STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 24, 2014

Onesmo Waziri Ticotico kuzikwa kesho Mafinga, wadau wamlilia

Herry Morris akimfariji dada wa marehemu Ticotico (Picha Zote kwahisani ya Geofrey Chambua)

Hili ndilo gari lililochukua uhai wa Ticotico, baadahi ya watu wakilishangaa
Inauma sana!
 


Ticotico (jezi no 11 akiwa na wachezaji wenzake wa Golden Bush katika pambano lililochezwa mjini Morogoro
MWILI wa marehemu Onesmo Waziri 'Ticotico' mmoja wa wadau wakubwa wa soka nchini unatarajiwa kuzikwa kijijini kwao Rugemba mjini Mafinga siku ya kesho.
Ticotico alikumbwa na mauti baada ya kupatwa na ajali usiku wa kuamkia Jumapili walipoenda mjini humo na klabu yake ya Golden Bush Veterani kwa ajili ya mechi za kirafiki za bonanza zilizokuwa zichezwe asubuhi ya Jumapili ambayo ingehusisha timu za Mafinga, Njombe na Makambako pamoja na Golden Bush ya jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa toka mjini humo zinasema kuwa mwili wa marehemu ambao uliharibika vibaya kutokana na ukubwa wa ajali hiyo utahifadhiwa kesho Jumatano baada ya taratibu zote za Ibada.
Inaelezwa kuwa marehemu alikumbwa na ajali hiyo karibu na kijiji chao baada ya kulivamia lori lililokuwa limeegeshwa pembeni na kuumia vibaya maeneo ya kichwani na kifuani, ikiwa ni muda mchache baada ya kuagana na wachezaji wenzake kwa ajili ya kujiandaa na bonanza hilo la siku ya Jumapili.
Kwa mujibu wa mmoja wa viongozi waandamizi wa Golden Bush, Geofrey Chambua ni kwamba Majira ya usiku akiwaaga wachezaji ambao aliambatana nao kwenye gari yake; Salum Sued 'Kussi', Mwarami Mohamed 'Shilton' Herry Morris na Sadiq Muhimbo kwamba anakwenda kulala.
"liwachukulia kabisa vyumba Mafinga ili waje naye asubuhi hapa Makambako kwa ajili ya Bonanza ambalo ilikua likutanishe timu toka Mafinga, Njombe na Makambako. Baadaye wakiwa wana mtrace (mpigia) kwenye simu akawa hapatikani hadi asubuhi zilipokuja taarifa kwamba amepata ajali na kufariki instantly. Mashushuda walioona gari wanasema inaonekana ilipasuka tairi na kubiringita na hapo ilipo ipo upside down ikiwa imebondeka sana," Chambua alidokeza kwenye ujumbe wa barua pepe.
Alidokeza kuwa 'Mchana wa Jumamosi baada ya kufika salama Mafinga, aliitambulisha Golden Bush Kijijini kwao Rungemba na kuwatambulisha nduguze kisha kusihi wapige picha ya ukumbusho.......Pia alikuwa na alikuwa mwenye furaha sana na alishikana mikono na karibu kila mchezaji  kana kwamba anawaaga (Goodbye!)
Kocha wa timu ya vijana ya Golden Bush, Shija Katina aliyekuwa Arusha wakati Ticotico anakumbwa na mauti, alisema mpaka sasa aamini kama kweli Mr Football ametangulia mbele ya haki.
"Inauma na kuhuzunisha mno, nilipata taarifa nikiwa safarini Arusha na ninageuza kuwahi kumzika rafiki yangu, siamini kama kweli Ticotico hatunaye tena, " alisema Shija kwa masikitiko na kusimulia alivyolia njia nzima baada ya kupewa taarifa hiyo.
Wadau wengine wa soka wamekielezea kifo cha Ticotico kama pigo kubwa kwa familia ya marehemu, jamaa ndugu na wadau wa soka kutokana na ukweli Ticotico alikuwa mtu wa watu na aliyependa mpira pengine kuliko hata kula....
Mungu Aiweke Mahali Pema Roho ya Marehemu Onesmo Waziri 'Ticotico'

No comments:

Post a Comment