STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 13, 2013

GOLDEN BUSH VETERANI WALIVYOISASAMBUA WAHENGA FC JANA

Mlezi wa timu ya Goldoen Bush Veterani, Onesmo Waziri 'Ticotico' akihojiwa na waandishi wa habari katika mchezo wao na Wahenga Fc ambapo timu yao ilishinda mabao 4-3.

Mshambuliaji Herry Morris akitafakari wakati wa mapumziki, ambapo alishatupia mabao mawili na kuisaidia Golden Bush kushinda mabao 4-3.

Wachezaji wa Golden Bush Veterani wakiwa mapumziko


Herry Morris akihojiwa na waandishi

Beki wa timu ya Golden Bush, Majaliwa 'Afande' akijohiwa pia kwenye mchezo huo

Yona Babadimo wa Wahenga Fc naye akihojiwa wakati timu yake ikichezea kipigo toka kwa Golden Bush jana jijini Dar es Salaam waliposherehekea Mapinduzi na kuukaribisha mwaka 2013


Mengi Matunda mchezaji wa Wahenga akijohiwa baada ya kupumzishwa na benchi lake la ufundi

Said Swedi 'Panucci' akikokota mpira katika pambano lao la jana

Njoo sasa! Ndivyo anayoelekea kusema beki wa Wahenga 'Mohammed huku Godfrey Katepa wa Golden Bush akimfuata

Achia wewe! Said Swedi (3) akichunana na mchezaji wa Wahenga katika pambano lao la jana

Kama Ronaldo! Mchezaji wa Wahenga akijiandaa kupiga mpira huku Shaaban Kisiga (19) wa Golden Bush akimfuatilia sambamba na wachezaji wenzake

Mimi ndio Macocha! Macocha Mayay wa Wahenga akimtoka Godfrey Katepa (kulia) huku akichungwa na Salum Swedi 'Kussi' wa Golden Bush Veterani.

Wachezaji wa Wahenga na Golden Bush wakiwajibika uwanjani timu zao zilipokutana jana na Golden Bush kushinda mabao 4-3

Macocha wa Wahenga Fc akijaribu kutafuta mbinu za kumtoka Saidi Swedi wa Golden Bush

Mzee Hamis wa Wahenga akikokota mpira pembeni ya uwanja wa TP wakati timu yake ilipoumana na Golden Bush na kuchezea kichapo cha mabao 4-3

Wazir Mahadhi (10) akichuana na wachezaji wa Wahenga wakati akiiongoza timu yake kulipa kisasi cha mabao 4-3 kwa wapinzani wao.

Pilikapilika uwanjani wakati Wahenga Fc na Golden Bush zilipomenyana jana jijini Dar es Salaam

Onesmo Waziri 'Ticotico' (4) akipongezwa na Athuman Machupa wakati wakimpisha uwanjani jana katika pambano lao dhidi ya Wahenga Fc.

Jamani Mpo Wapi! Beki wa Wahenga Fc akijiandaa kupiga mpira mbele

Mahadhi akichuana na mchezaji wa Wahenga katika mechi ya jana

Said Swedi 'Panucci' (3) akitafakari namna ya kuupiga mpira wakati wa pambano lao la Golden Bush dhidi ya Wahenga ambapo walifanikiwa kushinda mabao 4-3

Macocha Mayay wa Wahenga (kulia) akiwatoka wachezaji wa Golden Bush, Shaaban Kisiga (kushoto) na Shija Katina (8)

Berki wa Wahenga Fc akihamisha mpira mbele ya Herry Morris (kulia)

Hapa Kazi Tu!

