STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, April 27, 2013

HIVI NDIVYO GOLDEN BUSH WALIPOITOA NISHAI WAHENGA FC

Kikosi cha Golden Bush kilichoitambia Wahen ga Fc jana jijini Dar es Salaam

Kikosi cha Wahenga Fc kilichoendeleza uteja kwa Golden Bush jana
Mchezaji wa Wahenga akitafuta mbinu za kuwatoka wachezaji wa Golden Bush

Abuu Ntiro akiwahi pasi ya Athuman Machuppa huku Yusuf (9) wa Wahenga akiwanyemelea


HATARI! Lango la Wahenga Fc likiwa kwenye msukosuko

Ntiro akiwa akitafuta mbinu za kumnyanganya mpira Yusuf wa Wahenga madhara

Kama zamani Ntiro akitiririka pembeni kuelekea lango wa Wahenga, huku Kisiga akiwa tayari kumpa  msaada



Steven Marash na Wisdom Ndlovu wakiuza sura kabla ya kuanza kwa pambano la jana

Athuman Machuppa akiwania mpira na Wanchope wa Wahenga Fc

Machuppa (11) wa Golden Bush akiwania mpira wa Hamza (13) na Mcaremoon wa Wahenga katika pambano lao la jana

Wakati wa mapumziko mashabiki waq Wahenga wakifyeka nyasi ili kuwapa nafasi wachezaji wafanye vitu vyao na kuwarahishia Golden Bush kupata ushindi wa mabao 2-1

Wachezaji wa Golden Bush wakipasha kabla ya pambano hilo




Shaaban Kisiga akiwatoka wachezaji wa Wahenga

Macocha Tembele akiwafungisha tela Athuman Machupa na Godfrey Bonny, huku Kapeta akiwa tayari kumsaidia

HAPA HUPITI: Ni kama Ntiro (12) wa Golden Bush akimwambia Yusuf (9)  wa Wahenga



Kikosi cha Golden Bush Veterani kabla ya kuivaa Wahenga FC

HILI NDILO GARI LITAKAPIGANIWA NA MABONDIA CHEKA, MASHALI


Msemaji wa mbambano wa Thomasi Mashali na Fransic Cheka akiwa nyuma ya gari kuwaonesha wana habari gari hilo litagombaniwa kama zawadi na mabondia hawo

Yanga wanyakuta taji bila jasho, waapa hawabweteki

Wachezaji wa Yanga wakishangilia moja ya mabao yao katika ligi kuu msimu huu, ambapo jana kikosi chao kilitawazwa kuwa mabingwa bila kushuka dimbani baada ya Azam kung'ang'aniwa Mkwakwani.

NYOTA wa klabu ya Yanga jana wangeweza kuwa katika jumba la starehe wakinywa juice kupooza makoo, lakini wamerefusha rekodi ya kutwaa mara nyingi zaidi ubingwa wa Bara, baada ya sare ya 1-1 kati ya Coastal Union na Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani kuipa taji la 23 la ligi kuu bila jasho.
Kwa matokeo hayo, Azam iliyokuwa na matumaini ya mbali ya kuikatili Yanga katika kuwania ubingwa uliotemwa na Simba msimu huu, sasa itaweza kufikisha pointi 54 kama itashinda michezo yake mwili iliyobaki.
Idadi hiyo ni pointi mbili pungufu ya jumla ya alama za sasa za mabingwa wapya hao ambao pia wana michezo miwili kabla ya kumaliza msimu.
Kocha wa Azam ambayo mwishoni mwa wiki itakuwa Morocco kujaribu kuingia hatua ya 16 bora ya Kombe la Shirikisho la klabu za Afrika dhidi ya RAF, Stewart Hall alilaumu ubovu wa uwanja wa Mkwakwani kuwa ndiyo sababu ya kushindwa kuweka hai ndoto ya timu yake Bara.
Mwalimu wa Coastal ambayo sasa imefikisha pointi 34 na kujiimarisha katika nafasi za katikati ya msimamo wa ligi kuu, Hemed Morocco alimlaumu muamuzi Andrew Shamba kwa kuwapendelea wageni, kwa upande wake.
Agrey Moris aliipatia Azam bao la kuongoza kwa penalti katika dakika ya 59, baada ya muamuzi kuamuri adhabu hiyo kufuatia Gaudance Mwaikimba kuangushwa ndani ya eneo la hatari na Yusuf Chuma.
Ilimchukua Dany Lihanga wa Coastal Union dakika moja tu tangu kuingia kutoka benchini kusawazisha bao hilo katika robo ya mwisho ya mchezo, baada ya kumalizia wavuni pasi ya Ibrahim Twaha.
Lihanga aliingia kuchukua nafasi ya Selemani Kassim katika dakika ya 71.
Mbali na mwaka huu, tangu ligi kuu ya Bara (zamani ligi daraja la kwanza) ianze mwaka 1965 Yanga imetwaa ubingwa katika miaka ya 1968-1972, 1974, 1981, 1983, 1985, 1987, 1989, 1991-1993, 1996-1998, 2002, 2005, 2008-2009 na 2011 kwa tofauti ya magoli.

Makamu Mwenyekiti wa timu hiyo ya Yanga, Clement Sanga alisema pamoja na kufurahai kupata ubingwa mapema wakiwa na mechi mbili mkononi, hawatabweteka na badala yake watahakikisha wanashinda mechi hizo ili kuunogesha ubingwa wao.
Sanga alinukuliwa na kituo kimoja akisema furaha yao na sherehe zao za ubingwa zitanoga kama watawafunga Simba na hasa kurejesha kipigo cha aibu walichopewa msimu uliopita wa kunyukwa mabao 5-0.
Hata hivyo Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang'are  'Mzee Kinesi' amepuuza ndoto hizo za Yanga na kudai wasitarajie kitu kama hicho kwani Msimbazi wanataka kuivuruga furaha ya wanajangwani.
"Tunataka kuivuruga furaha ya mtani kwa kuwanyuka Mei 18 ili asherehekee kimya kimya ndani wakiwa na maumivu, tunajua hatuna ubingwa lakini tunataka kulinda heshima yetu," alisema Kinesi.

Ruvu Shooting walalamikia gharama, lakini yaionya Simba

Kikosi cha Ruvu Shooting Stars
UONGOZI wa Ruvu Shooting umesikitishwa na gharama ulizobebeshwa na serikali na shirikisho la soka, TFF, kufuatia kuahirishwa kwa pambano la ligi kuu ya Bara dhidi ya Simba juzi.
Lakini uongozi huo umesisitiza kuwa kipigo kwa 'mnyama' kipo palepale timu hizo zitakapokutana katika tarehe mpya - Mei 5.
TFF ilitangaza kuahirisha pambano hilo lililokuwa lichezwe kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam saa chache kabla ya kufanyika kwake na kupanga lifanyike Mei 5.
Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire aliimbia MICHARAZO jana kuwa wamekerwa na kusikitishwa na kitendo hicho kilichowatia hasara kubwa ya kuweka kambi, kufanya maandalizi na kusafiri kutoka Mlandizi mpaka Dar Es Salaam na kukaa siku kadhaa kisha kuahirishwa mechi.
Bwire alisema licha ya TFF kuwaomba radhi na kujitetea kuwa haihusiki na kuzuiwa kutumiwa kwa Uwanja wa Taifa kutokana na kupisha maandalizi ya sherehe za Muungano, lakini inastahili lawama kwa kitendo hicho kwani walipaswa kulifahamu hilo mapema na kuzipunguzia gharama timu husika.
"Tumeumizwa sana na kilichofanyika, tulifanya maandalizi yenye gharama kwa ajili ya mechi hiyo, hata hivyo hatuna mpango wa kudai fidia yoyote kwani TFF imeshajitetea kwetu na sasa tunafikiria mechi yetu ya Mei Mosi dhidi ya JKT Oljoro," alisema.
Bwire alisema pamoja na kuiwaza mechi hiyo ya Oljoro, lakini Simba wasifikirie tayari wameshaepuka kipigo kutoka kwao, kwani hata Mei 5 wakikutana lazima wakutane nacho kwa maandalizi waliyofanya na kiu yao ya kumaliza kwenye 'Nne Bora'.
"Kipigo kwa Simba kipo pale pale wameahirishiwa tu, tunataka kuonyesha kuwa Ruvu ni timu nzuri na tunataka tumalize katika Tatu au Nne Bora msimu huu, kwani kwa mechi zilizosalia tuna uwezo wa kufikisha pointi 42," alitamba Bwire.
Timu hiyo ipo katika nafasi ya saba ikiwa na pointi 30 ikiwa na michezo minne kabla ya kumaliza msimu wa 2012-2013.

