STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 22, 2015

Nafasi nyingine kwa Manchester Utd EPL


http://strettynews.com/wp-content/uploads/2015/02/UnitedvPreston.jpg
Mashetani Wekundu ambao wamekuja kivingine msimu huu
Chelsea
Watetezi Chelsea wanaopepesuka
KIVUMBI cha Ligi Kuu England kinaendelea leo kwa michezo kadhaa, lakini mapema saa 8;30 mchana Mashetani Wekundu watakuwa wakisaka nafasi ya kurejea kileleni japo kwa sasa kadhaa wakati watakapovaana na vibonde Newcastle United kwenye Uwanja wa Old Trafford.
Manchester United yenye pointi sita inaweza kuiengua Man City ambayo yenye itacheza kesho dhidi ya Everton kwa kufikisha pointi 9 kama itashinda huku ikiombea Leicester City ipoteze mchezo wake wa leo dhidi ya Tottenham Hotspur.
Ratiba kamili ya ligi hiyo kwa leo, kesho Jumapili na Jumatatu ambapo Arsenal itakuwa na kibarua kigumu cha kuibakaribisha Liverpool ipo hapo chini jionee mwenyewe;
Leo Jumamosi:
Manchester United     11 : 45    Newcastle United        
Crystal Palace     14 : 00    Aston Villa        
West Ham United     14 : 00    AFC Bournemouth        
Norwich City     14 : 00    Stoke City        
Sunderland     14 : 00    Swansea City        
Leicester City     14 : 00    Tottenham Hotspur        
Kesho Jumapili
West Bromwich Albion 12 : 30    Chelsea        
Everton     15 : 00    Manchester City        
Watford     15 : 00    Southampton        
Jumatatu
Arsenal     19 : 00    Liverpool

PATACHIMBIKA TAIFA, YANGA v AZAM NI SHEEDA!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjpjkGwXmOK250PzIJkj4gA7pkZ1mMpkKFXP2MG3mX3y_l3IHb7aHldzJdHcS2u-VTXyZldrrwgZtbd-yV0ndewKQDYjerOJ3aSNEVPxtJHCgeoHY8UgogGyJ-jYXVUU7COyj83XDERC6g/s1600/IMG_8065.JPG
Azam FC
Yanga
MABINGWA wa soka wa Tanzania, Yanga pamoja na Mabingwa wa Kombe la Kagame, Azam jioni ya leo wanatarajia kuonyeshana undava wakati zitakapokutana kwenye mchezo wa Ngao ya Hisani.
Mchezo huo maalum kwa ajili ya kuzindua msimu mpya wa Ligi kuu ya Tanzania Bara utapigwa dimba la Taifa, huku timu zote zikitarajiwa kuwakosa baadhi ya nyota wake kutokana na matatizo mbalimbali.
Yanga ambao imeonyesha kuupania mchezo huo hasa baada ya kutolewa nishai na Azma kwenye robo fainali ya Kombe la Kagame, huenda isiwe na Amissi Tambwe aliyekuwa akisumbuliwa na Malaria, japo Donald Ngoma anaweza kucheza akitoka kuuguza maumivu ya nyonga.
Azam wenyewe wanaosaka ushindi wa kwanza wa mchezo huo wa Ngao ya Hisani na pia kujaribu kufuta uteja kwa wapinzani kila wakikitana kwenye pambano hilo inaweza kumkosa Kipre Tchetche.
Hata hivyo vikosi vyote chini ya makocha wao, Stewart Hall kwa Azam na Hans van Pluijm wa Yanga wamenukuliwa wakitamba kuwa leo itakuwa kazi tu, na kuzipa matumiani timu yao kushinda.
"Yanga ni wazuri na ni timu kubwa na unapocheza nao ni kama ina wachezaji 12 kutokana na mashabiki wanaoiunga mkono, lakini tupo tayari na vijana wanagu wana ari ya kushinda," alisema.
Pluijm alisema kuwa ameandaa vijana wake kwa ajili ya kazi moja ya kushinda Taifa, hasa baaada ya kuridhishwa na mabadiliko aliyoyaona kwa safu yake ya mbele wakiwa jijini Mbeya kwenye kambi.
Bila ya shaka mashabiki wa soka watapata uhondo katika mchezo huo utakaochezeshwa na mwamuzi Martin Saanya baada ya refa wa awali, Israel Nkongo kupatwa na dharura ya kuugua na kuenguliwa.
Rekodi Azam Ngao ya Hisani:
2012: Simba 3-2 Azam
2013 Azam 0-1 Yanga
2014: Yanga 3-0 Azam
2015: Azam v Yanga???

