STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 27, 2014

NEC yatoa ratiba uchaguzi mdogo Jimbo la Chalinze

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza ratiba ya uchaguzi mdogo wa jimbo la CHALINZE, mtakumbuka kuwa jimbo hilo limekuwa wazi baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo bwana Said Bwanamdogo kufariki dunia tarehe 22 Januari 2014 kwenye hospitali ya MOI jijini Dar es salaam.

Ratiba ya uchaguzi kwenye jimbo hilo iko kama ifuatavyo:-

1. Uteuzi wa wagombea  - Tarehe 12 Machi 2014

2, Kampeni na Uchaguzi - Tarehe 13 Machi 2014

3. Siku ya Uchaguzi - Tarehe 6 April, 2014


Tarehe ya wagombea ubunge kuchukua Fomu za uteuzi kwa msimamizi wa uchaguzi ni kuanzia tarehe 03 Machi, 2014 hadi tarehe 12 Machi, 2014(Siku ya uteuzi) Kabla ya saa 10:00 Alasiri.


Wagombea wanatakiwa kuwasilisha fomu za uteuzi kwa msimamizi wa uchaguzi siku ya uteuzi si zaisi ya saa 10:00 Alasiri

No comments:

Post a Comment