STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 23, 2016

RB Battery yanogewa Mbeya City, yaongeza mkataba mpya

KAMPUNI ya BinSlum Tyre ya jijini Dar es Salaam, leo Alhamisi imesaini mkataba mpya wa miaka miwili wenye thamani ya Sh. 360 Milioni kuendelea kuidhamini klabu ya Mbeya City FC.
777
Mara baada ya kusaini mkataba huo, Kaimu Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Mohammed BinSlum alisema, licha ya City kuwa na matokeo yasiyoridhishwa kwa msimu uliopita, lakini wameridhishwa kwa kiasi kikubwa namna ambavyo timu hii ilishiriki katika kuitangaza bidhaa yao  na kuifikisha sehemu ilipostahili kufika.
“City haikuwa na matokeo mazuri msimu ulipopita, lakini hatuna shaka na namna walivyoitangaza bidhaa yetu, imani yetu kubwa ni kuwa  mkataba huu mpya itakuwa chachu kwao ya kufanya vizuri zaidi msimu ujao,”  alisema BinSlum.
Naye Meya wa Jiji la Mbeya, David Mwasilindi, aliishukuru kampuni ya BinSlum kwa kuthamini mchango wa City licha ya matokeo mabaya  msimu uliopita ambapo timu hiyo ilimaliza katika nafasi ya nane.
“Hatukuwa sawa msimu uliopita, matokeo tuliyoyapata si yale ambayo tumekuwa tukiyapata misimu miwili iliyopita, imani yangu kubwa tutafanya vizuri msimu ujao, nawashukuru BinSlum kwa kutambua mchango wetu kwao, hii ni chachu kwetu kuelekea mafanikio ya msimu ujao” alisema.
ccc

Chelsea yammezea mate Koulibaly wa Napoli,

http://img.20mn.fr/txPrUEwrTRCJig7saa8abQ/2048x1536-fit_kalidou-koulibaly-lors-lazio-naples-18-janvier-2015.jpg
Kalidou Koulibaly
IKIJIANDAA kumpokea Kocha wake mpya, Antonio Conte, klabu ya Chelsea imedaiwa ipo kwenye mawindo dhidi ya beki wa Napoli, Kalidou Koulibaly ikitoa  ofa ya Pauni Milioni 19.2.
Chelsea imekuwa ikimzimia kupita kiasi beki huyo wa kimataifa wa Senegal, ambaye ameingia katika mzozo na klabu yake kuhusiana na uhamisho wake.
Licha ya mzozo huo, tayari kuna taarifa kwamba ofa hiyo ya Chelsea imeshakataliwa na Napoli ikidaiwa inataka kitita cha Pauni Milioni 30, ili imuachie nyota huyo mwenye umri wa miaka 24.
Klabu ya Napoli ilichukizwa na Koulibaly kufuatia madai aliyotoa kuwa yuko tayari kuzungumza na Chelsea.
Beki huyo alisema hajazungumza na Kocha Antonio Conte, lakini anadhani hilo litafanyika hivi karibuni, baada ya kumaliza majukumu yake ya Euro akiiongoza timu ya taifa ya Italia iliyotinga hatua ya 16 Bora kwa sasa nchini Ufaransa

Copa America 2016 ni Chile na Argentina tena

Fun and games in Chicago. 
https://heavyeditorial.files.wordpress.com/2016/06/gettyimages-542227446.jpg?quality=65&strip=all&strip=allCHILE imetinga fainali za Copa America kwa mara ya pili mfululizo na watavaana na Argentina katiak mechi inayorejea fainali za mwaka jana ambapo ilibeba taji kwa ushindi wa bao 1-0.
Watetezi hao walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Colombia katika mechi ya Nusu Fainali iliyosimama kwa muda wa saa mbili kutokana na hali mbaya ya hewa ya jiji la Chicago lililotumiwa kwa mchezo huo mkali.
Mabao ya mapema ya kipindi cha kwanza kupitia kwa Charles Aranguiz aliyefunga dakika ya 7 na jingine la Jose Fuenzalida aliyetumbukiza kimiani dakika 11 yalitosha kwa Chile kutinga fainali na sasa itavaana na Argentina iliyotangulia mapema jana.
Argentina iliisasambua wenyeji Marekani kwa kuicapa mabao 4-0, huku nahodha Lionel Messi akifunga bao la tatu lililomfanya aweke rekodi ya kuwa Mfungaji Bora wa muda wote wa taifa hilo akifikisha bao la 55 na kuipiku rekodi ya Gabriel Batistuta aliye na mabao 54.
Katika fainali zilizopita Argentina ilikubali kipigo cha mkwaju ya penalti 4-1 na kuwapa wenyeji Chile taji lao la kwanza katika historia ya michuano hiyo iliyoasisiwa miaka 100 iliyopita (1916).
Pambano hilo la fainali za mwaka huu zitachezwa Jumapili kwenye Uwanja wa
MetLife, East Rutherford ambapo pia mbali na mataifa hayo kusaka ubingwa pia zitakuwa katika vita ya nyota wao, Eduardo Vargas wa Chile mwenye mabao 6 na Messi mwenye mabao matano watakaokuwa wakiwania Kiatu cha Dhahabu
.

Chile ilivyoifuata Argentina fainali za Copa America 2016

Ronaldo azinduka, Ureno yapenya 16 Bora, Ufaransa, Ireland kimbembe

ronaldo.jpg
Ronaldom akishangilia moja ya mabao yake ya usiku wa kuamkia leo yaliyoibeba Ureno kuambulia sare na kutinga 16 Bora
CRISTIANO Ronaldo ameondoa gundu kwa kuifungia timu yake mabao mawili wakati Ureno ikisaka sare ya tatu mfululizo katika mechi zake za Kundi F za michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya (Euro 2016) dhidi ya Hungary.
Timu hizo zilitoshana nguvu kwa kufungana mabao 3-3, huku Ureno kupitia Ronaldo wakilazimika kusawazisha mara zote kuambulia pointi iliyowabeba kama mshindwa bora.
Sare hiyo imeisaidia Ureno kuingia hatua ya mtoano ya 16 Bora kama mshindi wa tatu na sasa itakutana na Croatia katika mechi itakayopigwa Jumamosi hii.
Iceland inayoshiriki kwa mara ya kwanza imendelea kufanya maajabu kwa kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Austria na kusonga mbele kama mshindi wa pili wa kundi hilo wakilingana pointi na vinara Hungary.
Italia nayo ilipoteza mechi yake ya mwisho dhidi ya Ireland nma Belgium ikaizabua Sweden bao 1-0 na kumtia aibu Zlatan Ibrahimovic ambaye amestaafu timu hiyo akishindwa kuifungia timu yake bao lolote katika fainali hizo za Euro 2016. Sweden imeaga michuano hiyo ikiwa ina pointi moja na bao moja la kufunga.
Kwa mujibu wa ratiba ya hatua hiyo ya 16 Bora, wenyeji Ufaransa watavaana na Ireland na kukumbushia tukio la mwaka 2010 wakati Thierry Henry alipoivusha timu yake kwa bao la mkono dhidi na wapinzani wao hao.
Ratiba kamili ya 16 Bora ipo hivi:
Juni 25, 2016
Uswisi  v    Poland       
Wales    v   Ireland ya Kaskazini
Croatia v    Ureno

Juni 26, 2016
Ufaransa    v Ireland       
Ujerumani v Slovakia
Hungary    v Belgium       

Juni 27, 2016
Italia      v Hispania
England v Iceland