Simba yatishiwa Polisi, Machaku aapa Mnyama lazima akae


Kikosi cha Simba
Machaku Salum 'Balotelli' wa Polisi Moro
LICHA ya kuhitaji miujiza ili kubaki kwenye ligi kuu ya Bara msimu ujao, wachezaji wa Polisi Morogoro wana imani ya kujikwamua na janga hilo kwa kuanzia na kuifunga Simba katika mchezo baina ya timu hizo kwenye Uwanja wa Taifa kesho.
Polisi Morogoro ni ya pili toka mkiani katika ligi ambayo zitashuka timu tatu za mwisho, ikiwa na pointi 19.
Ili kubaki kwenye daraja hilo la juu zaidi Polisii nahitaji kushinda mechi zake tatu zilizobaki ili kufikisha pointi 25 na kupunguza tofauti ya magoli ya -10 iliyonayo.
Bahati mbaya kwa Polisi, hata hivyo, jumla hiyo imeshafikiwa na ama kupitwa na timu zote zilizo katika eneo la salama la kubaki kwenye ligi kuu na zikiwa si tu na michezo iliyobaki bali pia uwiano bora wa magoli.
African Lyon na Toto Africa nazo zina uwezo wa kufikisha pointi 25 lakini kwa kubakiwa na michezo miwili na mmoja, kwa mpangilio huo, zipo katika mazingira magumu zaidi ya Polisi Morogoro.
Mmoja wa wachezaji wa Polisi Salum Machaku alisema licha ya timu yao kuwa katika eneo la hatari, lakini hawajakata tamaa.
Amedai wachezaji wote wamejipanga kufanya kweli katika mechi zilizosalia dhidi ya Simba, Kagera Sugar na Coastal Union.
"Hatujakata tamaa na wala hatuamini kama Polisi itarudi daraja la kwanza," alisema na kueleza zaidi, "tumejipanga kupigana kiume katika mechi zilizosalia ili kubaki na Simba wakae chonjo kwani tutakufa nao Uwanja wa Taifa."
Mshambuliaji huyo aliyewahi kuichezea Simba na timu za Pan Africans, Azam na Mtibwa Sugar, alisema hakuna mchezaji wala mwana Polisi Moro anayetaka kusikia habari za kushuka daraja japo wamechelewa mno kuzinduka.
Machaku alisema ugeni wao katika ligi wakati wa duru la kwanza lililosababisha wapoteze mechi na pointi nyingi ndiyo iliyowagharimu kabla ya kuzinduka katika duru la pili wakiwa wamechelewa.

Machupa, Kisiga waibeba Golden Bush wakiipa kichapo Wahenga Fc

Shaaban Kisiga (Katikati) akiwatoka wachezaji wa Wahenga Fc

Nyota wa Wahenga Fc, Macocha Tembele akiwatok wachezaji wa Golden Bush

Yusuf (9) wa Wahenga, akitafuta mbinu za kumtoka Abuu Ntiro huku wachezaji wenzake wakiwa tayari kumpa msaada katika pambano lao lililochezwa jana na Wahenga kunyukwa mabao 2-1

Abuu Ntiro akimtoka Yusuf

Heka heka katika lango la Wahenga Fc

NYOTA wa zamani wa Simba na taifa Stars, Athuman Idd Machuppa na Shaaban Kisiga 'Marlon' jana waliisaidia Golden Bush Veterani kupata ushindi muhimu  wa mabao 2-1 dhidi ya wapinzani wao wa jadi Wahenga Fc katika pambano maalum la kusherehekea  Miaka 49 ya Muungano.
Timu hizo zilipambana katika mchezo mkali na uliosisimua uliochezwa kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza Darajani, ambapo Machuppa, Kisiga wakisaidiwa na nyota wa zamani wa Simba na Yanga walifunga mabao hayo katika muda wa dakika tano tu mara baada ya kurejea toka mapumziko timu zikiwa hazijafungana.
Machuppa ndiye aliyeanza kuifungia Golden Bush bao tamu katika dakika ya 68 akimalizia kazi nzuri ya Herry Morris kabla ya Kisiga kuongeza jingine dakika tano baadaye na kuzima matumaini na Wahenga Fc waliokuwa uwanja wa nyumbani kulipa kisasi ilichokutana nacho mwezi uliopita kwenye uwanja wa Kinesi.
Katika pambano hilo la Kinesi, Wahenga walinyukwa pia mabao 2-1 huku mvua ikiwanyeshea timu zote mbele ya aliyekuwa mgeni rasmi, Kamanda wa Polisi, Thobias Andengenye.
Golden Bush na kikosi kilichosheheni nyota waliowahi na wanaendelea kutamba nchini kama kipa Aman Simba, Abuu Ntiro, Godfrey Bonny 'Ndanje', Wisdom Ndlovu, Herry Morris, Said Sued, Salum Sued, Kisiga, Machuppa na wengine waliifanya Wahenga ishindwe kufuruka licha ya mara kadhaa kubisha hodi langoni mwa mwao.
Dakika chache kabla ya pambano hilo kumalizika huku kiza kikiwa kimeshaanza kutamba uwanjani, Wahenga walipata bao la kufutia machozi lililofungwa kwa mkwaju wa penati na nyota wa kikosi hicho, Macocha Tembele aliyekuwa akihaha uwanja mzima kuibeba timu yake.
Licha ya Wahenga kuendelea kushambulia lango la Golden Bush, mpaka kipyenga cha mwamuzi, Pondamali kulia walijikuta wakiendelea kuwa 'wateja' wa Wakali wa soka Dar es Salaam kwa kukubali kipigo kingine cha mabao 2-1.

