STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 31, 2013

Liverpool yazinduka EPL, yaifumua Aston Villa kwao

http://cache.images.globalsportsmedia.com/news/soccer/2013/3/31/315082header.jpg
Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard akishangilia bao la jioni ya leo

MABINGWA wa zamani waUlaya, Liverpool jioni ya leo imezinduka tena kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kupata ushindi wa mabo 2-1 ugenini mbele ya wenyeji wao Aston Villa.
Mkwaju wa penati iliyopigwa na nahodha Steven Gerrard katika dakika ya 60 ndiyo iliyoihakikisha Liverpool ushindi wa pointi tatu muhimu baada ya kwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa bao 1-0 lililotupiwa kambani na Mbelgium mwenye asili ya DR Congo, Christian Benteke.
Benteke alifunga bao hilo katika dakika ya 31, akimaliza kazi nzuri ya Gabriel Agbonlahor.
Wageni waliingia kipindi cha pili kwa kasi na iliwachukua dakika mbili tu kusawazisha bao kupitia Jordan Henderson na dnipo kwenye dakika ya 60 Gerrard akatupia mpira wavuni kwa penati  baada ya Luis Suarez kuangushwa langoni mwa Aston Villa alipokuwa akienda kumsalia kipa wa Brad Guzan.
Hata hivyo ushindi huo wa leo umeiacha Liverpool katika nafasi ya saba, ikiwa imecheza mechi 31, ikiwa nyuma ya wapinzani wao, Everton walioishinda jana bao 1-0 dhidi ya  Stoke City.

Maiti sasa zafikia 29 ajali ya jengo lililoporomoka Dar

Zoezi la kusaka miili zaidi ya watu likiendelea kufanywa kwa umakini mkubwa
Mojawapo ya magari kibao yaliangukiwa pia na jengo hilo
Wengine walikuwa ndani ya magari yao wakati mjengo ukiporomoka na kuwafunika
Jengo pacha... ujenzi wa jengo hili lililopakana na jingine lililoanguka umesitishwa kwa muda na serikali ili kupisha uchunguzi kwani mwenye jengo hili ndiye mmiliki wa lile lililoanguka na pia kampuni ya ujenzi ni ileile, mkandarasi ni yuleyule na mahala penyewe ni hapa hapa, kwenye makutani ya barabara ya Morogoro na Indira Gandhi.   

Jengo pacha la ghorofa 16... ujenzi wa ghorofa hili umesimamishwa kupisha uchunguzi. Mmiliki wa jengo hili ndiye mmiliki wa lile lililoanguka, kampuni ya ujenzi ni ileile, mkandarasi ni yuleyule na mahala penyewe ni hapa hapa kwenye makutani ya barabara ya Morogoro na Indira Gandhi.  
Idadi ya miili ya watu walionasuliwa kutoka katika kifusi cha jengo la ghorofa 16 lililoporomoka juzi wakati likiendelea kujengwa kwenye makutano ya Morogoro Road na Indira Gandhi sasa imefikia 29, imefahamika.  

"Hadi sasa tumeshapata miili ya watu 29 kutoka kwenye kifusi cha mabaki ya jengo lililoanguka," Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick amesema leo Machi 31, 2013.

Ameongeza kuwa waokoaji sasa wanaendelea kusaka miili zaidi katika lililokuwa jengo la chini ambako kulikuwa na ghala la vifaa na inadhaniwa kuwa huko ndiko kulikokuwa na watu wengi zaidi; na kwamba zoezi la kusaka miili litaendelea mpaka wahanga wote wapatikane.

Rais Jakaya Kikwete, ambaye alitembelea eneo la tukio juzi katika siku ya Ijumaa Kuu, ameagiza kwamba wahusika wote waliosababisha maafa hayo wafikishwe mbele ya mkono wa sheria na hadi sasa, polisi wamesema kuwa tayari wameshawatia mbaroni watuhumiwa wanne.

GOLDEN BUSH VETERANI YAIZAMISHA WAHENGA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEigEXcYZjHBYFe7oOEgW5OFabOhx7fWDF32Rsh1DNIyJgIuc8Evl-_yJ_6-t3SWerT20D7radHa4TQSZKy32dCj_g7jev9QWI1KeveOocs9OaXA0c4U8BREl7bBYDCuQ4pz95KuTxPJFBI/s1600/Golden+Bush+Veterani.JPG
Kikosi cha Golden Bush Veterani
 
