STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 24, 2013

Simba kuonyesha makali ya Oman leo Taifa

Kikosi cha Simba kinachotarajiwa kushuka dimbani leo


MABINGWA wa soka nchini, Simba iliyorejea jana kutoka Oman ilipokuwa kwenye kambi ya mazoezi, inatarajiwa kushuka dimbani leo kuonyesha mambo ya umangani itakapovaana na Black Leopards ya Afrika Kusini katika pambano la kirafiki la kimataifa.
Pambao hilo litakalopigwa majira ya jioni kwenye dimba la Taifa, jijini Dar es Salaam itakuwa pambano la mwisho kwa Simba kabla ya kuanza kwa duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Jumamosi.
Simba inatarajiwa kuanza duru hilo kwa kuvaana na African Lyon kwenye uwanja wa Taifa.
Black Leopards inayoshiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini, ipo nchini kwa ziara ya kujipima nguvu wakisubiri kuendelea na ligi yao iliyosimama kwa sasa kupisha michuano ya AFCON-2013 inayofanyika nchini mwao.
Timu hiyo jana iliendelea kuwa mnyonge kwa Yanga kwa kulazwa mabao 2-1 ikiwa ni siku chache tangu ichezee kichapo cha kukandikwa mabao 3-2.
Simba iliyoenda moja kwa moja kambini mara baada ya kuwasili jana mchana, imetamba kuwapa raha mashabiki wake ambao walimaliza duru la kwanza la ligi kuu kwa masononeko.
Mabingwa hao hiyo itakuwa mechi yao ya nne ya kujipima nguvu baada ya awali kucheza mechi tatu ughaibuni nchini Oman ikishinda mechi moja na kupoteza mbili.

Mashabiki wa soka wanatarajiwa kujitokeza kwa wingi katika pambano hilo la leo ili kutaka kushuhudia makali ya timu yao, baada ya watani zao Yanga waliokuwa Uturuki, walivyokonga nyoyo za mashabiki wao kwa kuisasambua Blac Leopards mara mbili.

Wanachama Yanga waanza kugeukana, kisa...!

Ramadhani Kampira, mmoja wa wanachama wa Yanga



BAADHI ya wanachama wa Yanga wameibuka na kuelezea hofu waliyonayo juu ya kupitishwa kwa vipengele vya katiba inayowapa madaraka makubwa Mwenyekiti na Makamu wake klabu hapo.
Wanachama hao walisema kupitishwa kwa vipengele vinavyowapa viongozi hao uwezo wa kumfuta uanachama mwanachama yeyote wa Yanga ni sawa na kuruhusu udikteta pamoja na kuivuruga Yanga.
Mmoja wa wanachama hao, Ramadhani Kampira, alisema japo wanachama wenzake waliafiki vipengele hivyo katika mkutano mkuu ulioitishwa mwishoni mwa wiki, lakini ukweli hakubaliani navyo.
Kampira aliyewahi kuichezea timu hiyo na kung'ara na TAMCO Kibaha na Sifa United, alisema kuruhusu hali hiyo inaweza kutumiwa vibaya na viongozi katika suala la chuki binafsi.
"Mtu anaweza kuamka usingizi au kutoka nyumbani akiwa kagombana na mkewe kisha kuamua kumfukuzisha mtu uanachama kwa chuki na kusiwepo wa kuwahukumu kwa vile lipo kwenye katiba," alisema Kampira.
Naye Mwinjuma Muumini, ambaaye ni mmoja wa waimbaji nyota wa muziki wa dansi, alisema hakubaliani na maamuzi hayo japo alikiri hajui kitu gani kilichowakumba wanachama wenzake na kuafiki jambo hilo.
Muumini, anayefahamika kama 'Kocha wa Dunia' au 'Mzee wa Chelsea' alisema kuwa maamuzi hayo ni kurejesha ukoloni na kuruhusu udikteta katika Yanga kwani haikubaliki hata kwa sheria ya nchi.
"Sijajua ajenda za mkutano huo zilikuwa zipi, lakini kilichofanywa na wanachama wenzetu ni msiba ambao utakuja kuigharimu na kuivuruga Yanga mbele ya safari, huo ni udikteta,:" alisema.
Juu ya suala la kutimuliwa kwa wanachama wenzao waliokuwa waajiriwa wa klabu hiyo, Louis Sendeu na Celestine Mwesigwa, Kampira yeye alisema taratibu na sheria za kazi zizingatiwe na zisiingizwe katika masuala ya michezo.
"Wale walikuwa waajiriwa na kama walitimuliwa kazi bila kuzingatiwa taratibu au kulipwa haki zao stahiki, walikuwa na haki ya kutafuta jasho lao mahali pengine, hivyo suala hilo lisitumiwe kuwaonea watu waliotendwa sivyo ndivyo,": alisema Kampira.
Wanachama wa Yanga waliafiki kwa kauli moja kuwatimua uanachama akina Sendeu kwa madai ya kosa la kukimbilia mahakamani ya usuluhishi kudai haki zao za malimbikizo na misharaha.
Pia mkutano huo uliafiki kubadilishwa kwa vipengele vya katiba yao kwa kuwaruhusu viongozi hao wa juu kuwatimua wanachama mara watakapobainika kufanya makosa bila kusubiri maamuzi ya wengi.

