga hatua, ingawa alisema bado haijawa na tija ya kutosha kutokana na kuwepo kwa wizi wa wajanja wachache.
Kisura huyo ambaye waliwahi kuhusishwa na marehemu Meddy Mpakanjia, hajaolewa wala
hana mtoto na mipango yake ni kujikita zaidi katika fani hiyo ili afike mbali ikiwezekana aje kumiliki kampuni yake binafsi ya kuzalisha filamu.
"Hizi ndizo ndoto zangu, kutamba kimataifa na kuja kumiliki kampuni yangu binafsi," alisema.
Aisha, alisema kwa umri wake na kiu ya mafanikio aliyokuwa nayo naamini atafika huko
akutakapo, muhimu Mungu amjalie umri na afya njema.

Saturday, February 19, 2011

Nyalawila apigiwa debe, Cheka ajipanga





MAPROMOTA wa Ngumi za Kulipwa nchini, wameombwa kujitokeza kumuandalia pambano la utetezi Bingwa wa Dunia wa WBF, Karama Nyalawila, ili asipoteze taji hilo.
Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBO, Yasin 'Ustaadh' Abdalla, alisema ili kumuepushia Nyalawila asipoteze taji lake alilotwaa mwishoni mwa mwaka jana nchini Ukraine ni vema mapromota wakajitokeza kumuandalia pambano la utetezi.
Ustaadh, alisema kwa kanuni zilizopo katika mchezo huo, bingwa yeyote akikaa muda mrefu bila kupigana, hupoteza sifa ya kushikilia taji na hivyo anahofia yasije yakamkuta Nyalawila.
"TPBO tunawaomba waratibu wa michezo ya ngumi za kulipwa nchini kumuandalia pambano Nyalawila ili kutetea taji na kuepuka kulipoteza taji hilo lenye hadhi kubwa katika mchezo huo duniani," alisema Usraadh.
Rais huyo alisema oganaizesheni yake ipo tayari kufanya kazi na promota yeyote atakayekuwa tayari kumuandalia bingwa huo wa WBF pambano hilo kwa lengo la kutaka Tanzania iendelee kung'ara kimataifa.
Alisema kwa kitambo kirefu mabondia wa Tanzania wameshindwa kung'ara kimataifa na hivyo ni vema Nyalawila, Francis Cheka na wengine wanaoshikilia mataji wakawa wanapewa kipaumbele kuandaliwa michezo.
Katika hatua nyingine, bingwa wa dunia wa WBC, UBO, ICB, Francis Cheka, anajifua kujiandaa na pambano lake la kuwania taji la IBF litakalofanyika April 2, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Micharazo toka Morogoro, Cheka, alisema pambano lake litafanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee na atapigana na Mmarekani, Marcus Upshaw.
"Natarajia kupanda ulingoni April 2 kwa kuzichapa na Mmarekani ambaye jina lake limenitoka, katika kuwania mkanda wa IBF uzito wa kilo 72," alisema.
Hilo litakuwa pambano la kwanza kwa Cheka tangu alipomshindwa kwa pointi Bingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Mada Maugo katika pambano lisilo la mkanda lililochezwa Januari Mosi, kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar.

Mwisho

Msama Promotion yawasaidia Wahanga wa Mabomu Gongo la Mboto






WAHANGA wa milipuko ya mabomu yaliyotoka eneo la Gongo la Mboto, wameendelea kupewa misaada, baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka nchini, Alex Msama kutoa misaada ya vyakula.
Misaada hiyo yenye thamani ya karibu Sh. Mil. 3, ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Msama kupitia kituo cha runinga cha Cloud's, kwa lengo la kufikishwa kwa waathirika na milipuko hiyo iliyotokea katikati ya wiki kwenye kambi ya Jeshi la Wananchi Tanzania, JWTZ, kikosi cha 521 KJ.
Msama alisema kama sehemu ya jamii walioguswa na tukio la milipuko hiyo ya mabomu wameamua kutoa misaada hiyo kuitikia wito wa serikali, huku akiwahimiza watu wengine wenye uwezo kufanya hivyo.
"Tusiiachie serikali pekee yake kufanya kazi hii, ndio maana sisi kama sehemu ya jamii tumeamua kutoa msaada huu japo mdogo, lakini uwasaidie wenzetu walioathirika na tukio hilo linalosikitisha," alisema Msama.
Msaada huo uliotolewa ni magunia manne ya Mchele, Unga wa Ngano gunia 10, gunia mbili za Maharage na Sukari pamoja na ndoo mbili za mafuta ya Gunia za maharage na ndoo mbili za mafuta ya kupikia.
Msama alisema, pamoja na msaada huo, kamati yao inafanya mipango zaidi ya kuongeza misaada yao kwa wahanga hao kwa nia ya kuisaidia serikali na asasi nyingine zilizojitolea kwa hali na mali kuwafariji waathirika wa mabomu hayo.
Tukio la ulipukaji wa mabomu la Gongo la Mboto ni la pili katika kipindi cha karibu miaka miwili, baada ya awali kulipuka April 29, mwaka juzi kambi nyingine ya jeshi eneo la Mbagala, pia jijini Dar es Salaam.
Katika tukio hilo la pili, karibu watu 20 wakiwemo watoto wameripotiwa kupotea uhai wao, huku wengine wanaokadiriwa kufikia 400 wakijeruhiwa, mbali na kusababisha uharibifu wa mali na miundo mbinu kadhaa.
Tayari serikali imetangaza kuwalipa fidia wote walioathirika na tukio hilo, ambalo lilitokea majira ya usiku, siku ya Jumatano na kuleta taharuki kwa wakazi wengi wa jijini na wale wa mikoani.