WAKALI wa soka la maveterani jijini Golden Bush Veterani jioni ya leo imeisherehekea vyema sikukuu ya Pasaka baada ya kuwafumua wapinzani wao wakuu, Wahenga Fc kwa kuwalaza mabao 2-1 katika pambano maalum lililochezwa kwenye uwanja wa Kinesi, Ubungo Dar es Salaam.
Mchezo huo uliochezwa huku mvua kubwa ikinyesha na kuhudhuriwa na Kamanda wa Polisi, Thobias Andengenye ulishuhudiwa Wahenga wakitangulia kupata baop la kuongoza lililotumbukizwa wavuni na Albert Shao.
Hata hivyo Golden Bush iliyokuwa ikiongozwa na nahodha wake, Onesmo Wazir 'Ticotico' ilisawazisha bao hilo kupitia kwa nyota wa pambano hilo, Sadick Muhimbo na kufanya hadi mapumziko timu hizo ziwe nguvu sawa.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko ya wachezaji ambapo iliongeza uhai wa pambano hilo ambalo pande zote zilionyesha kulikamia na kuhiotaji ushindi ili kulinda heshima mbele ya mwenzake, japo utelezi na maji yaliyosababishwa na mvua iliyokuwa ikinyesha ilipunguza utamu wa soka la timu hizo.
Golden Bush ilifanikiwa kuandika bao la pili la la ushindi kupitia kwa 'Super Sub' wao De Natale alifumua shuti kali baada ya mabeki wa Wahenga kuzembea kuokoa mpira langoni mwake.
Mpaka filimbi ya mwisho ya mwamuzi wa pambano hilo, Ally Mayay ilipolia kuashiria pambano hilo limemalizika Wahenga walijikuta hoi kwa wapinzani wao kwa kula kichapo cha mabao 2-1.

Saturday, March 30, 2013

Maiti 21 zapatikana ajali ya ghorofa, nane washikiliwa na Polisi

Ibrahim Kissoki (kushoto) anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dar kuhusiana na ajali ya jengo lililoporomoka jana asubuhi. Hapa alikuwa akimfafanulia jambo Naibu Waziri wa Ujenzi, Gerson Lwenge.


WAKATI maiti nyingine ikiwa imepatikana jioni hii na kufanya idadi ya waliokufa kwenye ajali ya jengo la ghorofa 16 lililoporomoka kufikia 21, watu nane akiwamo Diwani wa Goba, Ibrahim Kissoki wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kutokana na mkasa wa ajali hiyo.
Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, RPC Suleiman Kova, amenukuliwa hivi punde kuwa Kissoki ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni yua Ujenzi ya Lucky Construction Ltd na watu wengine saba akiwamo wamiliki wa jengo hilo na wakandarasi na maafisa wa Manispaa ya Ilala wanashikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano zaidi ili kubaini chanzo cha ajali hiyo.
Kova, alisema mpaka sasa wakati zoezi la uokozi likiendelea eneo la tukio mitaa ya Indra Ghandi na Zanaki watu waliofariki katika ajali hiyo ni 21, nane kati yao wakiwa wameshatambuliwa na ndugu zao.
Kamanda huyo alisema wanaendelea kusaka wahanga wa ajali hiyo kuona kama watapata miili minmgine ya waliozikwa na kifusi cha jengo hilo linalomilikiwa na mfanyabiashara maarufu nchini, Ally Raza.
Tunaendelea kufuatilia taarifa na tutawaletea hapa hapa.

Vita vya Ligi Kuu Bara ndiyo kwanza vimeanza


 
http://3.bp.blogspot.com/-4Yv7aB6pBF4/UQJ6EXASNmI/AAAAAAAAiMo/jfdsnoiqHiQ/s1600/VPL.png
MATOKEO ya mechi zilizochezwa jioni ya leo za Ligi Kuu Tanzania Bara yamebadili msimamo na kutoa dalilia kwamba vita vya kuwania ubingwa na vya kuepa kushuka daraja vimeanza upya.
Yanga na Azam zinaendelea kubanana kwenye uwaniaji wa ubingwa, huku Toto African, Polisi Moro, African Lyon zikiwa bado katika vita kali ya kuepuka kushuka daraja mkiani.
Sare ilizopata Toto African na Polisi Morogoro katika viwanja vyao vya nyumbani dhidi ya wapinzani wa jadi nchini, Simba na Yanga zimezifanya timu hizo kurejea mkiani wakiipokea Lyon.
Toto imerudi mkiani ikilingana pointi 18 na Polisi ila uwiano wa mabao ndiyo unaowatofautisha nyuma ya Lyon walioifumua Coastal bao 1-0 na kufikisha pointi 19.
Kileleni, licha ya Yanga kuendeleza rekodi ya kutopoteza mchezo wowote wa ligi hiyo ndani ya mwaka 2013, lakini imeshindwa kutimiza ndoto ilizokuwa nazo leo za kuivua Simba ubingwa iwapo ingeshinda mbele ya Polisi na sare iliyopata Simba jijini Mwanza.
Suluhu ya kutofungana imeifanya Yanga kufikisha pointi 49 na kuendelea kuipa nafasi Azam kuwakaribia baada ya wauza Lambalamba haop kushinda bao 1-0 uwanja wa Mabatini.
Kagera iliyosaliwa na mechi nne imenufaika na kucheza nyumbani kwa kushinda mechi ya pili mfululizo na kukwea nafasi ya tatu, ikiiengua rasmi Simba, huku Coastal Union yenye ndoto za kumaliza katika Tatu Bora imekwama mbele ya Lyon, huku JKT Ruvu iliyozinduka katika mechi yao ya mwisho dhidi ya Polisi Moro imeendelea kuchechemea msimu huu.
Misimu mitatu iliyopita JKT Ruvu ilitisha na ukali wake kwa sasa umehamia kwa Ruvu Shooting ambayo hata hivyo leo ilishindwa kukwepa kipigo cha nyumbani mbele ya Azam waliosalia nafasi ya pili katika msimamo huo wa ligi kuu.
Msimamo kamili wa Ligi hiyo ilioyosaliwa raundi chache kabla ya kufunga msimu ni kama ifuatavyo:

                                  P     W    D     L     F      A       D      Pts
1. Young Africans     21   15     4     2     37     12     +25   49
2. Azam                    21   13     4     4     36     16     +20   43     

3. Kagera Sugar        22   10     7     5     25     18     +7     37    
4. Simba                   21     9     8     4     30     19     +11    35 

5. Coastal Union      22     8     8     6     23     20     +3      32   
6. Mtibwa Sugar      22     8     8     6     24     22     +2      32   
7. Ruvu Shooting     21     8     5     8     21     19     +2      29    
8. JKT Oljoro FC     22     7     7     8     22     24     -2      28    
9. JKT Mgambo      21     7     3     11     14     21     -7     24
10.Ruvu Stars          21     6     4     11     19     34     -15   22
11.Tanzania Prisons 21     4     8     9       11     20     -9     20   
12.African Lyon      22     5     4     13     15     32     -17   19
13.Polisi Morogoro  22     3     9     10     11     21     -10   18   
14.Toto Africans      22     3     9     10     19     30     -11   18
            

Yanga yabanwa, Simba yaporomoka, Azam, Kagera zatakata

Yanga waliobanwa Morogoro
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara Simba imezidi kuporomoka kwenye msimamo wa Ligi kuu baada ya Kagera Sugar kuiengua nafasi ya tatu kutokana na kupata ushindi wa mabao 3-1 mbele ya Mtibwa Sugar wakati 'Mnyama' akiambulia sare ya mabao 2-2 jijini Mwanza mbele ya Toto African.
Simba iliyobanwa Mwanza na Toto African

Kagera imeilaza Mtibwa Sugar mabao 3-1 na kufikisha pointi 37 wakati Simba kwa sare hiyo ya Toto imefikisha pointi 35 na kutoa nafasi kwa Yanga na Azam kuzivua taji lake inalolishikilia kwa sasa.
Simba ilishtuliwa kwa bao la kuongoza la Toto lililofungwa dakika ya 25 kabla ya Simba kuchomoa dakika tatu baadaye kupitia ramadhani Mkopi na kufanya hadi mapumziko matokeo yawe 1-1.
Kipindi cha pili Simba ilifunga bao la pili kupitia Mrisho Ngassa kabla ya Toto kusawazisha kupitia kwa Ramadhani na kufanya timu hizo zigawane pointi moja moja.
Yanga iliyokuwa mjini Morogoro ilishindwa kuivua Simba ubingwa na badala yake kutoa mwanya kwa Azam kuendelea kuwafukuzia katika mbio zao za kuwania taji la ubingwa msimu huu baada ya kulazimishwa suluhu ya kutofungana.
Kikosi cha Kagera Sugar kilichoiengua Simba nafasi ya tatu
Azam ilipata ushindi wa bao 1-0 kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani na kufikisha pointi 43 na kupunguza pengo lililokuwa awali la pointi nane na kufikia sita.
Bao la Azam liliwekwa kimiani na kinara wa mabao wa Ligi Kuu kwa sasa Kipre Tchetche na kuifanya Azam kuiacha Simba kwa pointi 8.
Azam waliitungua Ruvu Shooting

Jijini Dar es Salaam African Lyon imeiduwaza Coastal Union kwa kuilaza bao 1-0 wakati Arusha wenyeji, JKT Oljoro waliilaza maafande wenzao wa JKT Ruvu kwa mabao 2-0 na kuzidi kuimarisha mbio zake za kuelekea kwenye nafasi ya kuepuka kushuka daraja.
Matokeo kamili ya mechi za leo ni kama ifuatavyo hapo chini:
 Polisi Moro v Yanga (0-0)
JKT Oljoro v Ruvu JKT (2-0)
Kagera Sugar v Mtibwa (3-1)
Toto African v Simba  (2-2)
African Lyon v Coastal (1-0   )
Ruvu v Azam   (0-1)

Idadi ya waliokufa ajali ya Ghorofa yaongezeka


IDADI ya watu waliofariki katika tukio la kuporomoka kwa ghorofa lilililokuwa likijengwa imeongeza na kwa sasa imefikia watu 20.
Tayari watu waliopoteza ndugu zao katika ajali hiyo iliyotokea jana kweye mtaa wa Indra Ghandi wamemiminika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kutambua miili ya ndugu zao.
Mpaka sasa miili ya watu nane imetambuliwa wakiwemo watu watatu wenye asilia ya Asia na wengine waliosalia wakiwa ni wafanyakazi waliokuwa wakijenga ghorofa hilo.
Pia hospitalini hapo imeonwa viungo vya watoto na watu wazima vilivyokatika na kutia hali ya simanzi, huku juhudi zikifanywa kupata majina ya watu waliopoteza uhai huo na wale ambao wamenusurika kwenye ajali hiyo.