Friday, August 21, 2015

3 zachemsha usajili Ligi Kuu Tanzania Bara 2015-2016

Stand United
Toto Africans
WAKATI dirisha la usajili kwa klabu vya Ligi Kuu nchini (VPL), Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) likifungwa juzi klabu tatu za VPL vimeshindwa kuwasilisha usajili wao wa wachezaji katika muda uliopangwa.
 Akizungumza na wandishi wa habari leo, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) alivitaja Klabu za Coastal Union ya Tanga, Stand United ya Shinyanga na Toto African ya jijini Mwanza kuwa zimeshindwa kuwasilisha usajili wao na kusema faini ni 500,000  kwa mchezaji mmoja hivyo klabu iliyochelewesha usajili au itakayobadili majina au kuongeza majina baada ya usajili kufungwa italazimika kulipia faini
“Usajili umefungwa jana (juzi) na timu tatu hazijawasilisha usajili wao hata wa mchezaji mmoja pamoja na TFF kuongeza muda wa usajili kwa wiki mbili”, alisema Kizunguto
Pia alisema si kwamba timu zingine zimefikisha idadi ya wachezaji wote kulingana na kanuni bali zingine zimesajili wachezaji 18, 24 hivyo hata wao endapo wataongeza watalipia faini.
Kizuguto alikumbusha timu ambazo zimesajili wachezaji wa kigeni kuwasilisha ada zao ili waweze kupata kbali cha kucheza ligi.
Awali TFF ilitoa muda wa wiki mbili kwa vilabu vyote nchini kukamilisha usajili, ambapo vilabu 13 vya ligi kuu vimeweza kukamilisha ndani ya wakati, klabu 24 vya ligi daraja la kwanza, klabu 24 ligi daraja la pili pia vimeweza kukamilisha usajili wao ndani ya muda uliopangwa.


Mkwasa ataja majembe yake ya Uturuki, Dida aachwa

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/06/Mkwasa-Stars.jpg
Kocha Mkwasa (kushoto) na Msaidizi wake, Hemed Morocco
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa ametangaza kikosi cha wachezaji 22 atakaoondoka nao kuelekea Uturuki kupiga kambi ya kuiwinda Nigeria.
Wachezaji hao 22 wanatarajiwa kuondoka nchini Jumapili  usiku kuelekea nchini Uturuki kwa kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria utakaochezwa Septemba 05, 2015. Akizungumza na wandishi wa habari leo, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Baraka Kizuguto, alisema kuwa kocha mkuu wa Taifa Stars, Charles Mkwasa ametoa orodha ya wachezaji 22 watakaosafiri usiku wa jumapili. “Orodha ya wachezaji 22 imetoka katika kikosi kilichotangazwa wiki mbili zilizopita na Mkwasa ambapo walipata nafasi ya kufanya mazoezi kwa takribani wiki moja katika uwanja wa Karume”, alisema Kizuguto. Kizuguto alisema wachezaji wote waliochaguliwa kujiunga na timu ya Taifa wanapaswa kuripoti kambini Tansoma Hotel Jumapili saa 5 asubuhi kwa maandalizi ya mwisho ya safari hiyo. Wachezaji waliochaguliwa ni All Mustafa Aishi Manula, Said Mohamed, walinzi Shomari Kapombe, Abdi Banda, Mohamed Hussein, Hassan Isihaka, Juma Abdul, Haji Mngwali, Kelvin Yondani, Nadir Haroub. Wengine ni Mudathir Yahya, Himid Mao, Frank Domayo, Salum Telela, Deus Kaseke, Said Ndemla, John Bocco, Farid Musa, , Rashid Mandawa, Saimon Msuva, na Ibrahim Ajib. Taifa Stars kwa usafiri wa shirika la ndege la Uturuki (Turkish Airlines), na itafika jijini Istambul jumatatu asubuhi, ambapo itaelekea katika mji wa Kocael   kuweka kambi ya wiki moja katika hoteli ya Green Park Kartepe.