Mwisho

Tuesday, February 15, 2011

TAMAGSARAI na mikakati yao dhidi ya uboreshwaji masoko


KUTOKANA na kuona hawana sauti ya pamoja na mahali pa kusemea matatizo na kero zinazowakabili katika shughuli zao, wauzaji wa mazao ya nafaka katika soko maarufu la Tandale waliamua kuunda umoja wao kama njia ya kupigania na kutetea haki zao.
Umoja huo wa wauza nafaka hao unafahamika kwa kifupi kama TAMAGSARAI ambao ni kifupi cha Umoja wa Wauza Nafaka na Wawekezaji wa Soko la Tandale kwa lugha ya Kiingereza na ulianzishwa rasmi mwaka 2000 ingawa usajili wake ulipatikana mwaka 2003.
Malengo makubwa ya umoja huo ulioasisiwa na watu 45 chini ya Uenyekiti wa Abeid Hamad Lunda na katibu Abdul Kambaya, mbali na kuwa sauti ya pamoja katika utatuzi wa kero na matatizo yao, pia kutaka kubadilisha mazingira na hali ya soko hilo na mengine Tanzania.
Mwenyekiti wa sasa wa umoja huo, Juma Dikwe, alisema masoko mengi nchini likiwemo lao la Tandale yana mazingira duni, machafu na hayavutii, kiasi kwamba yamekuwa yakikimbiwa na baadhi ya watu wanaoenda kwenye masoko ya kisasa maarufu kama 'Super Market'.
Dikwe, alisema kitu cha kinachowauma ni kwamba pamoja na masoko kuwa katika mazingira duni na machafu, kosi na ushuru utozwa kila siku na hazijulikani wapi zinapoenda wakati zilihitajiwa kuboresha masoko husika.
"Tunalipishwa kodi na ushuru, tegemeo letu fedha hizo zingerudi tena kwetu kwa kuboresha maeneo yetu ya kazi, lakini cha ajabu masoko yanakuwa machafu na kuhatarisha maisha yetu," alisema Dikwe.
Mwenyekiti huyo, alisema hata hivyo wanashukuru miaka karibu 10 tangu umoja wao uanzishwe wameweza kuielewesha serikali na kusaidia kuboresha soko lao na wanapigana zaidi kuona masoko mengine nayo yanakuwa katika na mazingira mazuri ya kufanyia kazi.
Alisema karibu masoko yote nchini hufanana kimazingira na hivyo ni vema yakafanyiwa marekebisho kuendana na wakati, ili kusaidia biashara kufanyika vema na kusaidia kuinua kipato cha wafanyabiashara, wakulima na taifa kwa ujumla.
Tangu umoja huo ulipoanzishwa hadi sasa una wanachama 105 ikiwa ni ongezeko la wanachama zaidi ya 60 kwa kipindi cha miaka saba iliyopita, huku ukiwa umesaidia kuandaa semina na mafunzo mara tatu kwa lengo la kuwaelimisha wanachama wao.
Semina ya kwanza ilifanyika mwaka 2007 iliyohusumu Elimu ya Utawala Bora iliyowahusisha viongozi wa serikali za mitaa na wanachama wao kwa lengo la kusimamia utekelezaji wa shughuli za serikali kwa ufanisi ikiwemo sekta ya masoko.
Kisha mwaka 2009 waliandaa mafunzo mengine yaliyohusu ufuatiliaji wa fedha za umma zilizotengwa kwa ajili ya sekta ya Masoko na mwaka huu waliandaa nyingine iliyohusu Usimamiaji wa Miradi na Rasilimali za Masoko ikiwa ni mradi wa miaka mitatu mfululizo.
Dikwe, alisema mradi huo, semina na mafunzo ya awali yaliandaliwa na umoja wao kwa msaada na ufadhili wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii, The Foundations for Civil Society na imekuwa ikiwahusisha wanachama wao na wachuuzi wengine wa masoko ya jijini Dar es Salaam.
"Mradi huu Usimamiaji wa Rasilimali za Masoko, ni wa miaka mitatu na tunashirikisha wachuuzi wa masoko karibu yote ya wilaya tatu za mkoa wa Dar es Salaam kwa vile matatizo ya masoko yanafanana kwa kiasi kubwa," alisema.
Mbali na kuendesha miradi na semina hizo, TAMAGSARAI pia huwasaidia wanachama wao wanapopata matatizo kama ya kufiwa na mengineyo kupitia fedha zinazopatikana toka kwa wafadhili wao na zile za michango ya ada inayotozwa kwa kila mmoja wao.
Pia husimama kama wadhamini kwa wanachama wao katika hupatikanaji wa mikopo toka kwa asasi za kifedha, ili kurahisisha kuboresha shughuli zao na kuihimiza serikali kuboresha masoko kwa kujenga mabanda ambayo yanakithi haja ya matumizi ya binadamu.
"Mabanda mengi yaliyopo kwenye masoko yetu ni mafupi na hayana ubora na imekuwa chanzo cha vifo vya wanachama na wachuuzi wengine kutokana na magonjwa ya kuambukiza kama Kifua Kikuu, na Kipindupindu na Homa ya Matumbo nyakati za mvua," alisema.
Alisema kwa takwimu za haraka kwa kipindi cha miaka saba, wanachama na wachuuzi wenzao 15 kati ya 50 walioathirika kwa ugonjwa wa Kifua Kikuu walifariki, huku wengine wakinusurika vifo wakati wa msimu wa mvua kutokana na ugonjwa wa Kipindupindu.
"Kwa kweli soko la Tandale na mengineyo nchini ni machafu na yanatisha nyakati za mvua na ndio maana TAMAGSARAI tumekuwa tukipigania kuboreshwa kwake, ili kuwaokoa watumiaji wake yaani wauzaji na wateja ambao wengi wanayakambia na kutukosesha mapato," alisema.
Moja ya mikakati yao kwa sasa ni kutaka kuunganisha nguvu zaidi katika umoja wao na kupanua huduma zao kutoka soko la Tandale tu na kuwa la nchi nzima likiunganisha wachuuzi na wauzaji wote wa nafaka, kwa lengo la kuwa na sauti moja yenye nguvu.
Pia wanajaribu kusaka mbinu na kuwaelimisha wanachama wao na wachuuzi wengine kwa ujumla juu ya upakiaji na uuzaji wa bidhaa zao katika hali ya kisasa ili kuvutia wateja hata wale ambao wanayachukulia masoko mengi kama ya watu wanyonge na wasio na hadhi.
"Tuimeshaanza kuwapa mafunzo wanachama wetu ili kupakia bidhaa zao kisasa, badala ya kuendelea kutoa huduma kizamani ambayo inachangia watu kukimbilia Super Market wakiona ni usasa zaidi, ingawa bidhaa ni zile zile na pengine zetu ni bora zaidi, " alisema.
Msisitizo wa umoja huo wenye safu kamili ya uongozi uliochaguliwa baada ya kuongozwa kwa muda na viongozi waasisi ni kuitaka serikali kutumia kodi na ushuru wanaotoza kwenye masoko kuboresha mazingira na masoko hayo kusaidia ajira na vipato vya watumiaji wake.
"Pia tunataka fedha zinazotengwa na serikali kwa ajili ya kuboresha huduma za masoko zitumike kwa malengo yaliyowekwa badala ya kufanyiwa ubadhilifu na wachache wenmye jukumu la kusimamia masoko," alisema Dikwe.
Aliongeza, pia ni vema masoko yakamilikishwa kwa vyama au wafanyabiashara wenyewe badala ya kuachiwa mawakala ambao wapo kifedha zaidi bila kuangalia uboreshaji wa mazingira ya masoko hayo kulingana na kodi na ushuru wanaotoza kila siku sokoni hapo.
Safu nzima ya umoja huo ambao kwa sasa unasaka soko la bidhaa zao nje ya nchi ni Mwenyekiti wake ni Juma Dikwe, Makamu wake, Juma Janga, Abdul Kambaya ndiye ni Katibu, wakati Sadiki Kubiga niu Mhazini.

