STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 28, 2014

Hakuna kama Lionel Messi-Pedro

http://images.latinpost.com/data/images/full/11964/lionel-messi.jpgMSHAMBULIAJI wa klabu ya Barcelona, Pedro amedai kuwa mchezaji mwenzake Lionel Messi ndiyo mchezaji bora kuliko yeyote duniani na anastahili kushinda tuzo ya Ballon d’Or mbele ya Cristiano Ronaldo. Messi amewahi kushinda tuzo hiyo kwa mara nne mfululizo kabla ya Ronaldo kuingilia kati na kunyakua tuzo hiyo mwaka jana ikiwa ni mara ya pili kwa upande wake.
Baada ya kuisaidia Real Madrid kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la Mfalme mwaka huu, Ronaldo ndiye anayepewa nafasi kubwa zaidi ya kunyakuwa tuzo hiyo katika sherehe zitakazofanyika Januari 12 mwakani.
Mafanikio makubwa aliyopata Messi kwa mwaka huu ni kuiongoza timu yake ya taifa ya Argentina kucheza fainali ya Kombe la Dunia nchini Brazil wakati golikipa wa Bayern Munich Manuel Neuer yeye ni mchezaji mwingine wa tatu aliyeyopo katika orodha hiyo.
Pamoja na kutopewa nafasi mwaka huu, Pedro anaamini kuwa hakuna mchezaji yeyote katika sayari hii anayeweza kumfikia Messi katika ubora wake uwanjani.

No comments:

Post a Comment