STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 24, 2013

TCAA yamwaga msaada kwa yatima wa New Life Orphans

 Afisa habari wa Mamlaka ya  Usafiri wa Anga  Tanzania (TCAA) Ally Changwila  akiwakabidhi  msaada wa madaftari Rahma Seif na Yusra Yahaya  ambao ni watoto wanaolelewa katika kituo cha yatima cha New Life Orphans Home kilichopo Kigogo jijini Dar es Salaam. Vyakula mbalimbali vilitolewa ikiwemo mchele na Maharage.
 Afisa habari wa Mamlaka ya  Usafiri wa Anga  Tanzania (TCAA) Ally Changwila  (kushoto) akiwa na wafanyakazi wenza katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto yatima wanaolelewa katika kituo  cha New Life Orphans Home kilichopo Kigogo jijini Dar es Salaam. Baada ya kuwa kabidhi msaada wa vyakula mbalimbali yakiwemo mafuta ya kupikia , mchele na sukari.
 Afisa habari wa Mamlaka ya  Usafiri wa Anga  Tanzania (TCAA) Ally Changwila  akiwakabidhi  msaada wa mafuta ya kula Mohamed Achume ambaye ni miongoni mwa  watoto wanaolelewa katika kituo cha yatima cha New Life Orphans Home kilichopo Kigogo jijini Dar es Salaam. Vyakula mbalimbali vilitolewa ikiwemo mchele na Maharage.
Mohamed Achume anayelelewa katika kituo cha kule yatima cha New Life Orphans Home kilichopo Kigogo jijini Dar es Salaam akikabidhiwa  msaada  wa gunia la mchele na  Afisa habari wa Mamlaka ya  Usafiri wa Anga  Tanzania (TCAA) Ally Changwila (kushoto) ikiwa ni sehemu ya vyakula mbalimbali vilivyotolewa na mamlaka hiyo kwa ajiri ya watoto hao kusherehekea sikukuu ya krismasi.

Arsenal yashindwa kurejea kileleni, yabanwa nyumbani na Chelsea



Chance: Olivier Giroud fires wide towards the end of the game
Oliver Giroud akikosa bao la wazi katika pambano lao la jana dhidi ya Chelsea
So close: Giroud looks on in disbelief after missing his chance to win the game
Hekaheka tupu langoni mwa Chelsea, Goroud akikosa tena bao la wazi
Agony: Giroud looks frustrated after missing the chance late on
Kudadeki imekuwaje lakini! Kama anasema Goroud wakati akisikitikia kukosa bao
High jump: Fernando Torres jumps for the ball in the Chelsea penalty area
Up close and personal: Lampard gets in tight on Mesut Ozil
Lampard na Ozil wakitunishia ubavu katika mechi ya jana
Sliding in: Per Mertesacker challenges Chelsea's Fernando Torres as he tries to get his shot away
Torres akijaribu kutumbukiza mpira wavuni bila mafanikio
Hitting the woodwork: Frank Lampard sees his effort hit the crossbar and bounce to safety
Hollaaaa! Lampard anakosa naye bao la wazi
Stop there: Eden Hazard is chased by Arsenal midfielder Aaron Ramsey
Eden Hazard akiwatoka mabeki wa Arsenal
LICHA ya kuwa uwanja wake wa nyumbani, Arsena jana imeshindwa kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kulazimishwa suluhu na Chelsea waliorejea nafasi ya nne wakiishusha Everton.
Arsena ilikuwa kileleni kwa muda mrefu hata hivyo imetoka nafasi ya tatu iliyokuwa inashika baada ya matokeo ya mechi za wikiendi na kukaa nafasi ya pili nyuma ya vinara Liverpool wakilingana pointi 36 ila wakitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa.
Katika mchezo huo wa usiku wa jana timu zote zilikosa mabao ya wazi na wachezaji kuchezeana kitemi wakati fulani licha ya mwamuzi Mike Dean kudhibiti hali hiyo.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea siku ya Alhamis kwa michezo kadhaa 10 itakazozikutanisha timu zote 20 zinzoshiriki ligi hiyo ambapo kivumbi kitakuwa kati ya Manchester City dhidi ya Liverpool itakayochezwa uwanja wa Itihad.
Mechi nyingine siku hiyo kwa mujibu wa ratiba ya EPL ni kama ifuatavyo hapo chini;
Hull City  vs  Manchester United
Aston Villa  vs  Crystal Palace
Cardiff City  vs  Southampton 
Chelsea  vs Swansea City
Everton  vs  Sunderland 
Newcastle United vs  Stoke City
Norwich City  vs  Fulham 
Tottenham Hotspur  vs  West Bromwich
West Ham United   vs  Arsenal
Manchester City  vs  Liverpool