Mwisho

Saturday, February 12, 2011

Vijana wahimizwa kujifunza uongozi, ujasiriamali

VIJANA wa Kitanzania wamehimizwa kujitosa kwenye masuala ya uongozi na ujasiriamali kwa lengo la kuja kuwa tegemeo la taifa hapo baadae.
Wito huo umetolewa na uongozi wa Chuo cha Viongozi wa Afrika, African Leadership Academy (ALA), kilichopo Afrika Kusini wakati wakitangaza ofa maalum ya kuwasomesha kwa muda wa miaka miwili bure wahitimu wa sekondari na vijana wa Kitanzania.
Mkurugenzi wa Usajili wa chuo hicho, Ivy Mwai, amesema kutokana na hali ilivyo duniani kwa sasa ni vema vijana wakajifunza masuala ya uongozi na ujasiriamali ili kuweza kujisaidia wenyewe na nchi yao kwa ujumla.
Mwai alisema vijana wenye ndoto za kuwa viongozi au wajasiriamali ni lazima wajisomee fani hizo kisha kujitokeza bila hofu yoyote kwa lengo la kuiletea nchi maendeleo.
"Vijana wa Kitanzania wenye vipaji vya uongozi na ndoto za kuwa wajasiriamali wajitokeze hadharani ili wapate ujuzi na uzoefu kwa manufaa ya taifa hapo baadae," alisema Mwai.
Mwai, alisema kutokana na kupenda kuona nchi za kiafrika zinapiga hatua kubwa kimaendeleo chuo chao kimetoa ofa Tanzania kwa kuwasomesha watakaojisajili na kufuzu kwenye mchujo utakaofanyika Mei mwaka huu.
Alisema usajili wa wahitimu hao wa sekondari na vijana wenye sifa utaanza kufanyika kuanzia mwezi ujao na watakaoshinda watatangazwa Mei kabla ya kwenda kujiunga na chuo hicho.
"Lengo letu ni kutaka kuona Tanzania na nchi za Kiafrika zinakuwa na viongozi wenye uchungu wa kuziletea mabadiliko nchi yao kimaendeleo na hivyo tumeamua kutoa ofa maalum kwa vijana wa hapa," alisema.
Mwai alisema kijana yeyote mwenye umri kati ya miaka 16-19 wanaweza kuichangamkia ofa hiyo itakayoambatana na kusaidiwa kutafutiwa vyuo vikuu vya kimataifa pale watakapofanya vema kwenye masomo yao ALA kwa kujaza fomu kupitia barua pepe admissions@africanleadershipacademy.org.
Mmoja wa wanafunzi wa Kitanzania aliyewahi kupata ofa kama hiyo ya ALA, Julius Shirima, ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Chama cha Wajasiriamlia Mkoa wa Dar es Salaam, DARECHA, alisema vijana hawapaswi kuipoteza bahati hiyo.

