STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, June 28, 2014

Kimbembe cha 16 Bora leo, nani kufuzu Robo Fainali?!


Colombia
Uruguay
KIVUMBI cha hatua ya mtoano cha 16 Bora cha Fainali za Kombe la Dunia 2014  kinatarajia kuanza kutimka rasmi leo wakati wenyeji Brazil na nchi nyingine tatu za Amerika Kusini zitakapochuana kuwania nafasi ya kutinga hatua ya Robo Fainali ya michuano hiyo inayoendelea nchini Brazil.
Brazil chini ya nyota wake wakiongozwa na Neymar watakawakabili majirani zao Chile, huku Colombia itapepetana na Uruguay itakayomkosa nyota wake Luis Suarez aliyefungiwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kwa kitendoi cha kumuuma mchezaji Giorgio Chiellini wa Italia.
Wenyeji waliongoza msimamo wa kundi A mbele ya Mexico watashuka dimbani mapema saa 1 usiku kwenye uwanja wa Governador Magalhães Pinto, kuwakabili Chile watakaomtegemea Alexis Sanchez katika mechi inayosubiriwa kwa hamu kuona kama Brazil watatoka salama kwa wapinzani wao.
Ingawa rekodi zinaonyesha kuwa, timu hizo zimeshakutana mara 68 na Brazil ikiwatambia wapinzani wao mara 48 na kufungwa mara 7 na kutoka sare michezo 13, huku wenyeji hao wakifunga jumla ya mabao 159-58 katika michezo waliyokutana, bado Chile siyo timu ya kubezwa.
Katika fainali za mwaka huu wakiwa kundi B waliweza kumaliza katika nafasi ya pili bila kutarajiwa mbele ya waliokuwa mabingwa watetezi Hispania na Australia walizozipatia katika mechi za makundi.
Katika michuano ya  Kombe la Dunia hatua ya Mtoano, Brazil na Chile zimekutana mara 3 na zote Brazil kushinda. Mwaka 1962, kwenye Nusu Fainali, Brazil ilishinda 4-2. Mwaka 1998, Raundi ya Mtoano ya Timu 16, Brazil walishinda 4-1 na huko Afrika Kusini, Mwaka 2010 pia Raundi ya Mtoano ya Timu 16, Brazil ilishinda 3-0.
Hata hivyo tayari kocha wa Chile, Jorge Luis Sampaoli Moya kutoka Argentina amesema watashuka dimbani leo kuhakikisha wanapata matokeo bora ili kuona kikosi chake kinavuka hatua hivyo, licha ya kukiri ni mtihani mgumu mbele ya Brazil yenye nyota kama Neymar.
Cha kuvutia katika mechi hiyo ni kwamba itachezeshwa na refa Howard Webb kutoka England ambaye hii itakuwa ni mara yake ya pili kuzipambanisha timu hizo katika hatua kama hiyo.
Ndiye aliyezihukumu katika Fainali zilizopita nchini Afrika Kusini ambapo Brazil waling'ara kwa kushinda kwa mabao 3-0 kabla ya kwenda kung';oka mbele na kuziacha Hispania na Uholanzi zikicheza fainali.
Pambano jingine litakalochezwa leo litazikutanisha timu za Colombia na Uruguay pambano litakalochezwa usiku wa saa 5 kwenye uwanja wa mkubwa wa Maracana.
Uguruay itashuka dimbani bila huduma za Suarez aliyerudishwa nyumbani kutokana na kitendo cha kufungiwa na FIFA kwa kosa la kumng'ata mchezaji wa Italia Giorgio Chiellini wakati wa mechi ya kufungia pazia la hatua ya makundi na Uguguay kushinda kwa bao 1-0 na kutinga bila kutrarajiwa nyuma ya Costa Rica.
Pambano hilo linatarajiwa kuwa tamu pengine kuliko lile la Brazil na Chile kutokana na Colombia kuwa miongoni mwa timu zisizotabirika na kati ya chache zilizoshinda kwa asilimia 100 michezo yao ya makundi.
Ikiongozwa na James Rodriguez aliyeziba kwa mafanikio pengo la Radamel Falcao ambaye aliondolewa kwenye kikosi hicho kutokana na majeraha, Colombia inatarajiwa kutoa upinzani mkali.
James Rodriguez ana mabao matatu mpaka sasa kwenye michuano hiyo akishika nafasi ya pili pamoja na nyota wengine wa timu zilizoshiriki michuano hiyo na atakuwa akisaidiana kusaka ushindi kuvuka hatua hiyo na wachezaji wenzake kama Jackson Martínez,Armero, Cuadrado na Gutierrez.
Hata hivyo Uruguay pamoja na kumkosa Suarez, bado ina silaha kali kama Edinson Cavani, Diego Godin, Arevalo na wengine kuhakikisha wanafanya kweli katika mechi hiyo ambayo itakuwa ni ya 15 kwa timu hizo kukutana katika michezo mbalimbali tangu mwaka 2005.
Rekodi zinaonyesha katika kukutana huko, Uruguay imeitambia Colombia mara 8 na kupoteza mechi nne na mbili zilizosalia walitoshana nguvu kwa kutoka sare.
Je, ni Brazil au Chile itakayokuwa ya kwanza kufuzu robo fainali na Colombia itaendelea kuwa mnyonge kwa Uruguay na kupigwa kumbo kutinga hatua inayofuata au watajitutumua na kuinyuka Uruguay bila ya Suarez? Tusibiri tuone baada ya kumalizika kwa mechi hizo kabla ya kesho kushuhudia kitupe kingine.

