STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 31, 2014

AC Milan yaitoa nishai Real Madrid Umangani

Ronaldo na El Shaarawy wakichuana
Beki wa Madrid Nacho akimdhiobiti mchezaji wa AC Milan
Karim Benzema akifunga bao la pili la Madrid kwa mkwaju wa penati
MSHAMBULIAJI Stephan El Shaarawy aliiwezesha timu yake ya AC Milan ya Italia kupata ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Mabingwa wa Ulaya, Real Madrid ya Hispania katika pambano la kimataifa la kirafiki lililochezwa mjini Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu.
El Shaarawy alifunga mabao mawili katika kipigo hicho kilichokuwa cha kwanza kwa vijana wa Carlo Ancelotti tangu Septemba na kuhitimisha 'ubabe' wa Madrid ambao walikuwa hawajapoteza mchezo wowote katika mechi 22 katika msimu huu.
Jeremy Menez wa Milan ndiye aliyeanza kufungua milango baada ya kufunga bao la kuongoza katika dakika ya 24 kabla ya El Shaarawy kuongeza goli la pili katika dakika 31 kwa shuti kali.
Dakika nne baadaye Madrid walifanikiwa kuchomoa bao moja kupitia kwa Mwanasoka Bora Duniani, Cristiano Ronaldo kufunga akiwa ndani ya 'boksi' akimtungua kipa  Diego Lopez na kuzifanya timu ziende mapumziko Milan wakiwa mbele kwa mabao 2-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na kushuhudiwa Milan wakiongeza bao la tatu dakika ya 49 kupitia tena kwa El Shaarawy kabla ya watokea benchi Giampaolo Pazzini na M'Baye Niang kushirikiana vyema na na Pazzini kuukwamisha mpira kimiani katika dakika ya 73 kuaindikia Milan bao la nne.
Real Madrid ilijipatia bao la pili la kujifutia machozi kupitia mshambuliaji wake wa Kifaransa Karim Benzema, aliyefunga bao kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 84.
Kwa ushindi huo AC Milan walikabidhiwa kombe lililopokewa na nahodha wake, Riccardo Montolivo.

KIPUTE CHA MAPINDUZI KUANZA KESHO, RATIBA HII HAPA

Kikosi cha Simba kitakachoanza kibarua cha Mapinduzi Cup dhidi ya Mtibwa Sugar usiku wa kesho
Mtibwa Sugar watakaivaa Simba kesho usiku katika Mapinduzi Cup
Yanga X1
Yanga safari hii imekubali kushiriki kamili gado
MSIMU mpya wa Michuano ya Kombe la Mapinduzi unatarajiwa kuanza rasmi kesho kwa michezo mitatu 'Mnyama' Simba akitarajiwa kushuka dimbani Usiku kuvaana na Mtibwa Sugar, huku Azam wakitarajiwa kuvaama na KCCA ya Uganda Ijumaa.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa ni kwamba kesho mechi ya kwanza itawakutanisha JKU na Mafunzo majira ya saa 9 alasiri kabla ya Polisi-ZNZ kuvaana na Shaba jioni.
Yanga ambayo imekuwa 'ikisumbua' ushiriki wake katika michuano hiyo safari hii imekubali kikamilifu kushiriki na wenyewe wataanza kibarua Jumamosi kwa kuvaana na Sports Club Villa ya Uganda.
Jumla ya makundi matatu yamegawanywa yakiwa na timu nne kila moja nayo ni;
Kundi A:  SC VILLA,  YANGA, POLISI,  SHABA.
Kundi B: KCCA,  AZAM,  KMKM na MTENDE.
Kundi C: SIMBA, MTIBWA, JKU, na MAFUNZO.
RATIBA KAMILI YA MAPINDUZI CUP IKO HIVI:
Alhamisi 1 Januari 2015:
Saa 9:00  JKU vs MAFUNZO.
Saa.11:00.  POLISI VS SHABA.
Saa 2:15.    SIMBA VS MTIBWA.

Ijumaa 2 Jan 2015 
Jioni saa 10:00  KMKM VS MTENDE              KUNDI        B
Usiku Saa 2:00 KCC VS AZAM.                        KUNDI       B

Jumamosi 3Jan 2015.
Jioni Saa 10:00 JKU VS MTIBWA                  KUNDI       C
Usiku Saa 2:00 YANGA VS SC.VILLA             KUNDI      A

Jumapili  4 Jan 2015                           
Jioni saa 9:00 KCC VS MTENDE                        KUNDI    B
Jioni saa 11:00 KMK VS AZAM.                          KUNDI    B 
Usiku saa 2:15. MAFUNZO VS SIMBA                KUNDI    C 

Jumatatu 5 Jan 2015                     
Jioni saa 10;00 SC VILLA VS SHABA               KUNDI    A
Usiku saa 2:00 YANGA VS POLISI                     KUNDI    A

Jumanne 6 Jan 2015
Jioni saa 9:00 AZAM VS MTENDE                   KUNDI     B
Jioni saa 11: 00  MTIBWA VS MAFUNZO        KUNDI     C 
Usiku saa 2:15. SIMBA VS JKU                           KUNDI    C

Jumatano 7 Jan 2015
Jioni saa 9;00  POLISI VS SC VILLA                KUNDI      A 
Jioni saa 11:00  KCC VS KMKM                         KUNDI     B
Usiku saa 2:15. YANGA VS SHABA                  KUNDI      A

Alhamisin 8 Jan 2015.
Jioni saa 10:00  WINNER B VS RUNNERS  A.
Usiku saa 2:00 WINNER  A VS BEST LOOSER 1

Ijumaa 9 Jan 2015
Jioni saa 11:00 WINNER C VS BEST LOOSER 2
Usiku saa 2;00 RUNNERS  B VS RUNNERS C.

Jumapili 11 Jan 2015.
SEMIFINAL 1 
Jioni saa 10:00. WINNER 1 VS WINNER 2
SEMIFANAL 2
Usiku saa 2:00  WINNER  3 VS WINNER 4
 Tarehe 13/1/2015 itakuwa fainali ya michuano hiyo itakayofanyika usiku katika uwanja wa amaan Zanzibar. kuhitimisha michuano hiyo.