SOMA MAELEZO KUKIJUA VEMA CHUO CHA ALA

African Leadership Academy is a world-class, pan-African secondary institution that aims to educate and develop outstanding students into principled, ethical leaders for Africa. It is an A level school, enrolling students aged 15-19 who are in their last two years of secondary and they sit the Cambridge International Examinations. The school, located in Johannesburg, South Africa seeks students who have demonstrated leadership, have good consistent academic performance, have an entrepreneurial/problem solving spirit, are involved in their communities and have a passion for Africa.


AFRICAN LEADERSHIP ACADEMY - AT A GLANCE


Our Mission
African Leadership Academy (ALA) seeks to transform Africa by developing and supporting future generations of African leaders. Opened in September 2008, African Leadership Academy brings together the most promising 16 -19 year old leaders from all 54 African nations for an innovative two-year program designed to prepare each student for a lifetime of leadership on the continent. Students are selected to attend the Academy based on merit alone and complete a unique curriculum with a focus on Leadership, Entrepreneurship, and African studies. ALA graduates attend the world’s finest universities and will lead Africa toward a peaceful and prosperous future. ALA is a non-profit institution located on the outskirts of Johannesburg, South Africa.

Our Team
African Leadership Academy was founded in 2004 by Fred Swaniker, Chris Bradford, Peter Mombaur, and Acha Leke. The founding team brings considerable experience as educators, entrepreneurs, consultants, and corporate executives in Africa and throughout the world. Our Advisors and Directors are internationallyrecognized luminaries in business, leadership development, secondary education, and social entrepreneurship.
These include Carly Fiorina, the former CEO and Chairwoman of Hewlett-Packard; Isaac Shongwe, Chairman of the African Leadership Initiative in South Africa; Futhi Mtoba, Chairwoman of Deloitte & Touche South Africa; Sir Sam Jonah, formerly President of Anglogold Ashanti; Jon Cummings, Director at McKinsey & Company; Ralph Townsend, Headmaster of Winchester College (UK); Ed Brakeman, retired Managing Director of Bain Capital; James Mwangi, CEO of Equity Bank, Kenya and Tunde Folawiyo, Executive Director of The Yinka Folawiyo Group, Nigeria. ALA also has a larger network of like-minded mentors, partners, and leaders to provide alumni with the long-term support system needed to lead Africa toward equitable and lasting development.

Our Successes

• In June 2005, ALA launched a pilot summer program to test and refine its concept and curriculum.
By 2008, more than 500 young leaders from 40 countries had participated in this innovative program.
• In June 2006, co-founders Fred Swaniker and Chris Bradford were named Echoing Green Fellows and described as two of the “15 best emerging social entrepreneurs in the world.”
• In April 2007, ALA secured a state-of-the art campus on the outskirts of Johannesburg to serve as the home of the institution.
• In June 2010, 93 students of the Inaugural Class graduated, many with full scholarships to attend top universities around the world.
• In July 2010, ALA sent offers of admission to 105 students from 33 countries, out of a pool of over 2,000 applicants. For the first time applicants from Guinea, the Gambia, Tunisia and Rwanda, were admitted to the Academy.
• In 2010, ALA students gained entrance into leading universities in USA, Europe and Africa such as Harvard, Oxford, Stanford, University of Cape Town and Ashesi University, Ghana.
• In 2010, ALA students received over $9.5 million in scholarship money to attend university.

Your Role
African Leadership Academy offers like-minded individuals and organizations a growing global network of local chapters and strategic partnerships committed to fostering our vision. To learn more, please contact admissions@africanleadershipacademy.org.