  

Golden Bush Veterani, Wahenga kesho hapatoshi Kinesi

Onesmo Waziri 'Tictico'
PAMBANO la kirafiki la kusherehekea sikukuu ya Pasaka kati ya Golden Bush Veterani na wapinzani wao wakuu, Wahenga Fc limehamishiwa uwanja wa Kinesi, Ubungo jijini Dar es Salaam.
Awali pambano hilo lilipangwa kufanyika kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza, lakini kutokana na mvua zinazoendelea jijini Dar zimeufanya uwanja huo kujaa maji na hivyo kutofaa kutuchezeka.
Mlezi na Msemaji wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema muda wa kuanza pambano hilo ni ule ule wa saa 10 jioni japo wamebadili uwanja.
"Napenda kutoa taarifa kwamba ile game yetu ya kesho imehamishiwa uwanja wa Kinesi, hii imetokana na hali ya mvua iliyoharibu kabisa uwanja wetu wa TP maarufu kama Nangwanda Sijaona. Game itaanza muda uleule wa saa kumi na nusu jioni.
Ticotico alisema kikosi chao kimejiandaa vya kutosha kuweza kula Pasaka vyema kwa kuilaza Wahenga Fc.





Twanga kusindikiza uzinduzi wa Miss Tabata 2013

Wanamuziki wa bendi ya Twanga Pepeta wakiwajibika jukwaani, kesho watazindua shindano la Miss Tabata 2013

UZINDUZI  wa shindano la kumtafuta Miss Tabata 2013 unafanyika kesho Da West Park, Tabata jijini Dar es Salaam.
Katika uzinduzi huo, jumla ya walimbwende 26 watambulishwa kwa mashabiki kwenye onyesho hilo ambalo litaenda sambamba na kusherekea sikukuu ya Pasaka.

Mratibu wa shindano hilo, Joseph Kapinga alisema jana kuwa warembo hao watatambulishwa pamoja na washiriki wa Miss Mzizima.

Kapinga aliwataja warembo wa Tabata watakaotambulishwa kuwa ni Martha Gewe (19), Zilpha Christopher (19), Hidaya David (22), Aneth Ndumbalo (19), Amina Ally (18), Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Kitereja (19),  Angela Fradius (19), Domina Soka (21), Rehema Kihinja (20), Glory Jigge (18) na Sophia Claud (21).

Aliwataja wengine ni Lilian Mpakani (19), Lilian Msanchu (19), Rita Frank (20), Pasilida Mandali (21), Rachel Mussa (19), Jasmin Damian (18), Angelina Mkinga (19), Mercy Mwakasungu (20), Tunu Hamis (19), Blath Chambia (23), Ray Issa (22), Shamim Abass (22) na Shan Abass (22).

Utambulisho wa warembo hao, utasindikizwa na burudani kabambe kutoka bendi ya Twanga Pepeta “Wazee wa Kisigino”.

Kapinga alisema wapenzi wa tasnia ya urembo Jijini Dar es Salaam, watapata fursa ya kuwaona warembo hao kabla ya shindano lenyewe litakalofanyika Mei mwaka huu.

Onyesho hilo limedhaminiwa na Konyagi, CXC Africa, Fredito Entertainment na Saluti5 na kuandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts.

Washindi watano kutoka Tabata watafuzu kushiriki Miss Ilala baadaye mwaka huu.

Anayeshikilia taji la Miss Tabata ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.

Simba kutema ubingwa leo? Azam, Ruvu patachimbika Pwani


Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, Simba

Azam watakaovaana na Ruvu Shooting mkoani Pwani
USHINDI wowote itakayopata  vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga  kwenye pambano lake dhidi ya Polisi Moro jioni ya leo na watani zao Simba kueteleza jijini Mwanza mbele ya Toto African itaipa Yanga nafasi ya kulishika taji la ubingwa kwa mkono mmoja ikisubiri kukabidhiwa rasmi mechi mbili zijazo.

Yanga itashuka dimba la Jamhuri kumenyana na wenyeji wao, ikiwa ina pointi 48 kibindoni, huku watani zao wanaoshikilia taji hilo kwa sasa wakiwa nafasi ya pili na pointi zao 34, sita nyuma ya wanaoshika nafasi ya pili Azam itakayokuwa dimba la Mabatini-Mlandizi, Pwani kuumana na wenyeji wao Ruvu Shooting.

Simba inahitajika kupata ushindi katika mechi yake ya leo itakayopigwa CCM Kirumba iwapo inahitaji kuendelea kutambulika kama bingwa mtetezi, kwani matokeo yoyote kinyume na ushindi itakuwa imelipema rasmi taji hilo na kuliachwa likigombewa na timu za Yanga na Azam.

Tayari kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu na baadhi ya wachezaji wa kikosi cha mabingwa hao wameapa kufa kiume leo Kirumba ili kufuta machungu ya kugaragazwa bao 1-0 na Kagera Sugar katika mechi yao iliyopita iliyochezwa siku ya Jumatano.

Julio alisema licha ya kuwakosa wachezaji wake kadhaa wakiwemo 'mapro', Mussa Mudde na Abel Dhaira na kuumia kwa Kiggy Makassy na Haruna Chanongo kuwa na hatihati ya kucheza leo, bado anaamini kikosi chake kitafanya vyema mbele ya Toto.