Liverpool sasa kumuua Suarez kuwabeba Lallana na Markovic

Suarez akiwajibika siku ya mechi dhidi ya England kabla ya kuja kuharibu wakiumana na Italia
KLABU ya soka ya Liverpool ipo kwenye mpango wa kumuuza nyota wake Luis Suarez katika klabu ya Barcelona, ili kupata fedha za kuwanyakua Adam Lallana na Lazar Markovic.
Barcelona imetajwa kuoingoza mbio za kumnyakua mchezaji huyo aliyefungiwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) baada ya kumng'ata beki wa Italia Giorgio Chiellini .
Klabu hiyo ya Hispania imeweka wazi kuwa hata kama Suarez amefungiwa miezi minne kucheza soka, hiyo haizuii nia yao ya kumsajili na mpaka sasa Liverpool hawajahangaika kutafuta mbadala wa mshambuliaji huyo hatari.
Ingawa Liverpool walikuwa wanaweka ngumu kwa dau hilo, lakini baada ya kupokea taarifa za FIFA kuhusu kumfungia Suarez wamelazimika kukubali na kumruhusu Muurguay huyo kuondoka klabuni hapo.
Licha ya kufungiwa, Liverool wanaamini Barcelona inaweza kulipa paundi milioni 80 na tayari mmiliki mkuu wa klabu hiyo John W Henry anaonekana kutokuwa tayari kumuuza kwa bei rahisi.
Mwanasheria wa Suarez Alejandro Balbi alikuwa Barcelona kujadili hatima ya mteja wake, wakati kocha mpya wa Barca Luis Enrique alisema hakuna tatizo lolote juu ya kumsajili nyota huyo mwenye miaka 27.
Alimfananisha Suarez na mshambuliaji gwiji wa Barca Hristo Stoichkov na alisema : ‘Stoichkov kiukweli aliwahi kufanya madhambi makubwa dhidi ya mwamuzi, lakini aliendelea kufirika kuwa mcheza mkubwa".
Kama Liverpool watamuuza Suarez kwa paundi milioni 80, hiyo itakuwa biashara nzuri kwa Brendan Rodgers ambapo atatumia mkwanja huo kuimarisha kikosi chake.
Wachezaji ambao Liverpool inawapigia jaramba kuwanasa ni Adam Lallana kutoka Southampton anayetajwa atakuwa mali ya Vijogoo hao wekundu  saa 24 zijazo baada ya Southampton kukubali ofa ya paundi milion 25 kwa mshambuliaji huyo wa England, na hii ni baada ya kupita wiki nne tangu apokee simu kutoka kwa maofisa wa Anfield ambao pia wameanza mbio za kumuwania mchezaji wa Benfica, Lazar Markovic.
Mserbia, Markovic ni moja ya wachezaji bora wenye umri mdogo katika soka la Ulaya na bei yake ni paundi milioni 20.

