STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 28, 2012

Uigizaji haulipi kama muziki-Kitale

MSANII KITALE AKTIKA KATIKA POZI TOFAUTI
MSANII nyota wa filamu cha vichekesho nchini, Mussa Yusuf 'Kitale' amedai licha ya fani ya uchekeshaji kutolipa kama muziki, lakini katu hawezi kuachana na fani hiyo. Akizungumza na MICHARAZO, Kitale alisema ndio maana kwa sasa akishirikiana na Husseni Mkiety 'Sharo Milionea' wameandaa filamu zao binafsi zaidi ya tano. Alisema katika muziki msanii ananufaika kwa vile huwa ni kazi yake binafsi tofauti na filamu ambapo mabosi ndio wanaoneemeka na msanii hutumika tu kama kibarua. "Kwenye filamu na uchekeshaji tunaambulia sifa tu, lakini kimasilahi ni kidogo tofauti na muzikio, hata hivyo siwezi kuachana na fani hii kwani nimeshaizoea na kwa sasa kuna kazi mpya ninazoandaa na Sharo Milionea," alisema. Alizitaja kazi hizo kuwa, "Sharo Madimpoz', 'Sharo Crazy', 'Sharo Taxi Driver' na 'Drug Dealer' ambazo anaziandaa kwa kushirikiana na Sharo Milionea ambaye wamekuwa wakiendana katika uigizaji wao. "Hizi ni baadhi ya filamu tutakazotoa ndani ya mwaka huu, sambamba na kazi zetu za muziki ambazo kila mmoja anaifanya na kumpa mafanikio makubwa," alisema. Kitale anayeigiza kama 'teja', alisema amepanga kabla ya kumalizika kwa mwaka huu albamu yake binafsi iwe imeshaingia sokoni.

Manyika avunja ukimya na Wololowololo

NYOTA wa zamani wa Yanga aliyetumbukia kwenye muziki, Manyika Peter, ameachia wimbo mpya uitwao 'Wolowolo', akijiandaa kutolea video yake. Akizungumza na MICHARAZO, kipa huyo aliywahi kung'ara na timu za Mtibwa Sugar, Sigara, Yanga na klabu kadhaa za kimataifa alisema kazi hiyo ni ya pili tangu alipotoa albamu yake mwaka 2004. Manyika, alisema 'Wololowololo' umetoka ikiwa ni miaka minne tangu atoe wimbo wake wake wa mwisho mwaka 2007 uitwao 'Manabii'. "Baada ya kimya kirefu nimetoka na wimbo wa 'Wololowololo' ninaouandalia video yake, hiki ni kibao cha pili baada ya albamu yangu ya 'Unanipeleka Puta' ilitoka mwaka 2004," alisema. Manyika, alisema tofauti na alipotumbukia kwenye fani hiyo mwaka 2001 wakati akiwa anaichezea Yanga, kwa kutoa albamu, safari hii hana mpango huo kwa madai utoaji wa albamu haulipi kama kutoa 'singo'. "Sina mpango wa kutoa albamu, nitaendelea kutoa wimbo mmoja mmoja kwa lengo la kupata shoo ambazo ndizo zinazolipa vema," alisema. Alisema wakati akihangaikia kuitolea video wimbo huo wa 'Wololowololo', tayari kuna nyimbo nyingine mbili ameshaziandika ambazo atazirekodi baadae ili kudhihirisha nia yake ya kujikita jumla kwenye muziki.
MANYIKA PETER KATIKA POZI TOFAUTI KAMA MSANII WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA

Mpeni muda Kim atufikishe mbali kimataifa-Manyika

NYOTA wa zamani wa kimataifa aliyewahi kuzichezea timu za Mtibwa, Sigara na Yanga, Manyika Peter, amewataka wadau wa soka nchini kumpa muda kocha Kim Poulsen, ili afanye kazi zake kwa manufaa ya soka la Tanzania. Pia, aliwataka wadau hao kutoweka matumaini makubwa ya timu yao ya taifa, Taifa Stars kufuzu fainali za Afrika 2013 au Kombe la Dunia 2014, ila nguvu ziwekezwe kwa fainali za mbele zaidi akiamini timu itakuwa imewiva. Manyika, alisema Tanzania imekuwa ikikwama kufika mbali kwa vile makocha wanaozifundisha timu za taifa na hata klabu hawapewi muda mrefu wa kukaa na timu husika, kitu alichotaka kisitokee tena kwa kocha wa sasa wa Stars. "Tumpeni nafasi Kim aweze kufanya kazi zake na naamini kwa uwezo alionao tunaweza kufika mbali zaidi na hapa tulipo, ila kama tutaendelea na tabia ya kulaumu kisha aondolewe tutadumaa hapa hapa kisoka," alisema. Alisema Kim, ni mmoja wa makocha wazuri kutokana na kufanya nae kazi akiwa kama Mkufunzi wa FIFA wa makipa wa timu za taifa za vijana, hivyo aliwataka wadau wa soka wasimbughudhi ili afanye kazi zake kwa ufanisi. Aliongeza, licha ya kuwataka wadau wawe na subira pia wasiweke tumaini kubwa la Tanzania kufuzu fainali zijazo za Afrika zitakazofanyika Afrika Kusini au Kumbe la Dunia la Brazil, ingawa alikiri lolote linaweza kutokea. "Tukifuzu itakuwa ni bahati, lakini nadhani tunapaswa kuweka nguvu kwa ajili ya fainali za mbele, tumechelewa mno kujipanga hivyo lolote litakalotokea tulichukulie poa na kujipanga zaidi ili tufuzu michuano ijayo," alisema. Tanzania ipo kwenye mbio za kuwania kufuzu fainali za Afrika ikitarajiwa kuvaana na Msumbiji katika mechi ya marudiano Juni 15 baada ya awali kutoka sare. Pia ipo kundi C na timu za Ivory Coast, Morocco na Gambia katika mbio za kuwania kucheza fainali za Kombe la Dunia za 2014 zitakazofanyika nchini Brazil, ikianza kibarua Juni 2 kwa kuumana na Ivory Coast.

Sijasaini kokote-Nsa Job

MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya Villa Squad, Nsa Job, amesema licha ya kuzungumza na watu wa Coastal Union ya Tanga, bado hajasaini fomu yoyote ya kujiunga kuichezea timu hiyo kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Kutokana na kutosaini, Nsa alisema milango i wazi kwa klabu yoyote ambayo imevutiwa naye, mradi aridhishwe na dau watakalokubaliana. Akizungumza na MICHARAZO, Nsa alisema ni kweli amefanya mazungumzo na Coastal Union, ila hawaafikiana na ndio maana hajasaini fomu na hivyo kutoa ruksa kwa timu nyingine kuweza kuzungumza nae. "Sijasaini kokote ndugu yangu, ingawa ni kweli nilishafuatwa na kuzungumza na watu wa Coastal Union," alisema. Nsa, alisema yeye kama mchezaji anaangalia masilahi hivyo timu yenye dau kubwa la kuvutia ndio atakayoichezea kwa msimu huo ujao. Nyota huyo aliyewahi kuzichezea timu za Moro United, Simba, Yanga na Azam, alisema hawezi kukurupuka kusaini timu bila kuangalia masilahi yake ikizingatiwa soka kwake ndio ajira inayomuingizia kipato. "Soka la sasa sio la kuchezea sifa, naangalia masilahi kwanza timu baadae," alisema.

Boxer Johnny Tapia has died at the age of 45

Tapia, whose career was marked by cocaine addiction, alcohol, depression and run-ins with the law, was found dead on Sunday in his hometown of Albuquerque, New Mexico. He won the WBO super-flyweight title in 1994, two belts at bantamweight and the IBF featherweight belt in 2002. Police spokesman Robert Gibbs said the death "did not appear to be suspicious". His tragic start in life - both parents were murdered, several stints in jail and numerous rivalries, garnered him a cult following in the sport. Tapia was orphaned at eight when his mother was murdered in brutal circumstances and, despite his successes in the ring, trouble stalked him for the rest of his life. Having been banned from boxing for three and a half years in the early 1990s because of his cocaine addiction, he beat Henry Martinez to become a world champion for the first time. Tapia went 11 years unbeaten as a professional before Paulie Ayala defeated him in 1999 in The Ring magazine's Fight of the Year, taking his WBA bantamweight title. Tapia lost a rematch with Ayala in 2000. In 2002 he beat Manuel Medina to secure the IBF featherweight crown and was good enough to take Mexican great Marco Antonio Barrera the distance later that same year. In 2007, he was hospitalised after an apparent cocaine overdose. Several days later, his brother-in-law and his nephew were killed in car accident on their way to Albuquerque to see the ailing boxer. In his 2006 autobiography, Tapia described how he had been declared clinically dead five times, each time due to a drug overdose. He also survived shootings, a bus crash and a near-drowning. Tapia last fought in June, outpointing Mauricio Pastrana. He finished with a 59-5-2 record.