STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 23, 2013

Mahafali ya Tano ya Kidato cha Nne Mwandege Boy's yalivyofana leo Mkuranga

Wanafunzi waliosalia shuleni wakisimama kumpokea mgeni rasmi
Hata wazazi na walezi nao walisimama wima
Pre Form One nao walikuwapo katika mahafali hayo
Wanafunzi wa kidato wa tatu wakionyesha onyesho la lugha ya Kiswahili kusherehesha mahafali hayo ya leo
Baadhi ya wahitimu wa Kidato cha nne wakiwa wametulia vitini
Mwandege Boys kuna vipaji vya uigizaji usipime!
Yaani ni Full Kidigitali Mwandege Boys
Igizo likiendelea kuhusiana na umuhimu wa kuzingatia masomo shuleni
Hata Bongo Movie hawaoni ndani kwa madogo hawa, vipaji vitupu
Wahitimu wa kidato cha Nne Jesse na Godwin wakisoma taarifa ya habari hawa jamaa nouma

Hashim Abdallah (kulia) akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wa kidato cha nne

Wanafunzi wa kidato cha nne wakitumbuiza
Leo tunawaaga kwaherini tuliwazoea kaka zetu, ndivyo wanavyoimbiwa wahitimu waliokaa na wanafunzi wenzao wa kidato cha tatu
Yaani ni full burudani


Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mhe. Mercy Silla (wa pili kulia) akiwasili eneo la tukio akisindikizwa na Mkuu wa Shule, Mwl Enock Walter (kulia)


Meza kuu ikishuhudia vipaji vya wanafunzi wa Mwandege Boys Sec
Mashairi nayo yalisomwa kuwaaga wahitimu
Mmoja wa wazazi akitoa nasaha zake

Mzazi wa kiume naye alitoa nasaha zake.
Mkuu wa Shule ya Mwandege Boys, Mwl Enock Walter akisoma risala

Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mercy Sillah akisoma risala yake ambapo aliwataka wahitimu kutojiingiza kwenye kishawishi cha biashara za dawa za kulevya kwa nia ya kutaka utajiri wa haraka badala yake wakomalie kujiendeleza kimasomo na kutumia vipaji walivyonayo kujiletea mafanikio maishani mwao.
Mgeni rasmi (kushoto) akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwandege, Joseph Awino sehemu ya vitabu vilivyotolea na uongozi wa Shule ya Mwandege Boys kwa shule hiyo ya msingi ili kusaidia kukuza taalum

Mwanafunzi wa Pre Form One, Benard Deogratius aliyefanya vizuri katika masomo yake hayo akikabidhiwa zawadi na Mgeni rasmi

Mhitimu akikadhiwa cheti chake
 

Hata walimu nao walitunukiwa vyeti kwa kufanya vyema shuleni MwandegeBoys Sec

Mmoja ya wahitimu akikabidhiwa cheti na DC Mercy Sillah

No comments:

Post a Comment