Man United wakatwa maini kwa Sadio Mane

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/05/16/16/28BDB01200000578-3084365-Southampton_s_Sadio_Mane_celebrates_the_first_of_the_first_half_-a-3_1431789411065.jpgKLABU ya Southampton imekiri kuwa Manchester United wanamuwania winga wao wa kimataifa wa Senegal Sadio Mane, lakini ikatamka wazi kwamba mkali huyo hauzwi ng'o.
Wiki iliyopita Southampton walikanusha taarifa za kupokea ofa yeyote kwa ajili ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 23. Mshambuliaji wa Barcelona Pedro amekuwa akihisiwa kujiunga na United lakini kwa sasa yupo katika hatua za mwisho za kijiunga na Chelsea kwa dau la pauni milioni 21. 
Kutokana na hali hiyo United wameamua kuongeza nguvu zao katika kumsajili Mane kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kiangazi. Mane amefunga mabao 10 katika mechi 32 alizocheza msimu uliopita baada ya kujiunga na klabu yake ya sasa akitokea Red Bull Salzburg ya Austria na yumo pia katika orodha ya wachezaji waliowahi kufunga magoli matatu -hat-trick kwa muda mfupi zaidi.
Hata hivyo mapema leo Ijumaa klabu hiyo ya Southampton imeweka bayana kwamba mchezaji huyo hauzwi hivyo Man United watafute pengine pa kupata mchezaji mpya.
Meneja wa The Saints, Ronald Koeman amefunguka kuwa mchezaji huyo hauzwi kwa bei yoyote.

Straika Msenegal atua Msimbazi, amtia tumbo joto Kiiza

Niang mwenye kofia akiwasili
Niang akipokea simu mara baada ya kuwasili kwenye hoteli aliyofikia jijini Dar es Salaam
Akiwaskiliana alipowasilia hotelin
KLABU ya Simba imezidi kujiimarisha baada ya mchana huu kumpokea straika kutoka Senegal, Papa Niang, ambaye anatarajiwa kupimwa Jumatatu wakati Simba ikiumana na Mwadui Shinyanga kabla ya kusainishwa mkataba wa kukipiga Msimbazi.
Niang ambaye ni mdogo wa nyota Mamadou Niang, mshambuliaji ambaye itachukua muda Watanzania kumsahau baada ya kuizamisha Taifa Stars kwa mabao 4 ametua akiambatana na meneja wake, Massouka Ekoko.
Ujio wa straika hutyo aliyekuwa akicheza soka la kulipwa El Salvador kunamaanisha kuwa kama mipango itaenda sawa basi kuna uwezakano wa dili la Mrundi Kevin Ndatisenga aliyeifungia Simba moja ya mabao mawili wakati wakiiua URA ya Uganda likafa.
Pia hata kibarua cha Hamis Kiiza 'Diego' ambaye ameanza kuwekewa zengwe huenda nacho kikaota nyasi, ili kutimiza idadi ya wachezaji saba wa kimataifa wanaohitajiwa na timu hiyo.
Mpaka sasa ina wachezaji sita wa kigeni ambao ni Justice Majabvi, Emiry Nibomana, Hamis Kiiza, Juuko Murshid na Simon Sserunkuma, huku pia ikiwa imetoa kwa mkopo Raphael Kiongera aliyepo KCB ya Kenya.
Wakati Niang akitua leo zipo taarifa kutoka Msimbazi kwamba straika mwingine mkali atatua siku yoyote kuanzia leo kumaliza na mabosi wa Simba, ikiwa ni mikakati ya kuimarisha kikosi hicho ambacho kwa misimu mitatu hakijaonja ladha ya ubingwa wa Tanzania Bara.

