STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 30, 2013

Twanga kusindikiza uzinduzi wa Miss Tabata 2013

Wanamuziki wa bendi ya Twanga Pepeta wakiwajibika jukwaani, kesho watazindua shindano la Miss Tabata 2013

UZINDUZI  wa shindano la kumtafuta Miss Tabata 2013 unafanyika kesho Da West Park, Tabata jijini Dar es Salaam.
Katika uzinduzi huo, jumla ya walimbwende 26 watambulishwa kwa mashabiki kwenye onyesho hilo ambalo litaenda sambamba na kusherekea sikukuu ya Pasaka.

Mratibu wa shindano hilo, Joseph Kapinga alisema jana kuwa warembo hao watatambulishwa pamoja na washiriki wa Miss Mzizima.

Kapinga aliwataja warembo wa Tabata watakaotambulishwa kuwa ni Martha Gewe (19), Zilpha Christopher (19), Hidaya David (22), Aneth Ndumbalo (19), Amina Ally (18), Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Kitereja (19),  Angela Fradius (19), Domina Soka (21), Rehema Kihinja (20), Glory Jigge (18) na Sophia Claud (21).

Aliwataja wengine ni Lilian Mpakani (19), Lilian Msanchu (19), Rita Frank (20), Pasilida Mandali (21), Rachel Mussa (19), Jasmin Damian (18), Angelina Mkinga (19), Mercy Mwakasungu (20), Tunu Hamis (19), Blath Chambia (23), Ray Issa (22), Shamim Abass (22) na Shan Abass (22).

Utambulisho wa warembo hao, utasindikizwa na burudani kabambe kutoka bendi ya Twanga Pepeta “Wazee wa Kisigino”.

Kapinga alisema wapenzi wa tasnia ya urembo Jijini Dar es Salaam, watapata fursa ya kuwaona warembo hao kabla ya shindano lenyewe litakalofanyika Mei mwaka huu.

Onyesho hilo limedhaminiwa na Konyagi, CXC Africa, Fredito Entertainment na Saluti5 na kuandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts.

Washindi watano kutoka Tabata watafuzu kushiriki Miss Ilala baadaye mwaka huu.

Anayeshikilia taji la Miss Tabata ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.

No comments:

Post a Comment