Campus Address
1050 Printech Ave, Honeydew 2040 South Africa
Postal Address
Postnet Suite 413, Private Bag X1
Northcliff 2115 South Africa
Phone: +27 11 699 3000 Fax: +27 11 252 6190
Email: info@africanleadershipacademy.org
First Ready Development 695 (Incorporated under Section 21) T/A African Leadership Academy
Directors: Peter B. Mombaur, Dr. Achankeng Leke, Frederick K. Swaniker
Reg. No. 2005/005377/08 - VAT No. 4670224122 - PBO No. 930020187
Gauteng Department of Education Reg. No. 400286
www.africanleadershipacademy.org


$9.5 million in University Scholarship Money Awarded to Outstanding
African Leadership Academy Graduates in 2010

The following are examples of just some of the leading universities that ALA students have been admitted to in 2010:
Fatoumata Fall, SENEGAL
University attending: Harvard University, USA
Also admitted to: Massachusetts Institute of Technology (MIT) (USA)
Subject: Engineering

Samuel Gichohi, KENYA
University attending: Princeton University, USA
Subject: Computer Science

Ifedolapo Omiwole, NIGERIA
University attending: Yale University, USA
Also admitted to: Oxford University (UK)
Subject: Economics

Mbali Zondi, SOUTH AFRICA
University attending: Barnard College, USA
Also admitted to: Ithaca College (USA), Lake Forest College (USA)
Subject: Journalism

Nkululeko Zigizendoda Yeni, SOUTH AFRICA
University attending: Yale University, USA
Also admitted to: Amherst College (USA), Colgate University (USA), Harvard University (USA),
University of Virginia (USA)
Subject: International Relations

Felix Tetteh, GHANA
University attending: Ashesi University, Ghana
Also admitted to: The College of Idaho (USA)
Subject: Business Economics & Music

Campus Address
1050 Printech Ave, Honeydew 2040 South Africa
Postal Address
Postnet Suite 413, Private Bag X1
Northcliff 2115 South Africa
Phone: +27 11 699 3000 Fax: +27 11 252 6190
Email: info@africanleadershipacademy.org

First Ready Development 695 (Incorporated under Section 21) T/A African Leadership Academy Directors: Peter B. Mombaur, Dr. Achankeng Leke, Frederick K. Swaniker
Reg. No. 2005/005377/08 - VAT No. 4670224122 - PBO No. 930020187
Gauteng Department of Education Reg. No. 400286
www.africanleadershipacademy.org

Dagbedji Fagnisse, CÔTE D’IVOIRE
University attending: Duke University, USA
Subject: Engineering
Awarded: Robertson Scholarship

Mehdi Oulmakki, MOROCCO
University attending: Dartmouth College, USA
Also admitted to: Amherst College (USA), Northeastern University (USA), Pomona College (USA)
Subject: Mathematics

Marie Shabaya, KENYA
University attending: University of Durham, London, UK
Also admitted to: Royal Holloway (UK), University of London (UK), School of Oriental and African
Studies (UK)
Subject: Economics

Imelda Rweyemamu, TANZANIA
University attending: Jacobs University Bremen, Germany
Also admitted to: Indiana University-Purdue University Indianapolis (USA)
Subject: Engineering

Rumbidzai Gondo, ZIMBABWE
University attending: Colby College, USA
Subject: History
Mariam Doumbia, MALI
School attending: Miss Hall’s School, Massachusetts, USA
Subject: Gap Year Program
Awarded: ASSIST-USA Gap Year Scholarship

JE WEWE UNAPENDA UONGOZI NA KUWA MJASIRIAMALI SOMA HAPA

CHUO CHA UONGOZI AFRIKA, AFRICAN LEADERSHIP ACADEMY CHA AFRIKA KUSINI KINASAKA WAHITIMU WA SEKONDARI NA VIJANA WENYE UMRI USIOZIDI MIAKA 19 KWA AJILI YA KUINGIA KWENYE MCHAKATO WA KUPATA OFA YA KUSOMESHWA UONGOZI NA UJASIRIAMALI PAMOJA NA KUFANYIWA MIPANGO SCHOLARSHIP KWA VYUO VIKUU VYA KIMATAIFA.
MCHAKATO HUO UNAANZA RASMI MWEZI UJAO NA MAJINA YA WATAKAOVUKA MCHUJO HUO YATATANGAZWA RASMI MEI MWAKA HUU.
CHUO HIKI KIMEKUWA KIKITOA OFA NA KUWASAIDIA WANAFUNZI NA VIJANA WA KIAFRIKA, AMBAPO WALIOPIOTIA KATIKA CHUO HICHO BAADHI YAO KWA SASA WANASOMA MAREKANI, UJERUMANI NA NCHI ZINGINE ZA ULAYA NA AMERIKA.

KWA MAELEZO ZAIDI MNAWEZA KUJIUNGA SASA KUPITIA admissions@africanleadershipacademy.org.