MTANIKOMA! Macocha akiwaacha wachezaji wa Golden Bush katika pambano la jana, mchezaji huyu ndiye aliyekuwa nyota kwa upande wa Wahenga, japo timu yake ililala kwa mabao 4-3


Jamani eeh inakuwaje magoli yamerudi? Ndivyo anavyoelekea kuhoji kocha Madaraka Seleman wa Golden Bush wakati wa mapumziko ambapo timu yake ilikuwa imefungana mabao 2-2 na Wahenga Fc licha ya wao kuongoza kwa mabao 2-0. Waliporejea uwanjani kwa ngwe ya pili walirekebisha makosa na kuisambaratisha Wahenga kwa magoli 4-3

MTANIJUA LEO! Nyota wa Wahenga Macocha Mayay akiwakimbiza wachezaji wa Golden Bush, Godfrey Katepa (9) na Majaliwa (14) wakati timu zao zilipomenyana jana kwenye mechi maalum ya kuukaribisha mwaka 2013 na kusherehekea sikukuu ya Mapinduzi. Golden Bush ilifanikisha kushinda mabao 4-3

MAKOSA YA STOKE YAIPELEKA CHELSEA NA.3 KWENYE LIGI

Eden Hazard (kulia) wa Chelsea akishangilia kufunga goli la nne la timu yake dhidi ya Stoke City kwenye Uwanja wa Britannia mjini Stoke-on-Trent, England jana Januari 12, 2013. Chelsea walishinda 4-0.
Frank Lampard wa Chelsea akishangilia kufunga goli la timu yake dhidi ya Stoke City kwenye Uwanja wa Britannia mjini Stoke-on-Trent, England jana Januari 12, 2013. Chelsea walishinda 4-0.
Frank Lampard (kulia) wa Chelsea akishangilia na Cesar Azpilicueta goli la timu yake dhidi ya Stoke City kwenye Uwanja wa Britannia mjini Stoke-on-Trent, England jana Januari 12, 2013. Chelsea walishinda 4-0.

JON Walters alitupia magoli mawili ya kujifunga na akakokosa na penalti wakati Chelsea ilipoisambaratisha Stoke 4-0 na kumaliza mendo wao wa kuvutia wa mechi 17 nyumbani bila ya kufungwa katika Ligi Kuu ya England.

Walters aliitumbukiza wavuni mwake kwa kichwa cha mkizi krosi ya Cesar Azpilicueta muda mfupi kabla ya mapumziko na akarudia tena kufunga kwa kichwa kwenye lango lao wenyewe kufuatia kona ya Juan Mata.

Frank Lampard alifanya matokeo yawe 3-0 kwa njia ya penalti baada ya Mata kuchezewa madhambi ndani ya boksi kabla ya Eden Hazard kufunga goli kali la nne kwa shuti la umbali wa 30 akitumia mguu wa kushoto.

Siku mbaya ya Walters ilikamilika wakati alipopaisha penalti yake juu ya mwamba katika dakika za lala salama.

Mchezaji huyo raia wa Jamhuri ya Ireland mwenye umri wa miaka 29 amesifiwa sana kwa kiwango chake akiwa na Stoke msimu huu lakini mechi yake ya 100 ya Ligi Kuu ya England iligeuka kuwa shubiri.

Chelsea walikwea hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo katika mechi walionekana kuwa na bahati lakini walisumbuliwa kwa muda mrefu na walishukuru macho sahihi ya mshika kibendera mwanadada Sian Massey kwa kukataa kihalali penalti waliyopewa Stoke wakati matokeo yakiwa 1-0.

Refa Andre Marriner aliamuru ipigwe penalti wakati Azpilicueta alipoteleza na kumuangusha Matthew Etherington ndani ya boksi, lakini Massey alikuwa tayari ameshamnyanyulia Etherington cha kuotea.

Stoke, ambao hawajawahi kuifunga Chelsea kwenye Uwanja wa Britannia, walianza mechi vizuri, wakiwashambulia wageni kwa mipira mingi ndani ndani ya boksi na wakamshuhudia Kenwyne Jones akifumua shuti pembeni kidogo ya lango.

Demba Ba alikuwa akicheza mechi yake ya kwanza ya Ligi akiwa na Chelsea lakini, katika dakika za awali, alikuwa 'bize' katika nesu yao ya uwanja na mara mbili aliokoa hatari langoni kwao.

Ba, ambaye alichezeshwa badala ya Fernando Torres mbele, alihusika katika matukio mengi katika kipindi cha pili.

Alimpasia kwa kisigino Lampard ambaye aliingia ndani ya boksi na kufumua shuti lililopanguliwa na kipa Asmir Begovic, na wakati mwingine alikimbia vyema na kumlazimisha kipa kuokoa kiufundi.