Neymar, Muiller, Messi wabanana kuwania kiatu cha Dhahabu

Neymar wa Brazil
Lionel Messi wa Argentina
Thomas Muiller wa Ujerumani  
WAKATI  kinyang'anyiro cha hatua ya mtoano ya 16 Bora ikianza rasmi leo kwa michezo miwili itakayozikutanisha timu za Amerika Kusini, hatua ya makundi ya Fainali za Kombe laDunia 2014 imevunja rekodi.
Jumla ya mabao 136 yamefungwa katika hatua hiyo, sita zaidi ya yale yaliyofungwa katika fainali za 2002.
Wachezaji watatu, Lionel Messi wa Argentina, Neymar wa Brazil na Thomas Muiller wa Ujerumani wanachuana kileleni katika orodha ya wafungaji bora.
Kila moja kati ya wachezaji hao amefunga mabao manne wakifuatiwa na wachezaji sita wenye mabao matatu kila mmoja.
Neymar ana nafasi ya kuongeza idadi ya mabao yake kama leo ataendelea kucheka kwenye mechi yao na Chile kuwania kufuzu Robo Fainali.
Messi atakuwa na nafasi ya kuendelea kunguruma wakati atakapoiongoza Argentina kuvaana na Uswisi siku ya Jumatatu katika mechi nyingine ya 16 Bora.
Ukiondoa wakati hao wenye mabao manne, wachezaji wenye magoli matatu kila mmoja ni pamoja na Robin van Persie, Arjen Robben wote wa Uholanzi, Karim Benzema wa Ufaransa, Enner Valencia wa Ecuador, James Rodriguez wa Colombia na Xherdan Shaqiri wa Uswisi.
Kati ya hapo ni Valencia tu ndiye hana nafasi ya kuongeza idadi yake ya mabao kwa vile timu yake imeshaaga michuano hiyo nchini Brazili.
Katika orodha ya wafumania nyavu hiyo pia wapo wachezaji wenye mabao mawili mawili ambao ni;Tim Cahill wa Australia, Mario Mandzukic wa Croatia, Martinez wa Colombia, Dempsey wa Marekani, Wilfried Bony wa Ivory Coast, Andre Ayew wa Ghana, Asamoah Gyan wa Ghana, Ahmad Mussa wa Nigeria na Slimani wa Algeria.
Ukimuondoa Dempey wa Marekani, Mussa wa Nigeria na Slimani wa Algeria waliosalia timu zaoi zimeshaaga michuano na hivyo hawana nafasi ya kuongeza idadi.

Mashetani Wekundiu wazidi kujiimarisha England

Jembe Jipya! Luke Shaw akiwa na jezi mpya ya klabu yake ya Manchester United
Ander Herrera alipotangazwa ramsi kujiunga kwa Mashetani Wekundu
MABINGWA wa zamani wa England, Manchester United imezidi kuimarisha kikosi chake baada ya kufanikiwa kumsainisha beki wa kushoto wa Southamptom na timu ya taifa ya nchi hiyo iliyotolewa kwenye Kombe la Dunia, Luke Shaw.
Kwa mujibu wa duru za kandanda za England zinasema kuwa, Mashetani Wekundu hao wamekamilisha uhamisho wa Shaw kwa gharama za Pauni Milioni 31.5 kwa mkataba wa miaka minne.rd.
Mchezaji huyo amekamilisha vizuri vipimo afya katika Uwanja wa mazoezi wa United, Carrington na ameambiwa atakuwa beki wa kushoto chaguo la kwanza la kocha Louis van Gaal.
Inafahamika amehakikishiwa namba na beki mkongwe mwenye umri wa miaka 33, Patrice Evra, ambaye atabakia United, anatarajiwa kupunguziwa majukumu klabuni hapo. 
Usajili wa Shaw umekuja siku moja baada ya klabu hiyo kufanikiwa kunyakua Ander Herrera kutoka Athletic Bilbao kwa ofa ya pauni milioni 29.
Man United ilikuwa na msimu mbaya ligi iliyopita chini ya kocha David Moyes ambaye alitimuliwa na nafasi yake kushikiliwa kwa muda Ryan Giggs kabla ya Luis van Gaal kupewa kibarua cha kuwa kocha mkuu sasa.

Soma orodha ya waliochaguliwa Kidato cha Tano 2014

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi nchini, imetoa  majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na shule mbalimbali kwa ajili ya kuendelea na elimu ya sekondari kidato cha tano, sanjari na vyuo mwaka 2014.

Orodha hiyo imetangazwa jijini Dar es salaam tangu Juni 17, ambapo idadi ya wasichana waliochaguliwa kwa nafasi hizo ni 9,378, waliochaguliwa katika machaguo 13 ya masomo mbalimbali ya kidato cha tano na masomo 11 ya vyuo vya ufundi.