Friday, February 11, 2011

Sikinde, Msondo zaanza tambo, zitakutana Februari 18

BENDI kongwe za muziki wa dansi nchini, Msondo Ngoma na Mlimani Park 'Sikinde' ambazo zinatarajiwa kuonyeshana kazi wiki ijayo, zimetambiana kwa kila moja ikijinasibu kuizima nyingine katika onyesho lao la pamoja litakalofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.r
Msondo na Sikinde zitakutana tena Februari 18 ikiwa ni mara ya pili katika kipindi cha miezi miwili baada ya kuchuana awali Desemba 30 katika onyesho lililofanyika ndani ya ukumbi wa Mzalendo Pub, uliopo Millenium Tower, Makumbusho Dar es Salaam.
Wakati siku zikikaribia kabla ya pambano hilo, viongozi wa bendi hizo wameanza kurushiana vijembe kila upande ukitamba kuwazima wenzake.
Msemaji wa Msondo, Rajabu Mhamila "Super D', alisema wanaamini kama walivyowazima Sikinde katika onyesho lao la Desemba, ndivyo watakavyofanya wiki ijayo kutokana na kikosi chao kinachoundwa na wanamuziki vijana na wachapakazi.
"Tunajua kwa sasa Sikinde watakuwa wanatafuta namna ya kutukabili, lakini kwa kifupi watarajie kufunikwa kama tulivyofanya kwenye onyesho la Mzalendo Pub," alisema Super D.
Hata hivyo, Sikinde ambao walikuwa visiwani Zanzibar kwenye Tamasha la Sauti za Busara wamejinasibu kuwa Msondo hawana ubavu mbele yao na kuwataka mashabiki wa muziki waende Diamond Jubilee kushuhudia ukweli wa wanachokisema.
Katibu wa Sikinde, Hamis Milambo alisema Sikinde ni zaidi ya Msondo kutokana na kukamilika kila idara kuanzia safu ya uimbaji, wapiga magitaa na wapuliza tarumbeta walichodai watatumia kama silaha ya kuwazima mahasimu wao.
"Sisi ni kama Barcelona, tuna safu kali ya ushambuliaji nikimaanisha waimbaji na viungo mahiri ambao ni wapuliza ala za upepo sikuambii wapiga magita, sijui kama Msondo watafua dafu," alisema Milambo.
Milambo alisema bendi yao inatarajia kurejea leo mchana kuendelea na utambulisho wa vibao vyao vipya vinavyoandaliwa kwa ajili ya albamu yao ijayo.

Friday, February 4, 2011

Wasanii wa kike tujiheshimu-Regina



MMOJA wa waigizaji wa filamu anayekuja juu nchini, Regina Mroni amewaasa wasanii wenzake hususani wa kike, kujiheshimu na kuepukana kufanya matendo yanayowachafua mbele ya jamii pamoja na kuidhalilisha fani yao kuonekana kama kazi ya wahuni.
Mroni, aliyeng'ara kwenye filamu kama Trip to Amerika, Mastress, Siri y Mama, Aisha na nyinginezo, alisema kuna baadhi ya wasanii hasa wa kike wamekuwa wakiona raha kujianika utupu na kuhusishwa na skendo chafu, wakiamini wanakuza majina yao wakati wanajidhalilisha.
Alisema umaarufu wa msanii yeyote unapatikana kutokana na ubora na umahiri wa kazi zake na sio matendo machafu na hivyo kuwataka wasanii wa kike wajiamini, kujituma na kuithamini kazi yao ili jamii iwaheshimu.
"Wapo baadhi yetu wamekuwa wakijihusisha na matendo machafu na kuandikwa kila mara, kitu ambacho tofauti na fikra zao kuwa wanajijengea majina na umaarufu, wanajidhalilisha na kuonekana mbele ya jamii kama watu wasio na maadili kitu ambachio ni kibaya," alisema Mroni.
Mroni, aliyetumbukia kwenye fani hiyo miaka miwili iliyopita akitokea kwenye urembo ambapo aliwahi Miss Utalii Morogoro, Miss Ukonga, Miss Singida na kushiriki Miss Tanzania, alisema sanaa ni kazi kama kazi nyingine na wanaishiriki waithamini na kuipenda.
Alisema 'wavamizi' wachache kwenye fani hiyo wasio na vipaji ndio wanaojiachia na kujianika na mwisho wa siku wanadhalilika na kisha kupotea wakiwaacha wasanii wa kweli wakiendelea kutamba.

Mwisho

TAFF yapewa kifyagio kwa tamasha la filamu la Nyerere

SHIRIKISHO la Filamu Tanzania, TAFF, limepewa heko kwa ubunifu wake wa kuanzisha tamasha la filamu za Kibongo ambalo litafanyika Februari 14-19 jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo la kwanza kufanyika nchini kwa filamu za Kitanzania litafanyikia kwenye viwanja vya Leaders kwa kuzunduliwa na Rais Jakaya Kikwete na kufungwa na mke wa hayati baba wa taifa, Mwl Nyerere, Mama Maria Nyerere.
Baadhi ya wadau wa filamu wakiwemo wasanii wa fani hiyo wamesema kitendo cha TAFF kubuni tamasha hilo ni jambo la kupongezwa kwa vile litasaidia kuinua soko la kazi za wasanii wa kibongo, mbali na kutoa fursa kwa wananchi kupata mwamko wa kuzipenda kazi hizo.
"TAFF wamefanya jambo la maana ambalo wadau wa filamu Bongo tulikuwa tunalisubiri kwa muda mrefu, kitu cha muhimu waliendeleze kama mengine," alisema Leila Mwambungu wa Kimara.
Leila, alisema tamasha hilo linaweza kusaidia kuamsha hisia wa watanzania kupenda kazi za nyumbani kwa madai wapo wengine wanazichukulia poa filamu za Kibongo na kuhusudu kazi za Nigeria au Marekani.
Mtayarishaji wa filamu anayekuja juu, Husseni Ramadhani 'Swagger' alisema tamasha hilo ni kama njia ya wadau wa filamu kujitangaza na kuwahimiza wenzake kujitokeza kwa wingi kulishiriki kuanzia mwanzo wake hadi siku ya ufungwaji wake.
"Nafasi kama hizi ni muhimu kuzichangamkia, kwa kweli nalipongeza TAFF kwa kubuni kitu kama hiki, kwani itatusaidia wengine kujifunza makubwa zaidi ya yale tunayoyajua katika sanaa hiyo kutokana na ukweli tumesikia kuna mafunzo kadhaa yatakayotolewa hapo," alisema Swagger ambaye anatamba na filamu kama Hazina, Who is a Killer na sasa Bangkok Deal.
TAFF kupitia viongozi wake chini ya Rais Simon Mwakifamba, walitangaza kuanzisha kwa tamasha hilo litakalozinduliwa wiki ijayo na Rais Kikwete kwa ajili ya kuonyesha kazi za kitanzania pamoja na kupambwa na burudani kadhaa za sanaa na mada mbalimbali za kifani.
***