Matokeo ya mechi za jana Jumamosi Jan. 12, 2013;

QPR 0-0 Tottenham
Aston Villa 0-1 Southampton
Everton 0-0 Swansea City
Fulham 1-1 Wigan
Norwich City 0-0 Newcastle
Reading 3-2 West Brom
Stoke City 0-4 Chelsea
Sunderland 3-0 West Ham
Mechi za leo
Manchester Utd v Liverpool
Arsenal v Machester City

AZAM YATETEA TAJI LAKE LA KOMBE LA MAPINDUZI ZANZIBAR

Mgeni rasmi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi (kushoto) akimkabidhi Kombe la ubingwa wa Mapinduzi, Nahodha wa Azam FC, Himid Mao Mkami usiku wa jana Uwanja wa Amaan, Zanzibar baada ya timu hiyo kutwaa taji hilo kwa kuifunga Tusker FC ya Kenya mabao 2-1 ndani ya dakika 120.

Mshambuliaji wa Azam FC, Gaudence Mwaikimba akigombea mpira na beki wa Tusker FC, Joseph Shikokoti katika mchezo wa fainali ya Kombe la Mapinduzi usiku wa jana kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Azam ilishinda 2-1 ndani ya dakika 120 na kutwaa Kombe hilo kwa mara ya pili mfululizo. 
Mshambuliaji wa Azam FC, Gaudence Mwaikimba akimtoka mpira na beki wa Tusker FC, Joseph Shikokoti katika mchezo wa fainali ya Kombe la Mapinduzi usiku wa jana kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Azam ilishinda 2-1 ndani ya dakika 120 na kutwaa Kombe hilo kwa mara ya pili mfululizo. 

Mshambuliaji wa Azam FC, Gaudence Mwaikimba akikimbia na mpira dhidi ya beki wa Tusker FC, Joseph Shikokoti katika mchezo wa fainali ya Kombe la Mapinduzi usiku wa leo kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Azam ilishinda 2-1 ndani ya dakika 120 na kutwaa Kombe hilo kwa mara ya pili mfululizo. 
Mwaikimba akifumua shuti
Mshambuliaji wa Azam FC, Seif Abdallah akimiliki mpira mbele ya beki wa Tusker FC, Bright Jeremiah katika mchezo wa fainali ya Kombe la Mapinduzi usiku wa jana kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Azam ilishinda 2-1 ndani ya dakika 120 na kutwaa Kombe hilo kwa mara ya pili mfululizo. 
Mshambuliaji wa Azam FC, Gaudence Mwaikimba akimtoka beki wa beki wa Tusker FC, Joseph Shikokoti katika mchezo wa fainali ya Kombe la Mapinduzi usiku wa jana kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Azam ilishinda 2-1 ndani ya dakika 120 na kutwaa Kombe hilo kwa mara ya pili mfululizo. 
Shuti la bao, Mwaikimba akiwa amefumua shuti kuifungia Azam bao la ushindi
Wachezaji majeruhi wa Azam, John Bocco 'Adebayor' kushoto na Abdulhalim Humud 'Gaucho' kulia wakiingia uwanjani
Mpira uko nyavuni, mkwaju wa Penalti wa Joackins Atudo umetinga kimiani kuipatia Azam bao la kusawazisha huku kipa Samuel Odhiambo akigagaa chini 
Hongera shujaa Mwaikimba, wachezaji wa Azam wakimpongeza mfungaji wa bao lao la ushindi
Kikosi cha ubingwa jana
Washindi wa pili Tusker FC kikosi chao cha jana
Nahodha Himi Mao akiinua juu burungutu la fedha, Sh. Milioni 10 za ubingwa 
Mgeni rasmi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi (kushoto) akimkabidhi donge nono la Sh. 300,000 mfungaji bora wa Kombe la Mapinduzi, Jesse Were wa Tusker FC aliyemaliza na mabao matano usiku wa jana Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Binti aliyevamia uwanjani dakika ya 89 akitolewa nje na askari Polisi