Hata hivyo kocha wa Toto, Athuman Bilal 'Bilo' alinukuliwa jana akisema kuwa wanaichukulia mechi yao ya leo kama fainali kwa kuhitaji pointi tatu muhimu ili wajinasue eneo la mkiani linalotishia kuirudisha timu yake kwenye Ligi Daraja la Kwanza.

Mechi nyingine za leo Azam watakuwa wakiendeleza harakati zao za kuifukizia Yanga kileleni kwa kuumana na Ruvu Shooting inayonolewa na kocha Charles Boniface Mkwasa.
Azam inahitaji ushindi ili kuweka hai matumaini ya kuweka rekodi ya kuwa bingwa wa Tanzania iwapo Yanga itateleza kileleni, licha ya kwamba imeachwa nyuma pointi 8 mpaka sasa.
Azam inaivaa Ruvu ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa mabao 3-0 iliyopata kwa Prisons Mbeya, na ikiwa inajiandaa kurudiana na Barracks YCII ya Liberia katika mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Mtibwa Sugar imesafiri mpaka Kagera kwa ndugu zao Kagera Sugar wanaoendelea kuchekelea ushindi dhidi ya Simba juzi Jumatano, kila moja ikisaka ushindi na pointi tatu kuimarisha nafasi yake katika msimamo wa Ligi hiyo inayoelekea ukingoni kwa sasa.
JKT Ruvu waliozinduka katrika mechi yao ya mwisho kwa kuilaza Polisi Moro mabao 3-2 itakuwa ugenini uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta, jijini Arusha kuumana na wenyeji wao JKT Oljoro iliyo chini ya kocha Mbwana Makatta.
Pambano la mwisho kwa mujibu wa ratiba inayoonyesha kuwa Coastal Union wamesafiri kutoka Tanga kuja Dar kuumana na African Lyon katika pambano linalotarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa Chamazi, huku Mgambo Shooting watakuwa wakila shushushu kama ilivyo kwa Prisons ya Mbeya.
Je ni timu ipi italia au kucheza jioni ya leo? Bila shaka ni jambo la kusubiri kuona baada ya dakika za 90 za mapambano hayo.

Waliokufa tukio la kuporomoka jengo Dar wafikia 18

Mashuhuda wakiangalia jengo lililoporomoka jana asubuhi katika makutano ya Morogoro Road na Indira Gandhi jijini Dar es Salaam.

Watu wa Msalaba Mwekundi wakibeba moja ya majeruhi wa tukio hilo la jana
 
Rais Kikwete alipotembea eneo la tukio la jengo lililoporomoka wakati likiendelea kujengwa
WAKATI zoezi la uokozi kwenye tukio la ajali ya kuporomoka kwa jengo la ghorofa lililokuwa likijengwa mtaa wa Indra Ghandi, likiendelea taarifa ambazo zilizothibitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadick zinasema kuwa miili ya watu 17 wakiwamo watoto wawili mpaka sasa imeshapatikana.Hata hivyo muda mfupi uliopita imeelezwa imeopolewa maiti nyingine na kufanya idadi sasa kufikia 18, huku taarifa ya awali ikisema miili ya watoto waliokolewa kwenye ajali hili iliyoacha majonzi kwa Watanzania wakijiandaa kuisherehekea sikukuu ya Pasaka ilikuwa wawili.
Mapema asubuhi Mkuu huyo wa mkoa alinukuliwa kwamba miili iliyopatikana mpaka usiku wa jana ni 15 ya watu wazima na miwili ya watoto na kwamba mmiliki wa jengo hilo na baadhi ya wakandarasi walikuwa wametiwa mbaroni kwa ajili ya kusaidia uchunguzi wa tukio hilo.
Mkuu wa Mkoa alisema kuwa bado juhudi zinafanywa kutafuta miili ya watu wengine ambapo idadi ya majeruhi waliokuwa wamenasuliwa kwenye mkasa huo walikuwa zaidi ya 20 mpaka mapema leo asubuhi.
Taarifa zaidi zitawajia japo inaelezwa ni vigumu kwa sasa kupatikana kwa mtu aliyehai katika kifusi kinachoendelea kufukuliwa kwa kushirikisha vikosi vya majeshi na wasamaria wema waliojitokeza tangu jengo hilo linalodaiwa la orofa 16 kuporomoka asubuhi ya jana wakati watu wakiendelea na ujenzi.

Albinus wa Namibia bingwa mpya wa Dunia






BONDIA  Albinus Felesianu wa Namibia leo ameudhihirishia ulimwengu kuwa yeye kweli ndiye Mfalme wa uzito wa unyoya duniani kwa vijana baada ya kumgalagaza bondia Herbert Quartey wa Ghana katika mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa Windhoek Country Club Resort  and Casino leo tarehe 29, March 2013.
Umati wa watu wasiopungua elfu 20 walijazana katika ukumbi huo wa burudani wakimshangilia kwa nderemo na vifijo bondia wao Albinus wakati alipokuwa anafanya vitu vyake kwenye ulingo.