Shule zilizopangiwa wanafunzi ni 201, ambapo shule za wasichana pekee ni 61, huku shule 34 zikiwa za jinsia zote mbili, wasichana na wavulana.

Idadi ya wanafunzi wavulana waliochaguliwa katika machaguo 13 ya masomo mbalimbali ya ngazi hiyo, ni 22,138.
Kupata Majina Hayo tafadhali bonyeza Links Hizi Hapa chini

Tuesday, June 24, 2014

Hatma ya Ivory Coast, Italia, Uruguay leo Brazili

Suarez ataendelea kuwatungua makipa leo Brazili?
Tembo wa Afrika watashangilia tena kama hivi kwa Ugiriki leo nchini Brazili?
HATMA ya Ivory Coast na Italia kuendelea kubaki kwenye Fainali za Kombe la Dunia inatarajiwa kufahamika leo wakati mechi za Kundi C na D zitakapochezwa usiku wa leo kukamilisha ratiba yao zitakapochezwa kwenye viwanja vinne tofauti.
Ivory Coast itavaana na Ugiriki ikihitaji ushindi ili kuungana na Colombia kucheza hatua ya 16 Bora, huku Italia itavaana na Uruguay inayochuana kuwania nafasi ya kuungana na Costa Rica kucheza hatua ya pili.
Italia ilitulizwa na Costa Rica katika mechi yao iliyopita na kuwafanya kuomba dua ishinde leo ili kufuzu hatua ya pili vinginevyo itaunga na England kutoka kwenye michuano hiyo.
England iliyopoteza mechi zake mbili zaawali itakamilisha ratiba kwa kuvaana na Costa Rica katika mechi nyingine ya kundi D ambapo matokoe yoyote hayawezi kubadilisha chochote kwa timu hizo mbili.
Katika mechi nyingine zinazochezwa usiku wa leo, Ivopry Coast wenye pointi tatu nyuma ya Colombia itakuwa na kibarua kigumu kuvaana na Ugiriki, wakati vinara wa kundi C, Colombia watavimbiana vifua na Japan.
Mpaka sasa katika kundi hilo ni Colombi tu iliyojihakikishia nafasi huku Japan, Ugiriki na Ivory Coast zote zikiwa na nafasi sawa kama watafanya vema katika mechi hizo za kufungia ratiba.
Japan ikipata ushindi kwa Colombia na Ugiriki ikailaza Ivory Coast moja ya timu hizo itafuzu kwa uwiano wa mabao au walivyoumana wenyewe kwa kwenyewe kuungana na Colombia.
Hata hivyo Ivory Coast wanaoshika nafasi ya pili wanapewa nafasi kubwa kufuzu hatua ya pili iwapo italazimisha sare dhidi ya Ugiriki, vinginevyo isubiri miujiza kama inayosubiri Italia kwa Uruguay.

Ratiba ya mechi za LEO:
Costa Rica  vs  England (Saa 1 Usiku)
Italia vs     Uruguay (Saa 1 Usiku)
Japan vs    Colombia (Saa 5 Usiku)
Ugiriki  vs Ivory Coast (Saa 5 Usiku)

Stars kuzivaa Botswana, Lesotho kirafiki ughaibuni

TIMU ya soka ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajia kucheza mechi mbili za kirafiki za kimataifa dhidi ya wenyeji Botswana na Lesotho kwa ajili ya kujiandaa kuivaa Msumbiji (Mambas) imeelezwa jana jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa, alisema kuwa tayari vyama vya soka vya nchi hizo mbili vimethibitisha kuwepo kwa michezo hiyo itakayofanyika jijini Gaborone.

Mwesigwa alisema kuwa Taifa Stars itaanza kuwakabili wenyeji Julai Mosi mwaka huu na baadaye Julai 5 itashuka kucheza mechi ya pili kwa kuivaa timu ya Taifa ya Lesotho.
Katibu huyo wa zamani wa Yanga alisema kuwa maandalizi ya safari yamekamilika na kikosi cha Stars kinatarajia kuondoka nchini leo saa 12:00 asubuhi kuelekea Gaborone.
Alisema kwamba nyota wote 26 waliotajwa wataondoka na wanaamini kambi hiyo itasaidia kukiimarisha kikosi hicho kinachohitaji ushindi ili kiweze kuingia hatua ya makundi.

