STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 24, 2014

Chuji, Luhende watupiwa virago Yanga, Barthez, Tegete wabakishwa

Chuji ametemwa
Barthez kabakishwa Jangwani

Tegete (kulia) aliyebakishwa akiwa na baba yake John Tegete
KLABU ya soka ya Yanga imetangaza kuwatema kundini nyota wake kama Athuman Idd 'Chuji', beki David Luhembe na Ibrahim Job, huku ikiwasainisha mikataba mipya wakali kama Ally Mustafa 'Barthez', Jerry Tegete na Oscar Joshua.
Kupitia tovuti ya klabu hiyo, ambayo msimu uliopita ilikua na kikosi bora kabisa ambacho kiliweza kuwatoa jasho Mabingwa wa Kihistoria Barani Afrika timu ya Natioal Al Ahly katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika, ambapo Mabingwa hao wa kutoka nchini Misri waliweza kusonga mbele kwa mikwaju ya penati imewatema jumla ya wachezaji 11.
Msimu uliopita Young Africans ilikuwa na kikosi cha wachezaji 30 kutoka timu ya Wakubwa na wachezaji watano (5) kutoka timu ya vijana (U20) waliokuwa wamepandishwa kwa ajili kupata uzoefu na kuingozea nguvu timu ya wakubwa katika michezo mbalimbali.
Kutokana na ripoti ya Benchi la Ufundi iliyowasilishwa mara baada ya kumalizika kwa Msimu wa Ligi Kuu 2013/2014 baadhi ya wachezaji hawataitumikia tena Yanga SC kwenye msimu ujao, wachezaji 11 wamemaliza muda wao na kumalizana na uongozi hivyo wapo huru kujiunga vilabu mbalimbali:
Wachezaji hao waliotemwa ni:
1. David Luhende
2. Athuman Idd “Chuji”
3. Geroge Banda -U20
4. Yusuph Abdul -U20
5. Rehani Kibingu -U20
6. Hamisi Thabiti
7. Reliants Lusajo
8. Bakari Masoud – U20
9. Shaban Kondo
10. Abdalllah Mguhi “Messi” U-20
11. Ibrahim Job

No comments:

Post a Comment