Baada ya mtangazaji wa ulingo kutamka kuwa “Na sasa bingwa mpya wa uzito wa unyoya duniani kwa vijana ni Albinus Felesianu” mayowe ya wapenzi wa ngumi waliojazana katika ukumbi huo yaliweza kusikika kilometa tatu mpaka katikati ya jiji la Windhoek.

Hata hivyo, haikuwa kazi rahisi kwa Albinus kuunyakua mkanda wa ubingwa wa dunia kwa vijana kwani Mghana Herbert Quartey naye alikuwa mbogo kwani alirusha kila aina ya masumbwi yaliyomo kwenye kitabu.

Wawili hao walichapana makonde mazito kama watu wenye uzito mkubwa na kama sio uwezo na ujuzi wa referii Deon Dwarte wa Afrika ya Kusini kazi ingekuwa ngumu sana kwani kila bondia alijaribu kumpata mwenzake katika sehemu zinazoumiza ili kuumaliza mpambano mapema lakini ujuzi na ubishi wa kila mmoja ulifanya kusiweko na knockout yoyote!

Hii ni mara ya kwanza kwa nchi ya Namibia kuweza kuandaa mpambano wa ubingwa wa dunia wa IBF na wakali hao waliweza kuufanya umati wote uliohudhuria kulipuka kwa makelele ya kushangilia kila wakati.

Alikuweko Harry Simon, ambaye ndiye Mnamibia aliyeweza kuufanya mchezo wa ngumi kupendwa na kuwa maarufu sana nchini humu. Uwezo na utukutu wa Harry Simon ulingoni umeufanya mchezo wa ngumi kupendwa karibu na kila Mnamibia.

Walikuweko pia wageni wengine wengi lakini kampuni ya simu ya Telecom ambayo ndio waliokuwa wadhamini wa mpambano huo imejikusanya kila aina ya sifa na upendo kutoka kwa wananchi wa Namibia jinsi inavyo dhamini mchezo wa ngumi!

Mpambano huu uliandaliwa na Kinda Nangolo wa kampuni ya Kinda Boxing Promotions ambayo ndio waandaaji wa mpambano ujao wa mwezi wa Mei wa bingwa wa IBF Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati katika uzito wa unyoya bondia Gottlieb Ndokosho. Mpambano wa IBF wa Kimataifa wa bondia Harry Simon nao utafanyika mwezi wa Juni.

Aidha, Immanuel “Prince’ Naidjala”wa Namibia na Lesley Sekotswe wa Botswana watarudiana tena mwezi wa July kumpata bingwa wa kimataifa wa uzito wa bantam baada ya kutoka sare walipokitana wiki iliyopota nchini Namibia.

Friday, March 29, 2013

PICHA ZA TUKIUO LA KUPOROMOKA KWA JENGO KATIKATI YA JIJI



 Mtoto Maisamali Karim (6) ambaye ameokolewa kutoka katika madrasa ya Msikiti wa Khoja Shia Ithna Asheri Jamaat iliyoangukiwa na jengo hilo katika mtaa wa Indira Gandhi.

 Changamoto ya uokoaji ni ngumu, lakini vikosi mbalimbali vinaendelea na zoezi hilo, ili kunusuru maisha ya waliofukiwa na kifusi.
 Hizi nia aina ya nondo ambazo kimsingi sio imara kuweza kuhimili ujenzi wa ghorofa ndefu kama hili, kuna haja mamlaka husika likatupia macho kampuni za ujenzi ili kuokoa maisha ya wajenzi na watumiaji wa majengo hayo.
 Askari wakiimarisha ulinzi wakati zoezi la uokoaji likiendelea.
  Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea, huku nondo nyembamba zikionekana na kuacha maswali miongoni mwa mashuhuda wa tukio hilo.
  Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea.
 Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea.
Waokoaji.


 Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (CP), Suleima Kova kuhusu jengo la ghorofa 16 lililoanguka majira ya saa mbili asubuhi katika makutano ya mtaa wa Indira Ghandi na Barabara ya Morogoro jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi. Katika ajali hiyo watu wawili wamekufa papo hapo. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
 Waokoaji wakiwa kazini.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum (CP), Suleima Kova.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum (CP), Suleima Kova akiwa katika eneo la tukio. Kulia ni Mbunge wa viti maalum (NCCR-Mageuzi James Mbatia.
 
PICHA ZIMEHAMISHWA HABARI MSETO

Maiti zaidi zapatikana ajali ya ghorofa lililoporomoka Dar


Mashuhuda wakiangalia jengo lililoporomoka asubuhi hii katika makutano ya Morogoro Road na Indira Gandhi jijini Dar es Salaam leo asubuhi Machi 29, 2013.
MIILI zaidi imedaiwa kupatikana katika tukio la ajali ya kuporomoka kwa jengo la ghorofa linalodaiwa kuwa 19 lililokuwa likiendelea kujengwa kuporomoka na kuwafunika watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 6o

Tukio hilo limetokea mishale ya asubuhi katika mitaa ya Posta, jirani na msikiti wa Shia katika eneo la makutano ya Morogoro Road na Indira Gandhi na hadi sasa, miili ya maiti 12 na pia majeruhi 30 wameshachomolewa.

