STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 30, 2013

Maiti 21 zapatikana ajali ya ghorofa, nane washikiliwa na Polisi

Ibrahim Kissoki (kushoto) anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dar kuhusiana na ajali ya jengo lililoporomoka jana asubuhi. Hapa alikuwa akimfafanulia jambo Naibu Waziri wa Ujenzi, Gerson Lwenge.


WAKATI maiti nyingine ikiwa imepatikana jioni hii na kufanya idadi ya waliokufa kwenye ajali ya jengo la ghorofa 16 lililoporomoka kufikia 21, watu nane akiwamo Diwani wa Goba, Ibrahim Kissoki wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kutokana na mkasa wa ajali hiyo.
Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, RPC Suleiman Kova, amenukuliwa hivi punde kuwa Kissoki ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni yua Ujenzi ya Lucky Construction Ltd na watu wengine saba akiwamo wamiliki wa jengo hilo na wakandarasi na maafisa wa Manispaa ya Ilala wanashikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano zaidi ili kubaini chanzo cha ajali hiyo.
Kova, alisema mpaka sasa wakati zoezi la uokozi likiendelea eneo la tukio mitaa ya Indra Ghandi na Zanaki watu waliofariki katika ajali hiyo ni 21, nane kati yao wakiwa wameshatambuliwa na ndugu zao.
Kamanda huyo alisema wanaendelea kusaka wahanga wa ajali hiyo kuona kama watapata miili minmgine ya waliozikwa na kifusi cha jengo hilo linalomilikiwa na mfanyabiashara maarufu nchini, Ally Raza.
Tunaendelea kufuatilia taarifa na tutawaletea hapa hapa.

No comments:

Post a Comment