Dondoo kuhusu Niang
Jina kamili: Papa Niang
Tarehe ya kuzaliwa: 5 Disemba, 1988 (miaka 26)
Mahali alipozaliwa: Matam Senegal
Urefu: Mita 1.81 
Nafasi anayocheza: Mshambuliaji
Klabu alizowahi kuzitumikia:
Kwasasa: Mchezaji huru
2005-2006: ASC Thies 
2007: FC OPA
2008: AC Oulu
2009-2012: FF Jaro
2013: FC Vostok
2013-2014: Al -Shabab SC
2014-2015: FC Mounana

Wednesday, August 19, 2015

Kocha Man City aanza kuchonga mapema

http://s.ndtvimg.com/images/content/2015/aug/806/pellegrini-smile-man-city-chelsea-win.jpgUSHINDI una raha bhana we acha tu!, Meneja wa vinara wa Ligi Kuu ya England, Manchester City, Manuel Pellegrini ameanza kuchonga baada ya chama lake kupata ushindi katika mechi mbili mfululizo.
Kocha huyo ambaye ameiongoza Man City kuitoa nishai mabingwa watetezi, Chelsea, wikiendi iliyopita amesema wachezaji wake wana njaa na kiu baada ya kulikosa taji la Ligi Kuu msimu uliopita. 
City walimaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita nyuma ya mabingwa Chelsea wakitofautiana kwa alama nane. 
Akihojiwa mara baada ya kikosi chake kuichapa Chelsea kwa mabao 3-0 jana, Pellegrini amesema pengine kilichotokea msimu uliopita kilikuwa ni uzoefu tosha kwao. 
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wachezaji wake hivi sasa wana njaa na kiu ndio maana wanataka kushinda katika kila mchezo. 
Mabao ya City katika mchezo huo yalifungwa na Sergio Aguero, nahodha Vincent Kompany na Fernandinho.
Kikosi hicho kinatarajiwa kushuka dimbani wikiendi hii ugenini kuvaana na Everton siku ya Jumapili.

Hii ni zaidi ya bao! Chelsea yaizidi ujanja Man United kwa Pedro

http://unitednews.club/wp-content/uploads/2015/07/pedro-rodriguez-barcelona-cordoba-liga-bbva-12202014_nkvqt53jxhxb1dqfil0bns4ci.jpgHII huenda ni taarifa isiyopendwa kusikika masikioni mwa mashabiki wa Chelsea, Vyombo vya Habari nchini Hispania vimetoa taarifa kuwa klabu ya Chelsea imefanikiwa kuizidi maarifa mahasimu wao Manchester United katika usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania Pedro Rodriguez kutoka Barcelona. 
Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na gazeti la Marca, zimedai kuwa taratibu zote za Pedro kujiunga na Chelsea zimeshakamilika baada ya klabu hizo kuafikiana uhamisho wa Euro Mil. 28, huku kukiwa na nyongeza ya Euro Mil. 2 itakayolipwa baadaye. Taarifa hizo ziliendelea kudai kuwa Pedro tayari ameshatua jijini London kufanyiwa vipimo vya Afya baada ya kupewa ruhusa na Barcelona. Mashetani Wekundu, Man United ilikuwa wakitajwa kwa wiki kadhaa kumuwania mshambuliaji huyo kwa kutoa ofa ya Euro milioni 25.

