STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 24, 2011

20% kuzindua Malumbano J'pili





MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abbas Hamis Kinzasa '20 Percent' anatarajia kuzindua na kuitambulisha rasmi albamu yake mpya iitwayo 'Ya Nini Malumbano' siku ya Jumapili.
Uzinduzi huo utakaosindikizwa na wasanii kadhaa nyota nchini unatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Club Masai, Oysterbay jijini Dar es Salaam chini ya utaribu wa kampuni ya King Kif Entertainment.
Akizungumza na Micharazo leo asubuhi, mkurugenzi wa kampuni hiyo, Sigfred Kimasa 'King Kiff', alisema maandalizi ya onyesho hilo yamekamilika ikiwemo wasanii nyota kibao kukubali kumsinidikiza mkali huyo ambaye anasifika kwa nyimbo zenye mafunzo na ujumbe mwanana.
"Msanii 20 Percent atazindua albamu yake ya Ya Nini Malumbano, akisindikizwa na wasanii kadhaa nyota, katika onyesho litakalofanyika Jumapili kwenye ukumbi wa Club Maisha," alisema.
Aliwataja wasanii watakaomsindikiza mkali huyo ambaye pia ni mahiri katika uigizaji filamu ni pamoja na 'swahiba' wake, Seleman Msindi 'Afande Sele'. Man Wter ambaye pia ni mtayarishaji wa albamu hiyo, Ney wa Mitego, Sajna, Linex na Uncle G.
Mbali na kibao cha Ya Nini Malumbano, albamu hiyo ya 20 Percent ina nyimbo nyingine kama Tamaa Mbaya ambao umekuwa ukitamba kwenye vituo kadhaa vya redio nchini, Neno la Mwisho na Nimerudi Salama.
Nyimbo nyingine ni Nyerere, Nia Yao, Mwema, Naficha, Kubadili Mwendo na Ya Nini Malumbano.
Hiyo ni albamu ya tatu ya msanii huyo ambaye anatamba pia na nyimbo za Money Money, Bangi na nyingine, awali alitoa albamu za Money Money na Mama Neema ambazo zinadaiwa kufanya vema sokoni licha ya nyimbo zake kumpa tuzo kadhaa za muziki nchini.

.