STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 26, 2012

Simba yaenda Zenji kuiwinda Yanga, Jangwani wakimbilia Bagamoyo








MABINGWA watetezi wa soka nchini Simba imeondoka jijini jana kuelekea Zanzibar kwa ajili ya kuweka kambi ya kujiwinda na pambano lao na watani zao Yanga litakalochezwa Jumatano ijayo.
Timu hizo mbili zinatarajiwa kukutana katika pambano la kwanza kwa msimu huu litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa na kurushwa 'live' na kituo cha Super Sport, huku Yanga ikiwa na deni kubwa la kipigo cha mabao 5-0 iliyopata katika pambano baiona yao lililofungia msimu uliopita.
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu', alinukuliwa jana kuwa wachezaji wote 29 wa timu hiyo wameondoka na wanatarajia kurejea keshokutwa kwa ajili ya kuvaana na Prisons ya Mbeya kabla ya kurejea tena visiwani humo kuweka kambi hadi siku ya mchezo wao na Yanga.
Alisema kuwa wakiwa Zanzibar wataendelea kufanya mazoezi ya ufukweni na ya uwanjani na wanaamini kambi yao itazaa mafanikio kwa kushinda mechi hizo zinazowakabili.


Wakati Simba ikienda kujichimbia Zenji, watani zao walikuwa katika mchakato wa kuelekea mjii Bagamoyo kwa ajili ya kujiandaa na pambano hilo la watani zao na lile la Jumamosi ijayo itakapoumana na African Lyon.


Yanga imepania kulipa kisasi cha mabao hayo 5-0 iliyofungwa na Simba Mei 6, lakini pia wakiwa na deni la miaka zaidi ya 30 ya kipigo cha mabao 6-0 ilichopewa na Simba mwaka 1977.

No comments:

Post a Comment