Beki Mtogo apewa namba ya 'gundu' Jangwani

BEKI mpya wa Yanga kutoka Togo, Vincent Bossou ameichagua jezi yenye namba inayodaiwa kuwa na 'gundu' klabuni hapo, iliyowahi kumtesa mapro wengine waliowahi kuichezea timu hiyo hivi karibuni.
Mastraika Gelinson Santos 'Jaja' kutoka Brazil na Kpah Sherman wa Liberia waliwahi kuivaa jezi namba 9 na kupata wakati mgumu Jangwani, kiasi Mliberia kutaka maombi ya kichungaji kurejesha makali.
Hata hivyo Bossou ambaye alianza kuichezea Yanga juzi Jumapili katika pambano lao dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya amesisitiza jezi hiyo namba 9 ndiyo chaguo lake.
"Napenda kuvaa jezi namba tisa, popote ninapoenda kucheza hupenda kuitumia hjata kwenye timu ya taifa, licha ya kwamba mimi ni beki, navaa jezi yenye namba hiyo na hapa Yanga vivyo hivyo," Beki huyo alinukuliwa, huku akiwataka Wanayanga kumpa muda kuzoea mazingira na kuwapa burudani.
Kauli ya Bossou ilikuja baada ya kutokung'ara vema katika pambano hilo la Mbeya ambalo Yanga ilishinda mabao 3-2, huku dakika 45 alizocheza akishirikiana na Kelvin Yondani kabla ya kutolewa kipindi cha pili Yanga ilikuwa mbele kwa mabao 2-1.
Jaja alishindwa kung'ara Yanga na jezi namba 9 na kutimuliwa baada ya mechi chache tu, huku Sherman alihenyeka na namba hiyo mpaka kuhitaji maombi kabla ya kutulia na kufanya yake akimaliza msimu uliopita na mabao manne na katika Kombe la Kagame alivalia jezi namba 10 iliyokuwa ikitumiwa na Jerry Tegete.
Kwa sasa Mliberia huyo yupo Afrika Kusini akicheza soka la kulipwa baada ya kuuzwa hivi karibuni.

Hassan Dalali ajivunia rekodi yake Msimbazi

Mwenyekiti wa zamani wa Simba, Hassan Dalali
Hassan Dalali akisalimiana na wachezaji wa Bongo Movie siku ya Simba day
MWENYEKITI wa zamani wa Simba, Hassan Dalali amesema yapo mambo matano ambayo anajivunia kuiongoza klabu hiyo na jambo moja linamtia simanzi mpaka sasa kwa kuona hakufanikiwa kutekeleza.
Akizungumza na MICHARAZO, Dalali aliyataja mambo anayojivunia kwa kuiongoza Simba kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2008-2010 ni kuanzisha Simba Day mwaka 2009 ambayo inaendelezwa mpaka sasa na viongozi waliomfuata.
"Kuipatia Simba kiwanja kule Bunju ni suala jingine, kuwaunganisha wanachama wote wa Simba na kuongea idadi yao ni mambo mengine yanayonipa faraja," anasema.
Mwenyekiti huyo ambaye kwa sasa amejikita zaidi kwenye masuala ya kisiasa akiwa Mwenyekiti wa CCM Jimbo la Kinondoni na Mjumbe wa Kamati ya Siasa wa Wilaya ya Kinondoni alisema kubwa la kujivunia ni kuiwezesha Simba kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu bila kufungwa hata mchezo mmoja msimu wa 2009-2010.
"Hili linanifanya nitembee kifua mbele na kujivunia, kuifanya Simba isifunguke, tukishinda mechi 18 kati ya 20 na mbili tukitoka sare, Azam walijitahidi msimu wa 2013-2014, lakini hawakufikia rekodi kwani walishinda mechi 18 na kutoka sare 8, japo tulitofautiana idadi ya michezo, wao walicheza mechi 26 sisi 22," alisema Dalali.
Kuhusu linalomtia simanzi ni kitendo cha kushindwa kufanikisha ujenzi wa uwanja wa klabu hiyo, na kitendo cha viongozi wenzake kushindwa kuuendeleza ingawa alimfagilia Ismail Aden Rage kwa kuweza kupunguza deni lililokuwapo kujimilikisha kiwanja hicho.
"Naamini kwa namna mimi na Mwina Kaduguda tulipokuwa tumefikia, hivi sasa Simba ingekuwa na eneo la kujivunia la kufanyia mazoezi yao kwa kujinafasi kwani tulikuwa tumeingia mkataba na kampuni ya kuuza jezi ya Marekani, ambapo hata hivyo ilisitisha."
"Ila naamini Simba itakuja kuwa na Uwanja wake na kama nitakufa basi wanachama wa Simba watanikumbuka kwa mambo hayo,  ya kiwanja na tamasha la Simba Day," alisema Dalali.

