STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 14, 2014

Suarez arejea na mabao Uruguay, afunga mbili wakiiua Oman x3

http://level3.soccerladuma.net/cms2/image_manager/uploads/News/166456/7/default.jpgMSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Luis Suarez amerejea uwanjani na makali yake yale baada ya usiku wa jana kuisaidia timu yake ya taifa ya Uruguay kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya wenyeji wao Oman.
Pambano hilo la kimataifa la kirafiki lililochezwa kwenye uwanja wa Sultan Qoboos mjini Muscat, Suarez aliyekuwa akicheza mechi yake ya pili ya kimataifa tangu alipotoka kifungoni alifunga mabao mawili.
Suarez alifunga mabao hayo kwenye dakika ya 57 akimalizia kazi nzuri ya Rolan na katika dakika ya 67 kwa pasi ya Ramirez kabla ya Jonathan Rodriguez kufunga la tatu dakika ya 87.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool alifungiwa na FIFA kutokana na kitendo cha kumng'ata beki wa Italia, Giorgio Chiellini katika michuano ya Kombe la Dunia zilizochezwa nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment