STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 3, 2014

Balotelli kuwakosa England mechi ya ufunguzi WC2014

MSHAMBULIAJI nyota wa AC Milan na timu ya taifa ya Italia, Mario Balotelli anakabiliwa na changamoto ya kuwa fiti kabla ya mechi ya ufunguzi ya Kombe la Dunia kutokana na kusumbuliwa na majeraha madogo ya msuli.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 anatarajiwa kuwa mchezaji muhimu katika mpango ya kocha Cesar Prandelli kwa ajili ya michuano hiyo baadae mwezi huu haswa kutokana na kuenguliwa kwa Giuseppe Rossi katika kikosi hicho.
Mkongwe Antonio Cassano na washambuliaji Alessio Cerci, Ciro Immobile na Lorenzo Insigne ndio wanatarajiwa kuwa mbadala katika safu ya ushambuliaji kama Balotelli hatakuwa fiti kwa asilimia mia moja. Kocha wa Italia Enrico Castlellaci amebainisha kuwa nyota huyo wa zamani wa Manchester City alipata majeraha ya msuli wakati akiwa kambini na timu hiyo huko Coverciano hivyo kumaanisha anaweza kukosa mechi ya ufunguzi dhidi ya Uingereza itakayochezwa huko Manaus Juni 14 mwaka huu.

Nyota Mtibwa, JKT waibeba Mbogamboga 'mchangani'

Mtibwa Sugar

Na Adam FungamwangoWACHEZAJI wa Mtibwa Sugar Mohamed Mkopi, Mohamed Ally 'Gaucho' na Jamali Machelenga wa JKT Ruvu, juzi waliibeba timu ya Mbogamboga FC ya Mwananyamala kuifunga Rendts ya Mikocheni mabao 3-2 kwenye uwanja wa shule ya msingi Mwananyamala.
Baada ya Ligi Kuu kumalizika wachezaji wa timu za Ligi Kuu wameshaanza kujimwaga kwenye viwanja vya mchangani wakizichezea timu zao za mitaani au kukodishwa kwa madau makubwa kwenye michuano mbalimbali nchini, hususan jijini Dar es Salaam.
Mastaa hao waliichezea timu hiyo kwenye michuano mipya iliyoanzishwa ya Wadau Cup iliyopanza wiki iliyopita kwenye uwanja huo na kuzishirikisha jumla ya timu 16 kutoka wilaya zote tatu katika jiji la Dar es salaam.
Michuano hiyo imeanzishwa na baadhi ya viongozi wa chama cha soka Kinondoni (KIFA) Gomigo Mketo na mratibu wake Omari Firigisi.
Uzoefu wa wachezaji hao wa Ligi Kuu ndiyo kwa kiasi kikubwa ulioibeba Mbogamboga kwani walikuwa wakipelekeshwa na vijana wasio na majina makubwa wa Rendts.
Mshambuliaji huyo wa Mtibwa alifunga goli la kwanza katika dakika ya tatu na kutengeneza bao la tatu baada ya kuachia shuti kali lililotemwa na kipa, kabla ya kumkuta mchezaji wa zamani wa Kagera Sugar Laurent Mugia na kuuweka wavuni.
Bao lingine la washndi lilifungwa na Kibwana Kibwana, huku mawili ya Rendts yalifungwa na Daudi Iddi na Dicky Daudi.

mwisho