RATIBA KAMILI YA LIGI KUU MSIMU WA 2015-2016 HII HAPA


Mabingwa watetezi Yanga

Azam
Simba
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) imeachia hadharani ratiba ya Ligi Kuu msimu wa 2015-2016, ikionyesha mabingwa watetezi wataanzia nyumbani katika mechi tano kaba ya kutoka kwenda Morogoro kuumana na Mtibwa Sugar.
Watetezi hao watavaana na watani zao, Simba Septemba 26, lakini ikianza mechi zake nyingi nyumbani huku wakitaabika kwa kumaliza mechi zao za mwisho mfululizo ikiwa ugenini.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo ligi itaanza Septemba 12 na kumalizika Mei 7, huku pia kukiwa na michuano ya Kombe la FA ambalo limerejeshwa upya baada ya miaka mingi ya ukimya.
MICHARAZO imekuweka ratiba nzima ya Ligi hiyo kwa msimu huu ili kujua nani na nani wataanzia wapi na ligi;

Sept 12, 2015
Ndanda vs Mgambo JKT
African Sports vs Simba
Majimaji vs JKT Ruvu
Azam vs Prisons
Stand Utd vs Mtibwa Sugar
Toto Africans vs Mwadui Fc
Mbeya City vs Kagera Sugar
 

Sept 13, 2015
Yanga vs Coastal Union
 

Sept 16, 2015
Yanga vs Prisons
Mgambo JKT vs Simba
Majimaji  vs Kagera Sugar
Mbeya City vs JKT Ruvu
Stand Utd  vs Azam
Toto Africans vs Mtibwa Sugar
Ndanda vs Coastal Union
 

Sept 17, 2015
Mwadui FC vs African Sports
 

Sept 19, 2015
Stand Utd vs  Africans Sports
Mgambo JKT vs Majimaji
Prisons vs Mbeya City
Yanga  vs JKT Ruvu
 

Sept 20, 2015
Mwadui Fc vs Azam
Mtibwa Sugar vs  Ndanda
Simba vs Kagera Sugar
Coastal Union vs Toto Africans
 

Sept 26, 2015
Simba vs Yanga
Coastal Union vs Mwadui Fc
Prisons  vs Mgambo JKT
JKT Ruvu vs Stand Utd
Mtibwa Sugar vs Majimaji
Kagera Sugar vs Toto Africans
 

Sept 27, 2015
African Sports vs Ndanda
Azam vs Mbeya City
 

Sept 30, 2015
Simba vs Stand Utd
Azam vs Coastal Union
Mtibwa Sugar vs Yanga
Ndanda vs Majimaji
Kagera Sugar vs JKT Ruvu
African Sports vs Mgambo JKT
Prisons vs Mwadui FC
 

Okt 01, 2015
Toto Africans vs Mbeya City


Okt 03, 2015
Mgambo JKT vs  Coasta Union
Majimaji vs Mwadui Fc
Toto Africans vs JKT Ruvu
Okt 04, 2015Stand Utd vs Mbeya City
Kagera Sugar vs Prisons
Azam vs Mtibwa Sugar
Ndanda vs Simba
African Sports vs Yanga
 

Okt 5-13, 2015
Afcon 2017QFL/Kirafiki/WC 2018 QFL
 

Okt 17, 2015                                            Yanga vs Azam
Majimaji vs African Sports
Mbeya City vs Simba
Ndanda vs Toto Africans
Stand Utd vs Prisons
Coastal Union vs Mtibwa Sugar
 

Okt 18, 2015Mgambo JKT vs Kagera Sugar
Mwadui vs JKT Ruvu
 

Kagera Sugar
Okt 21, 2015Yanga vs Toto Africans
Stand Utd vs Majimaji
JKT Ruvu vs Mtibwa Sugar
Prisons vs Simba
Coastal Union vs Kagera Sugar

 
Okt 22, 2015Mwadui vs Mgambo JKT
Mbeya City vs African Sports
Ndanda vs Azam
Okt 25, 2016

Uchaguzi Mkuu wa Taifa                                 
Okt 28, 2015                                            Toto Africans vs Mgambo JKT
Mwadui vs Yanga
Mtibwa Sugar vs  Kagera Sugar
Mbeya City vs Majimaji
Ndanda vs Stand Utd
Simba vs Coastal Union
 

