STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 30, 2013

Waliokufa tukio la kuporomoka jengo Dar wafikia 18

Mashuhuda wakiangalia jengo lililoporomoka jana asubuhi katika makutano ya Morogoro Road na Indira Gandhi jijini Dar es Salaam.

Watu wa Msalaba Mwekundi wakibeba moja ya majeruhi wa tukio hilo la jana
 
Rais Kikwete alipotembea eneo la tukio la jengo lililoporomoka wakati likiendelea kujengwa
WAKATI zoezi la uokozi kwenye tukio la ajali ya kuporomoka kwa jengo la ghorofa lililokuwa likijengwa mtaa wa Indra Ghandi, likiendelea taarifa ambazo zilizothibitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadick zinasema kuwa miili ya watu 17 wakiwamo watoto wawili mpaka sasa imeshapatikana.Hata hivyo muda mfupi uliopita imeelezwa imeopolewa maiti nyingine na kufanya idadi sasa kufikia 18, huku taarifa ya awali ikisema miili ya watoto waliokolewa kwenye ajali hili iliyoacha majonzi kwa Watanzania wakijiandaa kuisherehekea sikukuu ya Pasaka ilikuwa wawili.
Mapema asubuhi Mkuu huyo wa mkoa alinukuliwa kwamba miili iliyopatikana mpaka usiku wa jana ni 15 ya watu wazima na miwili ya watoto na kwamba mmiliki wa jengo hilo na baadhi ya wakandarasi walikuwa wametiwa mbaroni kwa ajili ya kusaidia uchunguzi wa tukio hilo.
Mkuu wa Mkoa alisema kuwa bado juhudi zinafanywa kutafuta miili ya watu wengine ambapo idadi ya majeruhi waliokuwa wamenasuliwa kwenye mkasa huo walikuwa zaidi ya 20 mpaka mapema leo asubuhi.
Taarifa zaidi zitawajia japo inaelezwa ni vigumu kwa sasa kupatikana kwa mtu aliyehai katika kifusi kinachoendelea kufukuliwa kwa kushirikisha vikosi vya majeshi na wasamaria wema waliojitokeza tangu jengo hilo linalodaiwa la orofa 16 kuporomoka asubuhi ya jana wakati watu wakiendelea na ujenzi.

No comments:

Post a Comment