STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 28, 2014

Diamond tena, atwaa tuzo Nigeria, Vee Money naye ang'ara

Vee Monye akiwa na tuzo yake
Peter Msechu akiwa na tuzo ya Diamond
NYOTA ya Supastaa wa Bongo, Diamond Platnumz imeendelea kung'ara baada ya usiku wa jana kunyakua tuzo nyingine ya AFRIMA 2014 nchini Nigeria, sambamba na mwanadada Vanessa Mdee 'Vee Money'.
Wasanii hao wametwaa tuzo hizo kupitia vipengele vya Wasanii Bora wa Afrika Mashariki, Diamond akinyakua kwa upande wa kiume na Vee Money kwa upande wa wasanii wa kike.
Tuzo hizo za AFRIMA zilizofanyika huko jijini Lagos nchini Nigeria, ambapo msanii mwingine wa Tanzania aliyekuwa akiwania tuzo hizo sambamba na Diamond ni Peter Msechu ambaye alimpokelea Diamond Tuzo yake.
Hiyo ilikuwa ni tuzo ya 13 kwa mwaka 2014 kwa Diamond baada ya awali kunyakua tuzo saba kwa mpigo katika Kili Music, kisha AFRIMMA, akafuatia na tatu za CHAOMVA na kumalizia ya The Future aliyotwa nchini Nigeria mara baada ya kutoka Afrika Kusini kunyakua tuzo tatu.
Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win
Vanessa Mdee akiwa na tuzo yake ya Best Female Artist in East Africa. Peter Msechu akiwa amebeba tuzo kwa niaba ya Diamond Platnumz. Peter Msechu, Vanessa Mdee na Victoria Kimani katika pozi huko Lagos, Nigeria. MWANAMUZIKI Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' usiku wa kuamkia leo ametwaa tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Kiume Afrika Mashariki (Best Male Artist in East Africa) kutoka Tuzo za 2014 AFRIMA zilizofanyika huko jijini Lagos nchini Nigeria. Mwanadada Vanessa Mdee yeye ameshinda tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Kike Afrika Mashariki (Best Female Artist in East Africa). Tuzo ya Diamond imepokelewa na mwanamuziki Peter Msechu aliyekuwepo katika zoezi hilo la utoaji tuzo maana na yeye alikuwa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania tuzo hizo

Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win

No comments:

Post a Comment