Sept 29, 2015JKT Ruvu vs Azam
Prisons vs African Sports
 

Okt 31,2015Simba vs Majimaji
Kagera Sugar vs Yanga
Mtibwa Sugar vs Mwadui
Prisons vs Ndanda
Coastal Union vs Mbeya City
 

Nov 01, 2015African Sports vs JKT Ruvu
Azam vs Toto Africans
 

Nov 02, 2015
Mgambo JKT vs Stand Utd
 

Nov 07, 2015Mgambo JKT vs Yanga
Kagera Sugar vs Ndanda
Stand Utd vs Mwadui
Mbeya City vs Mtibwa Sugar
Azam vs Simba
Majimaji vs Toto Africans
 

Nov 08, 2015JKT Ruvu vs Prisons
Coastal Union vs African Sports
Nov 9-17, 2015
Kirafiki/ WC 2018 QFL/Challenge/Mini Window (Nov 15-Dec 15)/ Nani Mtani Jembe (Dec 12)
 

Mtibwa Sugar
Dec 19, 2015Yanga vs  Stand Utd
Mwadui vs Ndanda
Kagera Sugar vs African Sports
Prisons vs Mtibwa Sugar
Toto Africans vs Simba
Majimaji vs Azam

 
Dec 20, 2015JKT Ruvu vs Coastal Union
Mbeya City vs Mgambo JKT
 

Dec 26, 2015Ndanda vs JKT Ruvu
Yanga vs Mbeya City
Majimaji vs Prisons
Mwadui vs Simba
Mtibwa Sugar vs  Mgambo JKT
Coastal Union vs Stand Utd
 

Dec 27, 2015Azam vs Kagera Sugar
Toto Africans vs African Sports
Jan 01-13, 2016
Mapinduzi Cup                                           
 

Jan 16, 2016JKT Ruvu vs Mgambo JKT
Toto Africans vs Prisons
Simba vs Mtibwa Sugar
Stand Utd vs Kagera Sugar
Mbeya City vs Mwadui
Coastal Union vs Majimaji
Azam vs  African Sports
 

Jan 17, 2016Yanga vs Ndanda
 

Jan 20, 2015Ndanda vs Mbeya City
Prisons vs Coastal Union
JKT Ruvu vs Simba
Stand Utd vs Toto Africans
Mgambo JKT vs Azam
 

Jan 21, 2016Mwadui vs Kagera Sugar
African Sports vs Mtibwa Sugar
Yanga vs Majimaji
 

Jan 23-24
FA CUP
 

Jan 30, 2016    Coastal Union vs Yanga
Simba vs African Sports
JKT Ruvu vs Majimaji
Prisons vs Azam
Mtibwa Sugar vs Stand Utd
Mwadui vs Toto Africans
Kagera Sugar vs Mbeya City
 

Jan 31, 2016Mgambo JKT vs Ndanda
 

Feb 03, 2016                                            Prisons vs Yanga
Simba vs Mgambo JKT
Kagera Sugar vs  Majimaji
JKT Ruvu vs Mbeya City
African Sports vs     Mwadui
Mtibwa Sugar vs Toto Africans
Azam vs Stand Utd
 

Feb 04, 2016Coastal Union vs Ndanda

Feb 06, 2016Kagera Sugar vs  Simba
Mbeya City vs  Prisons
JKT Ruvu vs Yanga
African Sports vs Stand Utd
Ndanda vs Mtibwa Sugar
 

Feb 07, 2016Azam vs Mwadui
Toto Africans vs  Coastal Union
Majimaji vs Mgambo JKT
Feb 12-14, 2016 CAF-CC&CL 

Feb 13, 2016Stand Utd vs Simba
Mgambo JKT vs African Sports
Yanga vs Mtibwa Sugar
Mbeya City vs Toto Africans
Ndanda vs Majimaji
JKT Ruvu vs Kagera Sugar
Mwadui vs Prisons
Coastal Union vs azam
 