Mgeni rasmi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi (kushoto) akimkabidhi Kombe la ushindi wa pili wa Mapinduzi, Nahodha wa Tusker FC, Joseph Shikokoti usiku Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Polisi wakimtoa nje binti aliyevamia uwanjani dakika ya 89

Azam wakisherehekea na Kombe lao

Mwaikimba akifuaria na mashabiki Kombe lililotokana na juhudi zake 
Azam wakisherehekea na Kombe lao
Brian Umony wa Azam amemuacha chini Joseph Shikokoti wa Tusker FC
Umony na Shikokoti
Mwaikimba aliyeruka hewani kuiga kichwa kwenye lango la Tusker kufuatia mpira wa kona
Mwaikimba mawindoni


Refa akijaribu kumzuia binti wakati anakatiza uwanjani
Mwaikimba mbele ya Shikokoti

Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
AZAM FC wamefanikiwa kutetea Kombe la Mapinduzi usiku wa jana kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar baada ya kuifunga Tusker FC ya Kenya mabao 2-1.
Kwa ushindi huo, Azam wamezawadiwa Sh. Milioni 10, wakati washindi wa pili Tusker wamepata Sh. Milioni 5.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Ramadhan Rajab Ibada ‘Kibo’ aliyesaidiwa na Mwanahija Makame Mfumo na Mgaza Kindundi, hadi mapumziko hakuna timu iliyofanikiwa kupata bao.
Azam ndio walioshambulia zaidi katika kipindi hicho, lakini hawakuwa na bahati ya kufunga bao japo moja. Gaudence Mwaikimba alipewa pasi nzuri na Brian Umony dakika ya 44, lakini shuti lake kali lilidakwa na kipa Samuel Odhiambo.
Kipindi cha pili, Tusker walirudi na moto mkali na kuanza kusukuma mashambulizi mfululizo langoni mwa Azam.
Hiyo iliwasaidia mabingwa hao wa Kenya kupata bao dakika ya 60, lililofungwa na Jesse Were aliyeunganisha kwa shuti kali la kimo cha mbuzi pasi ya Robert Omunok.
Hata hivyo, bao hilo halikudumu sana, kwani Azam FC walisawazisha dakika ya 72 lililofungwa kwa mkwaju wa penalti na beki Mkenya, Joackins Atudo baada ya beki wa Tusker, Luke Ochieng kuunawa mpira kwenye eneo la hatari.
Katika dakika mbili za nyongeza baada ya kutimu kwa dakika 90 za mchezo huo, alijitokeza binti mwenye umri kati ya 14 na 16 na kukatiza uwanjani akitokea jukwaa la Urusi.
Refa alijaribu kumsimamisha, lakini aliendelea kukatiza Uwanja hadi nje ambako alipokewa na askari Polisi na kutolewa nje kabisa ya Uwanja. Mtangazaji wa Uwanja wa Amaan, Farouk Karim aliwatuliza mashabiki akisema binti huyo ametoroka hospitali ya vichaa, Kidongo Chekundu na tayari Polisi wamemkamata na kumrejesha huko.
Hadi dakika 90 zinamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana bao 1-1 na ndipo zikaongezwa dakika 30.
Gaudence Exavery Mwaikimba aliipatia Azam bao la ushindi dakika ya pili tu tangu kuanza kwa muda wa nyongeza baada ya kuwazidi nguvu na maarifa mabeki wa Tusker.
Kikosi cha Azam leo kilikuwa; Mwadini Ally, Himid Mao, Samir Hajji Nuhu, David Mwantika, Joackins Atudo, Kipre Balou, Humphrey Mieno, Khamis Mcha, Gaudence Mwaikimba, Brian Umony/Malika Ndeule dk126 na Uhuru Suleiman/Seif Abdallah dk64.
Tusker FC; Samuel Odhiambo, Luke Ochieng, Bright Jeremiah, Martin Kizza, Joseph Shikokoti, Frederick Onyango/Mark Ochiambo dk93, Andrew Tolowa/Edwin Ombasa dk 55, Khalid Aucho/Benson Amianda dk 80, Jesse Were/Andrew Sekayambya dk54, Ismail Dunga/Michael Olunga dk52 na Robert Omunok.
 
KWA HISANI YA BIN ZUBEIRY