Aliwataja wachezaji watakaosafiri leo wakiwa chini ya Mholanzi, Mart Nooij, ni pamoja na Deogratias Munishi 'Dida', Aishi Manula, Benedictor Tinoko, Kelvin Yondani, Said Moradi, Nadir Haroub 'Cannavaro', Joram Nason, Shomari Kapombe, Oscar Joshua, Edward Charles, Aggrey Morris na Pato Ngonyani.

Wachezaji wengine ni Frank Domayo, Amri Kiemba, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Said Juma, Haroun Chanongo, Himid Mao, John Bocco, Simon Msuva, Kelvin Friday, Ramadhan Singano 'Messi', Khamis Mcha, Mrisho Ngasa na Mwegane Yeya.

Mechi ya kwanza kati ya Taifa Stars dhidi ya Mambas itakuwa kati ya Julai 19 na 20 na marudiano yatafanyika mjini Maputo baada ya wiki mbili.

Stars ilifanikiwa kusonga mbele katika mashindano hayo ya kusaka tiketi ya kucheza fainali za mwakani za Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuifunga Zimbabwe jumla ya magoli 3-2.

Chuji, Luhende watupiwa virago Yanga, Barthez, Tegete wabakishwa

Chuji ametemwa
Barthez kabakishwa Jangwani

Tegete (kulia) aliyebakishwa akiwa na baba yake John Tegete
KLABU ya soka ya Yanga imetangaza kuwatema kundini nyota wake kama Athuman Idd 'Chuji', beki David Luhembe na Ibrahim Job, huku ikiwasainisha mikataba mipya wakali kama Ally Mustafa 'Barthez', Jerry Tegete na Oscar Joshua.
Kupitia tovuti ya klabu hiyo, ambayo msimu uliopita ilikua na kikosi bora kabisa ambacho kiliweza kuwatoa jasho Mabingwa wa Kihistoria Barani Afrika timu ya Natioal Al Ahly katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika, ambapo Mabingwa hao wa kutoka nchini Misri waliweza kusonga mbele kwa mikwaju ya penati imewatema jumla ya wachezaji 11.
Msimu uliopita Young Africans ilikuwa na kikosi cha wachezaji 30 kutoka timu ya Wakubwa na wachezaji watano (5) kutoka timu ya vijana (U20) waliokuwa wamepandishwa kwa ajili kupata uzoefu na kuingozea nguvu timu ya wakubwa katika michezo mbalimbali.
Kutokana na ripoti ya Benchi la Ufundi iliyowasilishwa mara baada ya kumalizika kwa Msimu wa Ligi Kuu 2013/2014 baadhi ya wachezaji hawataitumikia tena Yanga SC kwenye msimu ujao, wachezaji 11 wamemaliza muda wao na kumalizana na uongozi hivyo wapo huru kujiunga vilabu mbalimbali:
Wachezaji hao waliotemwa ni:
1. David Luhende
2. Athuman Idd “Chuji”
3. Geroge Banda -U20
4. Yusuph Abdul -U20
5. Rehani Kibingu -U20
6. Hamisi Thabiti
7. Reliants Lusajo
8. Bakari Masoud – U20
9. Shaban Kondo
10. Abdalllah Mguhi “Messi” U-20
11. Ibrahim Job

