STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 23, 2013

TFF yaunda kamati zake ndogondogo, Zitto Kabwe, Wilfred Kidao waula

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametangaza wajumbe wa kamati ndogongo (standing committees) wakati zile za haki (judicial organs) na uchaguzi zitaundwa baadaye.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika leo (Novemba 23 mwaka huu) jijini Dar es Salaam, Rais Malinzi alisema kamati hizo zimeundwa kwa mujibu wa katiba ili kuisaidia Kamati ya Utendaji.

Pia ametangaza wajumbe wanne wa Kamati ya Utendaji aliowateua. Wajumbe hao ni Richard Sinamtwa na Ramadhan Nassib, wakati wengine wanaoingia moja kwa moja kwenye Kamati ya Utendaji kutokana na kamati wanazoziongoza ni Dk. Paul Marealle na Saloum Umande Chama.

Kamati ya Fedha na Mipango inaongozwa na Makamu wa Rais wa TFF, Wallace Karia wakati wajumbe ni Francis Ndulane (Makamu Mwenyekiti), Omari Walii, Eliud Mvella, Said Muhammed, Geofrey Nyange, Kidao Wilfred, Ayoub Nyenzi, Lina Kessy na Cyprian Kuhyava.

Geofrey Nyange anaongoza Kamati ya Mashindano wakati wajumbe ni Clement Sanga (Makamu Mwenyekiti), Msafiri Mgoyi, James Mhagama, Mohamed Nassoro, Moses Katabaro, Seif Ahmed, Gerald ambi, Davis Mosha, Said George na Nassoro Idrissa.

Kinara wa Kamati ya Ufundi ni Kidao Wilfred wakati wajumbe ni Athumani Kambi (Makamu Mwenyekiti), Vedstus Lufano, Blassy Kiondo, Rahim Kangezi, Patrick Kahemele, Daud Yassin, Nicholas Mihayo na Dk. Cyprian Maro.

Kamati ya Mpira wa Miguu wa Vijana inaongozwa na Ayoub Nyenzi, Khalid Abdallah (Makamu Mwenyekiti), Ali Mayay, Mulamu Ng’hambi, Apollo Kayungi, Said Tully, Luteni Kanali Charles Mbuge, Lameck Nyambaya na Ibrahim Masoud.

Lina Kessy anaongoza Kamati ya Mpira wa Miguu wa Wanawake wakati wajumbe ni Shyrose Bhanji (Makamu Mwenyekiti), Zena Chande, Amina Karuma, Dk. Cecilia Makafu, Zafarani Damoder, Beatrice Mgaya, Sofia Tigalyoma, Martin Mung’ong’o na Engrid Kimaro.

Kamati ya Waamuzi inaongozwa na Saloum Umande Chama, Nassoro Said (Makamu Mwenyekiti), Charles Ndagala (Katibu), Riziki Majala, Kanali Isaro Chacha, Paschal Chiganga, Victor Mwandike, Soud Abdi na Zahra Mohamed.

Hamad Yahya Juma ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi anaongoza Kamati ya Habari na Masoko wakati wajumbe ni Naibu Waziri January Makamba (Makamu Mwenyekiti), Tido Mhando, Yusuf Manji, Yusuf Bakhresa, Samwel Nyalla, Jack Gotham, Fredrick Mwakalebela na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA).

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji inaongozwa na Richard Sinaitwa, Moses Karuwa (Makamu Mwenyekiti), Zacharia Hanspoppe, Hussein Mwamba, Philemon Ntahilaja, Abdul Sauko na Imani Madega.

Kiongozi wa Kamati ya Ukaguzi wa Fedha ni Ramadhan Nassib wakati wajumbe ni Zitto Kabwe (Makamu Mwenyekiti), Nicholas Magarinza, Jackson Songora, Epaphra Swai, Kalilo Samson, Goodluck Moshi, Golden Sanga na Elias Mwanjala.

Dk. Paul Marealle anaongoza Kamati ya Tiba wakati wajumbe ni Dk. Fred Limbanga (Makamu Mwenyekiti), Dk. Mwanandi Mwankemwa, Dk. Nassoro Matuzya, Dk. Eliezer Ndelema na Asha Sadick.

