STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 30, 2013

Vita vya Ligi Kuu Bara ndiyo kwanza vimeanza


 
http://3.bp.blogspot.com/-4Yv7aB6pBF4/UQJ6EXASNmI/AAAAAAAAiMo/jfdsnoiqHiQ/s1600/VPL.png
MATOKEO ya mechi zilizochezwa jioni ya leo za Ligi Kuu Tanzania Bara yamebadili msimamo na kutoa dalilia kwamba vita vya kuwania ubingwa na vya kuepa kushuka daraja vimeanza upya.
Yanga na Azam zinaendelea kubanana kwenye uwaniaji wa ubingwa, huku Toto African, Polisi Moro, African Lyon zikiwa bado katika vita kali ya kuepuka kushuka daraja mkiani.
Sare ilizopata Toto African na Polisi Morogoro katika viwanja vyao vya nyumbani dhidi ya wapinzani wa jadi nchini, Simba na Yanga zimezifanya timu hizo kurejea mkiani wakiipokea Lyon.
Toto imerudi mkiani ikilingana pointi 18 na Polisi ila uwiano wa mabao ndiyo unaowatofautisha nyuma ya Lyon walioifumua Coastal bao 1-0 na kufikisha pointi 19.
Kileleni, licha ya Yanga kuendeleza rekodi ya kutopoteza mchezo wowote wa ligi hiyo ndani ya mwaka 2013, lakini imeshindwa kutimiza ndoto ilizokuwa nazo leo za kuivua Simba ubingwa iwapo ingeshinda mbele ya Polisi na sare iliyopata Simba jijini Mwanza.
Suluhu ya kutofungana imeifanya Yanga kufikisha pointi 49 na kuendelea kuipa nafasi Azam kuwakaribia baada ya wauza Lambalamba haop kushinda bao 1-0 uwanja wa Mabatini.
Kagera iliyosaliwa na mechi nne imenufaika na kucheza nyumbani kwa kushinda mechi ya pili mfululizo na kukwea nafasi ya tatu, ikiiengua rasmi Simba, huku Coastal Union yenye ndoto za kumaliza katika Tatu Bora imekwama mbele ya Lyon, huku JKT Ruvu iliyozinduka katika mechi yao ya mwisho dhidi ya Polisi Moro imeendelea kuchechemea msimu huu.
Misimu mitatu iliyopita JKT Ruvu ilitisha na ukali wake kwa sasa umehamia kwa Ruvu Shooting ambayo hata hivyo leo ilishindwa kukwepa kipigo cha nyumbani mbele ya Azam waliosalia nafasi ya pili katika msimamo huo wa ligi kuu.
Msimamo kamili wa Ligi hiyo ilioyosaliwa raundi chache kabla ya kufunga msimu ni kama ifuatavyo:

                                  P     W    D     L     F      A       D      Pts
1. Young Africans     21   15     4     2     37     12     +25   49
2. Azam                    21   13     4     4     36     16     +20   43     

3. Kagera Sugar        22   10     7     5     25     18     +7     37    
4. Simba                   21     9     8     4     30     19     +11    35 

5. Coastal Union      22     8     8     6     23     20     +3      32   
6. Mtibwa Sugar      22     8     8     6     24     22     +2      32   
7. Ruvu Shooting     21     8     5     8     21     19     +2      29    
8. JKT Oljoro FC     22     7     7     8     22     24     -2      28    
9. JKT Mgambo      21     7     3     11     14     21     -7     24
10.Ruvu Stars          21     6     4     11     19     34     -15   22
11.Tanzania Prisons 21     4     8     9       11     20     -9     20   
12.African Lyon      22     5     4     13     15     32     -17   19
13.Polisi Morogoro  22     3     9     10     11     21     -10   18   
14.Toto Africans      22     3     9     10     19     30     -11   18
            

No comments:

Post a Comment