Newz Alert! Mtuhumiwa wa Dawa za Kulevya apigwa risasi akitoroka


MTUHUMIWA wa kesi ya Dawa za Kulevya, anayedaiwa kuwa ni  raia wa Sierra Leone amepigwa risasi na kufariki katika harakati zake za kutaka kutoroka katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam.
Inadaiwa mtuhumiwa huyo Abdul Koroma alikuwa akitaka kuwaacha kwenye mataa askari Magereza kwa kuruka uzio kabla ya kuwahiwa kwa kupigwa risasi.
I





Bw' Misosi akifa hataki promo videoni

MSANII Joseph Rushahu 'Bwana Misosi' anajiandaa kurekodi video ya wimbo wake mpya uitwao 'Nikifa Sitaki Promo' ambao ameimba akishirikiana na waimbaji nyota wa muziki wa dansi Ramadhan Masanja 'Banzastone' na Athanas Montanabe wa  bendi ya Wana Extra.
Akizungumza kwa njia ya simu akiwa jijini Tanga alipoenda kwa mapumziko ya Sikukuu ya Mwaka Mpya, Misosi aliyetamba na nyimbo kama 'Nitoke Vipi', 'Mungu Yupo Bize' na 'Watoto wa Kitanga', alisema video ya wimbo huo alioutengenezwa katika studio za Plexity Records chini ya mtayarishaji aitwaye Zest inaanza kurekodiwa wiki ijayo akirejea jijini Dar es Salaam.
Misosi alisema alikwama kuitengeneza mapema video hiyo kutokana na pilikapilika za Krismasi na kuwepo nje ya jiji kwa waimbaji walioshirikiana kuutengeneza wimbo huo.
"Kwa sasa nipo Tanga na ninatarajiwa kurejea mwishoni mwa wiki ili kujipanga kuanza kutengeneza video ya wimbo wangu mpya," alisema.
Msanii huiyo alidokeza kuwa, mara baada ya kukamilika kurekodiwa kwa video hiyo ataiachia pamoja na 'audio' yake na alisema itakuwa ndani ya mwezi huu wa Januari.
"Haiwezi kuvuka mwezi huu kabla ya kazi hiyo mpya kutoka hadharani, nataka kuuanza mwaka nikiwa Misosi mpya," alisema.

Tuesday, December 30, 2014

Mwanasoka Bora Afrika kujulikana Januari 8 nchini Nigeria

http://www.football-marketing.com/wp-content/uploads/2012/01/PUMA-Yaya-Toure.jpg
Yaya Toure
SHIRIKISHO la Soka Afrika, CAF linatarajia kutoa tuzo kwa Wachezaji Bora kwa mwaka huu Januari 8 mjini Lagos Nigeria.
Kiungo wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, golikipa Vincent Enyeama wa Nigeria na kiungo Yaya Toure mmojawao ndiye atakayetwaa tuzo ya mwaka ya Mwanasoka Bora wa Afrika.

Mbali na hao pia wachezaji wengine watatu watachuana kwenye tuzo ya Mwanasoka Bora kwa wachezaji wa ndani ya Afrika
Wachezaji wanaowania tuzo hiyo ambayo ilikuwa ikishirikiliwa na Mohammed Aboutrika wa Misri ni;
Akram Djahnit (Algeria) El Hedi Belamieri( Algeria)Firmin Mubele Ndombe (DR Congo)
Kwa upande wa wanasoka wawanawake wanaowania tuzo hizo ni;
Annette Ngo Ndom (Cameroon) Asisat Oshoala (Nigeria) Desire Oparanozie (Nigeria)
Upande wa wanasoka chipukizi tuzo hiyo inawaniwa na Asisat Oshoala (Nigeria) Fabrice Ondoa (Cameroon),Uchechi Sunday (Nigeria)
Wanaowania tuzo ya kipaji kinachochipukia ni
Clinton N’jie (Cameroon) Vincent Aboubakar (Cameroon) Yacine Brahimi (Algeria)
Makocha wanaowania tuzo hizo za CAF ni;

Florent Ibenge (DR Congo) Kheireddine Madoui (ES Setif) Vahid Halilhodžić (kocha wa zamani wa Algeria)
Timu Bora ya Mwaka tuzo yake inawaniwa na; Algeria, Libya, Nigeria
Timu Bora ya Wanawake ya Mwaka ni;
Cameroon, Nigeria, Nigeria U-20
Klabu bora ya Mwaka
Al Ahly (Egypt) AS Vita (DR Congo) ES Setif (Algeria)
Huku Rais wa Tp Mazembe Moise Katumbi Chapwe akitarajiwa kupewa tuzo ya kiongozi bora wa michezo wa mwaka.

Real Madrid yasisitiza Gareth Bale HAUZWI kokote!

Bale celebrates winning the FIFA Club World Cup earlier in December 
Gareth Bale
RAIS wa klabu ya Real Madrid, Florentino Perez amesisitiza kuwa Gareth Bale hauzwi na kuzitaja taarifa kwamba amepokea ofa kutoka Manchester United ni upuuzi mtupu.
Bale, aliyejiunga na Real Madrid akitokea Tottenham kwa dau lililovunja rekodi ya uhamisho duniani ya karibu Pauni Mil. 85 Septemba 2013 amekuwa akidaiwa kuwa yu mbioni kurejea tena Ligi Kuu ya England.
United imedaiwa kuwa tayari kutoa Pauni 120 ili kumnyakua nyota huyo wa kimataifa wa Wales, lakini Perez amepuuza taarifa hizo na kudai Bale, 25 hawezi kuondoka Santiago Bernabeu.
Perez aliliambia gazeti la michezo la Marca: "Hatujapokea ofa yoyote kuhusu Gareth Bale, siyo klabu ya Manchester United wala klabu nyingine yoyote.,"
"Kadhalika hatutakuwa tayari kusikilizia ofa yoyote juu ya Bale kwani ni mchezaji muhimu mno kwetu," alisema Perez.
Bale amekuwa na wakati mzuri tangu ajiunge na kigogo hicho cha Hispania akiunda safu kali ya ushambuliaji akishirikiana na  Cristiano Ronaldo na Karim Benzema.
Nyota huyo wa zamani wa Southampton aliisaidia Real Madrid kunyakua taji la 10 la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuwafumua wapinzani wao wa Madrid, Atletico Madrid kwa mabao 4-1 katika fainali iliyozikutanisha timu hasimu za jiji moja.

Crsitiano Ronaldo kidume 2014, atwaa tuzo nyingine


MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo amemaliza mwaka kwa staili ya aina yake kwa kubeba tuzo nyingine ya mchezaji bora wa mwaka au Globe Soccer Awards huko Dubai.
Mreno huyo amekuwa na mwaka mzuri huku akivunja rekodi kwa kuwa na mabao mengi katika msimu mmoja wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati alipoiongoza Real Madrid kunyakuwa taji lake la 10 la michuano hiyo.
Ronaldo pia anapewa nafasi kubwa ya kushinda tuzo ya Ballon d’Or inayotolewa na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kwa mara ya pili mfululizo Januari 12 mwakani licha ya kukabiliwa na upinzani kutoka kwa Lionel Messi na Manuel Neuer alioingia nao kwenye 3 Bora ya tuzo hiyo.
Mchezaji huyo ambaye alikuwepo mwenyewe kupokea tuzo hiyo katika sherehe zilizofanyika katika Hotel ya Atlantis Palm aliwashukuru mashabiki, wachezaji wenzake na viongozi wa Real Madrid kwa ushirikiano wanaompa na kufanya kupata mafanikio hayo.
Aidhsa kocha wa Madrid Carlo Ancelotti naye alitunukiwa tuzo hiyo kama kocha wa bora wa mwaka kutokana na mafanikio aliyoipa timu hiyo kwa mwaka huu