Neymar aiua Cameroon, Spain yaondoa gundu, Mexico we acha









WAWAKILISHI wa Afrika Cameroon 'Wazee wa Posho' wameaga kwa aibu michuano ya Kombe la Dunia baada ya usiku wa kuamkia leo kukandikwa mabao 4-1 na wenyeji Brazil na kumaliza mechi zake bila kuambulia pointi hata moja, tofauti na waliokuwa watetezi Hispania walioondoa gundu kwa kuilaza Australia kwa mabao 3-0 katika mechi za kukamilisha michezo ya makundi.
Nyota wa Brazil anayekipiga Barcelona, Neymar ndiye aliyekuwa mwiba wa Cameroon baada ya kufunga mabao mawili na kukwea hadi kileleni kwenye orodha ya wafungaji wa fainali hizo za 20 za Kombe la Dunia akifikisha jumla ya mabao manne.
Neymar alifunga mabao yake katika dakika za 17 na 34, wakati mabao mengine yalifungwa na Fred dakika ya 49 na Fernandinho dakika ya 84, huku bao pekee la Cameroon likitumbukizwa kimiani na Matip dakika ya 26
Katika mechi nyingine ya kundi hilo la A, Mexico nayo ilimaliza na ushindi wa 3-1 dhidi ya Croatia, mabao yake yakifungwa na Rafael Marquez, Andres Guardado na Javier Hernandez. Bao la kufutia machozi la Croatia iliyompoteza mchezaji wake Ante Rebic aliyetolewa kwa kadi nyekundu mwishoni mwa mchezo, lilifungwa na Ivan Perisic.
Brazil inamaliza na pointi saba sawa na Mexico, lakini inakaa kileleni kwa wastani mzuri zaidi wa mabao na sasa wenyeji hao watavaana na Chile katika mechi ya 16 Bora huku Mexico wakivaana na Uhalanzi waliopata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Chile usiku wa jana.
Watetezi Hispania waliotemeshwa tajhi mapema waliaga michuano hiyo kwa heshima kwa kuicharaza Australia mabao 3-0, magoli yaliyowekwa kimiani na David Villa katika dakika ya 36, Fernando Torres dak.69 na Juan Mata dk. 82.
Katika mechi ya Uholanzi na Chile, mabaio ya washindi yaliwekwa kimiani na Fer katika dakika ya 77 na Depay na kumaliza kwenye kundi B ikiwa kinara kwa kushinda mechi zote na kufikisha pointi 9.

Onesmo Waziri Ticotico kuzikwa kesho Mafinga, wadau wamlilia

Herry Morris akimfariji dada wa marehemu Ticotico (Picha Zote kwahisani ya Geofrey Chambua)

Hili ndilo gari lililochukua uhai wa Ticotico, baadahi ya watu wakilishangaa
Inauma sana!
 


Ticotico (jezi no 11 akiwa na wachezaji wenzake wa Golden Bush katika pambano lililochezwa mjini Morogoro
MWILI wa marehemu Onesmo Waziri 'Ticotico' mmoja wa wadau wakubwa wa soka nchini unatarajiwa kuzikwa kijijini kwao Rugemba mjini Mafinga siku ya kesho.
Ticotico alikumbwa na mauti baada ya kupatwa na ajali usiku wa kuamkia Jumapili walipoenda mjini humo na klabu yake ya Golden Bush Veterani kwa ajili ya mechi za kirafiki za bonanza zilizokuwa zichezwe asubuhi ya Jumapili ambayo ingehusisha timu za Mafinga, Njombe na Makambako pamoja na Golden Bush ya jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa toka mjini humo zinasema kuwa mwili wa marehemu ambao uliharibika vibaya kutokana na ukubwa wa ajali hiyo utahifadhiwa kesho Jumatano baada ya taratibu zote za Ibada.
Inaelezwa kuwa marehemu alikumbwa na ajali hiyo karibu na kijiji chao baada ya kulivamia lori lililokuwa limeegeshwa pembeni na kuumia vibaya maeneo ya kichwani na kifuani, ikiwa ni muda mchache baada ya kuagana na wachezaji wenzake kwa ajili ya kujiandaa na bonanza hilo la siku ya Jumapili.
Kwa mujibu wa mmoja wa viongozi waandamizi wa Golden Bush, Geofrey Chambua ni kwamba Majira ya usiku akiwaaga wachezaji ambao aliambatana nao kwenye gari yake; Salum Sued 'Kussi', Mwarami Mohamed 'Shilton' Herry Morris na Sadiq Muhimbo kwamba anakwenda kulala.
"liwachukulia kabisa vyumba Mafinga ili waje naye asubuhi hapa Makambako kwa ajili ya Bonanza ambalo ilikua likutanishe timu toka Mafinga, Njombe na Makambako. Baadaye wakiwa wana mtrace (mpigia) kwenye simu akawa hapatikani hadi asubuhi zilipokuja taarifa kwamba amepata ajali na kufariki instantly. Mashushuda walioona gari wanasema inaonekana ilipasuka tairi na kubiringita na hapo ilipo ipo upside down ikiwa imebondeka sana," Chambua alidokeza kwenye ujumbe wa barua pepe.
Alidokeza kuwa 'Mchana wa Jumamosi baada ya kufika salama Mafinga, aliitambulisha Golden Bush Kijijini kwao Rungemba na kuwatambulisha nduguze kisha kusihi wapige picha ya ukumbusho.......Pia alikuwa na alikuwa mwenye furaha sana na alishikana mikono na karibu kila mchezaji  kana kwamba anawaaga (Goodbye!)
Kocha wa timu ya vijana ya Golden Bush, Shija Katina aliyekuwa Arusha wakati Ticotico anakumbwa na mauti, alisema mpaka sasa aamini kama kweli Mr Football ametangulia mbele ya haki.
"Inauma na kuhuzunisha mno, nilipata taarifa nikiwa safarini Arusha na ninageuza kuwahi kumzika rafiki yangu, siamini kama kweli Ticotico hatunaye tena, " alisema Shija kwa masikitiko na kusimulia alivyolia njia nzima baada ya kupewa taarifa hiyo.
Wadau wengine wa soka wamekielezea kifo cha Ticotico kama pigo kubwa kwa familia ya marehemu, jamaa ndugu na wadau wa soka kutokana na ukweli Ticotico alikuwa mtu wa watu na aliyependa mpira pengine kuliko hata kula....
Mungu Aiweke Mahali Pema Roho ya Marehemu Onesmo Waziri 'Ticotico'

