STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 30, 2013

Idadi ya waliokufa ajali ya Ghorofa yaongezeka


IDADI ya watu waliofariki katika tukio la kuporomoka kwa ghorofa lilililokuwa likijengwa imeongeza na kwa sasa imefikia watu 20.
Tayari watu waliopoteza ndugu zao katika ajali hiyo iliyotokea jana kweye mtaa wa Indra Ghandi wamemiminika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kutambua miili ya ndugu zao.
Mpaka sasa miili ya watu nane imetambuliwa wakiwemo watu watatu wenye asilia ya Asia na wengine waliosalia wakiwa ni wafanyakazi waliokuwa wakijenga ghorofa hilo.
Pia hospitalini hapo imeonwa viungo vya watoto na watu wazima vilivyokatika na kutia hali ya simanzi, huku juhudi zikifanywa kupata majina ya watu waliopoteza uhai huo na wale ambao wamenusurika kwenye ajali hiyo.

  

No comments:

Post a Comment