BABY MADAHA ANAKUJA NA SAINT & GHOST

http://api.ning.com/files/KtF8hZpsH-3lMXDW7ufVoIr4iNPkkwwMRNxku*jb0MDMU7Iz*sLL7Hfl9BdoYxrd9FpJEMbPW8DsGjHTHEQX05k1rl-IZhsZ/babymadaha.jpg
Baby Madaha
BAADA ya kutuymia muda mrefu akiwa amejichimbia Kenya kufanya shughuli zake za muziki, mwanadada Baby Madaha anajiandaa kuvunja ukimya kwenye soko la filamu kwa kuibuka na 'Saint & Ghost'  ambayo imesheheni nyota mbalimbali wa filamu nchini.
Akizungumza na MICHARAZO mapema leo, Baby Madaha alisema filamu hiyo inayotengenezwa kupitia kampuni yake, iitwayo Darkangel Film Production and Entertainment imewashirikisha wakali kama Kulwa Kikumba 'Dude', yeye (Baby Madaha), Hidaya Njaidi,  Grace Mapunda 'Mama Kawele', Ramadhani Ally 'Tafu', Ahmed Olotu 'Mzee Chillo' na wengine.
"Nimbo chimbo kwa sasa natengeneza filamu yangu iitwayo 'Saint and Ghost' ambayo naitengeneza kupitia kampuni yangu na inawashirikisha wasanii mbalimbali nyota nikiwamo mimi mwenyewe, Mzee Chillo, Mama Kawele, Mama Njaidi, Taffu, Dude na wengine na ni bonge la kazi la kuanzia mwaka 2015," alisema Baby Madaha.
Mwanadada huyo anayetamba na nyimbo kama 'Summer Holiday' akiwa na albamu mbili sokoni za Amore na Desperado' amejipatia umaarufu mkubwa katika uigizaji wa filamu baadhi ya kazi alizowahi kuzicheza ni 'Nani', 'Misukosuko3', 'Mpishi', House Na.44' na 'Ray of Hope' iliyoshinda tuzo ya kimataifa nchini Nigeria.

DECEMBER LIKIZO FESTIVAL KUFANYIKA KESHO MBEZI BEACH

TAMASHA la tatu la December Likizo Festival linatarajiwa kufanyika kesho jijini Dar es Salaam likihusisha na maonyesho ya muziki, mavazi na filamu sambamba na semina mbalimbali juu ya kuboresha ufanisi wa vipaji vya sanaa.
Mratibu wa tamasha hilo, Steven Sandhu 'Triple S',  alisema kwa wiki nzima kumekuwa na shughuli mbalimbali za tamasha hilo na leo ndiyo kilele chake.
Sandhu ambaye ni mwanamitindo na muigizaji filamu alisema kilele cha tamasha (le grand Finale) la mwaka huu litafanyika kwenye hoteli ya Landmark iliyopo Mbezi Beach.
"Tamasha la tatu la 'December Likizo Festival kwa mwaka wa 2014 litafikia kilele kesho kwenye Landmark Hotel kwa maonyesho mbalimbali na kwa wiki nzima kuelekea kilele cga tamasha hilo kulikuwa na shughuli mbalimbali," alisema.
Sandhu alisema anashukuru uitikiaji wa wito kwa wasanii na washiriki wengine wa tamasha hilo na kuongeza imani yake kama ilivyokuwa kwa matamasha mawili ya nyuma ya mwaka 2012 na 2013, hata la mwaka 2014 litafana zaidi," alisema.

KWA MASHABIKI WA WENGE MUSICA BCBG

Liverpool yaendelea 'maajabu' EPL, yaifumua Swansea City 4-1

The 26-year-old is mobbed by his Liverpool team-mates after helping his side towards a vital three points at Anfield
Liverpool wakishangilia mabao yao
Moreno now has two Premier League goals to his name since joining Liverpool from Sevilla in the summer
Moreno akishangilia bao la kuongoza la Livwerpool
Reds midfielder Lallana runs towards the Kop in celebration of his second half goal
Adam Lallana akishangilia moja ya mabao yake mawili
Three Swansea players look on as Lallana sends a left-footed finish past Fabianski to send Liverpool into a commanding lead
Lallana akiwatesa mabeki wa Swansea
MABAO mawili yaliyofungwa na Adam Lallana na moja la kujifunga la beki wa Swansea City imeiwezesha Liverpool kupata ushindi wake wa pili mfululizo katika Ligi Kuu ya England.
Ikiwa kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Anfield, Liverpool ilianza pambano hilo kwa mashambulizi langoni mwa wageni wao na kuandika bao la kwanza katika dakika ya 33 kupitia kwa Alberto Moreno aliyemalizia kazi ya Henderson.
Kipindi cha pili kilikuwa na mafanikio zaidi kwa vijana wa Branden Rodgers baada ya Lallana kuandika bao la pili dakika ya 51 kabla ya Swansea kuandikisha bao lao pekee dakika moja baadaye kupitia Gief Sigurdsson.
Adam Lallana alirudi tena kambani kwa kuandika bao la tatu la Liverpool dakika ya 61 na dakika tano baadaye beki wa Swansea City, Shelvey alijifunga katika harakati za kuokoa mpira na kuifanya Liverpool kupaata ushindi mnono wa mabao 4-1 na kuchupa hadi nafasi ya nane katika msimamo wa ligi hiyo.
Liverpool wamefikisha pointi 28 sawa na Swansea lakini imefanikiwa kuwashusha wapinzani wao kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Ushindi huo wa Liverpool wa mabao manne ni wa kwanza tangu nyota wao, Lusi Suarez kutimkia Barcelona.

