STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 28, 2014

Kavumbagu afufuka Taifa, Ndanda majanga

Ndanda Fc waliporomoka hadi mkiani katika msimamo wa Ligi ikiuaga 2014 na kukaribisha 2015
Didier Kavumbagu akishangilia moja ya mabao yake na wachezaji wenzake Himid Mao na Aggrey Morris
BAO la kuongoza la Azam limemzindua Didier Kavumbagu ambaye alikuwa hajafunga muda mrefu kuwakimbia washambuliaji wenzake na kuongoza msimamo wa orodha ya wafungaji bora katika Ligi Kuu Tanzania Bara, huku Amissi Tambwe akifungua akaunti ya mabao Jangwani.
Didier alifunga bao la kuongoza la Azam leo na kumfanya kufikisha mabao matano na kuongoza orodha ya wakali wa mabao wakati ligi kuu ikimaliza mwaka 2014 na kusubiri kuendelea tena mwakani.
Simon Msuva aliyefunga bao la pili la Yanga naye ameingia kwenye orodha ya wakali wa mabao akiwa na mabao manne akilingana na wachezaji wengine, Danny Mrwanda wa Yanga, Rama Salim (Coastal Union), na Ame Ally (Mtibwa)
Ligi ikiaga mwaka 2014, Mtibwa ipo kileleni, huku Ndanda ikiachiwa nafasi ya mkiani na Mbeya City waliowanyuka bao 1-0 leo jijini Mbeya.
Ndanda inazibeba timu zote ikiwa na pointi sita, wakati Mbeya City kwa ushindi wa leo imechupa hadiu nafasi ya 12.
Msimamo kamili wa ligi hiyo baada ya kumalizika kwa mechi za raundi nane ni kama ifuatavyo;
                                          P   W    D    L    F    A   GD   Pts
 01. Mtibwa Sugar              08  04   04   00  11  04   07   16
02. Yanga                          08  04   02   02   11  07  04   14
03.  Azam                          08  04   02   02   10  06  04   14
04.  Kagera Sugar             08   03   04   01   07  04  03   13
05.  Coastal Union             08   03   03   02   09  07  02  12
06.  Polisi Moro                 08   03   03   02   08  07  01  12
06. JKT Ruvu                    08   03   01   04   07   08  -1  10
07. Ruvu Shooting             08   03   01   04   05   07  -2   10
08.Stand Utd                     08  02   04    02   06   10  -4  10
09.Simba                           08  01   06    01   07   07  00  09
09. Mgambo JKT              08  03   00    05   04   09  -5  09
12. Mbeya City                 08   02  02     04  03   06   -3  08
13. Prisons                        08   01  04     03  06   07   -1  07
14. Ndanda Fc                  08   02  00     06  08   13   -5  06
Wafungaji Bora:
5-
Didier Kavumbagu (Azam)
4-
Rama Salim (Coastal), Danny Mrwanda, Simon Msuva (Yanga) Ame Ally (Mtibwa)
3-
Ally Shomari, Emmanuel Okwi (Simba), Rashid Mandawa (Kagera Sugar)
2- Shaaban Kisiga, (Simba), Nassor Kapama (Ndanda) Salum Kanoni (Kagera), Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Samuel Kamuntu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Heri Mohammed (Stand Utd), Ally Nassor (Mgambo),  Malimi Busungu (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi)
Mechi zijazo;
Jan 03, 2014
Coastal Union vs  JKT Ruvu
Ruvu Shooting vs Kagera Sugar
Azam vs Mtibwa Sugar
Stand United vs Polisi Moro
Mbeya City  vs  Yanga

Jan 4, 2015
Mgambo JKT vs  Simba 
Prisons vs  Ndanda

No comments:

Post a Comment