STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 27, 2014

Titina wa Extra Bongo ajiandaa kuacha kunengua

Mnenguaji Titi Mwinyi 'Titina' akiwa katika pozi
MNENGUAJI mahiri wa bendi ya Extra Bongo, Titi Mwinyiamir maarufu kama 'Titina' amesema anajipanga kuachana na fani hiyo baada ya kuitumikia kwa zaidi ya miaka 10.
Akizungumza na MICHARAZO, Titina aliyewahi kutamba na Double M Sound, Twanga Pepeta na FM Academia, alisema anataka kuachana na fani hiyo ili kujikita kwenye uimbaji.
Titina alisema muda aliotumika kama dansa tangu mwaka 2000 umeufanya mwili wake kuchoka na sasa anadhani ni muda muafaka kuhamia kwenye uimbaji ili kuendeleza kipaji alichonacho.
"Natarajia kuachana na unenguaji ili nijikite kwenye uimbaji, kipaji hicho ninacho tangu utotoni sema kunengua kuliniathiri na kukisahau, ila sasa sina jinsi zaidi ya kukiendeleza," alisema.
Dansa huyo alisema tayari ameanza mazoezi ya kuimba ili akiwiva vyema ahamie huko kufuata nyazo za akina Tshallah Mwana na Mbilia Bel waliowahi kutanga kwenye unenguaji kabla ya kuhamia kwenyue uimbaji na kuishika Afrika.
Titina, alisema anaamini bidii yake katika kujifunza kuimba kwa sasa ndiko kunakoweza kumfikisha pale walipofikia wakali hao kutoka Kongo au baadhi ya wanamuziki wa kike wanaotamba nchini kama akina Luiza Mbutu na wengine ambao walianzia kwenye unenguaji kabla ya kuwa waimbaji.

NEC yatoa ratiba uchaguzi mdogo Jimbo la Chalinze

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza ratiba ya uchaguzi mdogo wa jimbo la CHALINZE, mtakumbuka kuwa jimbo hilo limekuwa wazi baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo bwana Said Bwanamdogo kufariki dunia tarehe 22 Januari 2014 kwenye hospitali ya MOI jijini Dar es salaam.

Ratiba ya uchaguzi kwenye jimbo hilo iko kama ifuatavyo:-

1. Uteuzi wa wagombea  - Tarehe 12 Machi 2014

2, Kampeni na Uchaguzi - Tarehe 13 Machi 2014

3. Siku ya Uchaguzi - Tarehe 6 April, 2014


Tarehe ya wagombea ubunge kuchukua Fomu za uteuzi kwa msimamizi wa uchaguzi ni kuanzia tarehe 03 Machi, 2014 hadi tarehe 12 Machi, 2014(Siku ya uteuzi) Kabla ya saa 10:00 Alasiri.


Wagombea wanatakiwa kuwasilisha fomu za uteuzi kwa msimamizi wa uchaguzi siku ya uteuzi si zaisi ya saa 10:00 Alasiri

Da! Mwanamke ajifungua Barabarani


Mwanamke aliyejifungua barabarani
MWANAMKE mmoja raia wa Uingereza amejifungulia katika barabara moja mjini New Yorkakiwa njiani kuelekea hospitali kutokana na uchungu wa uzazi.
Polly McCourt, mwenye umri wa miaka 39,aliondoka nyumbani kwake katika mtaa wa East Side siku ya jumatatu na kujaribu kukodisha taxi hadi alipogundua kuwa mwanawe asingeweza kusubiri.
Wapita njia walimpa mama huyo koti na vitambaa walivyokuwa navyo kumfunika mwanawe hadi wahudumu walipofika kumsaidia na kumpeleka hospitaliini. Mama na mtoto walikuwa salama walipofikishwa hospitalini.
"alipiga mayowe akisema Mungu wangu mtoto wangu yuaja ,'' alisema shahidi mmoja.
Na niliweza kuona kichwa cha mtoto. Tulipomlaza mama chini kumsaidia, mtoto akawa tayari ametoka.''
Bi McCourt, anayetoka nchini Uingereza alijifungua mwanawe kando ya barabara.
Mama huyo alionekana akitabasamu alipoingia katika gari la ambulensi na kupelekwa katika hospitali ya Lennox Hill mjini New York.
Mumewe mama huyo alikuwa amekwama barabarani kutokana na msongamano wa magari alipopata simu kutoka kwa mkewe.
Wawili hao tayari wana watoto wengine wawili, Conor mwenye umri wa miaka sita na Adele mwenye umri wa miaka minne kulingana na jarida la New York Daily News.
Inaarifiwa walihamia mjini New York miaka minne iliyopita kutoka Dublin nchini Ireland.
BBC