Kumekucha! Patrick Phiri atimuliwa Simba, Kopunonic amrithi

Patrick Phiri (kushoto) aliyetimuliwa Simba wiki kadhaa baada ya Yanga kumtimua Marcio Maximo
http://umwungeri.com/wp-content/uploads/2014/09/1331248128Goran-Kopunovic.jpg
Kocha mpya wa Simba, Goran Kopunovic
BAADA ya Yanga kumtimua kocha wao Marcio Maximo kutokana na kipigo cha mechi yao na mtani wao Simba kwenye mechi ya 'bonanza' ya Nani Mtani Jembe2, Simba nao wamefuata mkumbo huo baada ya kutangaza kumtimua kocha wao Mzambia, Patrick Phiri.
Simba imemfukuza kocha huyo kutokana na kutoridhishwa na matokeo iliyopata timu yao katika msimu huu ikiwamo kipigo cha bao 1-0 ilichopewa na Kagera Sugar mwishoni mwa wiki.
Kocha huyo aliyemrithi Zdravkov Logarusic aliyetimuliwa mapema amekuwa hana matokeo mazuri tangu ajiunge na timu hiyo August mwaka huu.
Hii ni mara ya tatu kwa Phiri kuifundisha Simba tangu ajiunge na timu hiyo August mwaka huu ameiongoza katika michezo 22 na kushinda nane, kati ya hizo ni moja tu ya Ligi Kuu na moja ya Nani Mtani Jembe.
Aidha taarifa zinasema kuwa Mserbia Goran Kopunovic kutoka Polisi Rwanda ndiye atakayeinoa Simba na kocha huyo atawasili kesho Jumatano.
Kocha huyo mpya aliyewahi kuzinoa timu za APR atakuja na msaidizi wake Mnyarwanda Jean Marie Ntagawabila na kumaanisha kuwa hata kocha msaidizi wa Simba aliyekuwa na Phiri, Suleiman Matola naye ameenda na maji katika maamuzi yaliyofikiwa na uongozi wa juu wa Simba.
Simba na Yanga kwa muda mrefu sasa zimekuwa na utamaduni wa kutimua na kuajiri makocha wapya kila mara bila kujali vipindi wanavyokuwa na timu zao, jambo ambalo linadaiwa limekuwa likiwachanganya wachezaji kwa kushindwa kunasa mafunzo ya makocha wanaoletwa na kabla ya kuzoeana nao hutimuliwa.
Bahati mbaya ni kwamba klabu hizo zimekuwa zikitimua makocha hata wakati timu zao zikiwa katika nafasi nzuri tofauti na inavyoshuhudiwa Ulaya klabu zikiwatimua makocha kutokana na timu kufanya vibaya.

Sunday, December 28, 2014

Chelsea chupuchupu, yalazimisha sare ugenini

Sadio Mane  akishangilia bao la Southampton
Eden Hazard akishangilia bao la kusawazisha la Chelsea
VINARA wa Ligi Kuu ya England, Chelsea imeponea chupuchupu leo ugenini baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya Southampton katika pambano lililomalizika muda mfupi uliopita.
Southampton waliwakaribisha Chelsea katika uwanja wa St Mary kwa bao la mapema la dakika ya 17 kupitia kwa Sadio Mane kabla ya Chelsea kuchomoa dakika chache kabla ya mapumziko kupitia kwa Eden Hazard akimalizia kazi nzuri ya Cesc Fabregas.
Southampton ilijikuta ikicheza pungufu baada ya Morgan Schneiderlin kuonyesha kadi nyekundu dakika chache kabla ya kumalizika kwa pambano hilo

Kwa sare hiyo Chelsea wameendelea kung'ang'ania kileleni wakiwa na pointi 46, baada ya mechi 19 na kwa sasa mechi nyingine zinaendelea ambapo Manchester City wanaoongoza mabao 2-1 dhidi ya Burnley huku Arsenal ikiwa ugenini inaoongoza kwa mabao 2-1 dhidi ya West Ham United.

Kavumbagu afufuka Taifa, Ndanda majanga

Ndanda Fc waliporomoka hadi mkiani katika msimamo wa Ligi ikiuaga 2014 na kukaribisha 2015
Didier Kavumbagu akishangilia moja ya mabao yake na wachezaji wenzake Himid Mao na Aggrey Morris
BAO la kuongoza la Azam limemzindua Didier Kavumbagu ambaye alikuwa hajafunga muda mrefu kuwakimbia washambuliaji wenzake na kuongoza msimamo wa orodha ya wafungaji bora katika Ligi Kuu Tanzania Bara, huku Amissi Tambwe akifungua akaunti ya mabao Jangwani.
Didier alifunga bao la kuongoza la Azam leo na kumfanya kufikisha mabao matano na kuongoza orodha ya wakali wa mabao wakati ligi kuu ikimaliza mwaka 2014 na kusubiri kuendelea tena mwakani.
Simon Msuva aliyefunga bao la pili la Yanga naye ameingia kwenye orodha ya wakali wa mabao akiwa na mabao manne akilingana na wachezaji wengine, Danny Mrwanda wa Yanga, Rama Salim (Coastal Union), na Ame Ally (Mtibwa)
Ligi ikiaga mwaka 2014, Mtibwa ipo kileleni, huku Ndanda ikiachiwa nafasi ya mkiani na Mbeya City waliowanyuka bao 1-0 leo jijini Mbeya.
Ndanda inazibeba timu zote ikiwa na pointi sita, wakati Mbeya City kwa ushindi wa leo imechupa hadiu nafasi ya 12.
Msimamo kamili wa ligi hiyo baada ya kumalizika kwa mechi za raundi nane ni kama ifuatavyo;
                                          P   W    D    L    F    A   GD   Pts
 01. Mtibwa Sugar              08  04   04   00  11  04   07   16
02. Yanga                          08  04   02   02   11  07  04   14
03.  Azam                          08  04   02   02   10  06  04   14
04.  Kagera Sugar             08   03   04   01   07  04  03   13
05.  Coastal Union             08   03   03   02   09  07  02  12
06.  Polisi Moro                 08   03   03   02   08  07  01  12
06. JKT Ruvu                    08   03   01   04   07   08  -1  10
07. Ruvu Shooting             08   03   01   04   05   07  -2   10
08.Stand Utd                     08  02   04    02   06   10  -4  10
09.Simba                           08  01   06    01   07   07  00  09
09. Mgambo JKT              08  03   00    05   04   09  -5  09
12. Mbeya City                 08   02  02     04  03   06   -3  08
13. Prisons                        08   01  04     03  06   07   -1  07
14. Ndanda Fc                  08   02  00     06  08   13   -5  06
Wafungaji Bora:
5-
Didier Kavumbagu (Azam)
4-
Rama Salim (Coastal), Danny Mrwanda, Simon Msuva (Yanga) Ame Ally (Mtibwa)
3-
Ally Shomari, Emmanuel Okwi (Simba), Rashid Mandawa (Kagera Sugar)
2- Shaaban Kisiga, (Simba), Nassor Kapama (Ndanda) Salum Kanoni (Kagera), Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Samuel Kamuntu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Heri Mohammed (Stand Utd), Ally Nassor (Mgambo),  Malimi Busungu (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi)
Mechi zijazo;
Jan 03, 2014
Coastal Union vs  JKT Ruvu
Ruvu Shooting vs Kagera Sugar
Azam vs Mtibwa Sugar
Stand United vs Polisi Moro
Mbeya City  vs  Yanga

