STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 3, 2013

EXCLUSIVE: HATIMAYE NSA JOB APELEKA JINA LA KIGOGO TFF

MSHAMBULIAJI wa Coast Union, Nsa Job amewasilisha barua kwenye Shirikisho la soka (TFF) ambayo inamtaja kigogo ambaye alimpa rushwa.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), lilimtaka mchezaji huyo kujieleza kutokana na kukaririwa akiongeza katika kituo kimoja cha radio akikiri kupokea rushwa ya sh2mil kwa mmoja wa kiongozi wa timu kubwa ili acheze chini ya kiwango pindi walipokuwa wanacheza na timu hiyo.

Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema kuwa tayari mchezaji huyo amekwisha tuma barua ya kujieleza nao wameamua kulipeleka suala hilo katika kamati ya nidhamu ambayo inatarajiwa kukutana wiki ijayo.

Alisema mbali na suala hilo pia kamati hiyo itapitia mambo mbali mbali ya ligi kuu ambayo yametokea ikiwemo suala la viongozi ambao walikuwa wanatoa maneno ya uchochozi.

Alisema viongozi wanatakiwa kufuata taratibu na kanuni za soka sio kuongea ongea vitu visivyo na maana ambavyo vitaleta matatizo katika soka.

Moja ya Viongozi ambao watajadiliwa ni Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga baada ya kudaiwa kutoa maneno ya uchochezi pindi TFF, walipohairisha mechi yao dhidi ya Mgambo JKT ya Tanga.  


CHANZO:SHAFII DAUDA

No comments:

Post a Comment