Warembo 16 watemwa Miss Tabata



Warembo wa watakaoshiriki shindano la Miss Tabata 2013 wakiwa katika pozi tofauti kambi yao ya mazoezi Da West Park
 
JUMLA ya warembo 16 wametemwa katika kinyang’anyiro cha kumtafuta Redds Miss Tabata ambao utafanyika Mei 31 Dar West Park.
Mratibu wa shindano hilo, Godfrey Kalinga, alisema jana kuwa warembo hao wametemwa kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo utoro, kukosa sifa za kushiriki na utovu wa nidhamu.
Kalinga aliwataja warembo waliyotemwa kuwa ni Sophia Claud (21), Lilian Mpakani (19), Lilian Msanchu (19), Rita Frank (20), Pasilida Mandali (21), Rachel Mussa (19), Jasmin Damian (18), Angelina Mkinga (19), Mercy Mwakasungu (20), Tunu Hamis (19), Ray Issa (22), Shamim Abass (22), Shan Abass (22), Amina Ally (18), Magdalena Bhoke (21)  na Zilpha Christopher (19)
Kalinga aliwataja warembo wanoendelea na mazoezi katika umbumbi wa Dar West Park, Tabata kila siku kuwa ni Hidaya David (22), Aneth Ndumbalo (19), Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Kitereja (19),  Angela Fradius (19), Domina Soka (21), Rehema Kihinja (20) and  Glory Jigge (18).
Wengine ni Rachel Mushi (20), Caroline Sadiki (20), Kabula Juma Kibogoti (20), Blath Chambia (23), Suzzane Daniel Gingo (18), Upendo Lema (22), Pasilida Mandari (21) na Martha Gewe (19).
Washindi watano kutoka Tabata watafuzu kushiriki Redds Miss Ilala baadaye mwaka huu.
Anayeshikilia taji la Miss Tabata ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.
Redds Miss Tabata inaandaliwa na  Bob Entertainment na Keen Arts na chini ya Udhamini wa Redds, CXC Africa, Fredito Entertainment, Brake Points na Saluti5.
 

Cheka, Mashali patachimbika Mei Mosi


Reeling from the recent defeat in the hands of the German strongman Uensal Arik , TEAM Francis Cheka is back on the drawing board as it attempts to defuse negative impact of the loss in their forthcoming rumble against the man of the people and dreadlock Thomas MashaliThe duo is competing for the “IBF Continental Africa Super Middleweight Title” as optional defense for Cheka.
 
 
The tournament slated for 1st May, 2013 (May Day) has elicited a lot of excitements from thousands of boxing stakeholders in Tanzania and the whole of East African region. Thomas Mashali is the East & Central African Middleweight Champion and the biggest crowd puller in the region todate.

                                                                      Francis Cheka (right) and Uensal Arik (left)
 

Cheka’s recent defeat was kind of embarrassment as he took the fight as a warm up but alas, things turned bitter as the Germany strongman Uensal Arik sent him reeling to the floor before Thomas Mtua threw out the towel as SOS for the Tanzanian slugger! It was a defeat from “Manna”as this kind of taught Cheka a lesson or two about taking boxing serious as there is nothing as a small fight in boxing.


Adam Tanaka of Mumask Investment and Gebby Presure LTD, the man of the hour promoting this fight has been working over drive to have all the details finalized. Of the top priority is the arrival of the ring officials (all coming outside Tanzania) who have been summoned to preside over the rumble. This is so because Adam want to avoid complaints from either boxer should the decision goes against their expectations.