Irene Paul amuibua Kalunde

Msanii Irene Paul


BAADA ya kutumikishwa katika kazi za wasanii wengine, mwanadada mkali wa Bongo Movie, Irene Paul 'Brown Eyes', amefyatua filamu yake binafsi ya kwanza kupitia kampuni binafsi aliyoianzisha hivi karibuni.
Msanii huyo, aliiambia MICHARAZO mapema leo kuwa, filamu hiyo mpya inafahamikwa kwa jina la 'Kalunde' na ipo njiani kuachiwa mtaani ikiwa imewashirikisha wasanii kadhaa nyota nchini.
Irene aliwataja wasanii hao walioshiriki filamu hiyo inayozungumzia masuala ya ndoa za utotoni na changamoto zake, ni pamoja na Grace Mapunda 'Mama Kawele', Hemed Suleiman 'PHD', Ahmed Olotu 'Mzee Chillo', yeye na Richard Mshanga 'Masinde'.
"Kwa mara ya kwanza nimeibuka na filamu yangu binafsi iitwayo 'Kalunde' ambayo mbali na kuigiza mie mwenyewe pia imewashirikisha wasanii kadhaa mahiri nchini kama akina Mzee Masinde, Mzee Chillo, Mama Kawele, Hemed na wengineo," alisema Irene.
Irene alisema kwa sasa anamalizia mambo fulani kabla ya kuitoa hadharani kuwapa mashabiki wake burudani ambayo wamekuwa wakimshuhudia katika kazi za watu wengine.
Muigizaji huyo aliyewajio kuwa mtangazaji na pia mwanamitindo, alisema filamu hiyo imezalishwa na kampuni yake binafsi iitwayo Krema Production na kazi hiyo ni mwanzo wa kudhihirisha kwamba yeye hajabahatisha kuingia katika fani hiyo.

Kabla ya kuipakua kazi hiyo binafsi, mwanadada huyo alishacheza filamu kama Shujaa, I Hate My Birthday, Unpredictable, The Shell, Handsome wa Kijiji, Triple L, Fikra Zangu na nyingine zinazozidi 15 tangu atumbukie kwenye fani hiyo mwaka juzi.