Aidha, harakati zaidi za uokoaji zingali zikiendelea kufanywa na vikosi vya uokoaji. Katika eneo la tukio hilo, tayari viongozi kadhaa wa serikali na makamanda wa Polisi katika kanda maalum ya Dar es Salaam wamefika kusaidia shughuli za uokoaji, miongoni mwao akiwamo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick.

Baadhi ya mashuhuda wamedai kuwa mabaki ya jengo hilo yanaonyesha kuwa mchanga ulikuwa mwingi mno kulinganisha na saruji, hali inayodhaniwa kuwa ni miongoni mwa sababu za kuporomoka kwa mjengo huo uliogharimu mamilioni ya pesa.

Pamoja na mashuhuda wa tukio hilo kudai kuna zaidi ya miili ya watu 10 iliyotolewa kwenye uokozi na wengine 30 kukimbizwa hospitalini kwa matibabu kutokana na kujeruhiwa, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dar es Salaam, amesema ni watu wawili tu waliogundulika kufa mpaka sasa na waliokimbizwa hospitali ni 17 japo shughuli za uokozi zinaendelea.

BREAKING NEWSSSS: GHOROFA LAPOROMOKA DAR 60 wadaiwa kufukiwa


HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema jengo la ghorofa lililokuwa likiendelea kujengwa mitaa ya Indra Gandi jijini Dar es Salaam limeporomoka na kuwafukia watu wasiopungua 60.
MICHARAZO imedokezwa kuwa mpaka sasa watu 17 wameshaokolewa na miili ya watu wawili imepatikana katika mkasa huo unaohusisha ghorofa hilo la orofa 19.
Mtandao unaendelea kuzifuatilia taarifa hizo kisha tutawajulisha kinachoendelea, japo inaeleza juhudi za uokozi katika tukio hilo zinaendelea kunusu watu waliozikwa na kifusi cha jengo hilo.
Pia imeelezwa kuwa viongozi wa mkoa akiwemo Rc Mecky Sadick ametua katika eneo hilo akiambatana na wenzake kwa ajili ya kujua kinachoendelea. 
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova amethibitisha kuokolewa kwa watu 17 na wawili kupoteza maisha na kusema taarifa kamili itatolewa baadaye.

UCHAGUZI MIKUU BFT KUFANYIKA JIJINI MWANZA

Viongozi wa sasa BFT, Rasi Joan Minja (kulia) na Katibu Mkuu, Mashaga makore

UCHAGUZI Mkuu wa Shirikisho la Mchezo wa Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT) unatarajiwa kufanyika Mei mwaka huu jijini Mwanza.
Katibu Mkuu wa BFT, Mashaga Makore, aliiambia MICHARAZO asubuhi ya leo kuwa, kuwa uchaguzi huo utafanyika mara baada ya kumalizika kwa michuano ya kimataifa ya Majiji yanayotarajiwa kufanyika jijini humo kati ya Mei 20-25.
Makore alisema mchakato wa kuelekea kwenye kinyang'anyiro hicho ambacho kitatanguliwa na Mkutano Mkuu wa shirikishi hilo utatangazwa mara baada ya shamrashamra za sikukuu ya Pasaka.
"Uchaguzi Mkuu wa BFT utafanyika mwezi Mei jijini Mwanza mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya kimataifa ya ngumi inayoshiriki miji mikuu ya Afrika Mashariki na Kati, ambapo utatanguliwa na Mkutano Mkuu," alisema Makore.
Makore alisema maamuzi hayo yalifikiwa na Kamati yao ya Utendaji iliyokaa hivi karibuni na kutoa wito kwa wadau wa mchezo huo wenye uwezo na sifa za kuongoza shirikisho hilo kujiandaa kuijitosa kuwania uongozi kwenye uchaguzi huo.

Goti lamtia hofu Zahoro Pazi


MSHAMBULIAJI wa timu ya JKT Ruvu, Zahoro Pazi ameingiwa hofu na jeraha la goti alilopata wakati wa pambano lao dhidi ya Polisi Morogoro huenda ikamvurugia mipango ya safari yake ya kurejea Afrika Kusini kujaribu kuchezas soka la kulipwa.
Pazi ametakiwa kurejea tena nchini humo Mei mwaka huu kulingana na makubaliano yake na klabu ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini Bloemfotein Celtic, iliyomfanyia majaribio ya kuichezea yaliyofanyika Januari mwaka huu.

Hata hivyo mchezaji huyo alisema ameanza kupatwa hofu baada ya kupata maumivu makali alipoumia kwenye mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Polisi Moro, pambano lililoisha kwa JKT Ruvu kushinda mabao 3-2.
Akizungumza na MICHARAZO, Pazi alisema pamoja na uvimbe uliokuwapo katika goti hilo kuisha bado anahisi maumivu makali kwa ndani japo linalomnyima raha, ingawa alisema benchi la utabibu la klabu yake linamshughulikia vyema.
"Haya maumivu ya goti niliyonayo yananikatisha tamaa, nashindwa kuitumikia klabu yangu na wakati huo huo nina mwezi mmoja tu wa kujiandaa kabla ya kurejea Afrika Kusini kuendelea na majaribio yangu klabu ya Bloemfotein Celtic," alisema Pazi.
Mtoto huyo wa kipa wa zamani wa kimataifa nchini, Idd Pazi 'Father' anayeichezea JKT kwa mkopo akitokea Azam, alisema anatamani apone haraka goti hilo ili ajifue zaidi kusudi akienda Afrika Kusini awaridhishe mabosi wa Bloemfotein.

