![]() |
| Wachezaji wa Argentina wakipongeza kwa kuinyoa Hong Kong mabao 7-0 |
Ever Banega alianza kuiandika wageni bao dakika ya 19 kabla Gonzalo Higuan kuongeza la pili katika dakika 42 kwa pasi ya Vangioni na Nicolas Gaitan kuongeza la tatu sekunde chache kabla ya mapumziko.
Kipindi cha pili Higuan alikianza kwa kuongeza bao la tatu dakika ya 54 akimalizia kazi ya Gaitan na baada ya Messi kuingia dimbani aliongeza bao la tano dakika ya 66 kwa kazi nzuri ya Banega.
Gaitan hakutosheka kwa kufunga bao jingine lililokuwa la sita kwa Wanafainali hao wa Kombe la Dunia kwenye dakika ya 72 na Messi kuongeza bao la mwisho dakika sita kabla a filimbi ya mwisho.





TIMU ya soka ya taifa ya Morocco imeendelea kutoa dozi kwa wapinzani kwenye mechi za kirafiki baada ya usiku wa jana kuikong'ota Kenya Harambee Stars kwa mabao 3-0 ikiwa ni siku chache tangu iishindilie Jamhuri ya Afrika ya Kati kwa mabao 4-0 siku ya Ijumaa.
MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Luis Suarez amerejea uwanjani na makali yake yale baada ya usiku wa jana kuisaidia timu yake ya taifa ya Uruguay kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya wenyeji wao Oman.
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger, amesisitiza kwamba hajuti kumsajili Cesc Fabregas katika kipindi kilichopita cha usajili.