Sunday, June 22, 2014

Jahazi la timu ya Babi Malaysia majanga matupu

BAADA ya kugangamala katika mechi yake iliyopita kwa kupata sare ya 2-2 ikitokea kupokea kipigo cha mabao 4-0 katika Ligi Kuu ya Malaysia, timu ya UiTM anayoichezea kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Abdi Kassim 'Babi' imekutana na kiama baada ya kunyukwa mabao 8-0 na Felda United.
Hicho ni kipigo cha kwanza kikubwa kwa timu hiyo ikiwa na Babi aliyewahi kung'ara na timu za Yanga, Azam, Mtibwa Sugar, KMKM na Taifa Stars.
UiTM ilikumbana na pigo hicho uwanja wa ugenini wa Majlis Perbandaran, mjini Selayang baada ya Jumatatu iliyopita kupata sre ya 2-2 kwenye uwanja wake wa nyumbani dhidi ya PBAPP ikitokea ugenini kuchezea kichapo cha 4-0 toka kwa DRB-Hicom.
Katika mchezo huo wa juzi wakati UiTM ikizama kwa 8-0 magoli ya washindi yalifungwa naMohd Raimi katika dakika ya 20, Edward Junior Wilson aliyefunga mawili katika dakika ya  44 na 47 kabla ya Indra Putra Mahayuddin kufunga hat trick kwa magoli ya dakika za 62', 88' na 90 na mengine yakifungwa na '
Ndumba Makeche dakika ya  83' na Mohd Syahid Zaidon dakika moja baadaye.
Kwa matokeo hayo ya juzi, UiTM imeendelea kusaliwa na pointi 21 ikikamata nafasi ya 9 baada ya kushuka dimbani mara 21 mpaka sasa.

Magoli 76 yafungwa Brazili, mbio za kiatu cha dhahabu hatari

van Persie

Benzema
Valencia
Robben

Muiller

WAKATI ngwe ya mwisho ya mechi za raundi za pili zikitarajiwa kufikia tamati leo kwa mechi za Kundi F na H, mpaka sasa jumla ya mabao 76 yamefungwa kwenye Fainali za Kombe la Dunia zinazoendelea nchini Brazili.
Idadi hiyo imefika baada ya mechi za jana kushuhudia mabao sita yakifungwa katika mechi za kundi G na F ambapo Argentina ya Lionel Messi iliifunga Iran bao 1-0, Ghana na Ujerumani kutoshana nguvu kwa kufungana mabao 2-2 na Nigeria kuizodoa Bosnia ya Edin Dzeko kwa bao 1-0.
Mpaka sasa nyota kadhaa wanafukuzana kwenye mbio za kuwania kiatu cha Dhahabu wakiongoza wakiwa na mabao matatu kila mmoja na wengine wakifuata wakiwa na magoli mawili mawili.
Wachezaji wanaoongoza katika orodha hiyo ni Karim. Benzemawa Ufaransa, Thomas  Mueller wa Ujerumani, Enner Valencia wa Ecuador na Arjen Robben na Robin  van Persie wote wa Uholanzi.
Wachezaji wenye mabao mawili kila mmoja mpaka sasa ni pamoja na Tim  Cahill wa Australia, Neymar wa Brazili, Gervinho wa Ivory Coast, Lionel Messi wa Argentina, James Rodriguez wa Colombia, Luis Suarez wa Uruguay na Mario Mandzukic wa Croatia, wakifuatiwa na utitiri wa waliofunga bao moja moja.

