STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 24, 2013

Irene Paul amuibua Kalunde

Msanii Irene Paul


BAADA ya kutumikishwa katika kazi za wasanii wengine, mwanadada mkali wa Bongo Movie, Irene Paul 'Brown Eyes', amefyatua filamu yake binafsi ya kwanza kupitia kampuni binafsi aliyoianzisha hivi karibuni.
Msanii huyo, aliiambia MICHARAZO mapema leo kuwa, filamu hiyo mpya inafahamikwa kwa jina la 'Kalunde' na ipo njiani kuachiwa mtaani ikiwa imewashirikisha wasanii kadhaa nyota nchini.
Irene aliwataja wasanii hao walioshiriki filamu hiyo inayozungumzia masuala ya ndoa za utotoni na changamoto zake, ni pamoja na Grace Mapunda 'Mama Kawele', Hemed Suleiman 'PHD', Ahmed Olotu 'Mzee Chillo', yeye na Richard Mshanga 'Masinde'.
"Kwa mara ya kwanza nimeibuka na filamu yangu binafsi iitwayo 'Kalunde' ambayo mbali na kuigiza mie mwenyewe pia imewashirikisha wasanii kadhaa mahiri nchini kama akina Mzee Masinde, Mzee Chillo, Mama Kawele, Hemed na wengineo," alisema Irene.
Irene alisema kwa sasa anamalizia mambo fulani kabla ya kuitoa hadharani kuwapa mashabiki wake burudani ambayo wamekuwa wakimshuhudia katika kazi za watu wengine.
Muigizaji huyo aliyewajio kuwa mtangazaji na pia mwanamitindo, alisema filamu hiyo imezalishwa na kampuni yake binafsi iitwayo Krema Production na kazi hiyo ni mwanzo wa kudhihirisha kwamba yeye hajabahatisha kuingia katika fani hiyo.

Kabla ya kuipakua kazi hiyo binafsi, mwanadada huyo alishacheza filamu kama Shujaa, I Hate My Birthday, Unpredictable, The Shell, Handsome wa Kijiji, Triple L, Fikra Zangu na nyingine zinazozidi 15 tangu atumbukie kwenye fani hiyo mwaka juzi.

No comments:

Post a Comment