Humud apaa zake kwenda Jomo Cosmo



KIUNGO mahiri wa timu ya Azam, Abdulhalim Humud 'Gaucho' ameondoka nchini asubuhi hii kuelekea Afrika Kusini kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika kalbu ya Jomo Cosmo.
Meneja wa klabu ya Azam, Patrick Kahemele aliiambia MICHARAZO mapema leo kuwa, Humud
atakuwa nchini humo kwa muda wa siku 10 akifanyiwa majaribio na klabu hiyo  inayopigana kutaka kurejea kwenye Ligi Kuu ya Afrika Kusini (PSL).
Kahemele alisema Humud ameenda Afrika Kusini ikiwa ni utekelezaji wa mipango ya klabu yao ya Azam ya kupanua wigo wa wachezaji wa kitanzania kucheza soka nje ya nchi kwa manufaa ya nchi siku za baadaye.
"Humud ameondoka asubuhi hii (jana) kuelekea Afrika Kusini kufanyiwa majaribio katika klabu ya Jomo Cosmo na atakuwa huko kwa siku 10 kabla ya kurejea nchini" alisema Kahemele.
Klabu hiyo ya Cosmo inamilikiwa na kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Afrika Kusini (Bafana Bafana) Jomo 'Black Prince' Sono, na iwapo Humud atafaulu majaribio yake atafuata nyayo za wachezaji wa Kitanzani kuwahi kuichezea timu hiyo akitanguliwa na nyota wa zamani  Nteze John na Ally Shah kuwahi kufanya hivyo miaka ya nyuma.

Thursday, March 28, 2013

Hatma ya ubingwa Simba mikononi mwa Toto na Yanga J'mosi

 
Yanga


Simba

HATMA ya Simba kuendelea kulifukuzia taji lake la ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara inalolishikilia inatarajiwa kufahamika Jumamosi wakati itakapovaana na Toto African jijini Mwanza katikia mfululizo wa ligi hiyo iliyobakisha mechi tano kabla ya kufunga msimu.
Simba iliyojeruhiwa jana kwa kulambwa bao 1-0 na wenyeji wao Kagera Sugar, mjikni Bukoba itaikabilia Toto kwenye uwanja wa CCM Kirumba na matokeo yoyote mabaya kwao yatawafanya waliteme rasmi taji lao na kuliacha bila mwenyewe.
Kwa sasa mabingwa hao wana pointi 34, pointi 14 nyuma ya vinara wanaoongoza ligi hiyo Yanga ambayo nayo itakuwa dimbani wikiendi hii mjini Morogoro kuvaana na maafande wa Polisi Moro na ushindi wowote utamaanisha utawavua Simba ubingwa.
Hata hivyo Simba itavuliwa rasmi ubingwa Jumamosi iwapo Yanga itashinda kisha wao wapate sare au kipigo toka kwa Toto kwani haiataweza kufikisha pointi ambazo itakuwa imezikusanya Yanga yaani 51. Kwa sasa Yanga ina pointi 48.
Tayari Simba kupitia kocha wake msaidizi Jamhuri Kihwelu 'Julio' wameapa kupigana kiume CCM Kirumba ili kuhakikisha wanazoa pointi tatu toka Kanda ya Ziwa.
Wakati Simba ikiwa katika kitimtim hicho jini Mwanza, Yanga timu pekee ambayo haijapoteza mechi yoyote ndani ya mwaka huu wa 2013, itakabiliana na timu isiyotabirika ya Polisi ambayo tangu ifanye mabadiliko ya benchi la ufundi imekuwa tishio.
Kocha wa Yanga Ernst Brands amenukuliwa akisema kuwa vijana wake tayari kuendeleza rekodi ya ushindi ili kutangaza ubingwa mapema, licha ya kukiri Polisi sio timu ya kubeza.
Kwa mujibu wa ratiba ya ligi hiyo mbali na mechi hizo za watani wa jadi zinazochezwa viwanja tofauti, michezo mingine ya wikiendi hii inatarajiwa kuzikutanisha timu ndugu za Kagera Sugar itakayoialika Mtibwa Sugar mjini Bukoba, huku Azam wenyewe watakuwa Mlandizi kuvaana na Ruvu Shooting iliyotamba kuwashikisha adamu Jumamosi.
Mechi nyingine kwa wikiendi hii itazikutanisha timu zaJKT Oljoro watakaovaana na maafande wenzao JKT Ruvu mjini Arusha ambayo haitakuwa na nyota wake, Zahoro Pazi aliye majeruhi wa goti, huku African Lyon itaikaribisha Coastal Union uwanja wa Chamazi ikiwa inapigana kujinasua mkiani ilipokung'ang'ania kwa muda sasa.