Orodha kamili ya wafungaji;
 3-Karim. Benzema- France
Thomas  Mueller-Germany
Arjen Robben-Netherlands
Enner Valencia-Ecuador
Robin  van Persie-Netherlands

2-Tim  Cahill-Australia
Neymar- Brazil
Gervinho-Côte d'Ivoire
Mario Mandžukić-Croatia
Lionel Messi-Argentina
James Rodríguez-Colombia
Luis Suárez-Uruguay
Msimamo wa makundi:
Kundi A
                  P W D L F A PTS

Brazil          2  1  1  0  3  1  4
Mexico       2  1  1  0  1  0  4
Croatia       2  1  0  1  5  3  3
Cameroon  2  0  0  2  0  5  0

Kundi B
                    P W D L F A PTS

 Uholanzi       2  2  0  0  8  3  6
Chile            2  2   0  0  5  1  6
Australia       2  0   0  2  3  6  0
Hispania       2  0  0  2  1  7  0

Kundi C
                     P  W  D  L  F  A  PTS

 Colombia      2   2   0   0  5  1    6
Ivory Coast   2   1   0   1   3  3   3
Japan            2   0   1   1   1  2   1
Ugiriki           2   0   1   1   0  3   1   

Kundi D
                       P  W  D  L F A PTS

Costa Rica      2    2  0  0  4  1  6
Italia                2    1  0  1  2  2  3
Uruguay          2    1  0  1  3  4  3
England           2    0  0   2  2  4  0

Kundi E
                       P W D L F A PTS

Ufaransa          2  2  0  0  8  2  6
Ecuador           2  1  0  1  3  3  3
Uswisi              2   1  0  1  4  6  3
Honduras         2   0  0  2  1  5  0  

Kundi F
                             P W D L F A PTS

Argentina               2  2  0  0  3  1  6
Nigeria                  2  1  1  0  1  0  4
Iran                       2  0  1  1  0  1  1
Bosnia-Herze.       2  0  0  2  1  3  0

Kundi G
                           P W D L F A PTS

Ujeruman            2  1  1  0  6  2  4
Marekani            1  1  0  0  2  1  3
Ghana                 2  0  1  1  3  4  1
Ureno                 1  0  0  1  0  4  0

Kundi H
                  P W D L F A PTS

Belgium      1  1  0  0  2  1  3
Korea        1  0  1  0  1  1  1
Russia        1  0  1  0  1  1  1
Algeria       1  0  0  1  1  2  0

RATIBA :
LEO, Jumapili
Ubelgiji     v Russia        (1:00)
Korea Kusini     v Algeria    (4:00)
Marekani        v Ureno        (7:00)

KESHO, Jumatatu
Australia     v Hispania    (1:00)
Uholanzi     v Chile        (1:00)
Cameroon     v Brazili    (5:00)
Croatia        v Mexico        (5:00)

KESHOKUTWA, Jumanne

Costa Rica     v England    (1:00)
Italia         v Uruguay    (1:00)
Ugiriki         v Ivory C    (5:00)
Japani         v Colombia    (5:00)

JUMATANO, Juni 25
Bosnia        v Iran        (1:00)
Nigeria         v Argentina    (1:00)
Ecuador         v Ufaransa    (5:00)
Honduras     v Uswisi        (5:00)

ALHAMISI, Juni 26
Ureno        v Ghana        (1:00)
Marekani        v Ujerumani    (1:00)
Algeria        v Russia        (5:00)
Korea Kusini     v Ubelgiji    (5:00)

Watu 10 wauwawa nchini Nigeria

Kiongozi wa kundi la Boko Haram, Abubakar Shekau
TAKRIBAN watu kumi wameuawa katika shambulizi la kijiji kimoja kazkazini mashariki mwa Nigeria,karibu na eneo ambalo zaidi ya vijana 200 walitekwanyara mnamo mwezi Aprili.
Wakaazi wanasema kuwa watu waliojihami walivamia kijiji cha Korongi-nim kilichopo takriban kilomita 14 kutoka Chibok ambapo wasichana hao walitekwa nyara na wapiganaji wa Boko Haram.
Kiongozi moja wa eneo hilo ameiambia BBC kwamba wanamgambo hao walikichoma kijiji chote cha Koronginim.
Ripoti pia zinaarifu kuwa kundi hilo limedaiwa kuwatekanyara wanaume na wasichana kutoka kijiji chengine katika jimbo la Yaza siku ya alhamisi.
BBC