Jan 4, 2015
Mgambo JKT vs  Simba 
Prisons vs  Ndanda

Salha wa Hammer bado aota albamu na mumewe

Salha Abdallah
Salha Abdallah na mumewe, Hammer Q
MUIMBAJI mahiri wa taarab nchini  Salha Abdallah 'Salha wa Hammer' amesema licha ya kurejea kwenye muziki wa makundi, bado ataendelea kushirikiana na mumewe kutengeneza kazi zao binafsi.
Salha aliyejiunga na kundi la Five Star akitokea kwenye likizo ya uzazi alisema kuwa, bado mipango ya kutengeneza albamu ya pamoja na mumewe ipo pale pale japo anaendelea kupiga mzigo kazini kwake.
Muimbaji huyo wa zamani wa Dar Modern na aliyekuwa akilifanyia kazi King' s Modern kabla ya kwenda likizo ya uzazi, alisema kurejea kwake kwenye makundi hakuna maana kumemzuia mipango yake.
"Sidhani kama kurejea kwangu kuiimbia makundi kutanizuia kuendelea na mipango yangu na mwenza wangu kutengeneza albamu, nitaendelea nayo," alisema.
Wanandoa wao walishaachia nyimbo za 'Tunapendana' na 'Safiri Salama' na walikuwa katika mipangop ya kukamilisha nyimbo nyingine kuhitimisha albamu yao kabla ya Salha kupata likizo ya uzazi.

Yanga, Azam zashindwa kuing'oa Mtibwa kileleni

* Polisi Moroyainyoa Mgambo 2-0

* Mbeya City yainyuka Ndanda yatoka mkiani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiAlMSPylEzSarQeuwwxyvNic_FNhlU19qeAA0EqwEaeUv1t-irJyFqy0V0_v8zrKZbJJdoMwCFE5b149rj0rIQcHnDevbJMxeVokPk2AwVXIKKPKX00ASKmUQx9uhG9mEvfVkMRearhBAY/s1600/MMGM0086.jpg
Tambwe akifunga bao la kusawazisha la Yanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEieDhjSKUVk9dX5N494jFduosY7ZFKOiVRmL8lP6r3tS5FTyWBr_UVM062dtfJ9CzIm7b6k-rF8mFuk1GIHUvDm31hrHjWbaXr9adVoguy1hWXrYO8F-dcO2dr_sCLCpOFyEbG3txDHeRPf/s1600/MMGM0090.jpg
Tambwe akishangilia bao lake sambamba na Simon Msuva ambaye pia aliifungia Yanga bao la pili
Azam wakishangilia bao lao la kwanza dhidi ya Yanga leo kwenye uwanja wa Taifa
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2014/08/Mbeya-City.jpgPAMBANO la kukata na shoka baina ya Yanga na Azam limemalizika matokeo yakiwa ni yale yale ya mabao 2-2 na kuendelea kuwa nyuma ya Mtibwa Sugar wanaoongoza msimamo.
Yanga walikuwa 'nyumbani' walitanguliwa kufungwa bao dakika ya tano na Didier Kavumbagu baada ya mabeki wa Yanga kuchanganyana na kipa wao Deo Munishi 'Dida' na kumpa nafasi nyota huyo wa zamani wa Jangwani kukwamisha bao kirahisi.
Yanga walicharuka dakika mbili baadaye Amissi Tambwe aliisawazishia Yanga bao baada ya kuunganisha mpira wa krosi iliyopigwa na kiungo Salum Telela na kufanya matokeo yadumu hivyo hadi mapumziko.
Yanga iliingia kipindi cha pili wakiwa wamecharuka na kuandika bao la pili dakika ya 52 kupitia Simon Msuva aliyeunganisha kwa kichwa bao lililotokana na pasi murua ya Haruna Niyonzima aliyeshirikiana vema awali na Kpah Sean Sherman aliyeonekana tishio langoni  mwa Azam muda wote wa mchezo huo.
Hata hivyo nahodha John Bocco aliyekuwa akitokea benchi mpira wake wa kwanza kuugusa uwanjani ulizaa bao la kusawazisha la Azam baada ya mabeki wa Yanga kujichanganya tena na mchezaji huyo aliyekuwa majeruhi kufunga kirahisi kwa kichwa mpira wa krosi ya Himid Mao dakika ya 65.
Kwa matokeo hayo Yanga imeendelea kung'ang'ania nafasi ya pili nyuma ya Mtibwa ikiwa na pointi 14 sawa na zile za Azam isipokuwa wanatofautiana mabao ya kufunga na kufungwa.
Matokeo ya mechi nyingine Polisi Moro imeifyatua Mgambo JKT ya Tanga kwa mabao 2-0, mabao katika pambano hilo yalifungwa na Nicolaus Kibopile katika dakika ya 21 na Imani Mapunfda aliyekwamisha bao la ushindi dakika ya 85, huku Mbeya City ikipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Ndanda Fc ya Mtwara na hivyo kutoka mkiani mwa msimamo wa ligi hiyo.

Diamond tena, atwaa tuzo Nigeria, Vee Money naye ang'ara

Vee Monye akiwa na tuzo yake
Peter Msechu akiwa na tuzo ya Diamond
NYOTA ya Supastaa wa Bongo, Diamond Platnumz imeendelea kung'ara baada ya usiku wa jana kunyakua tuzo nyingine ya AFRIMA 2014 nchini Nigeria, sambamba na mwanadada Vanessa Mdee 'Vee Money'.
Wasanii hao wametwaa tuzo hizo kupitia vipengele vya Wasanii Bora wa Afrika Mashariki, Diamond akinyakua kwa upande wa kiume na Vee Money kwa upande wa wasanii wa kike.
Tuzo hizo za AFRIMA zilizofanyika huko jijini Lagos nchini Nigeria, ambapo msanii mwingine wa Tanzania aliyekuwa akiwania tuzo hizo sambamba na Diamond ni Peter Msechu ambaye alimpokelea Diamond Tuzo yake.
Hiyo ilikuwa ni tuzo ya 13 kwa mwaka 2014 kwa Diamond baada ya awali kunyakua tuzo saba kwa mpigo katika Kili Music, kisha AFRIMMA, akafuatia na tatu za CHAOMVA na kumalizia ya The Future aliyotwa nchini Nigeria mara baada ya kutoka Afrika Kusini kunyakua tuzo tatu.
Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win
Vanessa Mdee akiwa na tuzo yake ya Best Female Artist in East Africa. Peter Msechu akiwa amebeba tuzo kwa niaba ya Diamond Platnumz. Peter Msechu, Vanessa Mdee na Victoria Kimani katika pozi huko Lagos, Nigeria. MWANAMUZIKI Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' usiku wa kuamkia leo ametwaa tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Kiume Afrika Mashariki (Best Male Artist in East Africa) kutoka Tuzo za 2014 AFRIMA zilizofanyika huko jijini Lagos nchini Nigeria. Mwanadada Vanessa Mdee yeye ameshinda tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Kike Afrika Mashariki (Best Female Artist in East Africa). Tuzo ya Diamond imepokelewa na mwanamuziki Peter Msechu aliyekuwepo katika zoezi hilo la utoaji tuzo maana na yeye alikuwa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania tuzo hizo

Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win

Mtibwa Sugar yaendeleza rekodi Ligi ya Bara

* Ruvu Shooting yaizamisha JKT Ruvu

* Yanga, Azam zashikana mashati Taifa

* Mpaka sasa mabao 2-2

Mtibwa Sugar
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiyEobPE20ZtNi1R-UopKnA1am4dMWYZsa7756AEyfSHcvOosRNMAP-efMmHJrvyF7Ow87HahcM35Mc0PHS1WKnJYrQVgpIPDUG7wM0AXLdLATZWM_FgJbvsrDo8w3YZiZ3RL3zmCrX9Dff/s640/DSC_0125.JPG
JKT Ruvu waliochezea kichapo usiku wa jana kwa Ruvu Shooting
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Mtibwa Sugar imeendeleza rekodi yake ya kuwa imu pekee ambayo haijapoteza mchezo wowote msimu huu, baada ya asubuhi ya leo kulazimisha sare ya bao 1-1 na Stand United baada ya mchezo huo kushindwa kuendelea kuchezwa jana sababu ya mvua kubwa.
Pambano hilo lilichezwa jana kwa dakika sita na kurudiwa leo asubuhi dakika zilizosalia kwa timu hizo kushindwa kutambiana kwenye uwanja wa Manungu, Turiani Morogoro.
Wageni Stand ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Shaaban Kondo aliyefunga katika dakika ya 22, kabla ya Mtibwa kusawazisha katika dakika ya lala salama kupitia beki wake Saidi Mkopi na kuifanya timu hiyo iendelee kukaa kileleni ikiwa na pointi 16 baada ya mechi nane, ingawa inaweza lkujikuta iking'oka kileleni kama Yanga inayoumana na Azam itapata ushindi katika mchezo wao.
Azam pia ina nafasi ya kukwea kileleni kama itaishinda Yanga kwa uwiano mzuri wa mabao, ingawa hadi sasa timu hizo zimefungana mabao 2-0.
Azam walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Didier Kavumbagu kabla ya Amissi Tambwe kusawazisha kwa kichwa dakika chjache baadaye na katika kipindi cha pili, Simon Msuva aliiongezea Yanga bao la pili dakika ya 53 kabla ya John Bocco kufunga bao la kusawazisha hivi punde.
Katika mechi nyingine ya jana ya ligi hiyo Ruvu Shooting iliendelea ubabe wake kwa JKT Ruvu baada ya kuichapa bao 1-0 katika mechi iliyochezwa usiku kwenye uwanja wa Chamazi.
Bao pekee la Ruvu liliwekwa kimiani kwa mkwaju wa penati na Hamis Kasanga na kuifanya timu hiyo kufiksiha pointi 10 na kulingana na 'ndugu zap hao wa JKT ila wanatofautiana kwa mabao ya kufunga nba kufungwa.

MBAO FC YAKAMATA USUKANI SDL

TIMU ya soka ya Mbao ya Mwanza imekamata uongozi wa Kundi B la michuano ya Ligi Daraja la Pili (SDL) baada ya jana (Desemba 27 mwaka huu) kuizamisha JKT Rwamkoma ya Mara mabao 2-1.
Kwa matokeo hayo katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mbao FC imeitoa kileleni JKT Rwamkoma baada ya kufikisha pointi tisa kwa kushinda mechi zote tatu dhidi ya Arusha FC, Pamba na JKT Rwamkoma.
Mbao FC inafuatiwa na JKT Rwamkoma yenye pointi sita, Arusha FC pointi sita wakati Bulyanhulu na Pamba zikiwa za mwisho kwa pointi moja kila moja. Kundi hilo litakamilisha mzunguko wa kwanza Januari 3 mwakani kwa mechi kati ya JKT Rwamkoma na Arusha FC, na Bulyanhulu na Mbao FC.
Katika kundi A, Mji Mkuu (CDA) na Singida United ndizo zinazochuana kileleni kwa kufikisha pointi saba kila moja.
Timu hizo zinafuatiwa na Milambo yenye pointi nne, Mvuvumwa FC yenye pointi moja wakati Ujenzi Rukwa ni ya mwisho ikiwa haina pointi.
Hata hivyo, Mvuvumwa FC na Milambo ziko nyuma kwa mechi moja. Mechi hiyo ya kukamilisha raundi ya tatu kati ya timu hizo itachezwa kesho (Desemba 29 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.
Kiluvya United imeendelea kuchachafya kundi C baada ya kushinda mechi zote ne ilizocheza, hivyo kufikisha pointi 12. Inafuatiwa na Mshikamano yenye pointi saba huku Abajalo ikiwa katika nafasi ya tatu kwa pointi 6.
Nafasi ya nne inashikwa na Transit Camp yenye pointi nne, Cosmopolitan yenye pointi mbili ni ya tano wakati Kariakoo ambayo haina pointi ni ya mwisho. Hata hivyo, Cosmopolitan na Kariakoo zina mchezo mmoja mkononi.
Mechi zinazofuata za kundi hilo ni Januari 3 mwakani kati ya Kariakoo na Mshikamano na Mshikamano (Ilulu), Transit Camp na Abajalo (Mabatini), na Cosmopolitan na Kiluvya (Karume).
Kundi D, vinara bado ni Njombe Mji yenye pointi 12 ikifuatiwa na Wenda yenye pointi sita wakati Volcano FC iko nafasi ya tatu ikiwa na pointi tano. Mkamba Rangers ina pointi nne, Town Small Boys ina pointi moja wakati Magereza FC haina pointi.
Katika kundi hilo leo (Desemba 28 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Town Small Boys na Magereza itakayochezwa Uwanja wa Majimaji mjini Songea.  Januari 3 mwakani kutakuwa na mechi kati ya Town Small Boys na Njombe Mji, Volcano FC na Magereza, na Wenda na Mkamba Rangers.

Hakuna kama Lionel Messi-Pedro

http://images.latinpost.com/data/images/full/11964/lionel-messi.jpgMSHAMBULIAJI wa klabu ya Barcelona, Pedro amedai kuwa mchezaji mwenzake Lionel Messi ndiyo mchezaji bora kuliko yeyote duniani na anastahili kushinda tuzo ya Ballon d’Or mbele ya Cristiano Ronaldo. Messi amewahi kushinda tuzo hiyo kwa mara nne mfululizo kabla ya Ronaldo kuingilia kati na kunyakua tuzo hiyo mwaka jana ikiwa ni mara ya pili kwa upande wake.
Baada ya kuisaidia Real Madrid kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la Mfalme mwaka huu, Ronaldo ndiye anayepewa nafasi kubwa zaidi ya kunyakuwa tuzo hiyo katika sherehe zitakazofanyika Januari 12 mwakani.
Mafanikio makubwa aliyopata Messi kwa mwaka huu ni kuiongoza timu yake ya taifa ya Argentina kucheza fainali ya Kombe la Dunia nchini Brazil wakati golikipa wa Bayern Munich Manuel Neuer yeye ni mchezaji mwingine wa tatu aliyeyopo katika orodha hiyo.
Pamoja na kutopewa nafasi mwaka huu, Pedro anaamini kuwa hakuna mchezaji yeyote katika sayari hii anayeweza kumfikia Messi katika ubora wake uwanjani.

