STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 26, 2012

SHINDALO LA UCHORAJI KWA TAASISI ZA KIELIMU


Shindalo la Uchoraji Kwa Taasisi za Kielimu
Image Profession ikishirikiana na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa mara nyingine inatangaza kuanza kwa muhula mpya wa pili wa Shindano ya Uchoraji maalumu kwa Taasisi za elimu.
Shindano ambalo pia linajulikana Kama: Educational Drawing Competition au Image Profession Educational Drawing Competition, lina malengo ya kuibua vipaji katika fani ya uchoraji kwa kuzingatia uwekezaji kwa watoto na vijana.
Theme/Wazo kuu la mwaka huu: ART IMITATES LIFE au SANAA HUFUATISHA MAISHA
Makundi ya ushiriki
´ Chekechea,
´ Elimu ya Msingi,
´ Elimu ya Sekondari na  
´ Elimu  ya Juu
Kwa maelezo na taratibu za Shindano tembelea Facebook Page/Group “Tanzania Drawing Competition” au wasiliana na BASATA au
DRAWING COMPETITION – IMAGE PROFESSION,
P O BOX 92 DAR ES SALAAM.
SIMU: +255 222 664 740 / +255 713 484 040
/ +255 714 676 217 / +255 716 430 084
EMAIL: info@imageprofession.com

Kamanda Kova ambadili Waziri Makalla pambano la Cheka, Nyilawila

Kamanda Kova
KAMANDA wa Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova, amembadili Naibu waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Amos Makalla katika kuwa mgeni rasmi wa pambano la kimataifa la kuwania ubingwa wa UBO, kati ya Francis Cheka na Karama Nyilawila.
Mratibu wa pambano hilo litakalofanyika siku ya Jumamosi kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam, Robert Ekerege aliiambia MICHARAZO kuwa, kumekuwa na mabadiliko ya mgeni rasmi badala ya Waziri Makalla sasa atakuwa Kova ambaye ni mlezi wa ngumi Tanzania.
Ekerege alisema Kova amechukua nafasi ya Makalla kutokana na waziri huyo kupangiwa safari nje ya nchi ambayo itafanyika wakati pambano la Cheka na Nyilawila likifanyika PTA.
Mratibu huyo alisema kutokana na udhuru huo wameona ni vema nafasi hiyo achukue mlezi wao wa ngumi, Kamanda KOva ambaye ameshaitikia wito huo wa kuwa mgeni rasmi ambapo ndiye atakayemvisha mkanda mshindi wa pambano hilo la uzani wa Supermiddle la raundi 12 litakalochezwa na mwamuzi toka Malawi.
"Kwa sababu zilizo nje ya uwezo wetu, tumeamua kubadili mgeni rasmi wa pambano la jumamosi badala ya kuwa Waziri Makalla sasa ni Kamanda wa Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova, Waziri atakuwa safarini na hivyo hataweza kuhudhuria kama tulivyotangaza awali," alisema Ekerege.
Aliongeza, ugeni wa Kova katika pambano lao limewaongezea uhakika wa ulinzi wa kutosha siku ya mchezo huo ambao unawakutanisha Cheka na Nyilawila kwa mara ya tatu katika safari yao ya ngumi baina yao.
Ekerege alisema maandalizi mengine yanaendelea kama kawaida ambapo mabondia wote watakaopanda ulingoni wanatarajiwa kupima afya na uzito wao kesho kwenye ukumbi huo tayari kwa pambano la Jumamosi ambalo linadhaminiwa na kinywaji cha Coca Cola na kondomu za Dume na litapambwa na burudani toka kwa Mashujaa Band waliopania kuwachezesha wapenzi wa ngumi mtindo wao wa 'Kibega'.


Manchester City hoi Kombe la Ligi, Chelsea yaua

Wachezaji wa Man City wakiwa hoi baada ya kujifunga moja ya mabao yaliyoizamisha jana mbele ya Aston Villa

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City, imeanza vibaya msimu kwa kung'olewa   mapema kwenye michuano ya Kombe la Ligi baada ya kulazwa mabao 4-2 na Aston Villa, huku vinara wa ligi hiyo ya England, Chelsea ikitoa kichapo cha  mabao 6-0 kwa 'Mbweha'.
Kipigo hicho toka kwa Aston Villa, kimempa wakati mgumu kocha wa Man City, Roberto Mancini, kwani ni dalili za kushindwa kurejea mafanikio iliyopata msimu uliopita ilipotwaa taji la Ligi Kuu baada ya miaka 50.
Matokeo mengine ya mechi za jana za michuano hiyo ya Kombe la Ligi ni kama ifuatavyo;
Bradford iliinyuka Burton Abilion mabao 3-2 katika muda wa nyongeza, Chelsea  ilivuna ushindi wa mabao 6-0 kw Wolves, Crawley ilinyukwa mabao 3-2 na Swansea, Leeds United ikainyoa Everton magoli 2-1.


Wachezaji wa Chelsea wakishangilia moja ya mabao yao katika mechi ya Kombe la Ligi jana usiku
Mechi nyingine Manchester City vs Aston Villa baada ya muda wa nyongeza 2-4,MK Dons ikalala mabao 2-0 kwa Sunderland, Preston iliangukia pua mbele ya Middlesbrough kwa kichapo cha mabao 3-1 na Southmpton ilivuna ushindi wa mabao 2-0 kwa Sheffied Wed, Swindon iliinyuka Burnley 3-1 na wagonga nyundo wa West Ham wakalala mabao 4-1 kwa Wigan.

Mgunda afuata nyayo za Saintfiet atimuliwa Coastal Union

Hemed Suleiman 'Morocco' (kushoto) aliyetua Coastal Union
SIKU chake tangu klabu ya Yanga kumtimua kazi aliyekuwa kocha wake mkuu, Tom Saintfiet kutoka Ubelgoji, uongozi wa Coastal Union ya jijini Tanga umemtangaza, Hemed Suleiman 'Morocco' kuwa kocha mpya akichukua nafasi ya aliyekuwa kocha wao, Juma Mgunda.
Morocco, aliyekuwa akiinoa timu ya taifa ya Zanzibar, anatarajiwa kuiangalia Coastal ikicheza pambano  lao dhidi ya Kagera Sugar litakalofanyika kwenye uwanja wa Mkwakwani, chini ya kocha wa makipa, Juma Pondamali aliyekuwa ameachiwa timu baada ya Mgunda na msaidizi wake, Habib Kondo kutimuliwa.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana jijini, uongozi wa Coastal ulifikia maamuzi hayo katika kikao kilichofanyika jana asubuhi na kwamba wamewatimua kufuatia kutoridhishwa na kiwango cha wachezaji wa timu hiyo licha ya kutofungwa mechi.
"Tayari wameshajulishwa maamuzi haya na Morocco atakuwa jukwaani kesho na ndiye atakayeongoza jahazi," alisema kiongozi mmoja wa juu wa timu hiyo.
Chanzo hicho kilisema kuwa katika mchezo wa leo, kocha wa makipa, Juma Pondamali ndiye atakayeiongoza timu hiyo na wanaamini mabadiliko yatazaa matunda.
Mgunda mwenyewe alinukuliwa jana akidai kuwa ameamua kujiondoa Coastal kwa nia njema na mapenzi mkubwa aliyonayo kwa timu hiyo aliyowahi kuichezea kwa mafanikio enzi zake za uchezaji.
Mgunda alisema aliona ni bora ajiondoe kutokana na shinikizo kubwa lililopo ndani ya Coastal ambayo imejiwekea malengo makubwa katika msimu huu wa ligi na kuwataka mashabiki na viongozi wa timu hiyo kumheshimu na kuyaheshimu maamuzi yake yaliyokuja wakati Coastal ikiwa nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kutokana na kushinda mechi moja na kupata sare mechi mbili.

Simba yaenda Zenji kuiwinda Yanga, Jangwani wakimbilia Bagamoyo








MABINGWA watetezi wa soka nchini Simba imeondoka jijini jana kuelekea Zanzibar kwa ajili ya kuweka kambi ya kujiwinda na pambano lao na watani zao Yanga litakalochezwa Jumatano ijayo.
Timu hizo mbili zinatarajiwa kukutana katika pambano la kwanza kwa msimu huu litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa na kurushwa 'live' na kituo cha Super Sport, huku Yanga ikiwa na deni kubwa la kipigo cha mabao 5-0 iliyopata katika pambano baiona yao lililofungia msimu uliopita.
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu', alinukuliwa jana kuwa wachezaji wote 29 wa timu hiyo wameondoka na wanatarajia kurejea keshokutwa kwa ajili ya kuvaana na Prisons ya Mbeya kabla ya kurejea tena visiwani humo kuweka kambi hadi siku ya mchezo wao na Yanga.
Alisema kuwa wakiwa Zanzibar wataendelea kufanya mazoezi ya ufukweni na ya uwanjani na wanaamini kambi yao itazaa mafanikio kwa kushinda mechi hizo zinazowakabili.


Wakati Simba ikienda kujichimbia Zenji, watani zao walikuwa katika mchakato wa kuelekea mjii Bagamoyo kwa ajili ya kujiandaa na pambano hilo la watani zao na lile la Jumamosi ijayo itakapoumana na African Lyon.


Yanga imepania kulipa kisasi cha mabao hayo 5-0 iliyofungwa na Simba Mei 6, lakini pia wakiwa na deni la miaka zaidi ya 30 ya kipigo cha mabao 6-0 ilichopewa na Simba mwaka 1977.



