STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 24, 2014

Neymar aiua Cameroon, Spain yaondoa gundu, Mexico we acha









WAWAKILISHI wa Afrika Cameroon 'Wazee wa Posho' wameaga kwa aibu michuano ya Kombe la Dunia baada ya usiku wa kuamkia leo kukandikwa mabao 4-1 na wenyeji Brazil na kumaliza mechi zake bila kuambulia pointi hata moja, tofauti na waliokuwa watetezi Hispania walioondoa gundu kwa kuilaza Australia kwa mabao 3-0 katika mechi za kukamilisha michezo ya makundi.
Nyota wa Brazil anayekipiga Barcelona, Neymar ndiye aliyekuwa mwiba wa Cameroon baada ya kufunga mabao mawili na kukwea hadi kileleni kwenye orodha ya wafungaji wa fainali hizo za 20 za Kombe la Dunia akifikisha jumla ya mabao manne.
Neymar alifunga mabao yake katika dakika za 17 na 34, wakati mabao mengine yalifungwa na Fred dakika ya 49 na Fernandinho dakika ya 84, huku bao pekee la Cameroon likitumbukizwa kimiani na Matip dakika ya 26
Katika mechi nyingine ya kundi hilo la A, Mexico nayo ilimaliza na ushindi wa 3-1 dhidi ya Croatia, mabao yake yakifungwa na Rafael Marquez, Andres Guardado na Javier Hernandez. Bao la kufutia machozi la Croatia iliyompoteza mchezaji wake Ante Rebic aliyetolewa kwa kadi nyekundu mwishoni mwa mchezo, lilifungwa na Ivan Perisic.
Brazil inamaliza na pointi saba sawa na Mexico, lakini inakaa kileleni kwa wastani mzuri zaidi wa mabao na sasa wenyeji hao watavaana na Chile katika mechi ya 16 Bora huku Mexico wakivaana na Uhalanzi waliopata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Chile usiku wa jana.
Watetezi Hispania waliotemeshwa tajhi mapema waliaga michuano hiyo kwa heshima kwa kuicharaza Australia mabao 3-0, magoli yaliyowekwa kimiani na David Villa katika dakika ya 36, Fernando Torres dak.69 na Juan Mata dk. 82.
Katika mechi ya Uholanzi na Chile, mabaio ya washindi yaliwekwa kimiani na Fer katika dakika ya 77 na Depay na kumaliza kwenye kundi B ikiwa kinara kwa kushinda mechi zote na kufikisha pointi 9.

No comments:

Post a Comment