"The poster in Kiswahili language tells it all"

 
The man who has been charged with the responsibility to stand in as “the third man in the ring” is no other than the Zambian Army Officer, John Shipanuka who himself looks like a heavyweight boxer in refereeing uniform. Shipanuka’s body language and impatiality with boxers in the ring has illuminated his CV and make him one of the most sort-out ring officials in Sub Sahara Africa.

Arusha Mayor (left) and IBF/AFRICA' Onesmo Ngowi(right) crowing Cheka after his last defense 12/26/12

To assist him would be two Sedentary Generals of; Uganda Professional Boxing Commission (UPBC), master Simon Katogole and Daudi Chikwanje of Malawi Boxing Association (MBA). These two gentlemen would be in the company of one of the most experienced judges in East Africa Alhaj Ismail Sekisambu also from Uganda.


So, “the chickens have finally come home to roost" as any of the two has to face the consequences of his mistakes in the ring on that particular day.


So, as the clock ticks to the morning hours of May Day 2013, Dar Es Salaam landscape may turn into a “quicksand” for the two gladiators as fans from all walks of life jams the PTS Social Hall to witness yet another rumble of the year!
 
 
 Nothing has been left to chances as the World's premier professional boxing “top dog” the IBF has already given its blessing by sanctioning for the title!
 

Suarez akubali yaishe, aomba msamaha



LONDON, England
Mshmbuliaji wa Liverpool Luis Suarez ameomba msamaha baada ya kukubali adhabu ya kutocheza mechi 10 kwa kumng'ata Branislav Ivanovic wa Chelsea katika mechi ya ligi kuu ya soka ya Uingereza mwishoni mwa wiki iliyopita.
Muuruguay huyo alikuwa na muda mpaka mchana jana kupinga adhabu ya Chama cha Soka ya kuongeza mechi saba katika adhabu ya kawaida ya kukosa michezo mitatu kwa kosa la kufanya ukatili lakini akaamua kutobishia.
"Nataraji kuwa watu niliowaudhi Jumapili iliyopita watanisamehe na narudia tena kumuomba radhi binafsi Branislav," Suarez aliseka katika ukurasa wake wa Twitter.
"Ingawa ni wazi kwamba mechi 10 ni nyngi kuliko vifungo vilivyowahi kutolewa katika kosa kama hili huko nyuma ambapo wachezaji walijeruhiwa, nakubali kuwa kitendo changu kilikuwa hakikubaliki kwenye uwanja wa soka hivyo sitaki kuleta picha mbaya kwa watu kwa kukata rufaa."
Suarez, ambaye alimng'ata Ivanovic mkononi katika sare ya 2-2 kwenye uwanja wa Anfield wiki-endi iliyopita, hatoweza kuichezea Liverpool katika michuano ya ndani mpaka Septemba.
Liverpool, ambayo ilimpiga faini Suarez, ilisisitiza kusikitishwa kwake na uamuzi wa FA wa kumfungia Suarez kwa mechi 10.
"Adhabu dhidi ya Luis ilikuwa yake binafsi kuamua na ni lazima tuheshimu uamuzi wake wa kutokata rufaa kufungiwa mechi 10," mkurugenzi mtendaji Ian Ayre alisema.
Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers aikilaumu chama cha soka kwa ukali wa adhabu ya Suarez na palikuwa na kuungwa mkono na makocha wa timu pinzani jana.
"Katika kesi hii, ukubwa wa adhabu na kosa vinaonekana kupishana mno kulingnaisha na makosa ambayo wachezaji wengine wamewahi kuadhibiwa nayo," kocha wa Arsenal Arsene Wenger aliwaambia waandishi wa habari.
"Nadhani kilichommaliza kabisa Suarez ni historia yake, ambayo ina makosa mengi.
"Ndiyo sababu ameadhiwa vikali sana, ndiyo sababu pekee ambayo naweza kuiona."
Kocha wa Manchester City Roberto Mancini alisema katika mkutano wake wa Ijumaa na waandishi wa habari: "Mechi tano au sita zilitosha, huu ndiyo mtazamo wangu lakini sifanyi kazi FA."
Ni mara ya pili kwa Suarez, 26, kufungiwa kwa kumng'ata mchezaji wa timu pinzani baada ya kumng'ata Otman Bakkal wa PSV Eindhoven kwenye shingo wakati akiichezea Ajax 2010, na kufungiwa mechi saba.
Suarez alifungiwa pia mechi nane msimu uliopita baada ya FA kumuona ana kosa la kumbagua kwa rangi ya ngozi Patrice Evra wa Manchester United Oktoba 2011.
Reuters

Suarez