27 warejesha fomu Uchaguzi wa Taswa, Shafii Dauda 'achomoa'

Shafii Dauda aliyeshindwa kurejesha fomu ya uchaguzi wa Taswa
JUMLA ya waombaji 27 kati ya 28 wamerejesha fomu kuomba kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi wa Kamati mpya ya Utendaji ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) utakaofanyika Machi 2, 2014 jijini Dar es Salaam.

Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu hizo ilikuwa leo Alhamisi (Februari 27 mwaka huu) saa 9 alasiri.

Waliorejesha kwa nafasi ya ujumbe ni Arone Benedict Mpanduka, Elizabeth Rashid Mayemba, Emmanuel Augustino Muga, Hassan Maulid Bumbuli, Ibrahim Mkomwa Bakari, Masau Kuliga Bwire, Mbozi Ernest Katala, Mroki Timothy Mroki, Mussa Juma, Mwani Omary Nyangassa, Rehure Richard Nyaulawa, Salum Amiri Jaba, Tullo Stephen Chambo na Urick Chacha Maginga.

Mhazini Msaidizi ni Elius John Kambili, Zena Suleiman Chande wakati Mhazini Mkuu ni Shija Richard Shija na Mohamed Salim Mkangara.

Katibu Msaidizi ni Alfred Lucas Mapunda, Grace Aloyce Hoka na Patrick Raymond Nyembera. Katibu Mkuu ni Amir Ally Mhando pekee.

Waombaji nafasi ya Makamu Mwenyekiti ni Egbert Emmanuel Mkoko, Maulid Baraka Kitenge na Mohamed Omary Masenga. 
Waliojitosa kwenye nafasi ya Mwenyekiti ni George John Ishabairu, Juma Abbas Pinto.

Mgombea mwingine wa nafasi hiyo, Shaffih Kajuna Dauda hakurudisha fomu kwa madai ya kubanwa na moja ya vipengele vya katiba ya chama hicho na yeye ameonyesha kuridhika kujiweka kando bila kinyongo.

Wazambia watua, Twiga Stars yaapa kuing'oa Afrika

Twiga Stars wanaotarajiwa kuwapa raha watanzania kesho

WAKATI Zambia (Shepolopolo) imewasili leo mchana (Februari 27 mwaka huu), Twiga Stars imesema mazoezi yamewaingia barabara tayari kwa mechi dhidi ya Wazambia hao itakayochezwa kesho (Februari 28 mwaka huu). Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya kwanza ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) itafanyika Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi kuanzia saa 10 kamili jioni, na hakutakuwa na kiingilio. Wakizungumzia mechi hiyo, Kocha wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage na nahodha wa timu hiyo Sophia Mwasikili wamesema kikosi chao kimewiva kwa ajili ya mpambano huo baada ya kufanyia kazi upungufu uliojitokeza katika mechi ya kwanza.
Twiga Stars ilipoteza mechi ya kwanza iliyochezwa Februari 14 mwaka huu jijini Lusaka kwa mabao 2-1, na inahitaji ushindi ili iweze kusonga mbele kwenye michuano hiyo ambayo fainali zake zitafanyika Oktoba mwaka huu nchini Namibia.
Iwapo Twiga Stars itafanikiwa kuitoa Zambia katika mechi hiyo itakayooneshwa moja kwa moja na Azam Tv itacheza raundi ya mwisho na Zimbabwe.
Msafara wa Shepolopolo una watu 26 ambapo wachezaji ni Anita Mulenga, Annie Kibanji, Carol Howes, Debora Chisanga, Emelda Musonda, Esther Mukwasa, Grace Zulu, Hazel Nali, Hellen Mubanga, Lweendo Chisamu, Meya Banda, Mirriam Katamanda, Misozi Zulu, Mupopo Kabange, Noria Sosala, Rachel Lungu na Susan Banda.
Viongozi ni Maclean Daka, Charles Bwale, Kaluba Kangwa, Enala Phiri, Cornelia Chazura, James Nyimbili, Besa Chibwe, Dorothy Sampa na Kabungo Katongo.

