STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 26, 2012

Mgunda afuata nyayo za Saintfiet atimuliwa Coastal Union

Hemed Suleiman 'Morocco' (kushoto) aliyetua Coastal Union
SIKU chake tangu klabu ya Yanga kumtimua kazi aliyekuwa kocha wake mkuu, Tom Saintfiet kutoka Ubelgoji, uongozi wa Coastal Union ya jijini Tanga umemtangaza, Hemed Suleiman 'Morocco' kuwa kocha mpya akichukua nafasi ya aliyekuwa kocha wao, Juma Mgunda.
Morocco, aliyekuwa akiinoa timu ya taifa ya Zanzibar, anatarajiwa kuiangalia Coastal ikicheza pambano  lao dhidi ya Kagera Sugar litakalofanyika kwenye uwanja wa Mkwakwani, chini ya kocha wa makipa, Juma Pondamali aliyekuwa ameachiwa timu baada ya Mgunda na msaidizi wake, Habib Kondo kutimuliwa.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana jijini, uongozi wa Coastal ulifikia maamuzi hayo katika kikao kilichofanyika jana asubuhi na kwamba wamewatimua kufuatia kutoridhishwa na kiwango cha wachezaji wa timu hiyo licha ya kutofungwa mechi.
"Tayari wameshajulishwa maamuzi haya na Morocco atakuwa jukwaani kesho na ndiye atakayeongoza jahazi," alisema kiongozi mmoja wa juu wa timu hiyo.
Chanzo hicho kilisema kuwa katika mchezo wa leo, kocha wa makipa, Juma Pondamali ndiye atakayeiongoza timu hiyo na wanaamini mabadiliko yatazaa matunda.
Mgunda mwenyewe alinukuliwa jana akidai kuwa ameamua kujiondoa Coastal kwa nia njema na mapenzi mkubwa aliyonayo kwa timu hiyo aliyowahi kuichezea kwa mafanikio enzi zake za uchezaji.
Mgunda alisema aliona ni bora ajiondoe kutokana na shinikizo kubwa lililopo ndani ya Coastal ambayo imejiwekea malengo makubwa katika msimu huu wa ligi na kuwataka mashabiki na viongozi wa timu hiyo kumheshimu na kuyaheshimu maamuzi yake yaliyokuja wakati Coastal ikiwa nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kutokana na kushinda mechi moja na kupata sare mechi mbili.

No comments:

Post a Comment