Ray, Kanumba na Msondo kila mtu kivyake

Ray ana 'Second Wife, Deception noma!


WAKATI filamu ya Family Disaster ikiendelea kutamba mitaani kwa sasa, msanii nyota wa fani hiyo nchini, Vincent Kigosi 'Ray', yupo mbioni kuachia kazi nyingine mpya iitwayo 'The Second Wife'.
Filamu hiyo ya kimapenzi, imewashirikisha wasanii kadhaa nyota pamoja na waigizaji chipukizi ambao wameibuliwa na kampuni iliyotayarisha filamu hiyo, RJ Production.
Miongoni mwa waigizaji walioshiriki filamu hiyo ni pamoja na Ray mwenyewe, Colleta Raymond, Aisha Bui, Riyama Ally, Msungu, Ramla na mtoto aitwae Aisha ambaye ni chupukizi.
Ray ameanika kwenye mtandao wake kuwa, filamu hiyo ambayo ameigiza kama muumini wa Kiislam ipo katika hatua ya mwisho kabla ya kuachiwa ni moja ya kazi yenye mafunzo makubwa kwa jamii.
"Kama nilivyofanya kwenye The Divorce ndani ya filamu hii mafunzo ni yale yale na mashabiki mkae mkao wa kula kupata uhondo," alisema Ray.
Kwa mujibu wa taarifa hizo kama filamu zake nyingine, 'The Second Wife' itasambazwa na kampuni ya Steps Entertainment.
Wakati huo huo filamu mpya ya Steven Kanumba iitwayo Deception, aliyoigiza pamoja na Bakari Makuka, Rose Ndauka na Patcho Mwamba imekuwa ikinunuliwa kama njugu tangu iigizwe sokoni mapema wiki hii.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Nipashe, filamu hiyo imekuwa ikigombewa kununuliwa sambamba na Pete ya Ajabu na Family Disaster ambayo ina karibu mwezi sasa sokoni.
***


Msondo wapeleka mpya Songea


BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo Ngoma, kesho inatarajiwa kuzitambulisha nyimbo zao mpya zinazoandaliwa kwa ajili ya albamu ya 2011 mjini Songea mkoani Ruvuma.
Msondo inayotamba na albamu ya ya Huna Shukrani, itatumbuiza kwenye ukumbi wa Serengeti Bar, mjini huo.
Kwa mujibu wa kiongozi wa bendi hiyo, Said Mabera 'Diblo' ni kwamba Msondo itatumbuiza kwenye ukumbi huo nyakati za usiku, wakati jioni watakuwepo kwenye dimba la Majimaji kushuhudia pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Yanga na wenyeji Majimaji-Songea.
Mabera, alisema katika onyesho hilo, bendi yao itapiga nyimbo zao za zamani pamoja na zile mpya zinazoendelea kuandaliwa kwa ajili ya albamu yao ijayo.
"Tupo Songea na kesho tutafanya onyesho kwenye ukumbi wa Serengeti, wakazi wa Songea wakae mkao wa kupata uhondo mtupu," alisema Mabera mmoja wa wapiga solo mahiri nchini na mwanamuziki aliyedumu kwa muda mrefu Msondo tangu alipojiunga mwaka 1973.
Mabera alizitaja baadhi ya nyimbo watakazozipiga kwenye onyesho hilo ni pamoja na zile za albamu za Demokrasia ya Mapenzi, Ndoa Ndoana, Kilio cha Mtu Mzima, Piga Ua Talaka Utatoa, Kaza Moyo, Kicheko kwa JIrani na Huna Shukrani.
"Pia tutawapigia na kuzitambulisha nyimbo mpya za Lipi Jema, Dawa ya Deni, Kwa Mjomba Hakuna Urithi na Baba Kakura, yaani ni burudani kwa kwenda mbele," alisema.
Baadhi ya wanamuziki wa Msondo ambayo wiki iliyopita ilimpoteza mmoja wa waimbaji wake mahiri, Hamis Maliki 'Super Maliki' watakapanda jukwaani leo ni pamoja na Mabera, Roman Mng'ande, Huruka Uvuruge, Ibrahim Kandaya, Juma Katundu, Is'haka Katima, Eddo Sanga na wengineo.
***