Zola D ana Swahili Hip Hop


Zola D katika pozi
MSANII nyota wa muziki wa hip hop nchini, David Mlope 'Zola D' anajiandaa kupakua albamu yake ya kwanza tangu atuimbukie kwenye fani hiyo itakayokuwa na nyimbo 21.
Akizungumza na MICHARAZO, Zola D, alisema albamu hiyo itafahamikwa kwa jina la 'Swahili Hip Hop' ambayo imekusanya nyimbo zake zote alizozifyatua tangu aingie kwenye fani hjiyo mwaka 1995.
Zola D alisema, baadhi ya nyimbo zitakazokuwa katika albamu hiyo ni pamoja na kibao kilichompa ujiko miaka kadhaa iliyopita cha 'Moto wa Tipper', 'Jana Sio Leo', 'Sipati Mchongo', 'What Going On', 'Hustler King', 'Unde', 'Msela Sana', Rap Gangster' na 'Rudi'.
Nyingine ni nyimbo zake mbili za hivi karibuni ambazo zinaendelea kutamba katika vituo vya redio na runinga za 'Coast to Coast' na 'Knockout' alioimba na P Funk.
"Nimeshakamilisha kila kitu kabla ya kuitoa hadharani albamu yangu itakayokuwa ya kwanza tangu nitumbukie katika fani hii miaka karibu 20 iliyopita, itakuwa na nyimbo za zamani na mpya ambazo baadhi zinaendelea kutamba nchini na nje ya nchi," alisema.
Msanii huyo ambaye pia ni bondia wa ngumi za kulipwa wa uzito wa juu akiwa pia amesilimu kutoka dini ya Ukristo akifahamika kwa jina la Daud, alisema mashabiki wake ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiuulizia juu ya albamu hiyo waondoe shaka.

MBUNIFU ALLY REMTULLAH KUIPEPERUSHA BENDERA MAREKANI


Meneja Masoko wa Kampuni ya Tanzania Hair Industry ltd James Walwa – Jimmy akimkabidhi mbunifu wa mavazi nchini Ally Rehmtullah tiketi kwa ajili ya kwenda kuiwakilisha Afrika Mashariki katika mkutano wa ‘The Economics of the Africa Fashion Industry’ utakaofanyika nchini Marekani mwezi wa Februari. Tanzania Hair Industry ltd ambao ndio watengenezaji wa nywele maarufu aina ya Darling ndio wadhamini wa safari ya mbunifu huyu kwenye mkutano huo wa kihistoria utakaofanyika katika Kikuu cha Havard nchini Marekani.
 
Mbunifu mahiri wa mavazi nchini Tanzania Ally Remtullah amechaguliwa kuiwakilisha Africa Mashariki katika ‘East Africa Fashion Industry’ kuongea katika mkusanyiko wa Afrika Business Conference utakaofanyika Harvard Business School nchini Marekani.
 
Akizungumza na Lenzi ya Michezo  jijini Dar es Salaam jana, Mbunifu huyo Remtullah amesema shughuli hiyo itakayofanyika katika Chuo Kikuu cha Marekani cha Harvard ambacho ni kikubwa kuliko vyote duniani itafanyika Februari tarehe 15 mwaka 2013.
 
Akifafanua amesema kuwa kila mwaka Chuoni hapo kunafanyika mikutano ya ‘Africa Business Conference’ ikiwa na kauli mbiu tofauti na sasa mwaka huu yeye amechaguliwa kuwa mmoja wa wazungumzaji kuhusiana na ‘The Economic of Africa Fashion’.
 
Ally Remtullah amesema kwa ujumla anaiwakilisha Afrika Mashariki katika kategori hiyo ambapo anatarajiwa kuzungumzia changamoto zinazoikabili na fursa zinazopatikana katika tasnia ya fasheni Afrika Mashariki, ikiwemo tatizo la umeme na gharama za manunuzi ya vitambaa vya Pamba ambayo kimsingi huzalisha katika ukanda huu.
 
Amesema anafurahi kuchaguliwa na wandaaji hao kuziwakilisha nchi za Afrika Mashariki na sasa si kwenda tena kuonyesha mavazi, bali ni kuzungumza mbele ya wadau wakubwa wa kidunia kuhusu nafasi ya masuala ya ubunifu na uchumi.
Wazungumzaji wengine katika mkutano huo ni pamoja na mbunifu maarufu wa Afrika Magharibi Ituen Basi kutoka Nigeria.
 
