STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 27, 2014

Azam warejea kileleni, Mwaikimba adhihirisha bado wamo!

MSHAMBULIAJI 'ngongoti' wa Azam, Gaudence Mwaikimba jana alidhihirisha kuwa bado wamo baada ya kuifungia timu yake mabao mawili na kuiwezesha kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara wakiishusha mabingwa watetezi Yanga.
Mwaikimba aliyewahi kutamba na Yanga, Kagera Sugar, Moro United, Tukuyu Stars na Ashanti, alifunga mabao hayo katika kila kipindi wakati Azam wakiizamisha Ashanti United kwa mabao 4-0 kwenye mechi pekee ya ligi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Chamazi jijini Dar.
Kwa muda mrefgu mchezaji huyo maarufu kama 'Andy Carroll' hakuwa akipangwa na makocha wa timu yake mbele ya washambuliaji mahiri wa timu hiyo, John Bocco 'Adebayor' aliye majeruhi na Kipre Tchetche anayetumikia kadi nyekundu na aliitumia nafasi aliyopewa na kocha Joseph Umog kwa kufunga mabao hao.
Mabao mengine ya Azam yaliwekwa kimiani na mabeki wake wa kati Aggrey Morris aliyefungwa kwa mkwaju wa penati lililokuwa bao la kwanza la timu hiyo na jingine likiwekwa wavuni na Said Morad na kuifanya Azma kufikisha pointi 40, mbili zaidi na ilizonazo Yanga yenye pointi 38 na kurejea tena kileleni.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea wikiendi kwa michezo kadhaa lakini pambano linalosubiriwa kwa hamu kubwa ni lile la Simba itakayoumana na Ruvu Shooting zote zikiwa na maumivu wa vipigo ilivyopewa katika mechi zao zilizopita, Simba ikilala kwa maafande wa JKT Ruvu kwa mabao 3-2 na Ruvu Shooting wakifumuliwa na Yanga kwa magoli 7-0.

No comments:

Post a Comment