Kim Poulsen 'byebye' Taifa Stars, TFF yavunja mkataba wake

Kim Poulsen aliyevuniwa mkataba na TFF
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) na Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen wamekubaliana kuvunja mkataba katika makubaliano ambayo ni siri kwa pande zote mbili.
Uamuzi huo umetangazwa leo (Februari 27 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kwa pamoja na Rais wa TFF, Jamal Malinzi na Kocha Poulsen mbele ya waandishi wa habari.
Rais Malinzi kwa niaba ya TFF ametoa shukrani za dhati kwa Kocha Poulsen kwa ushirikiano na mchango ambao ameutoa kwa Tanzania kuanzia kwenye mpira wa miguu wa vijana.
Naye Kim amewashukuru Watanzania kwa ushirikiano waliompatia kwa kipindi cha miaka mitatu alichokaa nchini kuanzia Mei 2011 alipoteuliwa kuwa kocha wa timu za Taifa za vijana, na baadaye Taifa Stars.
Akizungumzia benchi jipya la ufundi la Taifa Stars, Rais Malinzi amesema linatarajiwa kutangazwa hivi karibuni likiongozwa na kocha kutoka nje ya Tanzania.
Amesema kwa upande wa mechi dhidi ya Namibia itakayochezwa Machi 5 mwaka huu jijini Windhoek, Stars itaongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi, Salum Madadi akisaidiwa na kocha Hafidh Badru kutoka Zanzibar.

Nyota wa Yanga waenguliwa Stars, Kado wenzake waula

Juma Luizio 'Ndanda' ameongezwa Taifa Stars


Baadhi ya nyota wanaotarajiwa kuiongoza Stars dhidi ya Namibia

Na Boniface Wambura
KAIMU Kocha Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Salum Madadi amewaondoa wachezaji watano wa Yanga katika kikosi kilichotajwa awali ili wapate fursa ya kuitumikia timu yao kwenye mechi mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al-Ahly ya Misri.
Wachezaji hao ni Athuman Idd, David Luhende, Deogratius Munishi, Frank Domayo, Kelvin Yondani na Mrisho Ngasa. Pia kipa Ivo Mapunda ameondolewa katika kikosi hicho baada ya kupata msiba.

Nafasi zao zimezibwa na wachezaji Abdi Banda (Coastal Union), Himid Mao (Azam), Juma Luizio (Mtibwa Sugar), Said Moradi (Azam) na Shabani Kado (Coastal Union).
Taifa Stars itaingia kambini keshokutwa (Machi 1 mwaka huu) jioni kwenye hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam, na itaondoka Machi 3 mwaka huu alfajiri kwa ndege ya South African Airways na kurejea nchini Machi 7 mwaka huu saa 8.15 mchana.