Tottenham Hotspur yaisimamisha Manchester United

Harry Kane tries to get away from Manchester United defender Paddy McNair as both sides looked to protect their recent unbeaten records
Harry Kane kimtoka beki wa Manchester United
Hugo Lloris makes himself big to deny Robin van Persie as United spurned several great chances in a goalless first half
Van Persie akikosa bao la wazi
Juan Mata sees his free kick deflected off the Tottenham wall and onto Hugo Lloris' post, resulting in a goalmouth scramble
Juan Mata akikosa bao la wazi langoni mwa Spurs
KLABU ya Tottenham Hotspur ikiwa uwanja wa nyumbani wa White Hartlane imeibana Manchester United na kwenda nao suluhu katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu ya England mchezo uliomalizika hivi punde.
Pamoja na kosa kosa nyingi katika kipindi cha kwanza, Manchester imeshindwa kuendeleza wimbi lake la ushindi na kuambulia pointi moja ugenini na kuifanya timu hiyo iendelee kukalia nafasi ya tatu.
Mashetani Wekundu walikosa mabao mengi ya wazi na kukosa makali kwenye kipindi cha pili na kufanya mechi hiyo iishe kwa timu hizo kutofungana na na kuifanya Spurs kufikisha pointi 31 na kuitambuka Arsenal wakati Mashetani Wekundu wamefikisha pointi 36.
Pambano linaloendelea kwa sasa ni lile la 'vinara' Chelsea iliyopo ugenini dhidi ya Southampton.

Kama Ustaadh, mcheki Cristiano Ronaldo katika vazi takatifu


Cristiano Ronaldo akiwa kwenye mavazi ya kiislam akipiga picha na mashabiki huko Dubai.

NYOTA wa klabu ya Real Madrid ya Hispania na timu ya taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo alionekana na kupigwa picha na mapaparazi kwenye matembezi yake binafsi Dubai akiwa amevalia mavazi ya Kiislam na yaliompendeza sana.

Cristiano Ronaldo ambaye yeye si Muislam, alionekana kupendeza kupita kiasi katika vazi hilona alidai alipendezwa na uvaaji huo baada ya kuina watu wengi waishio Dubai katika vazi hilo kuu na kujihoji vipi naye asiwe miongoni mwa waliovaa vazi hilo. 
Pia hakuwahi kuvaa vazi la dini hiyo alionelea avae kwa ishara ya kuiheshimu dini hiyo na kuona sio kitu kibaya kuwa miongoni kwao kimavazi.

Cristiano Ronaldo akiwa kwenye vazi jingine la kiislamu huko Dubai

Mchezaji huyo alikuwa Dubai wiki iliyopita kwenye mapumziko yake binafsi mbali na shughuli za kimpira. Alienda kutembea huko kabla ya wiki ya sikukuu za Krismasi sambamba na mwanae aliyemvisha pia vazi hilo la kanzu.
Alionekana ni mwenye kufurahishwa na mandhali ya mji huo pia utamaduni wao wa chakula pia kimavazi ndio mana nae alipendezwa kuvaa kama wao.

Vazi lingine alilovaa mchezaji Cristiano Ronaldo akiwa kwenye matembezi yake binafsi Dubai.

Mchezaji huyo alikaa Dubai kwa siku nne wiki iliyopita na baadae aliondoka kurejea Hispania ambapo alijiunga na wachezaji wenzake kwenye kambi ya maandalizi ya mechi zilizoendelea katika ligi ya nchi hiyo anakochezea.

Thursday, December 25, 2014

Ruvu Shooting yaanza tambo kisha Betram Mwombeki

KLABU ya Ruvu Shooting imetamba kuwa imelamba dume kwa kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Simba, Betram Mwombeki na kudai timu pinzania zijiandae kukabiliana naye kutokana na uwezo mkubwa aliouonyesha kwenye mechi yao dhidi ya Mwadui ya Shinyanga.
Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire amesema kuwa kwa mara ya kwanza amemuona Mwombeki akiichezea Ruvu Shooting na kubaini kuwa ni mchezaji ambaye atawasaidia mno, baada ya kutoa pasi ya bao la kwanza na kufunga bao la pili timu hiyo ilipotoka sare ya mabao 2-2 na Mwadui kwenye uwanja wa Mabatini Mlandizi mkoani Pwani siku ya Jumatatu.
"Nashangaa kuna timu zilimuona hafai, huyu Mwombeki amecheza kwa kiwango cha hali ya juu, ametoa pasi ya bao la kwanza lililofungwa na Abdurahman Mussa na kutufungia bao la pili, kwa kweli huyu ameziba kabisa pengo la Elius Maguri," alisema Masau.
Amezitahadharisha timu zote zinazoshiriki Ligi Kuu kuwa zitakutana na moto wa Mombeki, kwani amerejea kwenye kiwango chake cha kawaida, akicheza kwa kutumia nguvu kama kawaida yake na kuachia mashuti makali.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba, alisajiliwa na Ruvu kwenye kipindi hiki cha dirisha dogo kwa ajili ya kuziba pengo la Maguri ambaye kwa sasa yuko Simba.
Mwombeki alivuma akiwa na Simba msimu uliopita chini ya kocha Abdallah Kibadeni, lakini hali ilikuwa ngumu kwake alipokuja kocha matata Zdravko Logarusic ambaye hakupendezwa na aina yake ya uchezaji, kiasi cha kumtupia virago.
Ruvu ambayo itaanza kibarua cha ngwe nyingine ya Ligi Kuu kwa kuumana na ndugu zao Ruvu Shooting siku ya Jumamosi, imewasajili pia wachezaji wengine akiwamo Yahya Tumbo nyota wa zamani wa Africans Lyon na Yanga.

Ukishangaa fedha za Tegeta Escrow utayaona ya Yanga Jangwani!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiMKxD1F7u6O8EspppaCk5UUX9XveRzSV5K6ThUlsHL7YtSo6HErtvL3Tfy7BuEdDRN50QMWIPv20EXlb3DyuFDLPYtZ2imcLeQ7bmJcmXfFHr1w9EGT-DdwwUiDDjfA2ZdMj0-pKCw5zI/s1600/07.JPGWAKATI watanzania wakiendelea kuweweseka na jinamizi la wizi wa fedha za akaunti ya Tegeta Escrow, imefahamika 'wizi' kama huo umetokea ndani ya klabu ya Yanga kwa kudaiwa kutafunwa kiasi cha zaidi ya SH. Bilioni 2.
Tayari inadaiwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Benno Njovu na mwanadada mmoja aliyekuwa akihusika na Idara ya Fedha klabu hapo wameshafunguliwa mashtaka kwa tuhuma hizo.
Hata hivyo Jeshi la Polisi limesita kutoa taarifa juu ya uwapo wa taarifa za ubadhirifu wa fedha hizo kiasi cha Sh. bilioni mbili katika Klabu ya Yanga ya jijini hapa.
Taarifa za ubadhirifu huo zimeitikisa Yanga huku baadhi ya waliokuwa watendaji wa klabu hiyo kufikishwa kwenye vyombo vya usalama kwa tuhuma za kutafuna kifisadi kiasi hicho cha fedha hizo.