Katika maandalizi hayo Ally amesema pamoja na kusoma vitu vingi kuhusiana na uchumi katika tasnia ya fasheni na gharama za uzalishaji za viwanda vya nguo, pia amekutana na wafanyabiashara wakubwa wa viwanda vya kutengeneza nguo hasa za kiafrika akiwemo Mfanyabiashara Mkubwa nchini Mh. Mohammed Dewji ambaye kwa namna moja ama nyingine amempa ushirikiano wa kutosha.
 
Safari hiyo ya mbunifu wa mavazi nchini Ally Remtullah katika mkutano mkubwa wa kihistoria wa Boston nchini Marekani, imedhaminiwa na kampuni ya Tanzania Hair Industry Ltd, ambao ni wazalishaji wa nywele maafuru aina ya Darling.

YANGA YAILIZA TENA BLACK LEOPARDS CCM KIRUMBA-MWANZA



Wachezaji wa timu Yanga wakifurahia goli la pili lililofungwa na Jerry Tegete kipindi cha pili mnamo dakika ya 54 kwa njia ya penati.


Golikipa wa timu ya Black Leopards,Posnett Omony akisota kuokoa mpira uliotinga wavuni kutoka kwa mchezaji wa timu ya Yanga Jerry Tegete kwa njia ya penati mnamo dakika ya 54.Timu ya Yanga imeibuka kifua mbele mpaka dakika 90 kwa kuinyuka goli 2-1 timu ya Black Leopards kwenye mchezo wao wa marudiano wa kirafiki uliofanyika kwenye uwanja wa CCM-Kirumba jijini Mwanza.Picha na JICHIE BLOG-jijini Mwanza.


Mchezaji wa timu ya Yanga David Luhende akitaka kumchomoka mchezaji wa timu ya Black Leopards, Moses Kwena, kwenye mchezo wao wa marudio uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza jioni ya leo.


Pichani ni Golikipa wa Black Leopards Posnett Omony akijitahidi kuokoa mpira uliopigwa kwa kichwa na mchezaji wa Yanga, Said Bahanuzi na hatimaye kutinga kimiani mnamo dakika ya saba.


Mchezaji Hamis Kiza wa Yanga akifanya jitihada za kumtoka beki wa timu ya Black Leopards,Victor Kamhuka.


Mchezaji wa wa timu ya Yanga David Luhende akitaka kumtoka mchezaji wa timu ya Black Leopards, Moses Kwena, kwenye mchezo wao wa marudio uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.






Baadhi ya mashabiki wa Mpira wakiwa wamepanga mstari kwa ajili ya kununua tiketi na kujionea kandanda safi kabisa kati ya timu ya Yanga na Black Leopards ya Afrika kusini.


Kikosi cha Yanga kikiwa katika picha ya pamoja.


Sehemu ya umati wa watu waliokuwa wakishuhudia mchezo huo,ambapo timu ya Yanga imetoka kifua mbele goli 2-1 dhidi ya timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini, mchezo huo umechezwa leo kwenye uwanja wa CCM-Kirumba jijini Mwanza.


Mtanange ukikaribia kuanza.


Kikosi cha timu ya Black Leopards.


Benchi la ufundi la timu ya Yanga


Ilikuwa ni patashika nguo  kuchanika, mchezaji wa timu ya Yanga, Jerry Tegete akiwatoka baadhi ya mabeki wa timu ya Black Leopards, Jerry alifanikiwa kufunga goli la pili mnamo dakika ya 54 kipindi cha pili.





Nginja nginja tuu


Makocha wakipongezana mara baada ya mpira kuisha.


Sehemu ya Umati wa mashabiki wa timu ya Yanga.


Mashabiki wakiwa kwenye mstari kwa ajili ya kuingia uwanjani.