Kingwendu aja na Faza Hausi

MSANII wa filamu nchini Athumani Lali 'Budege' baada ya kucheza filamu za watu sasa ameamua kuja na filamu zake mwenyewe na kuwawezesha wasanii wenzie kuwa na kipato kizuri baada ya kuamua kufungua kampuni yake binafsi inayokwenda kwa jina la AJM Entatainment ambayo ina husika na maswala ya filamu za kibongo
Athumani Lali 'Budege'
akizungumza na mwandishi wa habari hizi Lali amesema kuwa kwa sasa yupo katika atua za mwisho kwa ajili ya kutoa filamu mpya inayokwenda kwa jina la Faza Hausi ambayo imeshilikisha wasanii wakongwe ndani yake akiwemo Mohamed Nurdini 'Chekbudi' ,Esha Buheti, Rashidi Mwishehe 'Kingwendu' Muogo Mchungu 
Filamu hiyo itakayo tolewa na Kampuni hiyo ya jijini Dar es salaam itakuwa moto wa kuotea mbali kwani si ya kukosa kabisa kwa mashabiki wa filamu nchini
filamu hiyo ya Faza Hausi itakuwa mtaani wakati wowote kuanzia sasa kwani takribani vitu vyote muhimu vimeshafanyika hivyo wadau wakae mkao wa kula kwani filamu hii si yakuikosa
Ambapo itapatikana Tanzania nzima nikianzia Dar es salaam na mikoa yote filamu hiyo itawafikia

Inspekta Harun kutambulisha mpya, akisdaka mrembo Mbeya

Inspekta Harun 'Babu' katika pozi
MSANII mkongwe wa muziki wa kizazi kipya nchini, Haruna Kahena 'Inspekta Harun' a.k.a Babu anatarajiwa kuitambulisha albamu yake mpya ya 'Sharubu za Babu' sambamba na video ya wimbo wake wa 'Hujachelewa' jijini Mbeya wikiendi hii.
Akizungumza na MICHARAZO, Inspekta alisema kuwa, utambulisho huo utafanyika siku ya Jumapili kwenye ukumbi maarufu jijini humo ambao utaambatana pia na shindano la kusaka kimwana wa kucheza filamu ya 'Mtoto wa geti Kali'.
Staa huyo wa nyimbo kama 'Nje Ndani', 'Simulizi la Ufasaha', 'Mtoto wa Geti Kali' na nyingine, alisema shindano hilo la kusaka mrembo wa kucheza filamu hiyo ya Mtoto wa Geti Kali utafanyika kila mahali atakapoenda kutambulisha albamu na video hiyo.
Alisema mwishoni watakaopatikana watashindanishwa kwa pamoja ili kupata kisura mmoja ambaye ndiye atakayekuwa mhusika mkuu wa filamu hiyo ambayo inatokana na wimbo wake uliowahi kutamba miaka ya nyuma wenyue jina hilo.
"Natarajia kuzindua video ya wimbo wangu mpya wa 'Hujachelewa' sambamba na kutambulisha albamu ya 'Sharubu za Babu'," alisema na kuongeza;
"Onyesho hilo litafanyika Machi 2, jijini Mbeya na litaenda sambamba na shindano la kusaka mrembo wa kucheza filamu yangu ya Mtoto wa Geti Kali na nitasindikizwa na wasanii kadhaa nyota wa jijini humo na wale wa Dar," alisema Inspekta Harun.
Msanii huyo alisema orodha ya watakaomsindikiza anatarajiwa kutangaza kesho ili kuwaweka tayari mashabiki wake kuwapokea vyema katika onyesho hilo la Jumapili.

Ikulu yabadilisha mwandishi wa hotuba za Rais

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
        Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Togolani I. Mavura kuwa Msaidizi wa Rais (Hotuba) kuanzia Februari 8, mwaka huu, 2014.
Taarifa iliyotolewa leo, Jumanne, Februari 25, 2014, mjini Dar Es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue inasema kuwa Bwana Mavura anachukua nafasi ya Bwana Msafiri Marwa ambaye amehamishimiwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kupangiwa kazi nyingine.
Kabla ya uteuzi huo, Bwana Mavura ambaye ni Ofisa wa Mambo ya Nje alikuwa Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 “Mwisho”
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
25 Februari, 2014

Azam warejea kileleni, Mwaikimba adhihirisha bado wamo!

