STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 4, 2011

Nyamwela aitema Twanga, adai miaka 11 imetosha





KIONGOZI wa muda mrefu wa madansa wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' Hassan Mussa 'Super Nyamwela', aliyetangazwa jana kujiunga na bendi ya Extra Bongo, amedai amefikia uamuzi huo kwa lengo la kutaka kubadilisha upepo baada ya kukaa bendi yke kwa miaka zaidi ya 10.
Akizungumza kwenye utambulisho wake na wenzake sita toka Twanga, Nyamwela alisema miaka 11 aliokaa ASET imemtosha na ndio maana ameondoka ili kuzaliwa upya.
Nyamwela alisema hata hivyo pamoja na kuondoka Twanga ikiwa ni bendi yake pekee kuifanyia kazi tangu alipochukuliwa toka kundi la Billbum, hawezi kuponda alikotoka kwa vile imemsaidia kwa mengi na kwa sasa akili yake ni kuwapa burudani mashabiki wa bendi yake mopya.
"Nimeondoka kwa kutaka kubadilisha upepo, mnanijua mie sina utamaduni wa kuhamahama, ila kwa kutaka kuleta mabadiliko katika fani na maisha yangu kwa ujumla nimeamua kuoka Twanga na watu wasinchukulie vingine natafuta maisha," alisema dansa huyo bingwa wa zamani wa Bolingo Dar.
Aliongeza kuwa kama alivyokuwa Twanga alipoipa mafanikio makubwa, ndivyo ambavyo amepania kufanya hivyo akiwa Extra Bongo ambao ameungana nao kambini kujiandaa kupakua albamu mpya.
"Nyamwela ni yule yule, ila kwa hapa Extra mashabiki wake watarajie mambo makubwa na mazuri zaidi, na imani kwa ushirikiano na wenzangu Extra Bongo itatisha," alisema Nyamwela.
Mbali na Nyamwela, katika utambulisho huo, pia madansa Otilia Boniface, Isaack Burhani nao walitambulishwa sambamba na wanamuziki, Rogart Hegga 'Catapillar', Saulo Ferguson, Hosea Mgohachi na God Kanuti waliokuwa Twanga Pepeta.
wanamuziki hao walitambulishwa kwa waandishi wa habai jana na Mkurugenzi wa bendi hiyo ya Extra Bongo, Ally Choki 'Kamarade'.

No comments:

Post a Comment