Feb 20, 2016Yanga vs Simba
Mgambo JKT vs Prisons
Stand Utd vs JKT Ruvu
Mbeya City vs Azam
Majimaji vs Mtibwa Sugar
Toto Africans vs Kagera Sugar
Feb 21, 2016Ndanda vs  African Sports
Mwadui vs Coastal Union
 

Feb 26-28, 2016 CAF-CC& CL
 

Mar 05, 2016Azam vs Yanga
African Sports vs Majimaji
Toto Africans vs Ndanda
Kagera Sugar vs Mgambo JKT
JKT Ruvu vs Mwadui
Prisons vs Stand Utd
Mtibwa Sugar vs Coastal Union
 

Mar 06, 2016Simba vs Mbeya City
Yanga vs African Sports
Mtibwa Sugar vs Azam
 

Mar 09, 2016Prisons vs Kagera Sugar
Coastal Union vs Mgambo JKT
Mwadui vs Majimaji
JKT Ruvu vs Toto Africans
 

Mar 10, 2016Simba vs Ndanda
Mbeya City vs  Stand Utd
Mar 11-13, 2016 CAF-CC&CLToto vs Yanga
Azam vs  Ndanda
 

Mar 12, 2016African Sports vs Mbeya City
Mtibwa Sugar vs JKT Ruvu
 

Mar 13, 2016Majimaji vs Stand Utd
Kagera Sugar vs  Coastal Union
Simba vs Prisons
Mgambo JKT vs Mwadui 

Mar 18-20, 2016 CAF-CC&CL                               
 

Mar 19, 2016                                    Coastal Union vs Simba
Yanga vs Mwadui
Azam vs JKT Ruvu
Kagera Sugar vs Mtibwa Sugar
Majimaji vs Mbeya City
Stand Utd vs Ndanda
 

Mar 20, 2016African Sports vs Prisons
 

Mar 21, 2016Mgambo JKT vs Toto Africas
 

Mar 21-29, 2016 Kirafiki/FA Cup
 

Apr 02, 2016Majimaji vs Simba
Yanga vs Kagera Sugar
Toto Africans vs Azam
Stand Utd vs Mgambo JKT
Ndanda vs Prisons
Mbeya City vs Coastal Union
 

Apr 03, 2016JKT Ruvu vs African Sports
Mwadui vs Mtibwa Sugar
 

Apr 08-10, 2016 CAF-CC&CLStand Utd vs Yanga
 

Apr 09, 2016Ndanda vs Mwadui                                   
African Sports vs Kagera Sugar
Mtibwa Sugar vs Prisons
Azam vs Majimaji
 

Apr 10, 2016Coastal Union vs JKT Ruvu
 

Apr 11, 2016Mgambo JKT vs Mbeya City
 

Apr 16, 2016Simba vs Azam
Ndanda vs Kagera Sugar
African Sports vs Coastal Union
Mwadui vs Stand Utd
Mtibwa Sugar vs Mbeya City
Prisons vs JKT Ruvu
Toto Africans vs Majimaji
 

Apr 17, 2016Yanga vs Mgambo JKT
 

Apr 18-20, 2016 CAF-CC&CL
 

Apr 23-24, 2016 FA Cup                                           
Apr 26, 2016JKT Ruvu vs Ndanda
 

Apr 27, 2016Mbeya City vs Yanga
Kagera Sugar vs Azama
Simba vs Mwadui
Stand Utd vs Coastal Union
African Sports vs Toto Africans
 

Apr 28, 2016Prisons vs Majimaji
Mgambo JKT vs Mtibwa Sugar
 

Apr 30, 2016Mtibwa Sugar vs Simba
Mgambo JKT vs JKT Ruvu
 

Mei 01, 2016Ndanda vs Yanga
Kagera Sugar vs Stand Utd
Mwadui vs Mbeya City
Majimaji vs Coastal Union
African Sports vs Azam
Prisons vs Toto Africans
 

Mei 07, 2016                            Mbeya City vs Ndanda
Coastal Union vs  Prisons
Simba vs JKT Ruvu
Toto Africans vs Stand Utd
Azam vs Mgambo JKT
Kagera Sugar vs Mwadui
Mtibwa Sugar vs African Sports
Majimaji vs Yanga
 

Mei 14, 2016 FA Cup