MSHAMBULIAJI 'ngongoti' wa Azam, Gaudence Mwaikimba jana alidhihirisha kuwa bado wamo baada ya kuifungia timu yake mabao mawili na kuiwezesha kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara wakiishusha mabingwa watetezi Yanga.
Mwaikimba aliyewahi kutamba na Yanga, Kagera Sugar, Moro United, Tukuyu Stars na Ashanti, alifunga mabao hayo katika kila kipindi wakati Azam wakiizamisha Ashanti United kwa mabao 4-0 kwenye mechi pekee ya ligi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Chamazi jijini Dar.
Kwa muda mrefgu mchezaji huyo maarufu kama 'Andy Carroll' hakuwa akipangwa na makocha wa timu yake mbele ya washambuliaji mahiri wa timu hiyo, John Bocco 'Adebayor' aliye majeruhi na Kipre Tchetche anayetumikia kadi nyekundu na aliitumia nafasi aliyopewa na kocha Joseph Umog kwa kufunga mabao hao.
Mabao mengine ya Azam yaliwekwa kimiani na mabeki wake wa kati Aggrey Morris aliyefungwa kwa mkwaju wa penati lililokuwa bao la kwanza la timu hiyo na jingine likiwekwa wavuni na Said Morad na kuifanya Azma kufikisha pointi 40, mbili zaidi na ilizonazo Yanga yenye pointi 38 na kurejea tena kileleni.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea wikiendi kwa michezo kadhaa lakini pambano linalosubiriwa kwa hamu kubwa ni lile la Simba itakayoumana na Ruvu Shooting zote zikiwa na maumivu wa vipigo ilivyopewa katika mechi zao zilizopita, Simba ikilala kwa maafande wa JKT Ruvu kwa mabao 3-2 na Ruvu Shooting wakifumuliwa na Yanga kwa magoli 7-0.

Real Madrid 'yaua', Chelsea angalau Ligi ya Mabingwa Ulaya

Didier Drogba akionyesha manjonjo yaike mbele ya John Terry wa Chelsea jana ambapo timu zao zilitoka sare ya 1-1

Bale na Ronaldo wakipongezana wakati wakiiua Schalke 04 nyumbani kwao Ujerumani jan
REAL Madrid ikiwa katika kiwango cha hali ya juu msimu huu imevunja mwiko wa kushindwa kushinda kwenye ardhi ya Ujerumani baada ya usiku wa kuamkia leo kuifumua Schalke 04 kwa mabao 6-1 na kunusu hatua ya Robo Fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, huku Chelsea ya England ikibanwa ugenini na Galatasaray na kutoka sare ya 1-1 nchini Uturuki.
Mabao ya Karim Benzema katika dakika ya 13, kisha Gareth Bale kwenye dakika ya 21 yaliifanya Madrid kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-0 kabla ya kurudi kipindi cha pili wakiwa moto zaidi na kuongeza mabao mengine manne.
Cristiano Ronaldo alifunga bao dakika ya 52 kabla ya Benzema kurudi tena nyavuni dakika mbili baadaye na Bale kuongeza jingine dakika ya 69 na Ronaldo kumalizi udhia dakika ya 89.
Wenyeji waliambulia bao lao la kufutia machozi dakika moja ya nyongeza (90+1) kupitia kwa mdachi,  Klaas-Jan
Huntelaar na kuifanya Schalke 04 kuwa na kibarua kigumu cha kuweza kupata ushindi wa mabao 5-0 ugenini ili kuing'oa vinara hao wa Ligi ya Hispania.
Katika pambano jingine la kuhitimisha mechi za mkono wa kwanza za 16 Bora Chelsea ikiwa ugenini ilitangulia kuwafunga wenyeji kwa bao la Fernando Torres dakika ya 9 tu ya mchezo na kutoa matumaini huenda vinara hao wa Ligi ya England wangeibuka na ushindi ugenini na kuifuta machozi nchi yao ambayo imeshuhudia timu zake nyingine tatu zikifungwa katika mechi zake za mkondo huo.
Hata hivyo Chelsea walishindwa kulinda bao hilo kwani wenyeji Galatasaray walikuja kuchomoa bao dakika ya 65 kupitia kwa Mcameroon,  Aurélien Bayard Chedjou  aliyemalizia mpira wa kona uliochongwa na Mdachi Wesley Sneijder na mabeki wa Chelsea wakazembea kumkaba na kumfunga kirahisi kipa wao Petr Cech .