Extra Bongo yaivunjavunja Twanga Pepeta





NENO zuri la kusema ni kwamba African Stars 'Twanga Pepeta' imevunjwavunjwa baada ya wanamuziki wake nyota saba kuihama bendi hiyo kwa mpigo na kutua Extra Bongo 'Wana 'Next Level' iliyoingia rasmi kambini kujiwinda na albamu mpya ya pili.
Wanamuziki hao saba walitambulishwa rasmi leo asubuhi na Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki, ambapo alisema lengo la kuwanyakua wakali hao ni kutaka bendi yake iwe matawi ya juu na kuleta mabadiliko ya muziki wa dansi nchini.
Choki aliwatambulisha wanamuziki hao ambapo ni waimbaji wawili, wapiga gitaa wawili na madansa watatu akiwemo mkali Hassani Mussa 'Super Nyamwela'.
Mbali na Nyamwela aliyeitumikia Twanga kwa miaka 11 mfululizo bila kuhama ni Rogart Hegga 'Catapilla' na Saul Ferguson ambao ni waimbaji, Hosea Mgohachi mpuiga gita zito la besi na Godi Kanuti anayecharaza magita yote.
Wanenguaji wengine waliomfuata Nyawela Extra Bongo ni Otilia Boniface na Issack Burhan maarudu kama Danger Boy.
Choki alisema wanamuziki hao wote wana mikataba na bendi yao na mchana huu wanatarajia kuungana na wanamuziki wenzao kambini eneo la Mbezi Mwisho kujipanga kwa albamu mpya.
Alisema kambi hiyo ya muda wa wiki tatu itatumika kuwapa fursa wanamuziki hao wapya kuzoeana na wenzao kabla ya kuanza kufanya vitu vyao hadharani wakiwa wamezaliwa upya.
Mkurugenzi huyo aliyesema tukio kama hilo la kuibomoa Twanga liliwahi kumtokea miaka minne iliyopita alipochukuliwa wanamuziki wa idadi kama hiyo na ASET na kuifanya Extra Bongo 3x3 Kujinafasi kuzimika hadi ilipofufuka mwaka jana.
Alisema wanamuziki hao wapya wamenyakuliwa na Extra Bongo tayari kuziba nafasi za waliotemwa akiwemo rapa machachai Greyson Semsekwa na wenzake kadhaa.
Wakizungumza kwenye utambulisho huo, Ferguson na Nyamwela walisema wamekuja kuthibitisha thamani yao na mashabiki wa Extra Bongo watarajie makubwa.
"watarajie kazi bab'kubwa kwani tunafahamika kwa vipaji vya fani hii," alisema Ferguson.

Nyamwela aitema Twanga, adai miaka 11 imetosha





KIONGOZI wa muda mrefu wa madansa wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' Hassan Mussa 'Super Nyamwela', aliyetangazwa jana kujiunga na bendi ya Extra Bongo, amedai amefikia uamuzi huo kwa lengo la kutaka kubadilisha upepo baada ya kukaa bendi yke kwa miaka zaidi ya 10.
Akizungumza kwenye utambulisho wake na wenzake sita toka Twanga, Nyamwela alisema miaka 11 aliokaa ASET imemtosha na ndio maana ameondoka ili kuzaliwa upya.
Nyamwela alisema hata hivyo pamoja na kuondoka Twanga ikiwa ni bendi yake pekee kuifanyia kazi tangu alipochukuliwa toka kundi la Billbum, hawezi kuponda alikotoka kwa vile imemsaidia kwa mengi na kwa sasa akili yake ni kuwapa burudani mashabiki wa bendi yake mopya.
"Nimeondoka kwa kutaka kubadilisha upepo, mnanijua mie sina utamaduni wa kuhamahama, ila kwa kutaka kuleta mabadiliko katika fani na maisha yangu kwa ujumla nimeamua kuoka Twanga na watu wasinchukulie vingine natafuta maisha," alisema dansa huyo bingwa wa zamani wa Bolingo Dar.
Aliongeza kuwa kama alivyokuwa Twanga alipoipa mafanikio makubwa, ndivyo ambavyo amepania kufanya hivyo akiwa Extra Bongo ambao ameungana nao kambini kujiandaa kupakua albamu mpya.
"Nyamwela ni yule yule, ila kwa hapa Extra mashabiki wake watarajie mambo makubwa na mazuri zaidi, na imani kwa ushirikiano na wenzangu Extra Bongo itatisha," alisema Nyamwela.
Mbali na Nyamwela, katika utambulisho huo, pia madansa Otilia Boniface, Isaack Burhani nao walitambulishwa sambamba na wanamuziki, Rogart Hegga 'Catapillar', Saulo Ferguson, Hosea Mgohachi na God Kanuti waliokuwa Twanga Pepeta.
wanamuziki hao walitambulishwa kwa waandishi wa habai jana na Mkurugenzi wa bendi hiyo ya Extra Bongo, Ally Choki 'Kamarade'.