STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 27, 2014

Nyota wa Yanga waenguliwa Stars, Kado wenzake waula

Juma Luizio 'Ndanda' ameongezwa Taifa Stars


Baadhi ya nyota wanaotarajiwa kuiongoza Stars dhidi ya Namibia

Na Boniface Wambura
KAIMU Kocha Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Salum Madadi amewaondoa wachezaji watano wa Yanga katika kikosi kilichotajwa awali ili wapate fursa ya kuitumikia timu yao kwenye mechi mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al-Ahly ya Misri.
Wachezaji hao ni Athuman Idd, David Luhende, Deogratius Munishi, Frank Domayo, Kelvin Yondani na Mrisho Ngasa. Pia kipa Ivo Mapunda ameondolewa katika kikosi hicho baada ya kupata msiba.

Nafasi zao zimezibwa na wachezaji Abdi Banda (Coastal Union), Himid Mao (Azam), Juma Luizio (Mtibwa Sugar), Said Moradi (Azam) na Shabani Kado (Coastal Union).
Taifa Stars itaingia kambini keshokutwa (Machi 1 mwaka huu) jioni kwenye hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam, na itaondoka Machi 3 mwaka huu alfajiri kwa ndege ya South African Airways na kurejea nchini Machi 7 mwaka huu saa 8.15 mchana.

No comments:

Post a Comment