Katibu Mkuu mpya wa Yanga, DK. Jonas Tiboroha amethibitisha kubainika kwa ubadhilifu wa fedha ingawa hakuwa tayari kutaja kiasi kamili kilichobainika kuchotwa kijanja na baadhi ya wafanyakazi wanaodaiwa kuwa ni wale waliomaliza muda wao katika klabu hiyo hivi karibuni.
Baadhi ya wafanyakazi wa zamani wakiongozwa na aliyekuwa katibu mkuu wa klabu hiyo, Beno Njovu na aliyekuwa mhasibu Rose Msamila, wamedaiwa kufikishwa kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Polisi (Central) mjini hapa jana kuhojiwa kuhusu ubadhirifu huo.
“Ni kweli kuna suala hilo, lakini siwezi kuliongelea zaidi ni kina nani hasa wanahusika na kiasi cha fedha kinachotajwa kwa sababu tayari suala hilo liko chini ya Jeshi la Polisi. Watakapomaliza uchunguzi wao, watatujuza na sisi (Yanga SC) tutaliweka wazi,” amesema Tiboroha.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova hakuwa tayari kulizungumzia suala hilo baada ya kutafutwa na mtandao huu mjini hapa leo akisema: “Muulize RPC Ilala.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Mary Nzuki amedai hana taarifa za kuhojiwa na Polisi kwa waliokuwa watendaji wa Yanga SC.
“Mimi nimefuatilia kwenye vituo vyetu mbalimbali lakini sijapewa taarifa kuhusu kuhojiwa kwa watu wa Yanga. Pengine suala hilo limefanywa na kitengo cha upelelezi, ngoja niwasiliane nao kupata ufafanuzi,” amesema kamanda huyo.
RPC huyo pia amekiri kuona picha mitandaoni zikiwaonesha baadhi ya waliokuwa viongozi wa Yanga SC wakiwa na Polisi.
“Waandishi wa habari wananiuliza sana kuhusu suala hilo, nimeona pia baadhi ya picha mitandaoni zikiwaonesha watendaji wa Yanga wakiwa na polisi lakini zijapata taarifa rasmi juu ya suala hilo,” amesema zaidi.
Baadaye jioni hii RPC huyo amesemaL “Tumeangalia kwenye mafaili yetu hatuna suala hilo Mkoa wa Ilala, labda kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (Ofisi ya Kova).”
Inadaiwa kuwa fedha zilitafunwa kijanja kupitia malipo ya kambi mjini Antalya, Uturuki, nauli za usafiri wa ndege wa baadhi ya nyota wa kigeni.
Mwishoni mwa wiki, Yanga ilimtangaza Tiboroha kuwa katibu mkuu wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Njovu. Mtangazaji wa zamani wa televisheni za ITV na TBC, Jerry Muro aliteuliwa kuwa Mkuu wa Habari na Mawasiliano, Omari Kaya aliteuliwa kuwa mkuu wa Idara ya Sheria ya klabu hiyo wakati Baraka Deusdetit aliteuliwa kuwa Mkuu wa Idara ya Fedha.
Muda mfupi baada ya uteuzi huo kumegundulika kulikuwa na kile kinacoelezwa kama ubadhirifu miongoni mwa watangulizi katika utendaji wa klabu hiyo ya Jangwani.

Alex Song atemwa Cameroon kuelekea Afcon 2015

http://c.smimg.net/14/25/alex-song-cameroon.jpgKOCHA wa timu ya taifa ya Cameroon, Volke Finke ametaja kikosi cha awali cha wachezaji 27 kwa ajili ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika itakayofanyika huko Guinea ya Ikweta. 
Kocha huyo raia wa Ujerumani ameteua wachezaji wengi waliokuwemo katika mechi za kufuzu, lakini amemuacha kiungo Alex Song. 
Song hajaichezea Cameroon toka alipotolewa nje kwa kadi nyekundu katika kipindi cha mabao 4-0 walichopata kutoka kwa Croatia katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil. 
Kiwango kizuri alichokionyesha msimu huu akiwa kwa mkopo katika klabu ya West Ham United akitokea Barcelona, kilizua tetesi kuwa angeweza kuitwa katika timu ya taifa. 
Cameroon wanatarajiwa kuanza maandalizi nyumbani na watacheza mechi ya kirafiki na Congo Brazzaville Januari 7 kabla ya kusafiri kwenda Gabon kwa ajili ya kambi yao nyingine na kucheza mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Afrika Kusini Januari 11.
Simba hao Wasiofugika wataanza kibarua chao katika michuano hiyo ya AFCON kama ratiba inavyoonesha hapo chini
20 Jan: v Mali in Malabo
24 Jan: v Guinea in Malabo
28 Jan: v Ivory Coast in Malabo
Kikosi kamili  kilichoteuliwa kabla ya kuchujwa baadaye ni hiki hapa;
Makipa: Joseph Ondoua (Barcelona, Spain), Guy Ndy Assembe (Nancy, France), Pierre Sylvain Abogo (Tonnerre Yaoundé)
Walinzi: Cédric Djeugoue (Coton Sport), Jérôme Guihi Ata (Valenciennes, France), Nicolas Nkoulou (Marseille, France), Ambroise Oyongo Bitolo (New York Red Bulls, USA), Brice Nlate Ekongolo (Marseille, France), Franck Bagnack (Barcelona, Spain), Henri Bedimo (Lyon, France),
Viungo: Stéphane Mbia (Seville, Spain), Enoh Eyong (Standard Liège, Belgium), Raoul Cedric Loe (CA Osasuna, Spain), Edgard Salli (Academica de Coimbra. Portugal), Georges Mandjeck (Kayseri Erciyesspor, Turkey), Franck Kom (Etoile du Sahel, Tunisia), Patrick Ekeng (FC Cordoba, Spain)
Washambuliaji: Eric-Maxim Choupo-Moting (Schalke 04, Germany), Benjamin Moukandjo (Reims, France), Jacques Zoua (Kayseri Erciyesspor, Turkey), Vincent Aboubakar (Porto, Portugal), Léonard Kwekeu (Caykur Rizespor, Turkey), Clinton N'Jie (Lyon, France), Franck Etoundi (Zurich, Switzerland)