YANGA HATARINI KUSHUSHWA DARAJA - MADENI YA PAPIC NA NJOROGE YAWAPONZA FIFA

Kikosi cha Yanga kilichopo hatarini kiushushwa daraja
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Oseah


Tumepokea barua kutoka Kitengo cha Sheria cha Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Mpirawa Miguu (FIFA) likitutaka tuitaarifu Yanga kuhusu mashtaka yaliyowasilishwa na kocha wazamani wa klabu ya Yanga, Kostadin Papic. Katika malalamiko yake, Papic anadai kuwa hajalipwa malimbikizo ya mshahara wake yanayofikia kiasi cha Dola 12,300 za Kimarekani. Katika barua yake, kocha huyo anadai kuwa alikuwa akiwasiliana na maofisa na viongozi wa Yanga, lakini hakupata ushirikiano na hivyo kuamua kwenda FIFA. TFF ilifanya juhudi za kuwasiliana na Yanga kuhusu malalamiko hayo ili kujaribu kumzuia kocha huyo asishtaki FIFA, lakini juhudi hizo hazikuzaa matunda.
Kama chombo kinachosimamia uendeshaji wa mpira wa miguu nchini, TFF imesikitishwa na habari hizo na inaiomba klabu ya Yanga kufanya kila jitihada kuhakikisha kuwa inawasilisha taarifa zote muhimu na nyaraka zinazohusiana na stahiki za kocha huyo ili kama ilishamalizana naye, sifa ya klabu ya Yanga isafishwe. Tayari barua imeshaandikwa kwa klabu ya Yanga kuitaka itekeleze utashi huo mapema iwezekanavyo.
Tukio hilo, si tu linachafua sifa ya klabu ya Yanga, bali soka ya Tanzania kwa ujumla kutokana na ukweli kwamba ikishadhihirika kuwa kuna tatizo la malipo ya makocha nchini, ni dhahiri kuwa itakuwa ni vigumu kwa klabu zetu na hata timu za taifa kupata makocha wazuri kutoka nje kwa kuwa watakuwa wamejengeka hofu ya kufanya kazi nchini.
Hili ni tukio la pili kwa Yanga baada ya mchezaji wake mwingine, John Njoroge kuishtaki klabu hiyo FIFA na kushinda kesi yake iliyoamuliwa mwezi Januari na Kitengo cha Usuluhishi wa Migogoro cha FIFA (DRC). Ushindi wa Njoroge unamaanisha kuwa iwapo Yanga itashindwa kutekeleza kumlipa mchezaji huyo kasi cha Sh milioni 17, inaweza kujikuta katika adhabu ambayo itatulazimisha tuishushe daraja; kuinyang’anya pointi kwa kiwango kitakachotajwa na FIFA; kuipiga faini au adhabu zote kwenda kwa pamoja. Tunaiomba Yanga itekeleze hukumu hiyo kwa wakati uliotajwa kwenye barua ya FIFA ili kuepuka hatua hizo.
Suala la Njoroge ni moja kati ya matukio mengi yanayohusu ukiukwaji wa taratibu za kuvunja mikataba yanayofanywa na klabu zetu. Kuna malalamiko ya wachezaji wengi dhidi ya klabu zao za zamani kuhusu kutolipwa stahiki zao. Hivyo TFF inatoa wito kwa klabu kujiepusha na vitendo hivyo kwa kuwa vinawanyima haki wachezaji, lakini pia vinachafua sifa ya nchi iwapo wachezaji wanachukua hatua za kwenda kwenye vyombo vya juu.
Tumekuwa tukisoma kwenye vyombo vya habari kuhusu kutimuliwa kwa sekretarieti nzima ya Yanga kutokana na kuonekana kuwa ina udhaifu. Taarifa hizo hazijaifikia rasmi TFF. Kiutaratibu, Yanga inatakiwa iwsasilishe majina ya maofisa watakaofanya kazi na TFF kwa sasa na itakapoajiri sekretarieti ya kudumu, basi itume barua nyingine ya kuwatambulisha watendaji wake.
Kama itakuwa imeitimua sekretarieti nzima, basi TFF inapokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa. Si nia ya TFF kutetea watendaji wazembe, lakini klabu hazina budi kufuatilia kwa karibu utendaji wa sekretarieti zao ili isije ikafikia wakati sekretarieti nzima inaondolewa kwa makosa ambayo yangeweza kusahihishwa kama kungekuwa na ufuatiliaji wa karibu. TFF imekuwa ikitoa mafunzo kwa watendaji wa klabu ili waweze kufanya kazi zao vizuri na kwa mintaarafu ya mpira wa miguu na hivyo kuondolewa kwa timu nzima kama hiyo kunamaanisha kuwa ni upotevu wa rasilimali ambayo imetumika kuwapa elimu ya kutenda kazi zao vizuri. TFF ilishafanya kozi ya Event Management kwa ajili ya watendaji wa klabu; semina ya kuangalia upya maazimio ya Bagamoyo kwa watendaji na viongozi na pia kozi ya utawala hivyo haipendi juhudi hizi zipotee kirahisi.
Angetile Osiah
KATIBU MKUU