TFF yamrejesha Rage madarakani yamtaka aitishe mkutano wa dharura

Rais wa TFF, Jamal Malinzi aliyetoa taarifa za Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage aitishe mkutano haraka baada ya awali kupiunduliwa na wajumbe wa kamati ya utendaji ya klabu yake akiwa nje ya nchi
MWENYEKITI  wa Simba, Ismail Aden Rage ameagizwa kuitisha Mkutano Mkuu wa Dharura wa klabu ndani ya siku 14 kuanzia sasa.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa agizo hilo baada ya kubaini kuwa mgogoro katika klabu baada ya kupokea barua mbili; moja kutoka Kamati ya Utendaji ikielezea kumsimamisha uongozi Rage, na nyingine kutoka kwa Mwenyekiti huyo ikielezea kutotambua kusimamishwa huko.

Uamuzi wa TFF umefanywa kwa kuzingatia Ibara ya 1(6) ya Katiba ya Simba inayosema: 
 
“Simba Sports Club ni mwanachama wa TFF, itaheshimu Katiba, kanuni, maagizo na uamuzi wa TFF na FIFA, na kuhakikisha kuwa zinaheshimiwa na wanachama wake.”

TFF itatuma wawakilishi wake katika mkutano huo, na kumuagiza Mwenyekiti wa Simba kuhakikisha wanachama wote wenye hoja wanapata fursa ya kusikilizwa.

Mahafali ya Tano ya Kidato cha Nne Mwandege Boy's yalivyofana leo Mkuranga

Wanafunzi waliosalia shuleni wakisimama kumpokea mgeni rasmi
Hata wazazi na walezi nao walisimama wima
Pre Form One nao walikuwapo katika mahafali hayo
Wanafunzi wa kidato wa tatu wakionyesha onyesho la lugha ya Kiswahili kusherehesha mahafali hayo ya leo
Baadhi ya wahitimu wa Kidato cha nne wakiwa wametulia vitini
Mwandege Boys kuna vipaji vya uigizaji usipime!
Yaani ni Full Kidigitali Mwandege Boys
Igizo likiendelea kuhusiana na umuhimu wa kuzingatia masomo shuleni
Hata Bongo Movie hawaoni ndani kwa madogo hawa, vipaji vitupu
Wahitimu wa kidato cha Nne Jesse na Godwin wakisoma taarifa ya habari hawa jamaa nouma

Hashim Abdallah (kulia) akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wa kidato cha nne

Wanafunzi wa kidato cha nne wakitumbuiza
Leo tunawaaga kwaherini tuliwazoea kaka zetu, ndivyo wanavyoimbiwa wahitimu waliokaa na wanafunzi wenzao wa kidato cha tatu
Yaani ni full burudani


Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mhe. Mercy Silla (wa pili kulia) akiwasili eneo la tukio akisindikizwa na Mkuu wa Shule, Mwl Enock Walter (kulia)


Meza kuu ikishuhudia vipaji vya wanafunzi wa Mwandege Boys Sec
Mashairi nayo yalisomwa kuwaaga wahitimu
Mmoja wa wazazi akitoa nasaha zake

Mzazi wa kiume naye alitoa nasaha zake.
Mkuu wa Shule ya Mwandege Boys, Mwl Enock Walter akisoma risala

Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mercy Sillah akisoma risala yake ambapo aliwataka wahitimu kutojiingiza kwenye kishawishi cha biashara za dawa za kulevya kwa nia ya kutaka utajiri wa haraka badala yake wakomalie kujiendeleza kimasomo na kutumia vipaji walivyonayo kujiletea mafanikio maishani mwao.
Mgeni rasmi (kushoto) akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwandege, Joseph Awino sehemu ya vitabu vilivyotolea na uongozi wa Shule ya Mwandege Boys kwa shule hiyo ya msingi ili kusaidia kukuza taalum

Mwanafunzi wa Pre Form One, Benard Deogratius aliyefanya vizuri katika masomo yake hayo akikabidhiwa zawadi na Mgeni rasmi

Mhitimu akikadhiwa cheti chake
 

Hata walimu nao walitunukiwa vyeti kwa kufanya vyema shuleni MwandegeBoys Sec

Mmoja ya wahitimu akikabidhiwa cheti na DC Mercy Sillah