STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 24, 2013

Arsenal yashindwa kurejea kileleni, yabanwa nyumbani na Chelsea



Chance: Olivier Giroud fires wide towards the end of the game
Oliver Giroud akikosa bao la wazi katika pambano lao la jana dhidi ya Chelsea
So close: Giroud looks on in disbelief after missing his chance to win the game
Hekaheka tupu langoni mwa Chelsea, Goroud akikosa tena bao la wazi
Agony: Giroud looks frustrated after missing the chance late on
Kudadeki imekuwaje lakini! Kama anasema Goroud wakati akisikitikia kukosa bao
High jump: Fernando Torres jumps for the ball in the Chelsea penalty area
Up close and personal: Lampard gets in tight on Mesut Ozil
Lampard na Ozil wakitunishia ubavu katika mechi ya jana
Sliding in: Per Mertesacker challenges Chelsea's Fernando Torres as he tries to get his shot away
Torres akijaribu kutumbukiza mpira wavuni bila mafanikio
Hitting the woodwork: Frank Lampard sees his effort hit the crossbar and bounce to safety
Hollaaaa! Lampard anakosa naye bao la wazi
Stop there: Eden Hazard is chased by Arsenal midfielder Aaron Ramsey
Eden Hazard akiwatoka mabeki wa Arsenal
LICHA ya kuwa uwanja wake wa nyumbani, Arsena jana imeshindwa kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kulazimishwa suluhu na Chelsea waliorejea nafasi ya nne wakiishusha Everton.
Arsena ilikuwa kileleni kwa muda mrefu hata hivyo imetoka nafasi ya tatu iliyokuwa inashika baada ya matokeo ya mechi za wikiendi na kukaa nafasi ya pili nyuma ya vinara Liverpool wakilingana pointi 36 ila wakitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa.
Katika mchezo huo wa usiku wa jana timu zote zilikosa mabao ya wazi na wachezaji kuchezeana kitemi wakati fulani licha ya mwamuzi Mike Dean kudhibiti hali hiyo.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea siku ya Alhamis kwa michezo kadhaa 10 itakazozikutanisha timu zote 20 zinzoshiriki ligi hiyo ambapo kivumbi kitakuwa kati ya Manchester City dhidi ya Liverpool itakayochezwa uwanja wa Itihad.
Mechi nyingine siku hiyo kwa mujibu wa ratiba ya EPL ni kama ifuatavyo hapo chini;
Hull City  vs  Manchester United
Aston Villa  vs  Crystal Palace
Cardiff City  vs  Southampton 
Chelsea  vs Swansea City
Everton  vs  Sunderland 
Newcastle United vs  Stoke City
Norwich City  vs  Fulham 
Tottenham Hotspur  vs  West Bromwich
West Ham United   vs  Arsenal
Manchester City  vs  Liverpool

No comments:

Post a Comment